CV ya Dr Slaa From Certificate to PhD

Status
Not open for further replies.

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
46,962
32,345
Hapa Dr Slaa alivyokuwa mbunge hana BA wala MA lakini ana PhD

Member of Parliament CV

GENERAL
SalutationHonourableMember picture
1253.jpg
First Name: Dr. Wilbrod
Middle Name:Peter
Last Name:Slaa
Member Type:Constituency Member
Constituent:Karatu
Political Party:CHADEMA
Office Location:P.O. Box 119, Karatu - Arusha
Office Phone: +255 784 666995
Ext.:
Office Fax: +255 22 2668866
Office E-mail: wslaa@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Date of Birth 29 October 1948
EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start DateEnd DateLevel
St. Thomas Aquinas UniversityAdvanced Diploma in Rural Development19801981ADV DIPLOMA
TransWorld Tutorial College, LondonCertificate in Management19851985CERTIFICATE
Kwermusl Primary School(Mbulu)Primary Education19581960PRIMARY
Daudi Primary SchoolPrimary Education19611961PRIMARY
Karatu Primary SchoolPrimary Education19621965PRIMARY
Dung'unyi Seminary SchoolO-Level Education19661969SECONDARY
Itaga Seminary SchoolA-Level Education19701971HIGH SCHOOL
Kibosho Seminary SchoolCertificate in Philosophy19721973CERTIFICATE
St. Urban University, RomePhD (JCD) Law19771981PHD
Kipalapala SeminaryCertificate in Theology19741977CERTIFICATE
International Eye H. CentreCertificate in Eye Health19931993CERTIFICATE
EMPLOYMENT HISTORY

JF Daima...:peace:
===================
Majibu ya Dr. W. Slaa
===================

Ndahani,
Ni haki Yao kujadili. Msiwapuuze wala kuwakatisha tamaa kujadili. Inawezekana kweli wapo ambao kwa nia njema hawajui mfumo wa Elimu wa Kanisa Katoliki ambao tok a Seminary Ndogo ( Form 1-V1) nimepitia Dungunyi Seminary and Itaga Seminary of which am very proud na ninatoa shukrani za dhati kabisa kwa waalimu wangu wote si tu kwa kunipa elimu bora, Bali pia kwa kunipa misingi imara ya malezi( formation) kwani elimu bora ni zaidi ya vyeti.

Aidha si wengi wanaojua Philosophia hasa wanafundisha nini. Kwa bahati mbaya kuna watu wanadhani wameelimika na kuwa mavuvuzela kumbe hawajui kitu, ndio maana ya msemo " nusu elimu ni hatari sana". Kuna watu Leo ukiwaambia kuwa masomo ya philosophia( falsafa) yanahusu subjects muhimu Kama 1) Ethics 2) Logic 3)Epistemology 4) Cosmology 5) Metaphysics 6) Psychology na philosophy yenyewe yaani misingi ya philosophy hawaelewi unazungumzia nini na si kosa lao. Kuhoji is not an issue, issue ni je anayehoji anahitaji kujifunza au anahoji kwa ushabiki tu! This is the issue at stake!

Wako watu wanafikiria Seminary Kuu unajifunza Theolojia ( Tauhidi). Hawajui kabisa kuwa miaka 5 ya masomo ya Theolojia ni pamoja na complete course on Sociology, Anthropology, Oratory,miezi Sita ya mwisho nilipata complete course ya ukunga kwa kuwa ukiwaambia Padre vijijini wewe pia ni ambalance, hivyo lazima ujue basics za kumhudumia mama mjamzito unayemkimbiza hospital ini na kadhalika. Msomi yeyote, kabla ya kuhukumu anaanza kwa kutafuta ukweli juu ya jambo na kufanya utafiti. Prospectus ya Seminary Kuu ambazo ziko affiliated kwa vyuo vikuu mbalimbali duniani zinapatikana, hivyo hakuna msingi wa mtu kufanya guess work, labda awe tu na sababu zake na au agenda yake ambayo nintofauti na lengo la elimu ambayo ni kutafuta "full truth" ambayo nayo ni msingi wa Somo la Epistemology katika masomo ya Philosophy(Falsafa).

Katika Vyuo vikuu, ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Urbaniana ( Roma) nilikosoma Mimi, pamoja na miaka 7 ya Seminary Kuu nilizosoma (Kibosho Major Seminary/ Moshi na Kipalapala Major Seminary ambazo zilikuwa affiliated kwa Kwa Makerere University na Ndiyo maana vyetu vyangu ni vya Makerere University na Urbaniana Pontifical University Rome, 1) Nilianza na Bacclaureate ( equivalent ya BA) na kuandika Paper baada ya Course Work, na Licentiate ( Masters) nayo nikaiandikia Paper na kufaulu, ndipo nikaruhusiwa kuendelea na JCD).
2) Napennda pia kuwafahamisha kuwa wengi kwa kutokuelewa wanafikiria kuwa JCD inafundisha tu Canon Law. Pamoja na Canon Law masomo mengine ni 1) Civic Law ( ambayo ni msingi wa sheria zote inayotokana na Roman Law), 2) Family Law( ikumbukwe Kanisa Katoliki ina mfumo kamili wa ki mahakama kuanzia Courts of First Instance hadi court of Appeal ( Sacred Rota) na Supreme Court ( signature Apostolica). Huu ni mfumo kamili wa ki mahakama, kwa kawaida ukijishughulisha na maswala yote ya ndoa,na Patrimony. 3) Jurisprudence 4) comparative Law French, Commonwealth, American, Russian kwa maana nyingine all major Legal Systems worldwide. 5) International Law na branches zake zote. 6) Principles of criminal Law ( elements ambazo haiku kwenye Comparative Law na Civic Law.

Ili kufanya Desertation yangu, nilipaswa kujifunza Lugha 5 ( nje ya Kiingereza ambayo kwa wanafunzi wa English Speaking Countries inahesabiwa kuwa Mother Tongue, Latin ambayo kwa aliyetoka Seminary Kama nilivyopitia Mimi inahesabiwa Kama original language, na Hebrew ambayo pia kwa mtu aliyepitia Seminary it was taken as on Original language, japo Mimi sikuwahi kujifunza Hebrew Seminarini). Hivyo nikachagua a)Ki Italiano ambayo pia ndiyo ilikuwa Mwdium of Instruction yaani lugha ya kufundishia,b) Kijerumani c)French d) Spanish na e) Portuguese. Hata hivyo focus yangu ilikuwa kwa Italian na German na mengine matte nilijifunza kuweza kufanya research yangu, na kuniwezesha kusoma lakini Siko fluent katika kuzungumza.Hii pia ni kutokana na muda mfupi. Nilipata course ya Wiki 3 tu ya kujifunza Lugha kabla sijaingia darasani kwa masomo proper.

Nimeyaweka kwa uwazi, na ninadhani wako wanaofahamu mfumo wa masomo katika vyuo vya Kanisa Katoliki wanaweza kujazia. Wako ambao tumesoma nao was mapadre katika Pontifical Universities za Rome, Leo wanashika nafasi kubwa katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au nafasi zinging mbalimbali kwenye Taasisi mbalimbali. Kwa kuwa nilienda Roma nikiwa tayari Mkurugenzi wa Maendeleo Jimbo Katoliki la Mbulu, nikawa Nina shuttle Kati ya Pontifical University ya Urbaniana na Pontifical University ya St. Thomas Aquinas, Rome ambako nilisomea Advance Diploma ya Rural Development.
Nadhani sasa mnaweza kupima kwa vigezo hivi hoja za mleta thread hii. Mnaweza kupima nini ni puma na nini ni mchele. Mnaweza pia objectively kuangalia depth ya masomo kwa kulinganisha na propaganda nyingi zinazopigwa kwa malengo tu ya upotoshwaji na au Propaganda. Vyuo vikuu Biko kwenye mitandao, mleta thread na wengine wa aina yake wakijisumbua kidogo tu kuingia kwenye Google watapata ukweli bila kutafuniwa na mtu. Tuweke uvivu wa kufikiri pembeni tunapojadili mambo makubwa na mazito. Nafasi ya kila mmoja kujipatia Elimu bora ipo Kama watu tutakubali kujisumbua na kuacha uvivu wa kufikiri. Nchi haitaendelea kwa propaganda na otoshwaji, Taifa halitaendelea kwa wivu....shika Kitabu. Soma. Jichimbie utavuna lakini Kama utakesha kwenye mitandao kufanya Propaganda badala ya kuchota elimu bora tena ya bure kwenye mitandao utaachwa unajiozea! Nawahimiza wote wenye kupenda Taifa lao kujichimbia. Innovation ni msingi wa maendelo na Innovation haipatikani kwa majungu na umbeya inapatikana kwa wanaochimbia vichwa vyao kwenye utafiti, kujisomea na kujiendeleza. Tupende Taifa letu, uzalendo uwe kwa matendo na sio Maneno matupu.
 
Nafikiri hili lilishadiliwa hapa......mwenye link atupe....Kwa sababu tovuti ya bunge siku hizi kimeo
 
Tehe tehe watu kwa kudiscuss za wenzao wamo wakiletewa za kwao wanakuja kama wamewashwa.Kama hupendi kusemwa na wewe usiseme watu.Kwa naona ndo fashion haya mambo ya macv siyapendi manake kila thread sasa hivi ni hii mijitu
 
Ritz usiziamini hizo cv za kwenye tovuti ya bunge, zimekorogwa. Mfano fungua ya J. Makamba, itakuonyesha hata primary hajawahi kusomea.
 
Last edited by a moderator:
kuna watu cjui wanatafutwa kukunwa.....huu ni *****...weka na cv yako tuone...
 
Tehe tehe watu kwa kudiscuss za wenzao wamo wakiletewa za kwao wanakuja kama wamewashwa.Kama hupendi kusemwa na wewe usiseme watu.Kwa naona ndo fashion haya mambo ya macv siyapendi manake kila thread sasa hivi ni hii mijitu

Huo ni ugonjwa wa coma sijui cv ya nini,? Bangi zingine
 
Unless kama kichwa kimejaa matapishi, lakini thread unayoleta hapa ipo majukwaani kwa miaka sasa. Shughulisha ubongo wako, sio kumtumikia mume bila kufanya hata vetting ya analokutuma.

Hakuna haja ya kutokwa na povu hii thread ni mpya JF kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums...halafu nikukumbushe acha kulia lia JF sio mali ya Chadema.
 
Basi tumvue udokta ili udokta pekee utakaobakia utakuwa ni ule wa kupewa kwa kutumia kura ya veto na sio kukaa darasani. What difference does it make? You can be a doctor and yet you deliver nothing!
 
Hakuna haja ya kutokwa na povu hii thread ni mpya JF kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums...halafu nikukumbushe acha kulia lia JF sio mali ya Chadema.

Hii topic tulijadili sana hapa mwaka jana Ritz, na nilidhani umeelewa. Na jitahada zilitumika sana kueleza elimu ya kanisa katoloki na utoaji wa vyeti wakati wa utawala wa Nyerere. Kama kuna mtu anaweza kuirejesha thread ya zamani naomba afanye hivyo.

NB: Hii topic umerudisha ghafla baada ya kuibuka uzi unaojadili CV/elimu ya Vicky Kamata. Sijui kwa nini unaona Dr Slaa wanatakiwa kujadiliwa katika level moja?
 
As soon u're goin 2b wife of my hog..just wait,sawa na jinga jukuu lake ovu lilozaa chuki
 
Ritz usiziamini hizo cv za kwenye tovuti ya bunge, zimekorogwa. Mfano fungua ya J. Makamba, itakuonyesha hata primary hajawahi kusomea.

Kuna ya mbunge mmoja wa tabora mwanaume afu picha ya Anne Kilango.Baba akiwa dhaifu.....!!!!???
 
Last edited by a moderator:
Hakuna haja ya kutokwa na povu hii thread ni mpya JF kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums...halafu nikukumbushe acha kulia lia JF sio mali ya Chadema.
Naona umeambiwa kwenye vijiwe vyenu vya kahawa ulete cv ya dr slaa
 
... kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums....

Haya nime-copy toka kwenye mjadala wa zamani. Huu mjadala ulinzia mwanabidii ukarukia JF. Nanukuu majibu ya mdau,


"Tukianza na Kipalapala, hapa mwanafunzi anasoma form 5 & 6 pamoja na masomo ya Theology na baada ya hapo huunganisha na degrii ya theology.

Kipalapla kama ilivyo Institutions zote za Kanisa Katoliki (kwa level ya Philosophy na Theology) iiko affiliated na vyuo vikuu mbalimbali duniani kutoka nchi moja hadi nyingine.

Mfano, wanaosoma Zomba Theological College Malawi (Theology) na Kachebere Philosophical College (Philosophy) mpakani mwa Malawi na Zambia wanafuata marking scheme ya Chancellor College - University of Malawi. Kuna chuo kingine kiko Balaka Consorsium Philosophical College nadhani kiko affiliated na St Urban University, Rome.

Missionary Institute London (MIL) iko affiliated kwa Middlesex University (chuo cha serikali cha Uingereza) na Luvein University (Belgium). Wanaofuata mfumo wa Middlesex University kupata BA wanasoma miaka 3 na passmark yao ni 40%. Wanaofuata mfumo wa Luvein University kupata BA wanasoma miaka 4 na passmark yao ni 60%. Muhula unaanza Oktoba na kwisha Juni (miezi 8).

Mfumo wa kutoa final mark ni 1) class presentation na participation 2) essay writing 3) oral examination 4) defence of dissertation mbele ya internal & external examiners. Pia mtu anayepata first class, papers zake lazima ziwe marked na internal na external examiners na ajadiliwe kama anastahili first class degree na siyo tu kupata kwenye karatasi. Pia anayeshindwa, paper zake zinasahishiswa na examiners tofauti ili kuonesha kashindwa kweli au kama amepunjwa marks.

