Dawa ya kuondoa msongamano Dar...

Mkuu Steve Dii unachosema ni kweli kabisa, lakini kungekuwa na utaratibu wa kuhakikisha viwango vya emissions level vinafuatwa nchini basi nina hakika baadhi ya magari nchini yasingeruhusiwa kuwepo barabarani na hivyo kupunguza msongamano huo wa magari japo kwa asilimia ndogo.

BAK, wazo la kuondoa magari kwasababu ya umri wake tu hata mimi sitoafikiana nalo. Siafikiani na wazo hilo maana roadworthy haitegemei umri wa gari; ni matunzo ya gari zaidi ndiyo huwa kigezo. Unaweza kuwa na gari la miaka minne lakini likawa linatoa moshi kuliko tairi la kuchoma kwenye maandamano! Lakini pia unawezakuwa na gari la miaka 12 ambalo limetunzwa na carbon emission yake ikawa chini sana. Hii inapelekea kukukumbushia moja ya jambo kwa wenzetu jinsi vile baadhi ya magari yaliyo 'antique' yanavyokuwa aghali kuliko mengi mapya.
 
Last edited by a moderator:

Hata hivyo, kuhusiana na suala zima la msongamano Dar, labda judadili kwa kuanzia na Dar Es Salaam Masterplan 2012 – 2032. Does it address the points you have raised? Will the new city planned be achieved by 2013?


Dar es Salaam Masterplan 2012 – 2032: Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development: http://www.planning4adaptation.eu/Docs/newsInfoMaterial/05-2013/08/FONTANARI_22_APRIL_2013.pdf

Imegharimu kiasi gani kuiandaa hii Dar Masterplan? Hata hivyo, mi nimeshindwa kabisa kuielewa!
 
Mkuu Steve Dii unachosema ni kweli kabisa, lakini kungekuwa na utaratibu wa kuhakikisha viwango vya emissions level vinafuatwa nchini basi nina hakika baadhi ya magari nchini yasingeruhusiwa kuwepo barabarani na hivyo kupunguza msongamano huo wa magari japo kwa asilimia ndogo.

Mimi nasema kungekuwa na idadi kubwa maana ukianzia kwenye daladala, uje kwenye milori, uende kwenye teksi, urudi kwenye mabasi ya kwenda mikoani, na hapo hujagusa magari tu ya watu binafsi wanayoyatumia kwenye shughuli zao za kibinafsi....aisee, mengi yasingekidhi vigezo.

Na umri wa gari wala siyo kigezo. Kama alivodokeza SteveDii, kuna magari mengi tu yenye umri mkubwa lakini siyo mikweche.
 
Hivi bongo sisi tuna emissions control laws?

Maana kuna magari mengi sana bongo ambayo kama labda tungekuwa na emissions control laws wala yasingekuwa hata barabarani.

Kwa nchi za wenzetu kuna sehemu gari haiwezi hata kupata usajili bila ya ku-pass emissions test. Na usajili unatakiwa kila mwaka. Hivyo kila mwaka kabla usajili wa mwaka uliopita haujaisha muda wake ni lazima ifanyiwe testing tena na lazima i-pass ili iweze kupata huo usajili. Ikifeli haipati.

Na kama gari haina usajili basi ni kinyume na sheria kuiweka barabarani. Ukiiweka na ukikamatwa hiyo faini yake utajuta.

Utaratibu huo nao hupunguza uwepo wa yale magari mabovu mabovu yanayoongeza idadi ya magari mabarabarani na kuchafua mazingira.

Lakini by the looks of it, idadi ya mikweche iliyopo kwenye mabarabara ya bongo inanifanya nidhani hatuna kabisa sheria za namna hiyo.

Haina haja ya kujipa mashaka ya emissions control laws kwa Tanzania kwa sasa, japo mawazo yako si mabaya. Hatuna idadi ya magari ya kuona kwamba yanachangia saana katika emission-related pollution na pia hatuna viwanda vya hali hiyo, kwa hiyo tusijiongezee gaharama kwa ajili ya suala hilo.

Kuhusu hii emission test ndio mashaka kabisa, je waweza kufikiria yatakayofeli yataenda wapi? Tuna viwanda vya recycling kwa components za magari? By the way, idadi ya magari Tanzania ni negligible (sidhani kama yanafika 1.5milioni) ambapo kwa baadhi ya nchi magari yanazidi raia wake. Bado naamini mfumo uliopo wa kupasishwa magari ungelikuwa unasimamiwa ipasavyo bado ingelifaa. Tuimarishe kwanza spending power zetu badala ya kuwaza mambo ya kujiletea ugumu. Mwenyewe umeshuhudia watu walivyolalamika kwa nyongeza za kodi zinazohusu magari.
 
Wakuu, kingine ambacho mimi nadhani kinaweza kusaidia kuondoa/kupunguza msongamano wa magari ni kujenga parking za magari pahala pengi. Sehemu kama Mwenge, Msimbazi-na-Uhuru, Fire, etc. pakiwepo na parking kubwa bila shaka msongamano utapungua, kwani yale magari yanayo randaranda kutafuta upenyo wa kupaki husababisha magari yaliyonyuma ku-slow na kusababisha build-up ya jam na baada ya muda mfupi gari zinasimama kabisa.

Sambamba na zoezi hilo juu, pia pajengwe parking kwenye vituo vikubwa vya DART na hata vituo vya train ya Mwakyembe. Ili huko mbeleni watu waweze kupark magari yao wakitokea majumbani kisha kupanda DART au train na kuelekea makazini.

Jambo jingine ambalo nafikiri linaweza kupunguza msongamano ni uzibaji wa mitaro pembezoni mwa barabara. Binafsi kwakweli miongoni mwa mambo yanayoudhi kuliko yote kwenye miundombinu yetu ni huu ujengaji wa mitaro ya maji inayoachwa wazi pembezoni mwa barabara. Inakera sana kuona ndani ya karne hii ya 21 tunajenga au kujaribu kuboresha mabarabara katikati ya miji na kuweka mitaro (mingi yake ni kama mahandaki vile)kisha kuiacha wazi. Kwanini makandarasi waliojenga mabarabara miaka ilee ya 60, 70 (karne ya 20) waliweza, tunashindwa nini hivi sasa?!!

Mitaro hiyo husabisha foleni kwani madereva wanapopata dharura ya magari yao kuharibika wanalazimika kubakia barabarani ili kutoingia mitaroni badala ya kusogeza magari pembeni na kusubiria huduma ya matengenezo au kuvutwa. Kubakia bararani husababisha magari yaliyonyuma kwenda polepole na punde foleni kujitokeza. Mitaro hiyo pia inachukua nafasi kubwa kwani pahala pengi inajengwa pande zote mbili za barabara. Hivyo kufanya barabara ziwe finyu na matokeo yake kulazimisha magari yanayopishana yaende taratibu jambo ambalo mwisho wake husababisha foleni, ukiachilia mbali kuwanyima watembea kwa miguu uhuru wa kutembea kwa amani.

Usiombe ukatikiwe na ball-joint au kupata matatizo ya usukani ukiwa unaendesha Dar... the likelihood kwamba unaumia kwa kugongana na gari jingine ni ndogo kuliko likelihood ya kutumbukia na kufia mtaroni!! Bila shaka mitaro hii imesababisha vifo vingi sana hapa nchini.

Steve Dii
 
Jambo jingine ambalo nafikiri linaweza kupunguza msongamano ni uzibaji wa mitaro pembezoni mwa barabara. Binafsi kwakweli miongoni mwa mambo yanayoudhi kuliko yote kwenye miundombinu yetu ni huu ujengaji wa mitaro ya maji inayoachwa wazi pembezoni mwa barabara. Inakera sana kuona ndani ya karne hii ya 21 tunajenga au kujaribu kuboresha mabarabara katikati ya miji na kuweka mitaro (mingi yake ni kama mahandaki vile)kisha kuiacha wazi. Kwanini makandarasi waliojenga mabarabara miaka ilee ya 60, 70 (karne ya 20) waliweza, tunashindwa nini hivi sasa?!!

