A
Anonymous
Guest
Hali ya barabara ya kuelekea Baraza la Mitihani kupitia Makonde, Mbezi Juu, Dar es Salaam inasikitisha sana na nashindwa kuelewa Serikali inawaza nini kiasi cha kushindwa kabisa kuirekebisha hii barabara na hata kuiwekea lami ukizingatia inaelekea kwenye moja ya Taasisi zake kubwa kabisa
Hali ya barabara hii sio adha tu kwa Watu au Wageni wanaoenda Baraza la Mitihani bali hata kwa sisi Watumiaji wa kila siku ambao ni wa tumiaji wa barabara hii mara kwa mara. Hapa imeharibika na bado inaendelea kuharibika na mara kwa mara hali huwa hivi hivi hadi wananchi tunajichanga na kuziba viraka kwa magunia ya mchanga. Serikali ione aibu kubwa sana kuwa na Taasisi kubwa kama hii lakini hii ndio njia ya kupita kwenda kwenye ofisi hizo
Kwa kweli inakuwa ni Mtihani kufika Baraza la Mitihani. Ikumbukwe barabara hii inaenda kuungana na barabara ya lami inayotoka Mbezi Shule hadi Mbezi Mwisho kwa kupitia Goba
Hali ya barabara hii sio adha tu kwa Watu au Wageni wanaoenda Baraza la Mitihani bali hata kwa sisi Watumiaji wa kila siku ambao ni wa tumiaji wa barabara hii mara kwa mara. Hapa imeharibika na bado inaendelea kuharibika na mara kwa mara hali huwa hivi hivi hadi wananchi tunajichanga na kuziba viraka kwa magunia ya mchanga. Serikali ione aibu kubwa sana kuwa na Taasisi kubwa kama hii lakini hii ndio njia ya kupita kwenda kwenye ofisi hizo
Kwa kweli inakuwa ni Mtihani kufika Baraza la Mitihani. Ikumbukwe barabara hii inaenda kuungana na barabara ya lami inayotoka Mbezi Shule hadi Mbezi Mwisho kwa kupitia Goba