Dear WEWE........

dear ctaki kuamini kuwa siku zote ulikuwa ukinifuatilia, ujumbe umefika
Ndio nimechukua muda mrefu sana na gharama kubwa sana hasa ukilinganisha na kipato changu kama nilivyoeleza kwenye hii season 1
 
Mh, sasa mbona unanikatisha tamaa tena jamani!
Hakukatishi tamaa, its time to show your man hood! Ni muda wa kujenga heshima ya kiume kutumia koo lako na mistari kama ulivyo anza badala ya kuamini katika vitu!Mtoto amekiri kesha kuelewa, go on with season 2, naisubiri bana!!
 
Hakukatishi tamaa, its time to show your man hood! Ni muda wa kujenga heshima ya kiume kutumia koo lako na mistari kama ulivyo anza badala ya kuamini katika vitu!Mtoto amekiri kesha kuelewa, go on with season 2, naisubiri bana!!
Hahahahaaa season 2 yaja mkuu, ngoja kwanza nifanye kazi nipunguze work log kidogo hapa kwa meza yangu then nitaendelea kushuka mistari wala usijali
 
Hahahahaaa season 2 yaja mkuu, ngoja kwanza nifanye kazi nipunguze work log kidogo hapa kwa meza yangu then nitaendelea kushuka mistari wala usijali

Tupo wengi tunaifuatilia kimyakimya sio mpaka kila kipande tureply. Kila lakhe... Na juhudi zako ila angalia usinyang'anywe viwalo ulivo azima kwa safiki yako mbele ya kadamnasi. si unajuwa uko unaingilia 'sphere of influence' za watu?
 
Dear WEWE.S02E01

Msichana baada ya kupokea mzigo ule na kuufungua, alishtuka kidogo kwani ulikuwa tofauti na vifurushi vingine alivyozoea kuvipokea. Tayari alikuwa amezoea kupokea maua na kadi za bei mbaya, mavazi ya gharama au mialiko ya sehemu mbalimbali za starehe. Lakini kifurushi hiki kilikuwa tofauti kidogo na hivyo vingine vilivyotangulia na hii ndiyo ilimfanya amtazame tena mtu aliyekileta lakini tayari alikuwa ameshaondoka. Aliteremka pale kwa yule sekretari rafiki yake na kumuuliza kama yule kijana alikuwa amemuelekeza kwake ameshatoka na yule sekretari kumwambia kwamba alitoka muda mfupi uliopita. Hakujua mzigo ulitoka kwa nani kwani hata hakupata muda wa kumuuliza yule aliyeuleta na wala hakupata nafasi ya kusign kwamba ameupata. Alirudi ofisini kwake kwa minajili ya kuufungua huo mzigo na kujua kilichokuwa ndani yake.

Mzigo aliokuwa ameletewa ulikuwa ni bahasha kubwa ya rangi ya khaki iliyokuwa imefungwa na kuandikwa jina la msichana kwa juu bila kitu kingine chochote. Ndani ya bahasha kulikuwa na ua jekundu linalojulikana kwa kiingereza kama hibiscus, biscuits paketi mbili ndogo ndogo na pembeni yake bahasha nyingine ndogo ya khaki iliyokuwa na waraka kama tulivyouona kwenye sehemu iliyopita. Aliifungua bahasha taratibu huku akiwa na uso wenye wasiwasi kidogo na alipoona vilivyoko ndani akaifunga tena kwa wasiwasi na kuisukuma pembeni ya meza yake na kuanza kuwaza ni nini hiki alikuwa ameletewa siku hiyo? Hata hivyo baadae alifungua na kutoa ile bahasha iliyokuwemo ndogo na kuifungua ili atoe ile barua iliyokuwa ndani.

Akiwa mmoja wa wafanyakazi waliokuwa kwenye kitengo cha masoko, mara nyingi huwa na kazi za nje zinazohusisha kutembelea wateja wao mbalimbali pamoja na mikutano ya hapa na pale, siku hiyo ilikuwa moja ya siku alizokuwa anatakiwa kuhudhuria mkutano muhimu sana. Akiwa ndio anaifungua ile bahasha mlango wa ofisi yake ulifunguliwa na bosi wake akaingia taratibu ndani na kummwambia muda wa kwenda kwenye mkutano na hivyo walitakiwa waondoke muda huo. Kama ilivyo kawaida ya wafanyakazi ambao bado wageni kwa maana ya kuwa kwenye ajira kwa muda mfupi huwa na tabia ya kuwaogopa sana mabosi wao na ndivyo ilivyokuwa kwa msichana. Wakati bosi wake anaingia alijikuta akiisukuma ile bahasha yenye waraka na ikadondoka kutoka mezani na bahati mbaya ikatumbukia kwenye kasha la kuweke karatasi zisizotumika tena.