Mitaro hiyo husabisha foleni kwani madereva wanapopata dharura ya magari yao kuharibika wanalazimika kubakia barabarani ili kutoingia mitaroni badala ya kusogeza magari pembeni na kusubiria huduma ya matengenezo au kuvutwa. Kubakia bararani husababisha magari yaliyonyuma kwenda polepole na punde foleni kujitokeza. Mitaro hiyo pia inachukua nafasi kubwa kwani pahala pengi inajengwa pande zote mbili za barabara. Hivyo kufanya barabara ziwe finyu na matokeo yake kulazimisha magari yanayopishana yaende taratibu jambo ambalo mwisho wake husababisha foleni, ukiachilia mbali kuwanyima watembea kwa miguu uhuru wa kutembea kwa amani.

Usiombe ukatikiwe na ball-joint au kupata matatizo ya usukani ukiwa unaendesha Dar... the likelihood kwamba unaumia kwa kugongana na gari jingine ni ndogo kuliko likelihood ya kutumbukia na kufia mtaroni!! Bila shaka mitaro hii imesababisha vifo vingi sana hapa nchini.

Steve Dii

Sijawahi kuona sehemu ingine yoyote ile mimitaro mikubwa kama iliypo Dar. Kuna wakati nilikuwa nadhani labda niko peke yangu tu ninayekereka kumbe pia wapo na wengine.

Huwa najiuliza sana - hivi ni nani huyo aliyeidizaini hiyo mimitaro?
 
NN ni kweli kabisa umri wa gari si kigezo cha kutoweza kufikia viwango vya emissions. lakini Watanzania walio wengi hawana tabia ya kulipeleka gari likafanyiwe service pale ambapo liko due kwa service. Ali mradi gari liko barabarani na halijaonyesha dalili yoyote ile ya ubovu basi wengi hawako tayari kuingia gharama hizo. Wengi hulipeleka gari kwa fundi pale ambapo lina ubovu wa kushindwa kuwepo barabarani na mara nyingi linapelekwa ka mafundi wa uchochoroni ambao ujuzi wao ni wa kubabiababia, hivyo gari lenye umri mkubwa Bongo ukichangia na wengi hawana kawaida ya kulifanyia service gari kwa mafundi wenye utaalamu basi gari hilo lina uwezekano mkubwa wa kutoweza kufikia viwango vya emissions levels kama vingekuwepo.

Mimi nasema kungekuwa na idadi kubwa maana ukianzia kwenye daladala, uje kwenye milori, uende kwenye teksi, urudi kwenye mabasi ya kwenda mikoani, na hapo hujagusa magari tu ya watu binafsi wanayoyatumia kwenye shughuli zao za kibinafsi....aisee, mengi yasingekidhi vigezo.

Na umri wa gari wala siyo kigezo. Kama alivodokeza SteveDii, kuna magari mengi tu yenye umri mkubwa lakini siyo mikweche.
 
Ni wazo zuri sana, lakini waswahili hatusarifiki, hatusadifiki
 
Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara
mfano bidhaa za nguo

maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe
mfano Pugu

maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta

Vipodozi yote yaende mwenge......

vifaa vya kilimo Tandika.....
posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi
na maduka ya nguo tu...
maduka ya furniture yote yaende Keko..

tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar
tuige nchi zingine basi.....
ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo...

huu utaratibu unaoshauri utasaidia vipi kupunguza foleni ya posta-mwenge-tegeta,posta-ubungo-kimara,posta-chang'ombe-g/mboto,magomeni-kigogo-chang'ombe wakati wa asubuhi na jioni??hawa nao wanaenda kariakoo/posta madukani??au umekusudia kupunguza foleni kariakoo tu.
 
Hii ninayo suggest mimi inatumika miji mingi mno
Kuanzia China hadi Dubai..
kupanga maduka na maeneo kwa aina ya bidhaa...

right now Kariakoo ndo Centre ya mauzo ya jumla na rejareja
ya nchi nzima na nchi jirani kwa bidhaa hizi
1.nguo
2.simu na vifaa vyake
3.spare za magari
4.vifaa vya ujenzi
5.computers na vifaa vya ofisi
6.vyakula
7.vifaa vya kilimo..
8,furniture..
9.mengineyo

inatakiwa kufanyika plan mpya ya kuondoa maduka
ya bidhaa zote kasoro moja
na kuyasambaza kwenye kona zingine za jiji

Kariakoo ni soko kubwa la bidhaa mbalimbali katika Afrika Mashariki na ya kati.

Kupanga ni kuchaguwa, naunga mkono hoja.
 
Kuongezekana kwa msongamano mijini kunahatarisha uchumi na maisha ya baadae ya mji husika. Kukukua kwa mji kunaongeza demand, lakini ukuaji huo unaweza kuwa hasara kwa mji kutokana na kuongezeka kwa msongamano.

Dar Es Salaam kuna msongamano wa magari na watu. Njia mojawapo ya kupunguza msongamano wa magari ni kuimarisha public transport. Hata hivyo, kutokana na Dar Es Salaam kuwa na public transport mbaya ni watu wachache sana wenye magari yao binafsi ambao watakubali kuyaacha nyumba na kupanda daladala. Afterall bado kuna baadhi ya watu ambao wangependa ku-show off what sort of a car they drive.

Kwa sasa hivi sioni concrete action yoyote inayotia matumaini kutatua tatizo sugu la msongamano jijini Dar Es Salaam. Badala yake, tatizo la msongamano linaendelea kuwa kubwa hasa baada ya kuingia kwa boda boda.

Lakini wakazi wa jiji nao wameshaliona tatizo la msongamano wa magari kama sehemu ya maisha yao. Mabadiliko ya jiji la Dar Es Salaam yataletwa na Wadadarisalama wenyewe kwa kukataa kufanya tatizo la msongamano kama sehemu ya maisha yao ya kila siku.

Mji wa Moshi siyo msafi kivile tuu. Wala barabara zake za mjini hazipigwi deki pindi tuu kunapokuwa na mgeni. Wao wameamua mji wao uwe msafi whether or not kuna mgeni. Afterall usafi ni kwa manufaa ya wakazi husika Wala haina maana kuwa wachaga ni wasafi sana maana wametapakaa pia kila kona ya Dar Es Salaam.

Hata hivyo, kuhusiana na suala zima la msongamano Dar, labda judadili kwa kuanzia na Dar Es Salaam Masterplan 2012 – 2032. Does it address the points you have raised? Will the new city planned be achieved by 2013?

Dar es Salaam Masterplan 2012 – 2032: Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development: http://www.planning4adaptation.eu/Docs/newsInfoMaterial/05-2013/08/FONTANARI_22_APRIL_2013.pdf

hio ndio solution....kutoa magari binafsi barabarani...na hii unaweza kuifanya kwa kuwa na reliable/affordable/comfortable public transport ambayo itamfanya mtu aache gari yake apande public transport...kuna nchi ma-CEO wnapanda train na mabasi
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Sijawahi kuona sehemu ingine yoyote ile mimitaro mikubwa kama iliypo Dar. Kuna wakati nilikuwa nadhani labda niko peke yangu tu ninayekereka kumbe pia wapo na wengine.

Huwa najiuliza sana - hivi ni nani huyo aliyeidizaini hiyo mimitaro?

Kwa kweli hiyo mitaro ya Dar ni balaa. Na kwa jinsi ilivyowazi, basi waswahili wanaitumia kama madampo ya uchafu. Pili, ni hatari sana kwa usalama wa watembea kwa mguu na kwa magari pia.

Nimesikia wajerumani wanaojenga DART wameziba na kupunguza ukubwa wa mitaro ya barabara ya Morogoro. Ila kuna waswahili wanaona wajerumani wanachemsha kupunguza na kufunika ile mitaro. Kuna thread moja humu inaelezea hili suala.

Kuhusu emission standards, ni kweli Tanzania hakuna utaratibu wa maana, zaidi wa ule wa kuongeza VAT na ushuru kwa magari yenye umri zaidi ya miaka 10. Yaani, ukiagiza gari lililotengenezwa mwaka 2002 kwa sasa, utakumbana na maumivu hayo. Huu utaratibu ni kwani kama alivyosema Steve Dii unaweza kukuta gari ya mwaka 1990, lakini matunzo yake yanaifanya iwe na emissions kidogo kuliko na gari ya mwaka 2005!!

Hivyo utaratibu wa kuchunguza emission standards kila mwaka ni mzuri sana. Hii kazi inaweza kufanywa na private sector, kama serikali itaona ni mzigo. Yaani inakuwa ni lazima kwa kila gari kuwa na certificate ama sticker yenye kuonyesha limepita hiyo emission test.

Ingawa pia kuna jitihada kidogo katika mafuta ya gari. Kuna unleaded gasoline; haya yanakuwa hayana lead, ambayo once combusted, inakuwa ni gesi mbaya kwa mazingira. Lakini sifahamu utumikaji wa mafuta hayo; kwani nadhani ni makampuni mengi ya mafuta hayana unleaded gasoline. Nimeshaona kwa PUMA, Total na Oryx.
 
Last edited by a moderator:
Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara
mfano bidhaa za nguo

maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe
mfano Pugu

maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta

Vipodozi yote yaende mwenge......

vifaa vya kilimo Tandika.....
posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi
na maduka ya nguo tu...
maduka ya furniture yote yaende Keko..

tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar
tuige nchi zingine basi.....
ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo...

Kaka;

Wengine tulishapiga kelele hadi tukachoka. Mpaka wakubwa wanaohusika tuliwaona na maoni yetu tuliwapa, lakini "sikio la kufa halisikii dawa". You may get a modern complete solution package kwa kupitia hapa: Traffic congestion - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Kulalamika Tz hakusaidii lolote!

wala watawala hawana mpano wa kuleta mabadiliko!

May be CHADEMA iwepo madarakani!
 
Chifu The Boss tatizo la msongamano wa magari Dar, kama walivyosema wadau hapa, linasababishwa na mpangilio mbovu wa mji. Dar imepangiliwa hovyo kuliko maelezo.

Baa kila mahala, showrooms za magari hata kwenye maeneo ya makazi; viwanda kuwekwa karibu na makazi; majengo marefu kujengwa yasipostahili; ofisi za serikali kuwa sehemu moja tu; njia za kuingia Kariakoo na Posta kwa watu wanaotoka eneo fulani kuwa moja tu, kwa mfano mtu anayekaa Mwenge ana route moja kubwa ya kumfikisha Posta,Ali Hassan Road, akitumia Shekilango-Morogoro road inakuwa maumivu kwake! Vilevile watu wanaokaa Gongolamboto, Segerea, Ukonga, Tabata na Vingunguti, nao njia zao za kwenda Posta na Kariakoo ni moja tu!

Vilevile hata mfumo wa incentives za usafiri kwa watumishi waandamizi wa umma ni wa kijinga. Hapa naongelea makatibu wakuu, wakurugenzi, wakuu wa vyuo na wasaidizi wao, wakuu wa idara za serikali n.k. Hawa wote wanapewa magari yao kuwapeleka ofisini na kuwarudisha majumbani kwao!! Kwa nyakati za asubuhi, hapo Dar, magari ya wakubwa hao hujaa barabarani!!!

Nini kifanyike sasa?

Kwa hali ilivyofikia sasa hivi, huwezi epuka suala la gharama katika kuja na mipango ya kuondoa msongamano wa magari hapo Dar. Hivyo basi, haya ni baadhi ya mapendekezo yangu, ambayo yataleta matokeo chanya kama yakitekelezwa sambamba:

1. Satellite towns: hii ni katika kutoa utegemezi wa wakaazi kwa mahitaji yao mbalimbali kutoka eneo moja. Mfano, Tegeta, Mbagala, Ukonga, Mbezi Juu/Kibamba na Tabata, zaweza kuendelezwa katika kiwango cha kuweka mahala pa kupata mahitaji yote ya msingi (hususani kwa yale yafuatwayo na watu wasio watumishi wa umma Posta na Kariakoo). Huduma za kibenki naona zimekuwa zikisogezwa karibu sana na hizo 'satellite towns'. Hii itaendana na kusimamisha ujenzi wa ofisi mpya za serikali na mashirika ya umma. Mfano mzuri, upo kwa TCRA; walivyoweka ofisi zao nje ya katikati mwa jiji ni vizuri sana. Hii itakuwa hivyo kama mpango wa kuhamia Dodoma utaendelea kusuasua. Ila kutekelezwa kwa mpango huo,kutakuwa ni moja ya masuluhisho makubwa ya msongamano Dar. Pia hili litaendana na kupiga marufuku ujenzi mpya wa majengo ya ofisi za mashirika binafsi katikati ya mji; majengo kwa ajili ya kuishi tu, ndiyo yanaweza kuruhusiwa.

2. Kuweka mfumo mpya wa usafiri wa umma. Katika hili mpango wa DART utakuwa ni moja ya suluhisho. Lakini hili litafanikiwa sana likienda sambamba na pendekezo la kwanza. Kuhusu hili mengi yameandikwa humu. Mfumo ukiwa mzuri, kuwepo na sheria kali juu ya matumizi na uingizaji wa magari binafsi katikati ya mji ili kudiscourage watumiaji wa magari hayo. Mfano, kuwe na ushuru mkubwa wa kuingiza gari binafsi katikati ya mji, na parking charges kuwa aghali kwa maeneo ya katikati ya mji. Hapa ni kutengeneza disincentives za mtu kutaka kuingia down town na gari binafsi na kuweka incentives kupitia mfumo mzuri wa usafiri wa umma. Hapa katika usafiri wa umma, nchi za Skandinavia zinatupa mfano bora kabisa wa mfumo mzuri wa usafiri wa umma.

3. Kuimarisha idara za mipango miji katika manispaa za Dar. Hapa jambo kubwa ni uwajibikaji wa watumishi wa idara hizi. Hawa wanapaswa kuwa makini katika kufuatilia matumizi ya ardhi na maeneo Dar. Baa kila kona ni tatizo; kwani nyingine, hazina parking, na kukuta kingo za barabara ndizo utumika kama parking! Kwa watumishi hawa, mkono wa sheria uwe wa chuma pale wanapotenda kinyume na mpangilio wa mji.

4. Ujenzi wa parking: kama alivyosema mdau mmoja humu, ukosefu wa parking spaces nao ni chanzo cha msongamano. Hii iendane na uwepo na ufuatiliaji wa sheria yenye kutaka kila jengo la ghorofa zaidi ya tano, ni sharti liwe na parking floor(s). Na ili kuleta kukubalika, mwenye jengo ndiye atakayekuwa akikusanya ushuru wa parking spaces, kwa wale watakaokua siyo wakaazi wa jengo hilo (kama ni la makazi) na watakaokua siyo watumishi (kama ni la ofisi).

5. Kubadilika kwa tabia za matumizi ya magari kwa watu binafsi na magari ya serikali. Kwa mfano, unakuta waziri wa nishati anatoka ofisini na kutaka kwenda ofisi za jiji pale, kwa ajabu ataenda kwa gari. Hii tabia pia ipo kwa watu binafsi wanaofanya kazi downtown. Ingekuwa vyema watu wakabadili tabia hizi; kwa mizunguko ya downtown, siyo lazima kuzunguka na gari. Kutembea kwa mguu kunapaswa kuwe ndiyo tabia. Ni jambo gumu, ila linawezekana kwa polepole.

Ni haya tu kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
The Boss,

I'm not completely disagreeing with you; what I'm saying is, let's put in place infrastructure that will move people quickly from one place to another. What you're talking about is a framework called "Business Clustering", which is well and good. Our Government has already been advised to set up Government Clusters in outer periphery areas, for example, such things as tax and land rent payments, etc. We already have the ICT infrastructure to facilitate this, but as you know, BRN or not, our Government takes YEARS to implement good advice. What we need are Immediate Results Now. Big Results? Ludicrous!
 
Last edited by a moderator:
Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara
mfano bidhaa za nguo

maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe
mfano Pugu

maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta

Vipodozi yote yaende mwenge......

vifaa vya kilimo Tandika.....
posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi
na maduka ya nguo tu...
maduka ya furniture yote yaende Keko..

tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar
tuige nchi zingine basi.....
ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo...

Foleni Dar haitoisha hadi daladala zitoke na kuwe na mass transport system ambayo itakuwa owned 100% by the government
 
mh sasa si ukiwa na shopping ya multiple items utazunguka jiji zima kwa siku moja?
 
Back
Top Bottom