Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Sikutarajia Slaa aongee tofauti na hivyo, eti wawekezaji walikuja awamu ya tano. Slaa anadhani kwakuwa aliwahi kuaminika hapo nyuma basi na sasa ataaminika.
Tumboni hakuna kitu anajua teuzi zinapatikana kwa kupiga yowe tumpuuze tu....
 
Siku hizi humu baada ya uzi ni matusi tu. Kwani mnaomtukana huyu mzee mnakosoa hoja ipi? Zamani watu wali quote sentensi na kupangua hoja! Mbona mambo mengi kaongea kwa ushahidi mzuri tu? Au mnataka kusikia yanayowasha masikio yenu tu!
Ushahidi wa kwamba aliletewa taarifa? kwanini hakuwaripoti polisi Msadieni Mzee wenu njaa itamuua Mtaani
 
Huyu mzee nitamtetea maeneo mengi bila kupepesa. Anaishi kwa principles kitu ambacho wanasiasa wetu wengi hawana. Hata umchukie vipi, facts zake hazibadilishwi kipropaganda.
Eti anaishi kwa principal huyu alieltewa habari za kutekwa kijana wake lkn akakaa kimya mpaka alipomaliza muda wake wa Ubalozi
 
Kuna watu wamepata access ndio wanafanya political spinning. Lakini hii inakwenda Bungeni na kupitia kamati zake facts zote zitafahamika.
..hoja kama hasara ktk mashirika ya umma nazo zinahitaji kusubiri wahusika wakajitetee ktk kamati ya bunge?

..binafsi ningefurahi kama mijadala ya kamati za bunge ingekuwa inaonyeshwa live au recorded.
 

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”

Chanzo: Dar24
Yaonekana, Dr Mihogo alipumbazwa na misifambuzi aliokuwa akimiminiwa na HASA mamluki wenzie/wahuni wa kijani.
Alikuja akaamini kuwa CDM bila ya yeye wangekwama. Sasa kakwama yeye mpaka nyumbani mwake.
Ana hasira sana HAYAMINI MACHO YAKE.....
 

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”

Chanzo: Dar24
Huyu atagombea urais ccm 2025. Mtakuja kuniambia wakiuu.
 
Hasara ( Loss) si kigezo cha ufisadi ni metrics zinazohitaji professional opinion after Audit queries response. Ukiukwaji wa procurement process inaweza kuwa ni upindishaji wa taratibu lakini usio na hasara!

Kwenye ukaguzi Auditor anafata muongozo ulivyopaswa kufanyika alafu anaangalia taratibu zilizofatwa. Kama utaratibu haukufatwa lazima iwe query na risks zake. Wakati wa kufunga hoja inaweza kubaki na sura hii 1) Utaratibu umekiukwa lakini haukuleta hasara 2 ) Utaratibu umekiukwa na kuleta hasara. Vyote ni tatizo na hapo ndio tunapaswa kuhukumu.

Kwasasa CAG ameona jambo ambalo hajapata jibu na ameainisha risks za hilo aliloona! Sasa kabla hatujaanza siasa tungesubiri kuona serikali wamefungaje hiyo hoja then tuanze kelele!

Kwasasa wanasiasa mandumilakuwili wamebeba findings na figures zake wanahukumu watu kuwa ni mafisadi kuliko wakati wowote nchi hii imepata kushuhudia! Purely cheap politics kwa watu ambao wanajua facts ila wanatumia ufahamu wao kudanganya umma! Ni dhambi hii!
Na serikali wanafungaje hoja za CAG?
Hiyo platform ya kuongea na umma sio ya hao unaowashutumu kwa ulaghai wa kisiasa peke yao. Hamna anayeizuia serikali na chama chake kutolea ufafanuzi pale wanapoona wameonewa na CAG.
Na kama facts zipo ila zimepindishwa tu na watu wenye nia ovu, hiyo itakuwa sahihi. Ila kuwazuia watu kuongea mpaka mtakapokuwa na narrative mnayoipenda nyinyi sio haki. Hizo ndio cheap politics za kutumia ubabe kuzuia mjadala.

Amandla...
 
Ujua wao wanaamini Mbowe ni malaika na wanachadema wote ni wema! Nakuambia ukianikwa ubaya na maovu ya Mbowe watashika kichwa! Hata Sumaye aliambiwa sumu haionjwi!

Sirro alisema hivyo hivyo. Ajabu DPP akaondoa mashtaka ya ugaidi mahakamani wakati mahakama imeshathibitisha kuwa Mbowe ana kesi ya kujibu! Kama sio “uswahili” huo ni nini?

