Dkt. Abbas na Abdul Nondo watofautiana namna watoto wa kike wanaopata mimba shuleni watakavyoendelea na masomo

Mwanao wa kike akipata mimba utampeleka mfumo upi..?
Kuna mambo ambayo lazima kama jamii yenye upekee wake tuyasimamie hata kwamba tunatofautiana kiitikadi.

Moja ya jambo hili ni mimba kwa wanafunzi. Siafiki mwanafunzi apate Ujauzito kurudi katika mfumo rasmi wa elimu kama wenzake ambao hawajapata.

Hapa tutahalalisha umama, baba na hata ushemeji katika shule/darasa na ile dhana ya uanafunzi kufa kifo cha kawaida.

Kila kitu kinautaratibu wake. Tutambue pia kuwa shule ni ni chombo ambacho jamii inawatengeneza wanajamii wa baadae katika kuiendeleza jamii husika kwa siku za usoni. Na kwamba, ni unapokuwa shuleni basi uzingatie ile miiko ambayo jamii imeona haipaswi kuvunja na watoto wake ndio maana wakapelekwa shule.

Sasa kama huyu aliyepelekwa shule ameona hawezi kufata misingi hiyo ya jamii ya nini kumuendeleza katika jambo ambalo hakulizingatia?


Shule zibaki kuwa shule na taratibu, sheria, utamaduni na majuzi zake zisimamiwe. Ikiwa ikatokea mwanafunzi akapata Ujauzito basi, apelekwe katika mfumo mbadala usio rasmi na ule aliokengeuka ili shule na malengo ya shule katika jamii yabaki kama ambavyo jamii inapenda iwe.


Sio kila atakalo mfadhili ni jambo jema ktk mfadhiliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dr Abbas ambaye ni msemaji mkuu wa serikali anasema wanafunzi wanaopata mimba shuleni hawatarudi kuendelea na masomo katika mfumo rasmi bali wataruhusiwa kupitia mfumo usio rasmi yaani private candidates.

Abdul Nondo boss wa vijana pale ACT wazalendo anapinga vikali yeye anataka wanafunzi hawa baada ya kujifungua warudi katika mfumo rasmi wa masome ili wawe na sifa ya kukopesheka na Bodi ya mikopo watakapochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu.

Mjadala ni mkali kweli kweli ndani ya kipindi cha Tuongee asubuhi. Star tv.

Nani yuko sahihi?

Maendeleo hayana vyama!
ila katika eneo ambalo ACT wamebugi ni kumuweka huyu dogo kama msemaji wa chama. yes, ana content lakini hana ile appropriate art ya kui present such that anaishia kuwa all over the kitchen!

yule dogo mwingine (aitwa nani vile? Shaibu something I think)..... yule alikuwa kifaa sana kwenye hii nafasi ya usemaji.

cc Zitto
 
haiwezekani ukapata mimba ukarudi tena kwenye mfumo rasmi je? si itakuwa kuruhusu mapenzi shuleni kila msichana atajiachia na kuzaa akijua atarud tena kuendelea na shule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ila katika eneo ambalo ACT wamebugi ni kumuweka huyu dogo kama msemaji wa chama. yes, ana content lakini hana ile appropriate art ya kui present such that anaishia kuwa all over the kitchen!

yule dogo mwingine (aitwa nani vile? Shaibu something I think)..... yule alikuwa kifaa sana kwenye hii nafasi ya usemaji.

cc Zitto
kwan huyu dogo ni msemaji au ni mwenyekiti wa ngome ya vijana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiitifaki, huyo bwana mdogo alitakiwa akutanishwe na Mwenyekiti wa UVCCM; Katibu Mkuu ni nafasi kubwa katika Utumishi wa Umma. Waandaji wa kipindi hawajatenda haki kwa Katibu Mkuu.

Katika mjadala huu, baadhi ya wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wanakusudia kuhujumu elimu yetu na taifa kwa ujumla kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Katika hili, msimamo wa serikali uungwe mkono.

Haikuwa interview ya nafasi ya kazi, bali ilikuwa ni kipindi kama vipindi vingine. Kilichokuwa kinafanyika ni kuelezea suala la mkopo wa bank ya dunia kwa Tanzania. Huyo msemaji wa serikali alisemea upande wa serikali, na Abdul Nondo alisimama kama mtu wa sera mbadala. Usitake kumuona huyo katibu mkuu ni so special kumbe ni wa kawaida sana.
 
Sijawahi na ntapiga kelele daima mtoto aliyepachikwa mimba kwangu marufuku kurudi shule.


Labda watengewe shule ya wazazi au wajawazito.
 
Serikali ishikilie msimamo wake, hakuna sababu ya kupoteza rasilimali kwa msichana aliyeshindwa kuwa makini na masomo wakati akiwa siyo mzazi, baada ya kuwa mzazi ndio awe makini na masomo?.Hizo rasilimali acha wazitumie wanaojitambua,na kuelewa umuhimu wa elimu.Hawa wasichana hata hao wanao wapa mimba huwa hawapo tayari kuwataja, halafu huyo mtu unataka arejee shule.Mimi binafsi sijawahi kuona msichana anayependa shule hata kama hana akili amepigwa mimba,achilia mbali wenye akili.Hao wanaopata ujauzito ni wale vilaza na wasiopenda shule.
 
Haikuwa interview ya nafasi ya kazi, bali ilikuwa ni kipindi kama vipindi vingine. Kilichokuwa kinafanyika ni kuelezea suala la mkopo wa bank ya dunia kwa Tanzania. Huyo msemaji wa serikali alisemea upande wa serikali, na Abdul Nondo alisimama kama mtu wa sera mbadala. Usitake kumuona huyo katibu mkuu ni so special kumbe ni wa kawaida sana.
Tofauti na wewe, kwangu mimi, mtumishi wa Umma anayehudumu kama Katibu Mkuu, kwa kutambua mamlaka na nguvu zinazotokana na wajibu na majukumu yake, siwezi kumwona kama mtu wa kawaida.
 
Tofauti na wewe, kwangu mimi, mtumishi wa Umma anayehudumu kama Katibu Mkuu, kwa kutambua mamlaka na nguvu zinazotokana na wajibu na majukumu yake, siwezi kumwona kama mtu wa kawaida.
Katibu mkuu unamwona kama nani?......malaika!
 
Tofauti na wewe, kwangu mimi, mtumishi wa Umma anayehudumu kama Katibu Mkuu, kwa kutambua mamlaka na nguvu zinazotokana na wajibu na majukumu yake, siwezi kumwona kama mtu wa kawaida.

Kama unaabudu sanamu, hilo ndio hitimisho. Lakini kama unajua cheo ni dhamana, hakuna namna utapata hofu na mtu mwenye cheo fulani.
 
Katibu mkuu unamwona kama nani?......malaika!

Hoja yangu haikuwa hiyo uliyoileta wewe. Badala yake, mzizi wa hoja yangu ulikuwa katika itifaki; huyo kiongozi wa ACT halingani kihadhi na Katibu Mkuu.

Hoja za kijana wa ACT zingeweza kujibiwa na kiongozi wa UVCCM anayeuelewa vizuri msimamo wa serikali au raia huru yeyote anayeweza kutoa hoja kinzani.

Kwa meneno mengine, pengine kwa uwazi zaidi, katika mjadala husika, wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wana hoja dhaifu mno zisizohitaji kujibiwa na Katibu Mkuu.

Hata kama tungejitahidi kudunisha nafasi ya Katibu Mkuu, hatuwezi kuondoa ukweli kwamba hiyo ni nafasi nyeti na muhimu serikalini.
 
Nondo anafata bosi wake Zitto anachotaka waseme, na hii point wanakomaa nayo kwa sababu ndicho wazungu wanataka kusikia.

Otherwise, ukishapata mimba hutakiwi kurudi kwenye mfumo ule wa mwanzo.
Hadi mkopo chuo kikuu unakosa sifa za kuapply?Tuweni serious!
Halafu kuna shida gani hao watoto wakijifungua kurudi kwenye mfumo rasmi?Mbona Kenya na Uganda wanawaruhusu?Twende huko tukapate uzoefu isiwe tunaendeshwa kwa hisia za mtu mmoja maana hili suala ni la JPM peke yake!CCM ilitunga sera 2015 na ikasema itaendelea kuwapa fursa watoto watakaojifungua kurudi shule katika mfumo rasmi,JPM ndiye aliyetengua maamuzi hayo ya think tank ya utangaji sera ya CCM!
 
johnthebaptist, Huyu Nondo ni mweupe kichwani, kwanza aliwahi kuona bodi ya mikopo inabagua kutoa mikopo kwa kigezo hicho, kimsingi bodi ya mikopo inakooesha Mtanzania yeyote vigezo vidogo ni kwa sababu ya kiwango kidogo cha pesa iliyopo.

Kingine anaposema warudi shule baada ya kujifungua pia afikirie hao si watoto pekee ata hao waliozaliwa na hao wazaziwatoto ni watoto na wanahizaji matunzo nani atawajibika nao?

Mimba nyingi za utotoni ni maisha duni na ukosefu wa elimu ya uzazi kwa watoto wetu, watoto wanaozaa mara nyingi huingia katika majukumu ya kuwalea watoto wao sasa hayo majukumu watayawezea wapi?

Huyu Nondo atakuwa kashikwa na kutu hafikirii ubishi wa watu wa kigoma poor him.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu anzisha mada hapa watu watoe ushuhuda walivyopatiwa mimba wakiwa shuleni na baadaye wakapambana na kupata fursa ya kurejea shuleni na leo ni watu wakubwa tu!Hilo la kulea ni jukumu lao na ndugu zao,watajua namna ya kufanya,cha msingi wapewe fursa ya kurudi shule katika mfumo rasmi!
Twendeni Kenya na Uganda tukapate uzoefu,wao wanawaruhusu watoto waliojifungua kurudi shule!Niliona siku moja kwenye Tv mtoto akihojiwa ambaye alikuwa amerejea shuleni huko Kenya!Nikasema kumbe inawezekana kabisa,tena wengi wao wanakuwa na juhudi na masomo maana wanakuwa wanajua makosa waliyoyafanya!
Nisema wazi tu,nje ya mfumo rasmi wengi wao huwa hawafanikiwi,yaani huko ni kama dumping area!
Timu ya utungaji sera ya CCM 2015 iliona umuhimu wa kuendelea kuwapa fursa watoto hawa kurudi shule na ikawekwa kwenye ilani,lakini ni maamuzi tu ya JPM binafsi kuwa yeye hawezi kusomesha watoto waliojifungua,anasema hayo utafikiri pesa ni yake na sio kodi za watanzania!
 
Kuna mambo ambayo lazima kama jamii yenye upekee wake tuyasimamie hata kwamba tunatofautiana kiitikadi.

Moja ya jambo hili ni mimba kwa wanafunzi. Siafiki mwanafunzi apate Ujauzito kurudi katika mfumo rasmi wa elimu kama wenzake ambao hawajapata.

Hapa tutahalalisha umama, baba na hata ushemeji katika shule/darasa na ile dhana ya uanafunzi kufa kifo cha kawaida.

Kila kitu kinautaratibu wake. Tutambue pia kuwa shule ni ni chombo ambacho jamii inawatengeneza wanajamii wa baadae katika kuiendeleza jamii husika kwa siku za usoni. Na kwamba, ni unapokuwa shuleni basi uzingatie ile miiko ambayo jamii imeona haipaswi kuvunja na watoto wake ndio maana wakapelekwa shule.

Sasa kama huyu aliyepelekwa shule ameona hawezi kufata misingi hiyo ya jamii ya nini kumuendeleza katika jambo ambalo hakulizingatia?


Shule zibaki kuwa shule na taratibu, sheria, utamaduni na majuzi zake zisimamiwe. Ikiwa ikatokea mwanafunzi akapata Ujauzito basi, apelekwe katika mfumo mbadala usio rasmi na ule aliokengeuka ili shule na malengo ya shule katika jamii yabaki kama ambavyo jamii inapenda iwe.


Sio kila atakalo mfadhili ni jambo jema ktk mfadhiliwa.
1.Hili jambo kwanza hakuanza kutaka mfadhili,CCM think tank yao kwa maana ya watunga sera walilijumuisha kwenye ilani yao 2015!Mabadiliko yaliyotokea ni matakwa binafsi ya JPM na sio timu ya CCM na serikali kwa ujumla!
2.Tumepima madhara kama wakirejea?Au tunaendeshwa na hisia binafsi kutokana na kwamba JPM kasema?Kwanini hatujaenda kufanya utafiti Kenya na Uganda ambao wamewaruhusu watoto watakaojifungua kirudi shule?
3.Vipi kwa mtu aliyempa mimba?Je,kama ni mwanafunzi mwenzake,naye kwakuwa anakuwa baba basi naye kikombe kimuhusu na afukuzwe shule?Au mzigo huu tunambebesha mtoto wa kike?
4.Mfumo usio rasmi ni mfumo wa kupunguza ujinga tu,ni kama dumping area,asilimia kubwa huwa wanafeli na hawaendelei na elimu za juu!Nenda vyuoni ukafanye utafiti ni wangapi wametoka nje ya mfumo rasmi!
5.Je,ni kweli wasiokuwa ndani ya mfumo rasmi hata wakifanikiwa,vigezo na masharti ya mkopo chuo kikuu inawaengua kuwa wanufaika?

Ungejiuliza maswali yake na kupata majibu,pengine ungekuwa na mtizamo tofauti!
Nchi kwa sasa tunakosa mijadala kutokana na siasa zilizogubikwa na UCCM na Upinzani!Nyeusi watu wataita nyeupe kisa tu iko upande wao!
 
Hadi mkopo chuo kikuu unakosa sifa za kuapply?Tuweni serious!
Halafu kuna shida gani hao watoto wakijifungua kurudi kwenye mfumo rasmi?Mbona Kenya na Uganda wanawaruhusu?Twende huko tukapate uzoefu isiwe tunaendeshwa kwa hisia za mtu mmoja maana hili suala ni la JPM peke yake!CCM ilitunga sera 2015 na ikasema itaendelea kuwapa fursa watoto watakaojifungua kurudi shule katika mfumo rasmi,JPM ndiye aliyetengua maamuzi hayo ya think tank ya utangaji sera ya CCM!

Kabla ya JPM utaratibu ulikuwaje?
 
Kabla ya JPM utaratibu ulikuwaje?
Kuna dada alipata ujauzito nikiwa darsa la 4 yeye la 6 enzi za mkapa,nilishangaa kukutana naye chuo tukiwa kozi moja pale CoET!Nikamuuliza ilikuwaje maana baada ya kupata ujauzito sikumuona tena mpaka hapo tulipoonana!Alinieleza alilazimika kukatisha masomo na kwenda kujifungua,akakaa nyumbani na baadaye akajiunga na shule nyingine akamaliza la 7 na kufaulu,alichaguliwa kwenda kidato cha kwanza na akaendelea na masomo mpaka hapo tulipokutana!Leo hii ni Engineer na yuko huko serikalini na tunawasiliana mara moja moja!Nawaza tu asingepata fursa kwenye mfumo rasmi,angeweza kufika huko?Achilia mbali 100% mkopo aliopata chuo kipindi cha JK maana CoET wote tulipata 100%!
Nikiona mjadala huu huwa namkumbuka rafiki yangu huyo na nashindwa kuwa mnafiki bali kusimama kwenye ukweli!
 
Kiitifaki, huyo bwana mdogo alitakiwa akutanishwe na Mwenyekiti wa UVCCM; Katibu Mkuu ni nafasi kubwa katika Utumishi wa Umma. Waandaji wa kipindi hawajatenda haki kwa Katibu Mkuu.

Katika mjadala huu, baadhi ya wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wanakusudia kuhujumu elimu yetu na taifa kwa ujumla kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Katika hili, msimamo wa serikali uungwe mkono.
Elimu yetu inahujumiwaje?
 
Back
Top Bottom