Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,962
- 32,345
Hapa Dr Slaa alivyokuwa mbunge hana BA wala MA lakini ana PhD
Member of Parliament CV
EMPLOYMENT HISTORY
JF Daima...eace:
===================
Majibu ya Dr. W. Slaa
===================
Member of Parliament CV
GENERAL | ||
---|---|---|
Salutation | Honourable | Member picture |
First Name: | Dr. Wilbrod | |
Middle Name: | Peter | |
Last Name: | Slaa | |
Member Type: | Constituency Member | |
Constituent: | Karatu | |
Political Party: | CHADEMA | |
Office Location: | P.O. Box 119, Karatu - Arusha | |
Office Phone: | +255 784 666995 | |
Ext.: | ||
Office Fax: | +255 22 2668866 | |
Office E-mail: | wslaa@parliament.go.tz | |
Member Status: | Current Member | |
Date of Birth | 29 October 1948 |
EDUCATION | ||||
---|---|---|---|---|
School Name/Location | Course/Degree/Award | Start Date | End Date | Level |
St. Thomas Aquinas University | Advanced Diploma in Rural Development | 1980 | 1981 | ADV DIPLOMA |
TransWorld Tutorial College, London | Certificate in Management | 1985 | 1985 | CERTIFICATE |
Kwermusl Primary School(Mbulu) | Primary Education | 1958 | 1960 | PRIMARY |
Daudi Primary School | Primary Education | 1961 | 1961 | PRIMARY |
Karatu Primary School | Primary Education | 1962 | 1965 | PRIMARY |
Dung'unyi Seminary School | O-Level Education | 1966 | 1969 | SECONDARY |
Itaga Seminary School | A-Level Education | 1970 | 1971 | HIGH SCHOOL |
Kibosho Seminary School | Certificate in Philosophy | 1972 | 1973 | CERTIFICATE |
St. Urban University, Rome | PhD (JCD) Law | 1977 | 1981 | PHD |
Kipalapala Seminary | Certificate in Theology | 1974 | 1977 | CERTIFICATE |
International Eye H. Centre | Certificate in Eye Health | 1993 | 1993 | CERTIFICATE |
JF Daima...eace:
===================
Majibu ya Dr. W. Slaa
===================
Ndahani,
Ni haki Yao kujadili. Msiwapuuze wala kuwakatisha tamaa kujadili. Inawezekana kweli wapo ambao kwa nia njema hawajui mfumo wa Elimu wa Kanisa Katoliki ambao tok a Seminary Ndogo ( Form 1-V1) nimepitia Dungunyi Seminary and Itaga Seminary of which am very proud na ninatoa shukrani za dhati kabisa kwa waalimu wangu wote si tu kwa kunipa elimu bora, Bali pia kwa kunipa misingi imara ya malezi( formation) kwani elimu bora ni zaidi ya vyeti.
Aidha si wengi wanaojua Philosophia hasa wanafundisha nini. Kwa bahati mbaya kuna watu wanadhani wameelimika na kuwa mavuvuzela kumbe hawajui kitu, ndio maana ya msemo " nusu elimu ni hatari sana". Kuna watu Leo ukiwaambia kuwa masomo ya philosophia( falsafa) yanahusu subjects muhimu Kama 1) Ethics 2) Logic 3)Epistemology 4) Cosmology 5) Metaphysics 6) Psychology na philosophy yenyewe yaani misingi ya philosophy hawaelewi unazungumzia nini na si kosa lao. Kuhoji is not an issue, issue ni je anayehoji anahitaji kujifunza au anahoji kwa ushabiki tu! This is the issue at stake!
Wako watu wanafikiria Seminary Kuu unajifunza Theolojia ( Tauhidi). Hawajui kabisa kuwa miaka 5 ya masomo ya Theolojia ni pamoja na complete course on Sociology, Anthropology, Oratory,miezi Sita ya mwisho nilipata complete course ya ukunga kwa kuwa ukiwaambia Padre vijijini wewe pia ni ambalance, hivyo lazima ujue basics za kumhudumia mama mjamzito unayemkimbiza hospital ini na kadhalika. Msomi yeyote, kabla ya kuhukumu anaanza kwa kutafuta ukweli juu ya jambo na kufanya utafiti. Prospectus ya Seminary Kuu ambazo ziko affiliated kwa vyuo vikuu mbalimbali duniani zinapatikana, hivyo hakuna msingi wa mtu kufanya guess work, labda awe tu na sababu zake na au agenda yake ambayo nintofauti na lengo la elimu ambayo ni kutafuta "full truth" ambayo nayo ni msingi wa Somo la Epistemology katika masomo ya Philosophy(Falsafa).
Katika Vyuo vikuu, ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Urbaniana ( Roma) nilikosoma Mimi, pamoja na miaka 7 ya Seminary Kuu nilizosoma (Kibosho Major Seminary/ Moshi na Kipalapala Major Seminary ambazo zilikuwa affiliated kwa Kwa Makerere University na Ndiyo maana vyetu vyangu ni vya Makerere University na Urbaniana Pontifical University Rome, 1) Nilianza na Bacclaureate ( equivalent ya BA) na kuandika Paper baada ya Course Work, na Licentiate ( Masters) nayo nikaiandikia Paper na kufaulu, ndipo nikaruhusiwa kuendelea na JCD).
2) Napennda pia kuwafahamisha kuwa wengi kwa kutokuelewa wanafikiria kuwa JCD inafundisha tu Canon Law. Pamoja na Canon Law masomo mengine ni 1) Civic Law ( ambayo ni msingi wa sheria zote inayotokana na Roman Law), 2) Family Law( ikumbukwe Kanisa Katoliki ina mfumo kamili wa ki mahakama kuanzia Courts of First Instance hadi court of Appeal ( Sacred Rota) na Supreme Court ( signature Apostolica). Huu ni mfumo kamili wa ki mahakama, kwa kawaida ukijishughulisha na maswala yote ya ndoa,na Patrimony. 3) Jurisprudence 4) comparative Law French, Commonwealth, American, Russian kwa maana nyingine all major Legal Systems worldwide. 5) International Law na branches zake zote. 6) Principles of criminal Law ( elements ambazo haiku kwenye Comparative Law na Civic Law.
Ili kufanya Desertation yangu, nilipaswa kujifunza Lugha 5 ( nje ya Kiingereza ambayo kwa wanafunzi wa English Speaking Countries inahesabiwa kuwa Mother Tongue, Latin ambayo kwa aliyetoka Seminary Kama nilivyopitia Mimi inahesabiwa Kama original language, na Hebrew ambayo pia kwa mtu aliyepitia Seminary it was taken as on Original language, japo Mimi sikuwahi kujifunza Hebrew Seminarini). Hivyo nikachagua a)Ki Italiano ambayo pia ndiyo ilikuwa Mwdium of Instruction yaani lugha ya kufundishia,b) Kijerumani c)French d) Spanish na e) Portuguese. Hata hivyo focus yangu ilikuwa kwa Italian na German na mengine matte nilijifunza kuweza kufanya research yangu, na kuniwezesha kusoma lakini Siko fluent katika kuzungumza.Hii pia ni kutokana na muda mfupi. Nilipata course ya Wiki 3 tu ya kujifunza Lugha kabla sijaingia darasani kwa masomo proper.
Nimeyaweka kwa uwazi, na ninadhani wako wanaofahamu mfumo wa masomo katika vyuo vya Kanisa Katoliki wanaweza kujazia. Wako ambao tumesoma nao was mapadre katika Pontifical Universities za Rome, Leo wanashika nafasi kubwa katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au nafasi zinging mbalimbali kwenye Taasisi mbalimbali. Kwa kuwa nilienda Roma nikiwa tayari Mkurugenzi wa Maendeleo Jimbo Katoliki la Mbulu, nikawa Nina shuttle Kati ya Pontifical University ya Urbaniana na Pontifical University ya St. Thomas Aquinas, Rome ambako nilisomea Advance Diploma ya Rural Development.
Nadhani sasa mnaweza kupima kwa vigezo hivi hoja za mleta thread hii. Mnaweza kupima nini ni puma na nini ni mchele. Mnaweza pia objectively kuangalia depth ya masomo kwa kulinganisha na propaganda nyingi zinazopigwa kwa malengo tu ya upotoshwaji na au Propaganda. Vyuo vikuu Biko kwenye mitandao, mleta thread na wengine wa aina yake wakijisumbua kidogo tu kuingia kwenye Google watapata ukweli bila kutafuniwa na mtu. Tuweke uvivu wa kufikiri pembeni tunapojadili mambo makubwa na mazito. Nafasi ya kila mmoja kujipatia Elimu bora ipo Kama watu tutakubali kujisumbua na kuacha uvivu wa kufikiri. Nchi haitaendelea kwa propaganda na otoshwaji, Taifa halitaendelea kwa wivu....shika Kitabu. Soma. Jichimbie utavuna lakini Kama utakesha kwenye mitandao kufanya Propaganda badala ya kuchota elimu bora tena ya bure kwenye mitandao utaachwa unajiozea! Nawahimiza wote wenye kupenda Taifa lao kujichimbia. Innovation ni msingi wa maendelo na Innovation haipatikani kwa majungu na umbeya inapatikana kwa wanaochimbia vichwa vyao kwenye utafiti, kujisomea na kujiendeleza. Tupende Taifa letu, uzalendo uwe kwa matendo na sio Maneno matupu.