Dk Kitila Mkumbo: Vijana wa BAVICHA wanahitaji kufundwa!

Ni jambo la kawaida kabisa na endelevu, yaani kuwafunda vijana. hakuna jipya hapo. Watakaa sawa hatuhitaji msaada wa CCM.
 
Kivipi nawachochea? Najikosha kwa nani? Unaweza kufafanua kidogo ueleweke?

Hayo ya kuwachochea vijana nawaachia wenyewe ila kuhusu Shibuda napingana na wewe Mkumbo, Shibuda anatakiwa apondwe kichwa, kila kauli yake ya kipumbavu ijibiwe na chama kwa ukali ili umma ujue kuwa hatakiwi hata kwenye chama
 
Mkumbo umekimbilia wapi? njoo ujibu hoja za watu hapa, vinginevyo tuamini kwamba wewe, Shibuda na Juliana lenu moja na ndiyo mnaoua CHADEMA. Ni katika mazingira gani unamweka Heche na Juliana katika kundi moja kwa haya yaliyotokea? acha kujificha na uje utuambie ni kwanini huyu Juliana wako anamshambulia Heche? Je katiba ya BAVICHA inampa mamlaka ya kuwa msemaji wa BAVICHA yeye Juliana?

Mkumbo nilikuwa nakuheshimu sana lkn sasa naanza kupata wasiwasi na ueledi wako ndani ya Chadema. Haiwezekani ukaweka kosa alilofanya Heche na Juliana kwenye kapu moja. Pia huwezi kukimbia hoja ya kuongelea kauli ya Shibuda kwamba HAKUNA CHAMA CHA UPINZANI KILICHOKOMAA NA KUWEZA KUKABIDHIWA DOLA, NA HAYO ANAYATAMKA KWENYE NEC YA CCM

Mkumbo naomba majibu otherwise nitaanza kuamini kwamba hata UDSM walipokunyima Udean majuzi kumbe walikuwa sahihi japo ulishatumika kama Head wa idara.

Mkumbo na yeye anaweza kuwa pandikizi. Eti anashauri kauli za Shibuda zidharauliwe, utazidharauje wakati kijijini Msoga, Kwanjeka, Mchambawima, Mchambia wembe na Mdaula wao hawajamdharau?
 
Yani unataka watu waache mambo ya msingi wamjadili Shibuda??
Kweli??
Who is shibuda katika politics za mageuzi??
He is nothing, he does not deserve the publicity he is even getting.

BAVICHA walichemka kutoa tamko, na huyo makamu nae kachemka. Wote ni vichwa maji tu.
The tamko wa unnecessary in all counts.

Mkuu unajua jinsi pumba za shibuda zinavyopewa kavereji? Umati anaoupollute mtaurudisha kwenye mstari kwa kumpuuza shibuda? unacheza wewe......
 
Yani unataka watu waache mambo ya msingi wamjadili Shibuda??
Kweli??
Who is shibuda katika politics za mageuzi??
He is nothing, he does not deserve the publicity he is even getting.

BAVICHA walichemka kutoa tamko, na huyo makamu nae kachemka. Wote ni vichwa maji tu.
The tamko wa unnecessary in all counts.

Mwili hauwezi kuwa na kidonda kidogo kikapuuzwa. A kingdom was lost because one soldier did not tie his shoelaces tight enough.

Waswahili wanakwambia usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Shibuda anaanzisha ufa, ufa huu unatakiwa kuzibwa haraka. Ukisema "mpuuzeni tu" ufa utakua na kuangusha ukuta mzima, kufikia hata kusababisha nyumba kubomoka.
 
dk mkumbo ukitaka kusema ukweli sema ukweli wote,
hapa tulipofika haturudi nyuma kama chadema wacpoweza bac tutach6nga hata sanamu lakini si ccm
 
Kivipi nawachochea? Najikosha kwa nani? Unaweza kufafanua kidogo ueleweke?
Kitila Mkumbo, mbona unaniacha hoi? Naomba ukumbuke ule usemi kuwa mdharau mwiba, mguu huota tende!

Kwanza, Heche ni mwenyekiti na kikatiba ndiye msemaji mkuu wa BAVICHA tofauti kabisa na Juliana ambaye ni msaidizi tu, mamlaka ya kuwaita waandishi wa habari anayatoa wapi Juliana?

Pili, ikiwa ni kweli Shibuda, Mbunge wa Maswa kupitia Chadema ni mtu wa kupuuzwa tu na kudharauliwa, aliwezaje kuaminiwa hadi kupitishwa na Chadema kuwa mgombea Ubunge 2010?

Tatu, Shibuda ni mjumbe wa Umoja wa Taasisi za Afrika inayoshughulikia utawala bora kanda ya Afrika Mashariki, je tamko lake la kuponda Upinzani hapa Tanzania, kweli halina madhara kwa Chadema?

Nne, Baraza la Vijana wa Chadema litawezaje kukaa kimya kama moja wa Wabunge wake hata akiwa kichaa anadiriki kukidhalilisha hadharani na mbele ya mahasimu wao wakuu, Chama cha Mafisadi?

Tano, je operation vua gamba vaa gwanda litachukuliwaje na wananchi ambao wameanza kuamka na kuweka tumaini lao kwa Chadema kama Shibuda anaruhusiwa kukikejeli anavyopenda bila karipio?

Sita, Chadema inategemea nini mwaka 2015 kama mmoja wa wabunge wake unataka wanachi wamwone kama chizi, je wapiga kura watashawishiwa vipi kukipa uongozi chama kinacholea machizi?

Saba, ni hasara gani Chadema inapata kutokana na tamko lililotolewa na msemaji mkuu wa Bavicha na je, kwa mtu kama Wasira kuchangamkia hiyo hali Chadema haistuki kwamba labda upo moshi unafukuta?

Nane, Kitila Mkumbo, kwa nini wewe nawe umeamua kutoa tamko kama ni kweli Shibuda ni wa kupuuzwa na kwa nini kifanyike kikao rasmi cha BAVICHA kulitolea tamko kama anavyodai Juliana, who is she?

Mwisho, naamini hili jambo halikutaji kikao rasmi na alichofanya Heche ni sahihi kabisa kwani ni wajibu wa vijana kuhakikisha heshima ya chama inalindwa na kama Mwenyekiti hili liko ndani ya uwezo wake.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani lipo jambo la kutomtendea haki Heche
1. Heche alitoa kauli ikiwemo ile ya mpinzani kukiri mbele ya chama pinzani kuwa upinzani hauwezi kushika dola.
Inapotokea mnachukua kauli moja na kuifanya kama mada mkijua yapo mengine aliyosema si kumtendea haki

2. Heche hana tatizo ndani ya BAVICHA. Alitoa msimamo kwa minajili ya chama. Kama alikosea basi 'ahukumiwe' kwa kusimamia na kukitetea chama. Kumuweka katika ulingo mmoja na makamu wake ni kumdhalilisha

3. Heche hajatoa kauli dhidi ya Shonza, kwahiyo hakuna mgogoro kati ya Heche na Juliana bali upo mgogoro wa Juliana dhidi ya Heche. Na si sahihi kumhusisha Heche kwa kauli za Shonza

4. Kuwafunda vijana si kuongea nao. Hawa waliweza kuomba kura na kujaribiwa kuwa wanaweza kutoa kauli zinazolingana na hadhi zao. Kuwafunda ilikuwa Kumtaka Makamu aombe radhi au awajibike na ikishindikana afukuzwe. Huko ndiko kuwafunda haswa kwa vitendo na si kauli.

Kuna njia nyingi sana zinatumika kumlinda Makamu mwenyekiti kwa mwamvuli wa Heche. Nabaki na hoja yangu kuwa kumlinda makamu mwenyekiti ambaye taarifa yake inaonekana kuwa kama dira ya mgogoro ni kulinda uzembe kama ule wa CCM na kundi la wahalifu. Ile dhana kuwa lipo kundi nyuma yake, sasa inaanza kubadili fikra hata kama ilikuwa ya uongo.

Kwanza ni lazima Makamu afundwe kwa kuwajibika. Halafu vijana wafundwe ili baleghe zisiwasumbue siku za usoni.
Hili la Makamu Juliana siyo baleghe ni ukorofi na ukorofi si sehemu ya baleghe.

Nitabaki na msimamo wa Juliana kuwajibika na kama CDM hawatamchukulia hatua watakuwa wamepoteza 'legitimacy' ya kukemea uwajibikaji
 
Dr naona ume base kwenye upande mmoja wa BAVICHA,may take ni kwamba mbona hujatolea maeleza ya huyu zuzu ambaye anazeeka vibaya?
 
Kwenye mambo muhimu na kazi muhimu sio vyema kupuuza. Chadema kumpuuza Shibuda ni kuumiza chama au kukubaliana na Wasira. Chadema ijue ni chama cha siasa sio dini. Shibuda anafanya kila awezalo kuiua Chadema. Kwa yeyote mwenye mapenzi ya ukweli na chama anafikia wakati haelewi kama chama kinaudhibiti madhubuti wa maadili, utendaji na uwajibikaji wa kauli, vitendo wa viongozi wake wa kuchaguliwa, kuteuliwa na kusimikwa.

Shibuda sio wa kupuuzwa hata kidogo, lazima ashughulikiwe kuliko kusubiri anavyoshughulikia Chama. Shibuda analeta makundi, anapoteza muda wa watu wengi, anakibomoa chama kwa kauli zake za ajabu.

Kama tunamlaumu JK kwa kuogopa kuchukua maamuzi magumu je sisi nasi sio tunakwenda huko huko kudharau mambo muhimu badala ya kuyatolea maamuzi magumu.

Kwa BAVICHA Hakuna mtoto pale, wenzetu wakiwa na miaka 18 wanapewa majukumu makubwa na wakishindwa hakuna anayesema eti wafundwe, unapewa kazi ikijulikana unaweza kama hawajajifunza uongonzi watolewe hakuna muda wa kufunda mtu kwenye mambo muhimu. Tanzania ya leo ina vijana wengi sana na wasomi wazuri wenye hekima, busara, ujuzi na uelewa wa kutosha sana. hakuna muda wa kuendekeza makosa ya reja reja tena ya kutumwa eti upate huruma ya chama. Shibuda na kundi lake lazima watoswe bila kigugumizi wal kusita. kama tunaogopa hasara ya jimbo tunalea hasara kubwa.

Kauli moja ya kipuuzi aliyoitoa General wa Obama akiwa Afghanistani iliambatana na yeye kukosa kazi bila kusubiri muda. Huwezi kuwa kwenye mkamkati na ulionao wanapingana na mkakati husika lazima uwatose uweze kusonga mbele. Watoswe wote wanaegemea na Shibuda halafu majeshi yasonge mbele. Chadema ni zaidi ya Shibuda. Makamu mwenyekiti wa BAVICHA ni pandikizi na mkililea litaiboama chama-Wasira at work.

Chief Mkwawa
Hatuwezi kuendelea kwa kuleana ujinga
 
Huu uongozi wa kupuuza puuza mambo si ndio huu huu tunaukataa kwa CCM?

Si ndiyo habari za Kikwete kusema "huu upepo tu, utapita" alipoambiwa kubadili mawaziri?

Sasa kama viongozi wasomi wenyewe wa CHADEMA ndio hawa kina Kitila Mkumbo wanakuja hapa macho makavu kabisa, wanaandika habari ndeeefu, tupuuze mambo yanayoonyesha muelekeo wa chama waziwazi, mtu mmoja analeta cancer katika chama halafu anaachiwa, tunaambiwa "tumpuuze", wananchi tunatakiwa tupate picha gani hapa?

Kwamba tunatakiwa kuwatoa wapuuzaji wa chama kimoja (CCM) na kuwaweka wapuuzaji wa chama kingine (CHADEMA) ?

Kama habari zenyewe ndiyo hizi hizi za kupuuza mambo muhimu, tofauti kati ya CCM na CHADEMA ipo wapi sasa?

Hawa wanasema "huu ni upepo tu, utapita", hawa wengine wanatuambia "puuzeni tu".

Wote naona falsafa yao moja, kufunika vichwa chini ya mchanga kama mbuni anayefukuzwa ambaye hataki kukubali ukweli, anataka kuishi katika dunia ya kufikirika ambayo watu hawatatui matatizo yao, wanayapuuuza tu.

Ndio uongozi mbadala huu? Unaolea cancer katika chama na kutuambia tuipuuze tu?
 
Gazeti la Rai Mwema | Jumatano, 24 Mei 2012


Malumbano baina ya Mwenyekiti wa BAVICHA na Makamu wake katika vyombo vya habari ni hatua ya kubalehe kisiasa, ambayo haipaswi kuwakatisha tamaa wapenzi wa mageuzi nchini. Bahati mbaya kubalehe huku kunaambatana na usumbufu na kero. Usumbufu na kero hizi zingekuwa za maana kama vijana hawa wangekuwa wanalumbana juu ya jambo la msingi la kifalsafa au kisera au kikanuni ndani ya chama na nchi. Bahati mbaya kwamba vijana hawa wanalumbana kwa jambo la kipuuzi. Ni upuuzi kulumbana juu ya kauli rejareja za Mbunge wa Maswa John Shibuda, mwanasiasa ambaye mbwembwe zake za kisiasa zinajulikana hata kabla hajahamia CHADEMA.

Kwamba Shibuda ametangaza kugombea urais ndani ya kikao cha CCM haiwezi kuwa tatizo kwa sababu kimsingi kufanya hivyo hakuvunji kanuni yeyote ndani ya CHADEMA kwa sababu hakuna kanuni yeyote inayoelekeza muda na mahali mwafaka pa kutangaza nia ya kugombea urais. Mwanachama anapaswa kuongozwa na busara zake tu juu ya muda na mahali pa kutangaza nia yake. Sasa kama mwanachama wa CHADEMA hana busara kiasi cha kutangaza nia ya kugombea urais ndani ya kikao cha ‘mpinzani’ wake CCM, na kama busara za mwanachama huyo ni finyu kiasi cha kumuomba mwenyekiti wa CCM ndiye awe meneja wa kampeni zake, kwa nini iwe tatizo kwa BAVICHA au CHADEMA?

Hivyo, haikutarajiwa kwamba kuna mtu mwenye akili sawasawa ndani ya CHADEMA angemjibu Shibuda pale alipotamka, ndani ya kikao cha CCM, kwamba angegombea urais kupitia CHADEMA mwaka 2015. Kauli ya Shibuda haikustahili kupewa umakini wowote hasa kwa kitendo chake cha kusema kwamba Rais Kikwete ndiye angekuwa meneja wake wa Kampeni. Hili peke yake lilitosha kuonyesha kwamba kauli za Shibuda ni mwendelezo wa mbwembwe zake kisiasa zisizostahili kupewa uzito wowote ule. Hivyo, kwa Mwenyekiti wa BAVICHA kutoa tamko kali juu ya Shibuda ilikuwa sawa na mtu mwenye akili timamu kujaribu kumkimbiza kichaa aliyekimbia na nguo zake. Ni vizuri wanasiasa vijana wakaielewa kwa upana wake dhana ya uhuru wa maoni. Uhuru wa maoni ni pamoja na kukubali kusikia yale usiyoyapenda na kuyataka.

Katika kujitutumua kisiasa, Makamu wa BAVICHA naye anatoa tamko la kumkana ‘bosi’ wake, tena hadharani na nje ya viwanja vya chama. Madai ya makamu huyu wa BAVICHA ni kwamba hakuna kikao kilichoidhinisha tamko la Mwenyekiti wa BAVICHA kusema hayo aliyoyasema. Haya, na yeye tunamuuliza kikao gani cha BAVICHA kiliidhinisha yeye kumpinga mwenyekiti wake hadharani mbele ya waandishi wa habari? Je, makamu wa BAVICHA aliona ugumu gani kwenda kumshtaki mwenyekiti wake kwenye vikao vya BAVICHA na/au CHADEMA?

Nafikiri vijana hawa wa BAVICHA wanahitaji kufundwa. Nawashauri viongozi wa CHADEMA kuchukua hatua muhimu za kuwafunda vijana wa BAVICHA ili ubalehe wao wa kisiasa upite bila madhara kwa chama. Kufundwa huko ni pamoja na kuwafundisha namna ya kufanya kazi na vyombo vya habari. Wanahitaji kuhariri matamko yao sawasawa, na kabla ya kuyatoa wapime athari za matamko yao kwa chama. Ukiona wewe ni kiongozi wa CHADEMA unatoa tamko na tamko hilo linapamba vichwa vya habari vya magazeti pinzani kwa chama chako kama vile Uhuru, ujue tamko lako limekiumiza chama.


Laiti viongozi wa BAVICHA wangekuwa makini wangejizuia kutoa matamko yao. Mwenyekiti wa BAVICHA angekuwa makini angetafakari maana ya kauli yake kabla hajaitoa, na angedundua kwamba tafsiri pana ya kauli yake ni kutaka kuzuia baadhi ya wanachama wa CHADEMA kugombea urais. Naye makamu wake angekuwa makini angetambua kwamba kumpinga mwenyekiti wake hadharani ni kutangaza mgogoro ndani ya chama, na ilikuwa ni kucheza mikononi mwa wapinzani wa CHADEMA. Viongozi hawa wanapaswa kutambua kwamba katika mawasiliano muhimu siyo unachosema, bali kile ambacho hadhira inasikia. Kwenye tamko la Mwenyekiti wa BAVICHA hadhira walisikia kwamba baadhi ya wanachama wa CHADEMA hawaruhusiwi kutangaza kugombea urais, na walichosikia hadhira ya makamu wake ni kwamba kuna mgogoro ndani ya CHADEMA! Je, huu ndio ujumbe ambao viongozi hawa walitarajia kuufikisha?