Alinyanyuka akaichukua ile bahasha kubwa na kuikunja ili bosi wake asione kilichokuwemo na kuitumbukiza nayo kwenye kasha la taka, akilini mwake akijua ile bahasha yenye waraka itakuwa imebaki mezani kwake. Akabeba kila kilichohitajika kwenye mkutano akatoka na bosi wake wakaondoka.

Nini kitaendelea usikose episode 2 ya season 2
 
Yaani kama mtu vile anataka kufika kileleni af chaga za kitanda ziporomoke!!! Kila kitu kinakata kwa muda. Tumesubiri kipande kitakacho fuata.
 
Dear WEWE.S02E02

Mkutano aliohudhuria msichana siku hiyo ulichelewa sana kwisha na hivyo wakati anarejea ofisini kuchukua mizigo yake ya kawaida hakuwa anakumbuka tena kama kuna tukio lilitokea mchana ambalo kimsingi hakuwa amefika tamati yake. Alifika na kuchukua mkoba wake na kutoka ofisini kwani bosi wake alikuwa anamsubiri na alitaka kumpa lift ya kumrejesha nyumbani kwa siku hiyo kwani muda ulikuwa umekwenda sana.

Kesho yake asubuhi wakati anaingia ofisini alipita kama kawaida kwa yule sekretari rafiki yake ambapo walipiga stori mbili tatu na ndipo yule sekretari akamuuliza sababu ya kumuulizia yule kijana aliyekuja jana kwani hawakuwa wamekutana tena jana yake baada ya kwenda mkutanoni. Ndipo alipokumbuka habari ya ile bahasha ndogo iliyoonekana kuwa na barua ndani lakini hakuwa ameisoma. Bila kujibu kitu aliondoka na kwenda ofisini kwake ambapo alitafuta karibu kila sehemu lakini hakuweza kuiona mahali popote. Kasha lake la kuwekea takataka tayari lilishatolewa na kijana wa usafi na karatasi zote zilishatupwa na hata wakati anaingia ofisini alikutana na gari la kukusanya takataka likiwa linatoka maeneo ya ofisini kwao na hivyo alijua fika kwamba kwa namna yoyote ile ilikuwa imeshapotea na hakukuwa na namna yoyote ya kuipata.

Msichana alibaki na maswali mengi kichwani ambayo sasa yalianza kumfanya apate hofu
  • Ni nani aliyekuwa ametuma mzigi ule usiokuwa wa kawaida kwake?
  • Kile ki ua chekundu kilikuwa na maana gani, maana kilikuwa kimoja tu tena kwasababu kilikuwa kimefunikwa kwenye mfuko kilishaanza kunywea.
  • Nini kilikuwa kimeandikwa kwenye karatasi zilizokuwa ndani ya bahasha ile ndogo?
Mh msichana aliendelea kuwaza kwa muda lakini baadae alisahau tukio lile na maisha yakaendelea kana kwamba hakukuwa na kitu chochote kilichotokea.

Je nini kitaendelea kwa jamaa atakapoona kimya? na nini hatima ya sakata zima?

Endelea kuwa nami..........
 
Dear WEWE.S02E02

Mkutano aliohudhuria msichana siku hiyo ulichelewa sana kwisha na hivyo wakati anarejea ofisini kuchukua mizigo yake ya kawaida hakuwa anakumbuka tena kama kuna tukio lilitokea mchana ambalo kimsingi hakuwa amefika tamati yake. Alifika na kuchukua mkoba wake na kutoka ofisini kwani bosi wake alikuwa anamsubiri na alitaka kumpa lift ya kumrejesha nyumbani kwa siku hiyo kwani muda ulikuwa umekwenda sana.

