Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
HIJAMAH/ BLOOD CUPPING/ CHUKU AU KUUMIKA:
Kuna faida nyingi sana za kupiga chuku au kuondoa damu chafu mwilini. Hijama/ chuku hutibu maradhi mengi ndani ya mwili wa binadamu kama vile kuondosha maumivu ndani ya mwili, maumivu ya miguu, mishipa, maumivu ya kichwa ya muda mrefu, kiuno, mgongo, mabega, shingo. Husafisha damu kwa kutoa sumu ndani ya damu ya mwanadamu, hutibu maradhi sugu yanayoenea katika damu, huwasaidia pia wenye matatizo ya pumu/asthma, huwasaidia pia waliosibiwa na matatizo ya uchawi na majini, huboresha mzunguko wa damu mwilini, huimarisha kumbukumbu, huboresha mfumo mzima wa uzazi kwa wanawake na wanaume huongeza nguvu za kiume, hutibu tatizo la mfumo wa usagaji wa chakula, matatizo ya ngozi,matatizo ya macho, moyo, kung'oka kwa nywele, mzio/allergy, gout, kiharusi/stroke na matatizo mengine mengi tu....
Kwa ujumla Hijama ina faida nyingi sana kwa binadamu......
Jitahidi na wewe hata kwa mwaka angalau mara tatu au nne na utaona faida yake