Msimamo wa CHADEMA dhidi ya kauli za Shibuda umekuwa ni ‘kumdharau’ kwani, pamoja na kwamba zinasababisha usumbufu, kauli zake zimekuwa hazina madhara ya msingi kisiasa kwa chama. Hata hivyo kauli za Shibuda iliyoripotiwa katika moja ya magazeti ya Jumapili ni zaidi ya usumbufu. Kwamba viongozi wa CHADEMA wanamchukia Shibuda kwa sababu ni msukuma ni kukigombanisha chama na wapiga kura wa kanda ya ziwa. Huu sasa sio usumbufu tena bali ni uharibifu. Usumbufu unavumilika, lakini uharibifu hauwezi kuvumilika. Ni wazi kuwa Shibuda amepania kuiharibu CHADEMA. Kwa hivyo kuna haja ya kuangalia upya sera ya kumdharau Shibuda.

Tukumbuke kwamba mambo yote haya yanatokea kipindi ambacho Waziri mwandamizi katika serikali ya CCM ameapa kuona CHADEMA inasambaratika ndani ya mwaka mmoja. Vijana wa BAVICHA yawapasa kuwa makini, vinginevyo wataonekana wapo katika mkakati wa kuisambaratisha CHADEMA. Tumewaonya!


Dk Kitila Mkumbo ni Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Nawashauri Vijana wa CHADEMA waachane na Shibuda. HAENDI POPOTE NOT COMMENT ANYTHING ANACHOONGEA NDIVYO ALVYO. NA HAENDI MAHALI POPOTE . NINAAMINI HAWEZI KUGUSA NUCLEUS YA CHADEMA. NA KAMA JIMBONI HAFANYI CHOCHOTE TUTAMTOA TU ASITUTISHE CHOCHOTE. TUNAMJUA IN AND OUT NI DEBE TUPU!
 
Dr Mkumbo.
Umeongea sawa kabisa hasa uliposema Shibuda kasema kampeni meneja atakuwa Kikwete, kwa mtu mwenye akili ya kawaida atatabua kwamba shibuda alikuwa anatania ama anatia mbwembwe zake za kawaida.

Lakini kwa mtu mwenye akili zilizo kwenda shule, kama ni mwana -CCM basi atachukia sana na kumshambulia Shibuda na kama ni CHADEMA basi atafurahi sana kwa sababu shibuda alikuwa anamwabia RAIS KIKWETE kuwa:
Mh Rais chama chako kinakufa na wewe si siku nyingi utakihama chama na kuingia CHADEMA, maana kimsingi hawezi kuwa kampeni meneja wake wakati JK akiwa ccm.

Na kuhusu kusema wanamchukia wala mie binfasi sioni usubufu na kukera, unafiki kwa kiongozi yoyote ni sumu, FULL STOP. Kama unaona unachukiwa kwanini useme ninapendwa?
 
Mkumbo,
ulijitokeza mwanzoni ulivyogundua kwamba makala yako haijajibu hoja za msingi za Juliana Shonza (mwanafunzi wako) na shwaiba wako SHIBUDA umeamua kukimbia jukwaa, kwani makala yako ililenga kumsafisha msaliti Juliana na Shibuda na kutaka kuonyesha kwamba Heche naye amekivua nguo CHADEMA kama walivyofanya Juliana na Shibuda kitu ambacho hakuna mtu mwenye uelewa anayeweza kukubaliana na wewe katika hilo, kwani HECHE hakufanya kosa sawa na Juliana.
 
Mkumbo,
ulijitokeza mwanzoni ulivyogundua kwamba makala yako haijajibu hoja za msingi za Juliana Shonza (mwanafunzi wako), kwani makala yako ililenga kumsafisha msaliti Juliana na Shibuda na kutaka kuonyesha kwamba Heche naye amekivua nguo CHADEMA kama walivyofanya Juliana na Shibuda kitu ambacho hakuna mtu mwenye uelewa anayeweza kukubaliana na wewe katika hilo, kwani HECHE hakufanya kosa sawa na Juliana.
Ndiyo maana nasisitiza kuwa huyu Juliana Shonza ana nguvu za kipekee ndani ya BAVICHA na Chadema

Jitihada za kumsafisha zimeanza hapa jamvini.
Tumeona watu wakisema huyu ni mtoto aachwe ajifunze. Hakuna mahali Juliana aligombea nafasi kwa kutumia wajihi, umri, jinsia au imani. Yeye ni Makamu mwenyekiti wa BAVICHA.