Hii ni serikali ya ajabu. Yaani ishindwe kumshughulikia Mbowe kisheria, itegemee sisi tushike vichwa kwa ubaya na maovu yake kuanikwa! Halafu akishasutwa ndio basi! Tangu lini nchi ikaendeshwa kwa mipasho na taarab?
 
Huyu mzee nitamtetea maeneo mengi bila kupepesa. Anaishi kwa principles kitu ambacho wanasiasa wetu wengi hawana. Hata umchukie vipi, facts zake hazibadilishwi kipropaganda.
Kama kweli nawe wayaamini hayo kutoka moyoni mwako, yafaa BASI uungane nae mkiwa na Madeluu muwapitie Dr Mollel, Mwita Waitara, Lijualikali, Ndugai na Suzana Masele, muyapeleke kwa Kingai, muanzishe kesi nyingine ya ugaidi.
 
HEBU TUJADILI HII STATEMENT YA @drslaa



SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.
Lissu hana haja ya kumjibu Slaa. Ila Slaa anazeeka vibaya. Pole mzee baba.

Au tumepata Msiba namba mbili?
 
Huyu mzee nitamtetea maeneo mengi bila kupepesa. Anaishi kwa principles kitu ambacho wanasiasa wetu wengi hawana. Hata umchukie vipi, facts zake hazibadilishwi kipropaganda.
Kama kweli nawe wayaamini hayo kutoka moyoni mwako, yafaa BASI uungane nae mkiwa na Madeluu muwapitie Dr Mollel, Mwita Waitara, Lijualikali, Ndugai na Suzana Masele, muyapeleke kwa Kingai, muanzishe kesi nyingine ya ugaidi.
 
..hoja kama hasara ktk mashirika ya umma nazo zinahitaji kusubiri wahusika wakajitetee ktk kamati ya bunge?

..binafsi ningefurahi kama mijadala ya kamati za bunge ingekuwa inaonyeshwa live au recorded.
Zipo hoja za CAG zinastahili mjadala maana hazistahili utata na zina direct impact na results zake ni hasara, hata ikipewa majibu ni sababu ya hasara iliyokwishatokea. Ila tatizo ukifatilia kwa makini report ya CAG inavyojadiliwa imejaa hatari ya kutumika kisiasa kuliko uhalisia.

JF huko nyuma watu walileta hadi screen shot ya sections za CAG report kujadiliana. Sasa hivi mtu anakuja na note book anaitisha press au kuandika JF na kutuhumu tu. Alafu hapa tunaangalia aliyesema au kuandika na kama ni mizania tofauti na yako ni kupinga au kuruka nayo kama vile tayari tuna facts.

Siasa za nchi yetu haziko kwenye hali nzuri maana kuna makundi yaliyotawala na kusigana ikijumuisha vyama vyote na kubakiza vyama kama vivuli tu. Sisi huku tunalishwa na hiyo misigano na kama tusipokuwa watu wa kutulia na kufatilia facts tutakaangana sana.
 
Siku hizi humu baada ya uzi ni matusi tu. Kwani mnaomtukana huyu mzee mnakosoa hoja ipi? Zamani watu wali quote sentensi na kupangua hoja! Mbona mambo mengi kaongea kwa ushahidi mzuri tu? Au mnataka kusikia yanayowasha masikio yenu tu!
Ushahidi mzuri ni upi hapo?.au mtu kueleza mtazamo wake ambao unaweza kua sio kweli kwako ndo ushaidi mzuri?
 
We unafikiri KWA heshima ya Dr.slaa enzi na enzi angeamua kuuza utu wake KWA pesa angekua wapi?Mmezoea wanasiasa malaya malaya ndo Tatzo,leo mnamuita Fisadi kesho ndo apeperushe bendera ya chama
Msimuache basi, mchukueni huko kwenye vyama vyenu, ili akili yake itulie.
 
Dr Salaa ni miongoni mwa watu waliokuwa na heshima sana nchini

Katika siku za karibuni Salaa amekuwa na 'project' ya kuharibu integrity and credibility yake

Kazi ya ubalozi ni kama asali, ameshailamba na sasa anataka kuchonga mzinga.

Dr ana uhuru wa kutoa maoni, kinachosikitisha ni maoni yaliyojengwa juu ya chuki
Chuki imeutawala moyo wake hata kufikia mahali ukweli anauona ni sumu kuliko chuki aliyobeba

Kuhusu TL , swali hilo anaulizwa mara nyingi na kila anapojibu wasomaji wanabaki ''WHAT?
''Waandishi'' humuuliza ku'push agenda bila kujua au kwakujua anafanya kile kilichokusudiwa

Anamsema TL kwa kuonyesha mfano wa 'Chadema walivyowahi kudhuriana'' .
Fact aliyo nayo ni kuambiwa na red brigade aliyekataa kumwambia kabla.

Dr Salaa anamaanisha tukio la TL kupigwa risasa lina utata ''hawezi'' kulizungumzia huku akiwa tayari kalizungumzia kwa tuhuma za red brigade. Nafsi inamsuta na anajificha ficha! anajua anachosema si kweli kina maumivu kwa Tundu Lissu na Rais wema duniani, anazunguka zunguka

Kila mtu anajua nani alifanya nini. CCM wanaomba maridhiano wasiyosema ni ya nini

Dr Slaa anajua masaa machache kabla ya TL kupigwa risasi JPM alisema nini

Mr Slaa anajua Camera zimeondolewa , Walinzi waliondolewa na hakuna uchunguzi
Hata waliojaribu kwenda kumsalimia TL baada ya risasi lukuki mwilini waliona cha mtema kuni.

Anajua matibabu ya TL yalizuiwa kwa makusudi

Badala ya kueleza mfano wa kipuuzi aliokutana nao Padr Slaa ange address controversies ambazo serikali haiwezi kuzieleza.

Tundu Lissu, Mhanga, anasema wazi waliopanga na waliotekeleza. Hakuna anayepinga hilo.

Dr Slaa anaweka doubt kwamba TL alishambuliwa kwa risasa.

Bwana Slaa amefikia kiwango cha chini sana kimaadili '' moral decay' kujidhalilisha

TL ni mlemavu , anaishi kwa maumivu ! Dr Salaa alitoroka kwasababu anawindwa.

TL hakuwindwa bali anaishi majeraha ya kuwindwa. TL ana makovu mwilini ana risasi imebaki

Dr Slaa anaamini kuna ufeki katika hilo, na kwamba, pengine ni wenzake! hatafuti fact tena

Dr Slaa unachokifanya kinakuondolea thamani ya utu., kwamba Uhai wa mwanadamu unautweza na kuuweka katika mizani na matamanio ya nafsi yako! upate mkate kwa kudhalilisha Utu.

Jaribu kuushinda ubinafsi ili uutukuze UTU! Uamini katika ubindamu si nafasi au teuzi!

Dr Slaa ukifungua mdomo jitathmini! sidhani kama umefikia kiwango hicho!


JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
AMEN
 
Zipo hoja za CAG zinastahili mjadala maana hazistahili utata na zina direct impact na results zake ni hasara, hata ikipewa majibu ni sababu ya hasara iliyokwishatokea. Ila tatizo ukifatilia kwa makini report ya CAG inavyojadiliwa imejaa hatari ya kutumika kisiasa kuliko uhalisia.

JF huko nyuma watu walileta hadi screen shot ya sections za CAG report kujadiliana. Sasa hivi mtu anakuja na note book anaitisha press au kuandika JF na kutuhumu tu. Alafu hapa tunaangalia aliyesema au kuandika na kama ni mizania tofauti na yako ni kupinga au kuruka nayo kama vile tayari tuna facts.

Siasa za nchi yetu haziko kwenye hali nzuri maana kuna makundi yaliyotawala na kusigana ikijumuisha vyama vyote na kubakiza vyama kama vivuli tu. Sisi huku tunalishwa na hiyo misigano na kama tusipokuwa watu wa kutulia na kufatilia facts tutakaangana sana.
Facts gani unazozingumzia? Report yeyote inaweza kutumika kisiasa maana hizo unazoita facts zinategemea anaezitafsiri ni nani. Wanasiasa kutumia ripoti ya CAG kisiasa sio dhambi. Sisi wananchi tutafaidika kwa kuona pande mbili au tatu za hizo "facts" na kujifanyia maamuzi yetu maana sisi ndio maboss wao.

Usituambie kuhusu hizo JF za huko nyuma maana tulikuwepo. Na kilichokuwa kinafanyika ni hiki kinachofanyika hivi sasa. Mjadala wa wazi kuhusu taarifa bila upande mmoja kutuambia tusubiri mpaka tutafuniliwe kwanza. Unadhani watu wangegoja Kamati za Bunge zijadili masuala ya IPTL na shutuma nyingine ndio wajadili kuna kitu kingefanyika? Huyo Slaa mwenyewe alisimama Mwembe Yanga na aliwashutumu watu bila kungoja taarifa ya kamati za Bunge. Leo amehamia upande wa pili ndio anataka na sisi tumfuate! Ukigeu geu wake abaki nao. Sisi tutampinga kila anapotaka kutupotosha bila kujali kuwa kuna wakati alisimamia upande wa haki.

Amandla...
 
Back
Top Bottom