DCI Manumba alielezea mpango wa mahsuusi wa polisi?

enzihuru

Member
Aug 6, 2012
82
10
Mkutano wa DCI wavunjika

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba hakutaka kuzungumzia suala hilo akisema: “Hayo yote yameundiwa tume ngoja tuiachie ifanye kazi yake.”
Awali, DCI Manumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari mkoani Iringa, ambao hata hivyo, ulivunjika baada ya kutokea kutoelewana baina yao.

Manumba alitaka kueleza ripoti ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, lakini waandishi hao walikataa kumsikiliza wakisema hawauamini uchunguzi huo kwa kuwa ulifanywa na polisi peke yao.

Kabla Manumba, hajaanza kuzungumza, Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Iringa (IPC), Frank Leonard alisema kutokana na msimamo wa waandishi wa habari wa mkoa huo hakutakuwa na uhusiano wa kikazi na polisi hadi pale tume zilizoundwa kuchunguza kifo hicho zitakapotoa taarifa sahihi juu ya mauaji hayo.

“Msimamo wetu ni kusitisha uhusiano wa kikazi baina yetu na jeshi la polisi hususan Mkoa wa Iringa, tumekuja hapa kwa sababu DCI umetuita na kama unataka kutupa taarifa ya kifo cha ndugu yetu basi waambie hao maofisa wa jeshi wa Iringa watoke nje,” alisema Leonard.

Akijibu madai hayo Manumba alisema: “Nia yangu ni kutoa taarifa ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, ndiyo maana niliwasiliana na mwenzenu ili tuweze kuzungumza, Polisi Iringa wataendelea kuwepo na waandishi wa habari mtaendelea kuwepo, matukio kama haya yapo na yataendelea kuwepo
Licha ya maelezo hayo, hakuna mwafaka uliofikiwa na mkutano huo ukavunjika.
Chanzo: Gazeti la Mwananci 6/9/2012.
Wanahabari na wananchi wote mnapaswa kuangalia ujumbe wenye maandishi mekundu kwa hadhari kwani yamkini DCI ameshatoa tahadhali ya kuendelea matukio kama yale yaliyomsibu ndugu Mwangosi popote na muda wowote ule. Kwa elimu yake, sidhani kama ulimi wake ulitereza kusema hiyo kama alisema hivyo.Kama alijua kuwa kuna tume juu ya kifo hicho yenye uwezo wa kutolea maelezo, yeye nani kampa kazi hiyo ya kuelezea chanzo cha kifo wakati si Daktari na si mwanatume? Atakayekaidi tahadhari ya muheshimiwa huyu, litakalomkuta asimlaumu mtu kwani hata Msajiri wa vyama vya siasa alishasema kuwa, zana za kazi za polisi ni silaha kama kalamu na komputa zilivyo kwa waandishi.
 
Daaaa wanazidi kuumbuka yani na bado watajisema tu! Kweli damu ya mtu haipotei hivihivi!
 
Masikini Tanzania Mungu ameibarikiwa kwa kila kitu isipokuwa AMANI tu ee mungu turehemu kwa hilo
 
DCI hana jipya kwani bado angeendelea kuwasingizia chadema si ndivyo walivyokubaliana ikulu na mwema ,jk, nepi, na kina mkama
 
Mkutano wa DCI wavunjika

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba hakutaka kuzungumzia suala hilo akisema: “Hayo yote yameundiwa tume ngoja tuiachie ifanye kazi yake.”
Awali, DCI Manumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari mkoani Iringa, ambao hata hivyo, ulivunjika baada ya kutokea kutoelewana baina yao.

.
Mbona waziri wake amesema ameunda Kamati yeye anasema Tume kweli nchi hii tuna viongozi vilaza kweli, wasimamizi wa sheria ndo hawajui sheria, BIG UP TUNDU LISSU Umegonga penyewe.
 
comment za TL zimewavuruga, zimewatoa kwenye reli, sasa sijui itaitwa tume! au kamati, na kama ni kamati kisheria itawaondoa waandishi Wa habari and judge IHEMA for check and balance, waziri anatakiwa sasa adeal na wizara yake ya ulinzi tu, achukue watalaam wake wamsaidie, hata hivyo bado kamati hiyo haiwezi kuwa na tija kwani na yenyewe ni watuhumiwa,
 
Nimekuwa nikiamini hivyo tangu utoto wangu kwamba polisi hawana akili, taaluma yao imejengwa katika misingi ya kutumia nguvu zaidi kuliko kufikiria. Nakiri nimeshawahi kumwuuliza polisi mmoja kuwa kwa nini hawapendi kutumia akili. Hakuna mtu ambaye anaweza kunishawishi mimi kuwa askari polisi katika muda wowote wa maisha yangu hapa Tanzania. Nikimsikia mtu hata ndugu yangu anawaza kazi ya upolisi huwa namwona kama hana akili timamu.

Lakini kwa upande mwingine huwa nafurahishwa na polisi wa nchi zingine kama UK jinsi wanavyofanya kazi zao, hasa kukabiliana na matukio kama ya vurugu na jinsi ambavyo wanajaribu kufanya shughuli zao bila kumwonea mtu. Achilia mbali taaluma ya polisi wa Tanzania ya kupokea rushwa na kufanya biashara za kupora, ujangili na magendo! Sitaki kuongelea hilo kwani ujambazi na wizi wanaoufanya huenda ni kwa sababu ya kipato chao kidogo, sijui.

Nimekuwa nikijiuliza kwa mfano matukio ya mauaji ambayo wamekuwa wakifanya polisi, Morogoro, North Mara, Arusha, Iringa, na kwingineko Tanzania kwa kuwavamia viongozi wa Chadema na wafuasi wao wakiwa kwenye maandamano, mikutano au mazungumzo tu ya kawaida, je:

1. Ni kwamba uwezo wenu mdogo wa kufanya kazi ndio ambao unasababisha vifo katika kile ambacho mnakiita kuzuia fujo?

2. Ni amri ya kuua mnayopewa na wakuu wenu ili kufanya kile wanachodhani ni kupunguza nguvu na hamasa ya M4C kuelekea mapinduzi ya ukombozi?

3. Nyie mnafaidika vipi na mauaji mnayoyafanya, mnapandishwa vyeo? Mnapewa hela? Au ni sifa kwa polisi kuua?

Kama jibu lenu ni amri mnayopewa na wakuu wenu, je hamuwezi kutumia njia mbadala au akili kidogo kukwepa yale mnayoagizwa?

Nimewasikia mara nyingi mkilalamikia mazingira magumu ya kuishi, mishahara midogo na kuwa serikali haiwajali!

4. Inakuwaje serikali hiyohiyo mnayoilaumu iwatumie vibaya hivyo kama mpira wa kufanyia ngono? Kwa namna hiyo raia (nikiwemo mimi) hawatawaona nyie ni mahayawani kweli?

Nilitegemea kuona polisi ndio wanakuwa wa kwanza kuungana (hata kama sio moja kwa moja) na nguvu ya umma ili kudai haki na nchi yetu iliyoibiwa na mafisadi, lakini mnapokuwa kinyume na nguvu ambayo hata nyie inawapigania, mtanishawishi vipi niache kuamini kuwa nyie uwezo wenu wa kufikiri ni mdogo?

Polisi nipeni majibu ya haya maswali ili nifute dhana ya kwamba nyie hamwezi kufikiria sawasawa ambayo imejengeka kwa muda mwingi katika maisha yangu.

Samahanini kwa kuwa muwazi na kueleza mawazo yangu bila kificho.
 
Unawauliza vichaa maswali kama haya? Wanajua kumtetea Kikwete aliyeizamisha nchi kwenye mauwaji na basi. Mungu tunusuru watanzania na wapuuzi hawa wanaiharibu nchi yetu kiasi hiki kila kukicha. Mungu uliangalie hili jeshi la polisi linalomwaga damu, kunyenyasa raia kwa rushwa na ujambazi, na kuwakwaza na kuwapotosha watoto wetu.
 
Kweli nimeamini jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza...
Mkuu ni pm nikupe namba ya baba angu akusaidie kujibu maswali yako. He is a policeman...
 
Binafsi naichukia kazi ya upolisi, mazingira yake kiutendaji yanaendana na DHULUMA KUWATENDEA WENGINE VIBAYA. na ikitokea ukawa kwenye serikali mbovu kama hii, ndo unaweza ukapanda daraja ukafikia hata ngazi ya SHETANI MKUU, kwa sababu polisi utakuwa huru kufanya ujambazi, polisi utakuwa huru kula rushwa, polisi utakuwa huru kufanya ubakaji, polisi utakuwa huru kudhulumu, polisi utakuwa mlevi, polisi utafanya maovu yoyote na usichukuliwe hatua yoyote. INASIKITISHA SANA.
 
Polisi wa Tanzania wengi wao hawatumii akili
Pili wako kimapato zaidi wanajali ulaji kuliko uhai
 
Back
Top Bottom