Dalili 5 za Mtoto aliyekosa umakini au uhusiano Mzuri kutoka kwa Mzazi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1709122795231.png

Anatafuta Kupewa Umakini Kila Wakati:
Mtoto huyu anakuwa ni mwenye kutaka sifa au kutambulika kwenye kila kitu hata vitu vidogo

Kuwa na Hasira za Haraka:
Mtoto anatumia hisia za Hasira katika kuonesha vile anavyojisikia ili tu apewe umakini kwenye mambo yake

Anakuwa Sio Mtulivu:
Mtoto aliyekosa uhusiano mzuri au umakini kwa mzazi, anakuwa mtukutu, anapenda kelele, sio msikivu, anavunja miongozo bila hofu kwa wazazi

Kuwa King'ang'anizi:
Mtoto anakuwa hawezi kukaa mbali na mzazi au mlezi, anakuwa na hofu ya kuachwa au kutelekezwa muda wowote

Kuonesha Tabia Mbaya Hadharani:
Mtoto aliyekosa umakini wa mzazi/mlezi haoni shida kuonesha dharau au kiburi kwa Wakubwa zake wakiwemo Wazazi wake
 
Back
Top Bottom