Kwa Tanzania, kwa sasa vyuo vyote kwa level ya Philosophy na Theology viko affiliated na St Urban University, Rome. Zamani, falsafa ilikuwa miaka 2 (sasa ni 3) na teolojia ilikuwa miaka 3 (sasa 4).
Mtu akimaliza (Tanzania) alikuwa anapata certificate siyo kwa sababu masomo yalikuwa level ya chini ila kwa sababu maaskofu walikuwa hawajaridhia wahitimu wao kupata digrii licha ya kuwa walikuwa wanaombwa wanafunzi wapewe magamba kama ilivyokuwa kwenye vyuo vingine. Ilichukua muda kidogo.

Lakini kama mtu aliendelea na masomo ya juu walithamanisha masomo yale kwa chuo ambacho mtu anaenda kusoma maana content ya syllabus ya masomo ya falsafa na teolojia ni (universal) kwa vyuo vyote vya Kanisa Katoliki duniani tofauti ni kwa kila nchi wanaongeza mambo yanayohusu cultural understanding ya nchi husika including its legal system.

Uganda mtu akimaliza Jinja Philosophical College (Philosophy) anapata BA katika Philosophy. Akiendelea na Theology chuo kingine, anapata BA katika Theology na kuna vyuo vingine akimaliza Theology anapata MA. Inategemea chuo kina mfumo gani na kinafundisha nini - maana kuna baadhi ya masomo kama mtu hakuyafanya wakati wa philosophy atayafanya wakati wa theology.

Kwa baadhi ya vyuo, mtu mwenye BA ya Philosphy na BA ya Theology, akiendea na masomo ya juu 'specialisation', anaenda moja kwa moja kusoma PhD kulingana na vigezo walivyoweka (mfano, vyuo ambavyo vinafundisha Philosophy na Theology kwa pamoja).
Kwa baadhi ya vyuo masomo haya yanatenganishwa - yaani, mwanafunzi anaamua ku'specialise' kwenye pure philosophy au pure theology. Na katika masomo yote mwanafunzi anafundishwa the secular view na religious view.

Maana ni hasa kumwezesha mwanafunzi kupata "solid and consistent knowledge of man, the world and God... The students should rely on that philosophical patrimony which is forever valid, but should also take account of modern philosophical studies, especially those which have greater influence in their own country, as well as recent progress in the sciences. Thus, by correctly understanding the modern mind, students will be prepared to enter into dialogue with their contemporaries." ( Vatican II, Training of Priests, Paragrapah No 15).

Kuna vyuo kama alikosoma Dr Slaa lecturers wote ni wa level ya profesa na kwenda kusoma huko mpaka uwe 'exceptional student' nadhani kama sikosei wanachukua wale tu wenye 'first class'.

Kitu kingine ninachoona kinampa wasiwasi (jina limehifadhiwa) ni pale anaposoma "Canon Law" au "Catholic Education" kwa kudhani padre anasoma tu biblia au mafundisho ya Kanisa. Mfano, Dr Slaa amespecialise katika Canon Law ambayo ndiyo mother of secular law na kusoma Canon Law ni lazima kuanza na how law developed na mpaka kuja kugawanyika into secular na religious laws.

Advantage ya Dr Slaa si tu kwamba ana'knoweldge' ya Canon Law lakini pia nini kinaitwa secular law na kwa nini - tofauti na similarities. Mfano, definitions of what is an irregurality, malice aforethought, the difference between legality and validity of an act, what is a valid marriage and a legal marriage, etc.

All Catholic Universities undertake secular studies mfano ni Catholic University of East Africa (CUEA), Kenya, ambako hata Waislamu wanasoma huko, St Augustine, Mwanza, Luvein University etc. kwa hiyo mtu akihitimu kwenye vyuo hivyo, huwa haangaliwi kuwa amesoma elimu ya dini bali kwamba ni mtaalamu katika taaluma fulani aliyoisomea.

Tofauti kwa mapadre ni kwamba mfumo wao wa mafunzo unachukua muda mrefu na wanajifunza mambo mengi - maana hadi kufikia upadre ni mpaka uwe walau umesoma miaka 10 baada ya Form VI". (mwisho wa kunukuu)


Ukitaka mjadala mzima. https://www.jamiiforums.com/jamii-intelligence/168414-kuhusu-cv-na-phd-ya-dr-slaa.html
 
Ritz usiziamini hizo cv za kwenye tovuti ya bunge, zimekorogwa. Mfano fungua ya J. Makamba, itakuonyesha hata primary hajawahi kusomea.

Mungi,

Kwani Dr Slaa, BA, MA, kasoma University gani?
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom