Dkt. Abbas na Abdul Nondo watofautiana namna watoto wa kike wanaopata mimba shuleni watakavyoendelea na masomo

Kiitifaki, huyo bwana mdogo alitakiwa akutanishwe na Mwenyekiti wa UVCCM; Katibu Mkuu ni nafasi kubwa katika Utumishi wa Umma; waandaji wa kipindi hawajatenda haki kwa Katibu Mkuu.

Katika mjadala huu, kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, baadhi ya wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wanakusudia kuhujumu elimu yetu na maendeleo endelevu ya taifa kwa ujumla.
Katika hili, msimamo wa serikali uungwe mkono.
 
data

mkuu, una binti nyumbani kwako ?
alafu mbona hata hawa wanaosoma mfumo rasmi wanabeba sana mimba na wanazitoa, kuna jamaa yangu tulipokuwa high school demu wake alitoa mimba 3
hili swala mnabidi mtoe maamuzi like parents,


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mambo ambayo lazima kama jamii yenye upekee wake tuyasimamie hata kwamba tunatofautiana kiitikadi.

Moja ya jambo hili ni mimba kwa wanafunzi. Siafiki mwanafunzi apate Ujauzito kurudi katika mfumo rasmi wa elimu kama wenzake ambao hawajapata.

Hapa tutahalalisha umama, baba na hata ushemeji katika shule/darasa na ile dhana ya uanafunzi kufa kifo cha kawaida.

Kila kitu kinautaratibu wake. Tutambue pia kuwa shule ni ni chombo ambacho jamii inawatengeneza wanajamii wa baadae katika kuiendeleza jamii husika kwa siku za usoni. Na kwamba, ni unapokuwa shuleni basi uzingatie ile miiko ambayo jamii imeona haipaswi kuvunja na watoto wake ndio maana wakapelekwa shule.

Sasa kama huyu aliyepelekwa shule ameona hawezi kufata misingi hiyo ya jamii ya nini kumuendeleza katika jambo ambalo hakulizingatia?


Shule zibaki kuwa shule na taratibu, sheria, utamaduni na majuzi zake zisimamiwe. Ikiwa ikatokea mwanafunzi akapata Ujauzito basi, apelekwe katika mfumo mbadala usio rasmi na ule aliokengeuka ili shule na malengo ya shule katika jamii yabaki kama ambavyo jamii inapenda iwe.


Sio kila atakalo mfadhili ni jambo jema ktk mfadhiliwa.
Sasa ukiona mtu kama Sarungi na Fatuma Karume wanavyojishaua na wengine kule twitter huwa nashangaa sana!

Alafu mtu kama Zitto tulifikiri msomi atoe mawazo chanya kwa jamii lakini lenyewe lipo tu kutetea ujinga halina tofauti kabisa na ccm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wote wanasimamia misimamo ya maboss zao, suala la hizo pesa ni la kimkataba na sio zawadi Tz tumekubali masharti you tuliyopewa na WB kuhusiana na wanafunzi wenye mimba kurudi kusoma ktk mfumo rasmi au usio rasmi, kinachosema kwenye mkataba ndicho kitafuatwa na sio maneno ya Hawa wanaosifu mabwana zao bila kuangalia uhalisia was mkataba.
 
Hao wote wanasimamia misimamo ya maboss zao, suala la hizo pesa ni la kimkataba na sio zawadi Tz tumekubali masharti you tuliyopewa na WB kuhusiana na wanafunzi wenye mimba kurudi kusoma ktk mfumo rasmi au usio rasmi, kinachosema kwenye mkataba ndicho kitafuatwa na sio maneno ya Hawa wanaosifu mabwana zao bila kuangalia uhalisia was mkataba.
Duh......!
 
mkuu, una binti nyumbani kwako ?
alafu mbona hata hawa wanaosoma mfumo rasmi wanabeba sana mimba na wanazitoa, kuna jamaa yangu tulipokuwa high school demu wake alitoa mimba 3
hili swala mnabidi mtoe maamuzi like parents,


Sent using Jamii Forums mobile app
Akalee mtoto... Mtoto akikua naye atakua amekua.. Atachagua mfumo atao ona unafaa akajiendeleze. Ipo mingi...
 
Dogo kinachombeba ni upande aliopo wala si hoja zake
Dr Abbas ambaye ni msemaji mkuu wa serikali anasema wanafunzi wanaopata mimba shuleni hawatarudi kuendelea na masomo katika mfumo rasmi bali wataruhusiwa kupitia mfumo usio rasmi yaani private candidates.

Abdul Nondo boss wa vijana pale ACT wazalendo anapinga vikali yeye anataka wanafunzi hawa baada ya kujifungua warudi katika mfumo rasmi wa masome ili wawe na sifa ya kukopesheka na Bodi ya mikopo watakapochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu.