Tumeona watu wakijiunga au kutumia ID nyingine ili kumsafisha kwa kutudanganya na habari aliyopeleka kwa wanahabari
Tumemsikia Mwenyekiti Mbowe akisema huu ni mgogoro mdogo tu hata kama ni ukweli usiohitaji fikra kujua kuwa huu ni mgogoro mzito sana na unaelekea kukivuruga chama wakati huu au muda mfupi ujao
Tunaona sasa makala ambazo zinajaribu kumuita Juliana ni kijana anaye'balehe' na anahitaji kufundwa

Kinachosikitisha sana ni kuona kuwa katika jitihada hizi za 'kundi' na uongozi wa Chadema kumsafisha Juliana, wamekuwa wakifumbia macho ukweli unaomtetea Heche, wamekuwa wanamweka Heche katika kapu moja na Juliana kana kwamba Heche ana ugomvi na Juliana! si kweli hii ni spinning tu! Heche hajatoa neno hata moja kumjibu Juliana.

Siku zote huwa nasiamamia penye ukweli na wala sina mrengo wa kisiasa, hata kama kufanya hivyo nitamuudhi mtu au watu.Hili la Juliana Shanzo ambaye pia anahusishwa sana na 'mahusiano' linaharibu taswira ya CDM.

Ni wiki sasa hakuna kinachopamba kurasa za magazeti au blog zaidi ya fyongo aliyoisema Juliana.
Ni wakti sasa tuseme ukweli, jitihada za kumlinda Juliana zitafanikiwa tu endapo wanaotaka kufanya hivyo wataweka wazi kwanini Juliana alindwe iwe kisiasa au kijamii. Vinginevyo tutasimamia ukweli pale CDM itakapopoteza 'moral authority and legitimacy' ya kumnyooshea kidole mwingine.
Huwezi ukajizatiti kuondoa kibanzi kwenye jicho la mwenzako huku una boriti kwenye jicho lako! never!

Juliana Shanzo amesababisha uharibifu(damage) kubwa sana na uwepo wake katika uongozi utaendelea kusababisha uharibifu iwe leo, kesho au miaka ijayo.

Juliana analindwa na uongozi wa Chadema, na uwezekano kuwa ametumwa upo! Sasa kama ametumwa, je ametumwa na nani ndani ya chama. Sina shaka kuwa Juliana kwa kutumia kivuli cha Heche analindwa kwa gharama yoyote ya chama.
Kwanini analindwa tutaendelea kufukua na kuchambua bila haya aibu au kumuonea mtu.
 
1. Vijana wa BAVICHA wanahitaji kufundwa baada ya kuharibu mambo? I expected this to be a standard procedure!

2. Wewe unayeona Shibuda ni wa kupuuzwa, wakati huohuo unahubiri kuamini nguvu ya umma! Hivi sauti yako na sauti ya maelfu ya wapiga kura wa Maswa ipi ni muhimu. Kitila unaelewa kweli maana ya nguvu ya umma au unaiimba tu kama bolingo?

3. Nimeisoma taarifa ya Julianna. Its is clear kwamba ile taarifa siyo yake binafsi. Ile taarifa imeandikwa na kikundi cha watu ambao wamempa Julianna confidence ya kuita waandishi wa habari akijua kuwa "some big guys" in CDM are behind it.

4. Kitila usikimbie mjadala. Kama uliweza kuwafuata Raia Mwema ukatoa mawazo yako "hafifu" na kama unadhani hatuyatendei haki maoni yako, njoo ufafanue. Wanasiasa wa Tanzania mmezoea sana unidirectional communication ya kuita waandishi wa habari na kutoa matamko!!! Tuna safari ndefu...
 
1. Vijana wa BAVICHA wanahitaji kufundwa baada ya kuharibu mambo? I expected this to be a standard procedure!
Nimeisoma taarifa ya Julianna. Its is clear kwamba ile taarifa siyo yake binafsi. Ile taarifa imeandikwa na kikundi cha watu ambao wamempa Julianna confidence ya kuita waandishi wa habari akijua kuwa "some big guys" in CDM are behind it.Kitila usikimbie mjadala njoo ufafanue. ...
Kwamba tunatakiwa kuwatoa wapuuzaji wa chama kimoja (CCM) na kuwaweka wapuuzaji wa chama kingine (CHADEMA),tofauti kati ya CCM na CHADEMA ipo wapi sasa?Hawa wanasema "huu ni upepo tu, utapita", hawa wengine wanatuambia "puuzeni tu".
Ndio uongozi mbadala huu? Unaolea cancer katika chama na kutuambia tuipuuze tu?
This is a missed opportunity! so sad. Tulitaraji CDM wasimame kidete na kusema, Shibuda enough is enough!, siyo kwa hoja ya kugombea urasi bali kwa hoja ya kuingiza ukabila katika chama kwa kauli yake ya 'naandamwa kwa usukuma'. Chama kinachojengewa tuhuma za namna hiyo na maadui mara ikitokea mbunge wake kuthibitisha ukabila kitatokea nini hapo.
Mara ya kwanza 'walimpuuza' sasa ametoa kauli za ukabila watampuuza, ametoa tuhuma za Dr Slaa kuwatuma vijana atapuuzwa. Atapuuzwa kama alivyopuuzwa EL, Chenge, RA n.k. Mtu anakigawa chama bado anapuuzwa.

Wakati Shibuda akipuuzwa tunaambiwa Heche anamgogoro na Juliana. Kwamba maneno ya dhalili aliyotoa Juliana si ya kupuuzwa yanahitaji kufundwa pamoja Heche.

Tumeona Mbowe akimgeuzia kibao Heche kwa kumkingia kifua Juliana Shonza. Tukasoma katika mitandao jinsi walivyomgeuzia kibao Heche. Mimi nikisoma kauli za Heche na wadhifa wake sioni alikosea wapi. Chadema haijawahi kutoa 'internal memo' ya kumpuuza Shibuda sasa Heche amekosea wapi kutetea chama.

Kwanini watu wachague sentensi moja waache zingine zenye mashiko alizosema Heche? Kwanini watu waongee na kuandika kwa mfano wa Juliana Shanzo? Huyu Juliana ana nguvu gani ndani ya chama?

Hapa ndipo CDM walitakiwa wasema, Shibuda out, Juliana step down. Halafu waendelee M4C. Wananchi wangejua naam sasa nidhamu inarudi na kiu ya maendele inaonekana.

Kwa hili CDM wamepoteza nguvu ya kusota kidole kwa CCM. Wanamlinda Juliana kama wanamvyo mlinda Chenge.
Wana Lowassa wao anaitwa Shibuda na wameshindwa kumwajibisha kwasababu zile zile.

Hii damage ni kubwa sana! Nasikitika kuona mamia ya wananchi wanaoacha shughuli zao za dola moja kwa siku wakimwagika mabara barani kwa matumaini ya ukombozi.
Wanatoa hadi rasilimali zao ili wauone ukombozi, kisha wanaangushwa na viongozi kwa kuwalinda Juliana na Shibuda.

CDM WAKE UP! read between the lines please!
 
Kitila Mkumbo, mbona unaniacha hoi? Naomba ukumbuke ule usemi kuwa mdharau mwiba, mguu huota tende!

Kwanza, Heche ni mwenyekiti na kikatiba ndiye msemaji mkuu wa BAVICHA tofauti kabisa na Juliana ambaye ni msaidizi tu, mamlaka ya kuwaita waandishi wa habari anayatoa wapi Juliana?

Pili, ikiwa ni kweli Shibuda, Mbunge wa Maswa kupitia Chadema ni mtu wa kupuuzwa tu na kudharauliwa, aliwezaje kuaminiwa hadi kupitishwa na Chadema kuwa mgombea Ubunge 2010?

Tatu, Shibuda ni mjumbe wa Umoja wa Taasisi za Afrika inayoshughulikia utawala bora kanda ya Afrika Mashariki, je tamko lake la kuponda Upinzani hapa Tanzania, kweli halina madhara kwa Chadema?

Nne, Baraza la Vijana wa Chadema litawezaje kukaa kimya kama moja wa Wabunge wake hata akiwa kichaa anadiriki kukidhalilisha hadharani na mbele ya mahasimu wao wakuu, Chama cha Mafisadi?

Tano, je operation vua gamba vaa gwanda litachukuliwaje na wananchi ambao wameanza kuamka na kuweka tumaini lao kwa Chadema kama Shibuda anaruhusiwa kukikejeli anavyopenda bila karipio?

Sita, Chadema inategemea nini mwaka 2015 kama mmoja wa wabunge wake unataka wanachi wamwone kama chizi, je wapiga kura watashawishiwa vipi kukipa uongozi chama kinacholea machizi?

Saba, ni hasara gani Chadema inapata kutokana na tamko lililotolewa na msemaji mkuu wa Bavicha na je, kwa mtu kama Wasira kuchangamkia hiyo hali Chadema haistuki kwamba labda upo moshi unafukuta?

Nane, Kitila Mkumbo, kwa nini wewe nawe umeamua kutoa tamko kama ni kweli Shibuda ni wa kupuuzwa na kwa nini kifanyike kikao rasmi cha BAVICHA kulitolea tamko kama anavyodai Juliana, who is she?

Mwisho, naamini hili jambo halikutaji kikao rasmi na alichofanya Heche ni sahihi kabisa kwani ni wajibu wa vijana kuhakikisha heshima ya chama inalindwa na kama Mwenyekiti hili liko ndani ya uwezo wake.

Nadhani kauli hii inaweza kutoa tumaini ya majibu ya baadhi ya maswali yako hasa hapo kwenye red
QUOTE=n00b;3928028]

Msimamo wa CHADEMA dhidi ya kauli za Shibuda umekuwa ni ‘kumdharau' kwani, pamoja na kwamba zinasababisha usumbufu, kauli zake zimekuwa hazina madhara ya msingi kisiasa kwa chama. Hata hivyo kauli za Shibuda iliyoripotiwa katika moja ya magazeti ya Jumapili ni zaidi ya usumbufu. Kwamba viongozi wa CHADEMA wanamchukia Shibuda kwa sababu ni msukuma ni kukigombanisha chama na wapiga kura wa kanda ya ziwa. Huu sasa sio usumbufu tena bali ni uharibifu. Usumbufu unavumilika, lakini uharibifu hauwezi kuvumilika. Ni wazi kuwa Shibuda amepania kuiharibu CHADEMA. Kwa hivyo kuna haja ya kuangalia upya sera ya kumdharau Shibuda.

Dk Kitila Mkumbo ni Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam[/QUOTE]

tumaini liko kwenye red hapo juu
Huu uongozi wa kupuuza puuza mambo si ndio huu huu tunaukataa kwa CCM?

Si ndiyo habari za Kikwete kusema "huu upepo tu, utapita" alipoambiwa kubadili mawaziri?

Sasa kama viongozi wasomi wenyewe wa CHADEMA ndio hawa kina Kitila Mkumbo wanakuja hapa macho makavu kabisa, wanaandika habari ndeeefu, tupuuze mambo yanayoonyesha muelekeo wa chama waziwazi, mtu mmoja analeta cancer katika chama halafu anaachiwa, tunaambiwa "tumpuuze", wananchi tunatakiwa tupate picha gani hapa?

Kwamba tunatakiwa kuwatoa wapuuzaji wa chama kimoja (CCM) na kuwaweka wapuuzaji wa chama kingine (CHADEMA) ?

Kama habari zenyewe ndiyo hizi hizi za kupuuza mambo muhimu, tofauti kati ya CCM na CHADEMA ipo wapi sasa?

Hawa wanasema "huu ni upepo tu, utapita", hawa wengine wanatuambia "puuzeni tu".

Wote naona falsafa yao moja, kufunika vichwa chini ya mchanga kama mbuni anayefukuzwa ambaye hataki kukubali ukweli, anataka kuishi katika dunia ya kufikirika ambayo watu hawatatui matatizo yao, wanayapuuuza tu.

Ndio uongozi mbadala huu? Unaolea cancer katika chama na kutuambia tuipuuze tu?
 
The Kitila Mkumbo niliyepata kumfahamu miaka yote ndiye huyu huyu hapa kwenye superb logical thinking and sound arguement WITHOUT PREJUDICE the least.

Hebu kamtambue huyu rafiki yangu kuwa ni mtu wa ina gani kwa kupitia japo hicho kijipande hapo chini. Hakika Mkumbo kamaliza kila kitu kwa kuniibia mawazo yangu juu ya kiji-mzozo uchwara ndani ya BAVICHA - Vijana sasa elekezeni nguvu kwenye 'Vua Gamba' na ktu msiende huko anakowatafutia Mzee Shibuda - Mzee ambaye anazeeka vibaya baba yetu huyu:


... Kwamba Shibuda ametangaza kugombea urais ndani ya kikao cha CCM haiwezi kuwa tatizo kwa sababu kimsingi kufanya hivyo hakuvunji kanuni yeyote ndani ya CHADEMA kwa sababu hakuna kanuni yeyote inayoelekeza muda na mahali mwafaka pa kutangaza nia ya kugombea urais. Mwanachama anapaswa kuongozwa na busara zake tu juu ya muda na mahali pa kutangaza nia yake. Sasa kama mwanachama wa CHADEMA hana busara kiasi cha kutangaza nia ya kugombea urais ndani ya kikao cha ‘mpinzani’ wake CCM, na kama busara za mwanachama huyo ni finyu kiasi cha kumuomba mwenyekiti wa CCM ndiye awe meneja wa kampeni zake, kwa nini iwe tatizo kwa BAVICHA au CHADEMA? ....

Na unaisemeaje busara ya kauli kwamba hakuna chama kinachoweza kushika dola zaidi ya ccm, hiyo nayo iachwe kama busara ya mwanachama? Huo ni uhaini na sisi BAVICHA tunaongoza mapambano ys kuitoa ccm madarakani hstuwrzi hata siku moja vumilia kauli kama hii!
 
Back
Top Bottom