Kesho yake asubuhi wakati anaingia ofisini alipita kama kawaida kwa yule sekretari rafiki yake ambapo walipiga stori mbili tatu na ndipo yule sekretari akamuuliza sababu ya kumuulizia yule kijana aliyekuja jana kwani hawakuwa wamekutana tena jana yake baada ya kwenda mkutanoni. Ndipo alipokumbuka habari ya ile bahasha ndogo iliyoonekana kuwa na barua ndani lakini hakuwa ameisoma. Bila kujibu kitu aliondoka na kwenda ofisini kwake ambapo alitafuta karibu kila sehemu lakini hakuweza kuiona mahali popote. Kasha lake la kuwekea takataka tayari lilishatolewa na kijana wa usafi na karatasi zote zilishatupwa na hata wakati anaingia ofisini alikutana na gari la kukusanya takataka likiwa linatoka maeneo ya ofisini kwao na hivyo alijua fika kwamba kwa namna yoyote ile ilikuwa imeshapotea na hakukuwa na namna yoyote ya kuipata.

Msichana alibaki na maswali mengi kichwani ambayo sasa yalianza kumfanya apate hofu
  • Ni nani aliyekuwa ametuma mzigi ule usiokuwa wa kawaida kwake?
  • Kile ki ua chekundu kilikuwa na maana gani, maana kilikuwa kimoja tu tena kwasababu kilikuwa kimefunikwa kwenye mfuko kilishaanza kunywea.
  • Nini kilikuwa kimeandikwa kwenye karatasi zilizokuwa ndani ya bahasha ile ndogo?
Mh msichana aliendelea kuwaza kwa muda lakini baadae alisahau tukio lile na maisha yakaendelea kana kwamba hakukuwa na kitu chochote kilichotokea.

Je nini kitaendelea kwa jamaa atakapoona kimya? na nini hatima ya sakata zima?

Endelea kuwa nami..........

Utamu unogile.
 
Dear WEWE.S02E03

Jamaa baada ya kuacha ule mzigo kwa yule msichana, alitoka haraka mule ofisini muda ambao yule msichana alikuwa anajaribu kutafuta sehemu iliyokuwa inaweza kumuonyesha mzigo ulikuwa unatoka kwa nani. Alifanya hivyo makusudi ili asiulizwe maswali mengi kwani kwa kipindi kile hakuwa kwenye hali ya kuweza kusema neno lolote kutokana na woga uliokuwa umemjaa. Sasa tuendelee kwa upande wa mshikaji,

Dear wewe, basi siku ile nilipotoka pale ofisini kwenu nilijikuta tu niko nyumbani, sikujua kama nilipanda daladala au nilitembea kwa mguu ila ninachokumbuka ni kuwa nilishtuka niko mlangoni kwangu na moja kwa moja mpaka kitandani nikitaraji kupata usingizi ambao nao hukutokea. Sikuwa nasikia njaa kwahiyo hata mpango wa kula sikuwa nao kwa siku hiyo. Kimsingi sikuwa najua nini kitafuatia baada ya mimi kuleta ile barua yangu pale ofisini kwenu, sikuwa natarajia unijibu kwa jibu lolote lile, sikuwa natarajia unitafute kimsingi sikuwa natarajia chochote kutoka kwako ingawa pia sasa nilianza kujilaumu kwa kitendo nilichokifanya maana sasa nijua ntalazimika kuhama kituo cha daladala pale ninapokuona mara kwa mara, nilijua sasa mkataba wangu na wale watoa taarifa wangu utakufa maana sikuwa tayari kupokea majibu yoyote kutoka kwako na kibaya zaidi, pamoja na kwamba mwanzo nilikuwa natamani kujua kila unachokifanya sasa sikutaka kujua chochote unachokifanya kwani nilijawa na uoga wa ajabu kiasi cha kuwa kama mgonjwa kwa siku kadhaa.

Baada ya siku mbili nilianza tena kwenda kazini kwani nilijua kabisa maisha yangu yalikuwa yanategemea kibarua hicho na kama nisingeenda kwa siku nyingine moja tu basi nisingekuwa nacho tena. Ila sasa nililazimika kuhama rasmi kituo cha kupandia basi, nikalazimika kubadilisha muda wa kwenda na kurudi kazini ili tusiweze kukutana mimi na wewe ingawa bado sikuwa na uhakika sana hata kama unamjua mtu aliyekuwa ameandika ujumbe ule au hata kumkubuka yule aliyekuletea pale ofisini kwenu.