Mjadala ni mkali kweli kweli ndani ya kipindi cha Tuongee asubuhi. Star tv.

Nani yuko sahihi?

Maendeleo hayana vyama!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu tunaongea kana kwamba Watoto wa kike ni jamii kutoka sayari nyingine.

Hizo mimba wanapewa na kina nani?

Kwa nini mnataka wakishapata mimba waingizwe kwenye kundi tofauti kabisa na jamii? kana kwamba wameshatoka kwenye ubinaadamu wa kawaida na sasa wao hawafai tena.

Ningetamani sana nao wabaki na heshima ile ile hata baada ya kupata mimba na kujifungua. Kama tuliwaheshimu awali sioni kwa nini tuwapotezee heshima hiyo baada ya kuzaa.

Kwa upande mmoja tutajifanya ni jamii yenye kumuheshimu Mwanamke na upande mwingine tunamnyanyapaa Mwanamke huyo huyo kwa kisingizio cha kuzaa mapema, ili hali aliyempa mimba ni huyo huyo Mwanaume.

Hizi vita na mabavu yetu dhidi ya Mabinti hawa Wadogo, ni bora tungeelekeza kwenye kuhakikisha Wanaume Mabazazi hawawapi Mabinti hawa hizo mimba.

Tuheshimu Wanawake na tuheshimu karama yao ya uzazi...Mama ni Mama hata kama alikuzaa akiwa anasoma, tena wapo wanaoongea hovyo ili hali nao wamezaliwa na Mama aliyekuwa bado anasoma.
 
Kiitifaki, huyo bwana mdogo alitakiwa akutanishwe na Mwenyekiti wa UVCCM; Katibu Mkuu ni nafasi kubwa katika Utumishi wa Umma. Waandaji wa kipindi hawajatenda haki kwa Katibu Mkuu.

Katika mjadala huu, baadhi ya wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wanakusudia kuhujumu elimu yetu na taifa kwa ujumla kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Katika hili, msimamo wa serikali uungwe mkono.
Kweli kabisa maana dogo kapwaya sana, alikuwa anaongea kama amekaririshwa maneno na ZZK. Alikua anag'ag'ana tu ubaguzi ubaguzi. Haangalii hata hoja ya msingi kama mwanafunzi anatakiwa asome katika mazingira ya saikolojia nzuri,sio mazingira yanayompa fikra kuwa ngono na mimba ni jambo la kawaida.
 
Kweli kabisa maana dogo kapwaya sana, alikuwa anaongea kama amekaririshwa maneno na ZZK. Alikua anag'ag'ana tu ubaguzi ubaguzi. Haangalii hata hoja ya msingi kama mwanafunzi anatakiwa asome katika mazingira ya saikolojia nzuri,sio mazingira yanayompa fikra kuwa ngono na mimba ni jambo la kawaida.
Hizo nafasi tu, hata Waitara ni N/waziri lakini huwezi mweka meza Mona na Nondo kihoja.
 
Watoto wa kike hawatakiw kusamehewa hata kidogo wanafanya makusudi
Wewe ni mojawao?Umefahamuje ni makusudi wanafanya?Huwa wanabebeshwa mimba kama ndoo ya Maji?Hukumu ya wanaowapa ujauzito nayo iwe kuhasiwa,maana hiyo ndiyo angalau italingana na hukumu Kali ya kifungo cha ujinga kwa maisha yao yote.
Tuwe fair,tutafute namna ya kuwahakikishia wasichana hawapati ujauzito,wanaowabebeaha ujauzito wapewe adhabu itakayotoa funzo kwa wanaotarajia kujihusisha na wanafunzi kingono(wabakaji) badala ya kuwahukumu wahanga.
 
Bodi ya mikopo Kama umesoma private o level mkopo utausikia kwa jirani
johnthebaptist, Huyu Nondo ni mweupe kichwani, kwanza aliwahi kuona bodi ya mikopo inabagua kutoa mikopo kwa kigezo hicho, kimsingi bodi ya mikopo inakooesha Mtanzania yeyote vigezo vidogo ni kwa sababu ya kiwango kidogo cha pesa iliyopo.

Kingine anaposema warudi shule baada ya kujifungua pia afikirie hao si watoto pekee ata hao waliozaliwa na hao wazaziwatoto ni watoto na wanahizaji matunzo nani atawajibika nao?

Mimba nyingi za utotoni ni maisha duni na ukosefu wa elimu ya uzazi kwa watoto wetu, watoto wanaozaa mara nyingi huingia katika majukumu ya kuwalea watoto wao sasa hayo majukumu watayawezea wapi?

Huyu Nondo atakuwa kashikwa na kutu hafikirii ubishi wa watu wa kigoma poor him.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom