Diwani kata Mlangali Ludewa ajinyonga

duh .... anadai halafu anajinyonga ..... angedaiwa je?

RIP

Huyu diwani inaelekea alikuwa dalali sasa hizo hela alitakiwa azirudishe kwa wenyewe na maadam aliyemkopesha au kufanya nae dili alikuwaamemrusha hakuwa na jinsi ya kuwalipa wenye mali hivyo akaona afadhali asepe!!
 
Mwana sisiemu tulikupenda lkn mungu kakupenda zaidi, kata nyingine tena hiyo sisiemu tunaikosa
 
R.I.P Diwani tutakukuta siku yetu ikifika.

Angejaribu kwanza kumshitaki kabla ya kuchukua uamuzi wa kujinyonga
 
Wanyalu wameachiwa urithi mbaya sana toka kwa Chifu Mkwawa.. Solution kwa matatizo yao ni kujirestisha in peace..!! Ukiwadai wanajiua.. Wakikudai wao wanajiua.. Wakikacirika wanajiua.. Wawe basi na ujasiri wa kujivika na mabomu na kujilipua..
 
images.jpg

Marehemu Rudolph CHaula a.k.a Kacheche kushoto

Kwa sasa sababu za kujinyonya diwani huyu hazijajulikana, hii ya madai sh milioni 81 ni mambo ya vijiweni, bora tusubiri taarifa kamili baadaye, maana hata nasoma mahali familia yake walikuwa wnamtafuta hadi walipoamua kuvunja chumba alichojifungi na kumkuta ananing'inia na kamba shingoni.
 
jamani, naomba mnisaidie, hivi kwanini watu wa pande zile wanapenda sana kujipiga kamba. yaani ukimuudhi tu anajitundika. yaani hata mademu wa kule akifumania message anakimbilia kujimaliza. rip diwani.
 
Huyo diwani ni mhehe nadhani maana wenyeji Ludewa ambao ni wapangwa wao design yao ni kuroga ukiwadhulumu
 
Watu wa Iringa kwa Kujinyonga! Sasa hapa kuna kusema r.i.p kweli wakati mtu amejimaliza mwenyewe!
Tangulia salama diwani
 
Diwani kacheche asingejinyonga, tungeshangaa. Hii ni laana ya padre volka paroko wa kanisa la katoliki la mlangali. Kabla ya kuwa diwani, bwn. Kacheche alikuwa anafanya kazi parokia ya mlangali na aliondolewa pale kwa tuhuma za wizi wa fedha nyingi za padre volka.

Padre volka alimsihi sana arudishe zile pesa na jamaa akagoma kata kata. Na ulaaniwe, yaelekea padre volka alimsomea albadili. Anyway tumwombee.
 
[h=3][/h]

Marehemu Rudolph Chaula a.k.a Kacheche kushoto

Chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Ludewa mkoa mpya wa Njombe kimepata pigo kubwa kufuatia diwani wake wa kata ya Mlangali Rudolph Chaula maaarufu kwa jina la Kacheche kujinyonga .

Taarifa ambazo mtandao huu wa Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima umezipata hivi na kuthibitishwa na katibu wa CCM wilaya ya Ludewa Eva Degeleki zinadai kuwa diwani huyo amekutwa akiwa kajinyonga katika moja kati ya vyumba vya nyumba yake ambavyo katika enzi ya uhai wake alikuwa akitumia kama ofisi yake ya udiwani.

Katibu huyo wa CCM Ludewa amesema kuwa hadi sasa hana taarifa za chanzo cha kifo chake ila anataarifa ya kujinyonga kwa diwani huyo na kuwa amepokea taarifa hiyo mida ya saa 8.15 usiku huu kujulishwa juu ya kifo hicho.


Imedaiwa kuwa diwani huyo toka mida ya mchana familia yake ilikuwa ikimsaka bila mafanikio baada ya wageni kufika kumuulizia na jitihada za kutafuta huku na kule zilimezao matunda usiku huu baada ya kuwa na wazo la kuvunja chumba hicho na kumkuta diwani huyo akiwa kajinyonga.

Source: Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima
 
Diwani kacheche asingejinyonga, tungeshangaa. Hii ni laana ya padre volka paroko wa kanisa la katoliki la mlangali. Kabla ya kuwa diwani, bwn. Kacheche alikuwa anafanya kazi parokia ya mlangali na aliondolewa pale kwa tuhuma za wizi wa fedha nyingi za padre volka.

Padre volka alimsihi sana arudishe zile pesa na jamaa akagoma kata kata. Na ulaaniwe, yaelekea padre volka alimsomea albadili. Anyway tumwombee.

Zamani nilikuwa sijui unyeti wa hizi mali za kanisa, siku hizi baada ya kuzungukia hili tufe na kuona source ya wanaotoa misaada hiyo, kweli si shangai mtu kupata laana ukiiba. Wengi wanaotoa misaada hiyo ni maskini, wajane ambao hudunduliza change na kuokoteza kila kidogo kinachopatikana na kututumia ili kusaidia tulio wanyonge wenzao. Sasa wenye mtazamo wa kiwango kifupi ndio hao wanaofikiria ndio pa kujitajirisha, ole yatakupata mabaya hata ukose raha ya peponi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom