David Mathayo David wasifu wako ndio huu. Ya nini kuwadanganya Watanzania?

Blood Hurricane

JF-Expert Member
Jun 21, 2012
1,175
301
Jina
Jina la kwanza ni Mathayo David Msuya. Ila baada ya kuingia anga za siasa, aliamua kulibadili jina lake kuwa Mathayo David Mathayo na kuondoa jina la ukoo "Msuya" ambalo ni jina la baba yake halisi David Msuye aliyewahi kuwa waziri mkuu.

Masomo
Matayo David Msuya alisoma Tosamaganga Iringa, alifanya CBG (1989-91) aliishi bweni la Mwenge. Uwezo wake wa kimasomo haukuwa mkubwa ila alishangaza wenzanke na waalimu alipopata daraja la kwanza kwa pointi 7. Alipata msaada sana kutoka kwa kaka yake aliyekuwa akifundisha chuo cha ualimu Mkwawa, Iringa.

Matayo ulikwenda JKT itende, Mbeya. Baada ya hapo, alichanguliwa kwenda kusoma Makerere Uganda kwa kupitia mfuko wa mwalimu Nyerere. Mathayo alinufaika kwa fedha hizo ila hakwenda Uganda, akaamua kusoma SUA ya tiba ya mifugo (Bachelor of Veterinary Medicine) mwaka 1993-1997. Huko SUA Matayo alikuwa ni mwanafunzi pekee aliyekuwa na radio yenye double deck, (system) na TV set.

Uwezo wa kifedha ulisaidia kumpa Mathayo maisha ya kifahari chuoni SUA ambapo alikuwa na wasichana kadhaa ikiwa ni pamoja na Mugros na Betty Manase

Mwanzo wa siasa
Siasa alizianza rasmi mwaka 1995 alitumia TV yake kwenda kuonyesha vijijini madhara ya vyama vingi, alitumia mapigano ya Rwanda na Burundi kama kutishia wananchi wasikubali upinzani na kipindi kile wananchi walikuwa wepesi kuelewa kumbuka TV hazikuwa nyingi Tanzania kipindi kile. Alijijengea umaarufu sana ndani ya chama mkoani Morogoro na kitaifa.

Aligombea ujumbe wa NEC mkoa wa Morogoro kundi la vijana alishinda. Mathayo alimaliza SUA 1997 na kupata kazi ya kufundisha chuo kimoja huko Serowe Botswana. Kwa kuwa mjumbe wa NEC alikuwa karibu na akina Lowasa, JK na vingunge wengine aliweza kuwa anaonana na akina Makamba na akawa ni mwanamtandao. Wakati huo Matayo alikuwa akirudi Tanzania kufanya shughuli zake za kisiasa wakati bado ni mwajiriwa wa serikali ya Botswana.

Kwa mfano wakati mmoja alirudi Tanzania na kuwahamasisha wanafunzi wa SUA (kama 200 hivi) na kuwapeleka Dodoma kupokea kadi za CCM chini ya mwenyekiti wa CCM Mkapa. Wanafunzi walahidiwa wangepatiwa ajira kwa kufanya hivyo. Hii ilimjenga sana Matayo ambaye aliisha kuwa maarufu kwenye ofisi za chama Dodoma, kama mjumbe wa NEC na mkutano mkuu.

Mwaka 2000 aligombea Ubunge Same Magharibi na kushinda na kuteuliwa kuwa waziri mdogo. Wakti huu aliisha tamka kwamba amesomea Afrika Kusini digrii ya falsafa (PhD). Prof Msolla wakati aliyekuwa waziri wa elimu ya juu na sayansi ambaye aliwahi kufundisha SUA alimjua sana Matayo na alimwita Matayo na kumuuliza kuwa PhD alifanya lini na wapi na pia aletee PhD thesis yake. Prof Msolla alisema "Matayo aliogopa sana na alikili mbele yangu, kuwa Prof mimi nimetumia hii title kisiasa zaidi, sina MSc wala PhD"1.

Kashfa ya vyeti bandia
Dr Mathayo ni mmoja wa wabunge vijana waliochaguliwa na Raisi Kikwete kuwakilisha ngwe yake ya "Nguvu mpya" kama naibu waziri. Katika awamu hii Kikwete alionekana amechagua vijana wenye vipaji na elimu. Vyeti vya Mathayo's zimeleta kizaazaa tangu alipochaguliwa kwenye uwaziri mwaka 2005. Matayo alihitimu chuo kikuu cha Kilimo (SUA) mwaka 1997 kama daktari wa mifugo. Baada ya hapo alitoka nje ya nchi kwenda kutafuta ajira Botswana ambako aliajiriwa na serikali ya Botswana kama mwalimu kweny chuo cha kilimo huko Serowe.

Mathayo anadai kwa mwaka huo huo alianza digrii ya MSc 1998-2001, halafu PgDip (2000-2001), na PhD (2001-2003). Watu wengi wanaomfahamu ikiwa ni pamoja na waalimu wake wa SUA wanashangaa Mathayo aliwezaje kusomea vyeti vyote hivyo kwa muda wa miaka mitano huku akifanya kazi kama mtumishi wa serikali Botswana? Pia kashfa kwamba alikuwa akipokea mishahara miwili ya uwaziri na utumishi wa serikali ya Botswana haijajibiwa hadi leo.

Source: Waliosoma nae.
 
Mhh makubwa.mie sifahamu lolote kwa kweli kuhusu huyu Mheshimiwa.Ila shukrani kwa info.
 
Kwa mwanachama wa magamba hilo siwezi kulishangaa. Akikabwa sana koo, utasikia anajitetea kwamba uDr wake ni wa tiba za wanyama na siyo PhD. Magamba ndiyo yanayoididimiza nchi hii kwa mavyeti ya kufojifoji tu ili mradi siku zinakwenda. Ole wenu siku zenu zinayoyoma kama barafu juani. Mwisho wa siku, mtatamani mkimbilie nje ya nchi kujiokoa.
 
Hivi huyu jamaa yukoje vile? Maana kwa sura simjui uongo dhambi!!!

Mweye picha yake aiweke basi...
 
nasikia akiwa Tosa alikuwa anasoma sana pamoja na kujihusisha na mambo ya siasa. Alikuwa ni kiongozi wa umoja wa vijana wa shule ya Tosa enzi hizo.kwahiyo ile division one haikuwa ya bahati mbaya. Hata hivyo CBG used to take the best!
 
Nikweli huyu jamaa anafahamika kwa ujasiriamali kwenye kila kitu kilichombeleyake. Nakumbuka alikuwa akitumia VIDEO yake enzi hizo kwa kuonyesha mikanda yangono kwa kiingilio, wewe kama upon aye karibu muulize kisusio uoneatakavyostuka. Alinyesha mkanda wa yale maafa ya MV.Bukoba kwa kiingilio piapale multipurpose hall. Jina lake halisi ni David Mathayo Msuya ndilo alilokuwaakitumia. Na sote tulifahamu kuwa ni motto wa waziri mkuu mstaafu Mzee Cleopa DavidMsuya. Alikuwa ni kati ya wanafunzi wawili wa undergraduate wenye gari (ilailikuwa choka mbaya sana). Kuhusu Mugro naomba nilihifadhi hilo, ila ametushangazasana jinsi alivyopata PhD hiyo, na tulimsikia Spika Sitta enzi hizo akimsafishahuyu jamaa bungeni kuwa elimu yake ni ya halali. Pia kunawakati alishajiitaProfesa kwenye Nyanja za uchumi, ila hili alilipotezea hewani. Tunawasiwasisana na kushinikiza kitendgo cha accreditation cha Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania(TCU) watoe ripoti yake nzuri. Pia tunawasiwasi hata kuibiwa kwa computers nyeti pale TCU wanamweza kuwa wamehusika hawakatika kupoteza ushahidi wa kudanganya elimu zao. Pia tunawasiwasi kuwa nimmoja aliyemshawishi JK kumtosa Prof. Msola (Mbunge wa Kilolo-Iringa) asiwepokwenye uwaziri tena, kwani alipokuwa elimu ya juu alimuumbua kuwa huyu jamaahana PhD. Bahati mbaya sana vyombo vyetu vya serikali na watu wetu wa usalamahawashughuliki na kuhakiki CV za watu ambao wanakuja kupewa madaraka makubwakuliko uwezo wao na kupelekea ufanisi mbovu na kuliingizia Taifa hasara kubwa. Tumeshangaakuona tena Technician Stella Manyanya akijulikana ni Engineer na alishapewanafasi ya kuongoza Shirika la Tanesco, siajabu amechangia sana kuliuwa hilishirika. Nashauri Serikali ifanye uhakiki wav yeti kwa watumishi wote wa ummakama ilivyofanya kwa wanataaluma vyuo vikuu. Hili litasaidia kupatikana mtumwenye sifa halisi kulingana na majukumu anayopewa.
 
Lazima wewe unamfahamu vizuri na pia ulisoma naye SUA. Kwa jinsi ulivyoeleza haiwezekani source ikawa waliosomanaye maana ni 99 % true. Namfahamu Matayo ingawa siyo rafiki yangu na huyu bwana ni kweli at one time alikuwa Pretoria Msc in Animal Science na alikuwa anafanya thesis na pia ana mpango wa register for PhD Free State wakati anamalizia. Ila kitu ambacho siwezi kuthibitisha kama alimaliza hiyo PhD degree program yake maana sijaona publication yeyote kwenye google yenye jina lake. Kawaida vyuo vya RSA huwa vinapublish thesis kwenye mtandao. Halafu kitu kingine huwezi kugraduate PhD RSA bila kupublish paper!! Sasa unaweza ku-google ili kuthibitisha hilo baada ya kuandika hisia zako na kjalibu kumchafua mtu bila sababu.
 
To hell with their PHDs' and DVDs' kwani zinaliwa ili watugawie na sie??
 
Hivi huyu jamaa yukoje vile? Maana kwa sura simjui uongo dhambi!!!

Mweye picha yake aiweke basi...

Mpaka mama wa kwanza amenuna bana

MK+wa+WAMA+Mama+Salma+Kikwete+akimnadi+Mgombea+ubunge+(CCM)+Jimbo+la+Same+Magharibi+David+Mathayo.JPG
 
Jina
Jina la kwanza ni Mathayo David Msuya. Ila baada ya kuingia anga za siasa, aliamua kulibadili jina lake kuwa Mathayo David Mathayo na kuondoa jina la ukoo "Msuya" ambalo ni jina la baba yake halisi David Msuye aliyewahi kuwa waziri mkuu.

Masomo
Matayo David Msuya alisoma Tosamaganga Iringa, alifanya CBG (1989-91) aliishi bweni la Mwenge. Uwezo wake wa kimasomo haukuwa mkubwa ila alishangaza wenzanke na waalimu alipopata daraja la kwanza kwa pointi 7. Alipata msaada sana kutoka kwa kaka yake aliyekuwa akifundisha chuo cha ualimu Mkwawa, Iringa.

Matayo ulikwenda JKT itende, Mbeya. Baada ya hapo, alichanguliwa kwenda kusoma Makerere Uganda kwa kupitia mfuko wa mwalimu Nyerere. Mathayo alinufaika kwa fedha hizo ila hakwenda Uganda, akaamua kusoma SUA ya tiba ya mifugo (Bachelor of Veterinary Medicine) mwaka 1993-1997. Huko SUA Matayo alikuwa ni mwanafunzi pekee aliyekuwa na radio yenye double deck, (system) na TV set.

Uwezo wa kifedha ulisaidia kumpa Mathayo maisha ya kifahari chuoni SUA ambapo alikuwa na wasichana kadhaa ikiwa ni pamoja na Mugros na Betty Manase

Mwanzo wa siasa
Siasa alizianza rasmi mwaka 1995 alitumia TV yake kwenda kuonyesha vijijini madhara ya vyama vingi, alitumia mapigano ya Rwanda na Burundi kama kutishia wananchi wasikubali upinzani na kipindi kile wananchi walikuwa wepesi kuelewa kumbuka TV hazikuwa nyingi Tanzania kipindi kile. Alijijengea umaarufu sana ndani ya chama mkoani Morogoro na kitaifa.

Aligombea ujumbe wa NEC mkoa wa Morogoro kundi la vijana alishinda. Mathayo alimaliza SUA 1997 na kupata kazi ya kufundisha chuo kimoja huko Serowe Botswana. Kwa kuwa mjumbe wa NEC alikuwa karibu na akina Lowasa, JK na vingunge wengine aliweza kuwa anaonana na akina Makamba na akawa ni mwanamtandao. Wakati huo Matayo alikuwa akirudi Tanzania kufanya shughuli zake za kisiasa wakati bado ni mwajiriwa wa serikali ya Botswana.

Kwa mfano wakati mmoja alirudi Tanzania na kuwahamasisha wanafunzi wa SUA (kama 200 hivi) na kuwapeleka Dodoma kupokea kadi za CCM chini ya mwenyekiti wa CCM Mkapa. Wanafunzi walahidiwa wangepatiwa ajira kwa kufanya hivyo. Hii ilimjenga sana Matayo ambaye aliisha kuwa maarufu kwenye ofisi za chama Dodoma, kama mjumbe wa NEC na mkutano mkuu.

Mwaka 2000 aligombea Ubunge Same Magharibi na kushinda na kuteuliwa kuwa waziri mdogo. Wakti huu aliisha tamka kwamba amesomea Afrika Kusini digrii ya falsafa (PhD). Prof Msolla wakati aliyekuwa waziri wa elimu ya juu na sayansi ambaye aliwahi kufundisha SUA alimjua sana Matayo na alimwita Matayo na kumuuliza kuwa PhD alifanya lini na wapi na pia aletee PhD thesis yake. Prof Msolla alisema "Matayo aliogopa sana na alikili mbele yangu, kuwa Prof mimi nimetumia hii title kisiasa zaidi, sina MSc wala PhD"1.

Kashfa ya vyeti bandia

Dr Mathayo ni mmoja wa wabunge vijana waliochaguliwa na Raisi Kikwete kuwakilisha ngwe yake ya "Nguvu mpya" kama naibu waziri. Katika awamu hii Kikwete alionekana amechagua vijana wenye vipaji na elimu. Vyeti vya Mathayo's zimeleta kizaazaa tangu alipochaguliwa kwenye uwaziri mwaka 2005. Matayo alihitimu chuo kikuu cha Kilimo (SUA) mwaka 1997 kama daktari wa mifugo. Baada ya hapo alitoka nje ya nchi kwenda kutafuta ajira Botswana ambako aliajiriwa na serikali ya Botswana kama mwalimu kweny chuo cha kilimo huko Serowe.

Mathayo anadai kwa mwaka huo huo alianza digrii ya MSc 1998-2001, halafu PgDip (2000-2001), na PhD (2001-2003). Watu wengi wanaomfahamu ikiwa ni pamoja na waalimu wake wa SUA wanashangaa Mathayo aliwezaje kusomea vyeti vyote hivyo kwa muda wa miaka mitano huku akifanya kazi kama mtumishi wa serikali Botswana? Pia kashfa kwamba alikuwa akipokea mishahara miwili ya uwaziri na utumishi wa serikali ya Botswana haijajibiwa hadi leo.

Source: Waliosoma nae.

MATAYO CLEOPA DAVID MSUYA: TAMAA YA UKUBWA WA KITAALUMA YA NINI? UNAJUA UNGEWEZA KUENDELEA NA MAISHA BILA BUGHUDHA YOYOTE .WATANZANIA WANAKUAMINI. LAKINI MIMI MWENYEWE HILI LIMENITIA SIMANZI. KWANINI UKANE JINA LA UKOO WAKO

LAANA YA BABU ITAKUPATA TU. MAMBO MENGINE YASINGEJULIKANA LAKINI KUTOKANA NA KUJIKWEZA UMEUMBUKA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!. AJIKWEZAYE HUSHUSHWA. KAMA NI UONGO LETA DATA ZA KIUKWELI HAPA DOGO. SASA MAMBO HADHARANI YAANI HADI MUGROS. KWA TAARIFA MUGROS (CHEAP GIRLS) NI WASICHANA WA KAZI WALIOKUWA WAKIWAPIKIA WANAFUNZI VYUMBANI KULE SUA. SIFA YAO NI KUWA TAYARI KUONDOKA NA YEYOTE BAINA YA MAROOM MATES. SOMETIMES . MAROOMATES HUGONGANA KWA KUSINGIZIA KUTOKWENDA AU KUTOROKA DARASA; KILA 1 AKIAMUA KURUDI KWA WAKATI WAKE NA MATOKEO NI KUGONGANA. LAKINI MBAYA ZAIDI MUGROS WALIKUWA PRONE TO STI KUTOKANA NA KUCONJUGATE NA WANAFUNZI TOFAUTI UNPROTECTEDLY.KWASASA CHUO CHA SUA KILIPIGA MARUFUKU SHUGHULI ZA KUPIKIA VYUMBANI NA HIVYO KUSITISHA VIBARUA VYA MUGROS TANGU WAKATI HUO AUTOMATICALLY.
D. MSUYA, WENZIO WANASOTEA SUA 2-3 MSc, 3-6 PhD we mwenzetu unaukwaa kiulaini. kudos prof Msolla kwa kubainisha ukweli otherwise this guys would be respected undeservingly. adios amigo
 
Back
Top Bottom