Mwezi ulikatika na kwa bahati nzuri mipango yangu ya kukukwepa ikawa imefanikiwa kwani katika kipindi chote hicho hatukuwa tumekutana wala sikuwa nimekuona kwa namna yoyote ile. Siku moja ya jumapili nilipanga kwenda kumtembelea rafiki yangu yule aliyenipa viwalo kama nilivyokwambia, naye alikubali niende kwake na kwamba angekuwepo nyumbani siku hiyo kwani alikuwa anategemea kuwa na mgeni mwingine nyumbani kwake siku hiyo kwahiyo itakuwa vizuri tukijumuika kwa pamoja. Nilijiandaa vizuri baada ya kufanya usafi nyumbani kwangu na kuelekea huko kwa rafiki yangu.

Kama nilivyoeleza hapo awali kwamba huyu rafiki yangu alikuwa anakaa upande tofauti kidogo na huku kwetu hivyo ilinilazimu kupanda daladala ili kuweza kufika huko. Nilifika majira ya saa sita kamili za mchana hivi na kumkuta rafiki yangu yule. Kimsingi sikutaka kumsimulia tena habari zako na wala zile za kwamba nilimuona akikushusha pale ofisini kwenu siku moja. Nilikuwa nimeamua tu kupotezea na kuendelea na masisha yangu.

Majira ya saa saba kasorobo mlango uligongwa wa hapo nyumbani kwa rafiki yangu, kwakuwa yeye alikuwa jikoni akiandaa chakula aliniomba nimfungulie huyo anayegonga. Nilitoka na kwenda mlangoni harakaharaka kwani kwa wakati huo nilikuwa naagalia zile Bongo movi zetu kwenye chaneli moja ya dstv nafikiri. Ile nafungua mlango tu nusura nipoteze fahamu, ulikuwa ni wewe ukiwa umesimama mlangoni.....................

Dah! Ilikuwaje baada ya hapo..........Tutaendelea tena kesho
 
Ua jekundu la hibiscus, biskuti pakiti 2 ndogo!!Hapa patakuwa na ujumbe uliofichika, nasubiri maana ya pakiti hizo mbili za biskuti, ua jekundu kwa mapenzi si jambo geni!!!

M'Jr umenikumbusha enzi zile nikiwa skuli Caigo, kuna mdada mmoja (Preta), nilimpenda sana aliniaga ya kuwa anaenda sokoni, nikamwomba akaniletee zawadi ile ambayo yeye angeona inanifaa!! Mkuu nililetewa NYANYA moja iliyoiva pyuuu, aliileta kwa mbwembwe nyingi sana!!!Mpaka leo hii nikimkumbuka huyu Preta wangu, hakika namwona mpya! Maana ya ya ile nyanya hajanambia mpaka leo, ila anasema siku si nyingi atanambia!!
 
Dear WEWE.S02E03
Majira ya saa saba kasorobo mlango uligongwa wa hapo nyumbani kwa rafiki yangu, kwakuwa yeye alikuwa jikoni akiandaa chakula aliniomba nimfungulie huyo anayegonga. Nilitoka na kwenda mlangoni harakaharaka kwani kwa wakati huo nilikuwa naagalia zile Bongo movi zetu kwenye chaneli moja ya dstv nafikiri. Ile nafungua mlango tu nusura nipoteze fahamu, ulikuwa ni wewe ukiwa umesimama mlangoni.....................

Dah! Ilikuwaje baada ya hapo..........Tutaendelea tena kesho

Daah!! Pole sana, haya ndo madhara ya woga, umejiroga mwenyewe!!! Kheri mimi nilishavunja ukimya kwa Preta wangu
 
Ua jekundu la hibiscus, biskuti pakiti 2 ndogo!!Hapa patakuwa na ujumbe uliofichika, nasubiri maana ya pakiti hizo mbili za biskuti, ua jekundu kwa mapenzi si jambo geni!!!

M'Jr umenikumbusha enzi zile nikiwa skuli Caigo, kuna mdada mmoja (Preta), nilimpenda sana aliniaga ya kuwa anaenda sokoni, nikamwomba akaniletee zawadi ile ambayo yeye angeona inanifaa!! Mkuu nililetewa NYANYA moja iliyoiva pyuuu, aliileta kwa mbwembwe nyingi sana!!!Mpaka leo hii nikimkumbuka huyu Preta wangu, hakika namwona mpya! Maana ya ya ile nyanya hajanambia mpaka leo, ila anasema siku si nyingi atanambia!!

Hahahaa hiyo nimeipenda, niruhusu niitumie kwenye sehemu mojawapo ya simulizi mkuu
 
Dear Wewe,

Yapata wiki ya tatu sasa nakuona ukiwa unatokea upande wa kaskazini wa pale ninapokuona kila siku asubuhi. Najua huenda hunijui lakini mie nakufahamu vyema kwani katika kipindi cha wiki tatu hizi nimefanya homework ya haja kiasi cha kujua mpaka nyumba uliyohamia. Labda nikukumbushe tu kama utanikumbuka, mi ni yule kijana niliyekusalimia siku ile ulipodondosha pochi yako baada ya kusukumwa na yule muuza matunda aliyekuwa na toroli pale kituoni, ingawa wakati najiandaa kuanzisha mazungumzo likatokea lile gari jeusi lenye namba za stk na ukapanda na kuondoka huku mi nikizuiliwa kuingia ingawa gari lilikuwa tupu.

Natumaini sasa umeweza kunikumbuka japo kidogo, najua utakuwa unajiuliza maneno meengi haya ninayoandika yana lengo gani, ntajaribu kupunguza maneno ili isiwe kama tuko kwenye mkutano wa siasa kule katani kwetu maana wale wanasiasa hupiga maneno mengi na dakika tano za mwisho ndipo husema lengo lao kubwa la kuwa kwenye mkutano ule. Basi mi nitaenda moja kwa moja kwenye dhumuni kuu ya waraka huu.

Baada ya kukuona siku ya kwanza na nakumbuka tulipanda wote daladala kuelekea mjini, moyo wangu ulihisi kupata ganzi. Sio kwakuwa we u mrembo sana, bali ni hali isiyoweza kuelezeka ya nguvu kali ya uvutano toka kwako ingawa nina shaka kama nguvu hii itakuja kuwa inatoka kwa pande zote mbili. Hata hivyo kwa kipindi chote hiki nimejaribu kufanya homework yangu ili kuweza kukufahamu nikisaidiwa na FBI ya kichwa changu, na LPD ya miguu yangu, CIA ya macho yangu na KGB ya masikio yangu. Pia nikapata msaada mkubwa wa Reuters na CNN ya karatasi na kalamu zangu ili kufanikisha mchakato mzima huu. Mchakato huu umefanikisha kujua mahali unapoishi, pale unapofanyia kazi, siku gani unazokwenda kazini na siku za mapumziko na hata kumjua yule rafiki yako ambaye nimekuja kugundua kuwa ni secretary wa pale kazini kwenu (yule mwenye maneno meeengi kama radio iliyowekwa betri mpya)

Jambo lililonopa moyo na mshawasha wa kuendelea na mpango wangu ni kutoona hata siku moja binadamu wa jinsia ya kiume akiingia ama kutoka pale nyumbani kwako. Hii ni kwa msaada wa CCTV kali za yule mama wa gengeni pale pembeni yenu, fundi viatu wa pale mwembeni pamoja yule dogo mjukuu wa mama mwenye nyumba wako ambao either nimelazimika kuwa mteja wa bidhaa zao au kulazimika kufadhili baadhi ya mahitaji yao ili kufanikisha kazi yao ya kuku-cctv na mimi kupata habari zote bila chenga.

Sasa hili ndilo langu ninalotaka kulileta kwako...........................................

Dont miss episode 2

Story umeifanya ndefu wakati ni fupi na pia sijapenda lugha ulizotumia, CCTV, FBI, CNN, CIA, LPD n.k na pia ulipomwambia rafiki yake anaongea kama radio iliyowekwa btri, sasa huyo ni rafiki hujawaona NDUGU si utaandika vitabu na kuwatungia movie kwa kuwa descibe????????
 
Story umeifanya ndefu wakati ni fupi na pia sijapenda lugha ulizotumia, CCTV, FBI, CNN, CIA, LPD n.k na pia ulipomwambia rafiki yake anaongea kama radio iliyowekwa btri, sasa huyo ni rafiki hujawaona NDUGU si utaandika vitabu na kuwatungia movie kwa kuwa descibe????????

Challenge yako ni nzuri. Lakini linapo kuja suala la kufananisha kitu kimoja na kingine(simile) kiutunzi mi naona inafaa. Anyway ngoja nisubiri mtunzi mwenyewe akujibu.
 
Back
Top Bottom