Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Yasema ni wababaishaji wasio na agenda
:: Yawahusisha Zitto, Kiwelu na watuhumiwa EPA
:: Wao wakiri kuwa na undugu na wanaotuhumiwa
:: Mbatia naye awataja kuwa ni waongo wa hoja
Benedict Sichalwe na Eliya Mbonea
CHAMA Cha Wananchi (CUF) kimewatuhumu viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa ni mafisadi, wanafiki na waongo na hivyo hawawezi kuaminiwa na Watanzania kuongoza mageuzi ya kisiasa nchini.
Chama hicho kimeibua tuhuma hizo nzito kufuatia kauli za viongozi wa Chadema wa kitaifa na taarifa iliyotolewa na viongozi wa Chadema wa Mkoa wa Tanga kukituhumu CUF kwamba kinashirikiana na CCM kudhoofisha upinzani wa kweli.
Akizungumza na Rai katika mahojiano maalumu, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa CUF, Ismail Jussa, alisema Watanzania hawana haja ya kuelezwa ni chama kipi na viongozi wapi wamekuwa mstari wa mbele kupambana kufa kupona kuleta mabadiliko ya kisiasa Tanzania na wapi ni wanafiki.
Viongozi takribani wote wa CUF tumeonja sulubu za CCM na serikali zake katika kupigani mabadiliko. Mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti Machano Khamis, Katibu Mkuu Seif Sharif Hamad, Manaibu Katibu Mkuu, Juma Duni na Wilfred Lwakatare, Kiongozi wa Upinzani Bungeni Hamad Rashid na wajumbe wengi wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa wa CUF wamekwenda jela na hata kuchezea vipigo vya vyombo vya dola kuleta mageuzi hapa nchini. Ni kiongozi gani wa Chadema aliyejitoa muhanga kama huu kwa ajili ya Watanzania, aliuliza Jussa.
Aliongeza kwamba ni muhanga wa wanachama wa CUF wa Januari 26 na 27, 2001 uliofungua mlango wa mageuzi ya msingi ya kidemokrasia hapa nchini na kuhoji tena ni kipi cha maana kimefanywa na CHADEMA hata leo wawe na uthubutu wa kuisema CUF ni kibaraka wa CCM.
Jussa alisema ili kuongoza mageuzi ya aina yoyote yale, ni lazima wale walio mstari wa mbele kuyapigania wawakilishe taswira ya mageuzi hayo na waonekane kuwa ni tofauti na wale wanaowapinga.
Mahatma Gandhi, mmoja kati ya viongozi ninaowaheshimu sana ulimwenguni alisema Be the change you want to see (Onyesha mabadiliko unayoyataka katika nafsi yako kwanza). Sasa ni vipi mafisadi wa CHADEMA wanaweza kupambana na mafisadi wa CCM?, alihoji Jussa.
Akitoa ushahidi wa madai yake, aliwataka viongozi wa Chadema kuwaeleza Watanzania wana ushirikiano gani na watuhumiwa wa ufisadi wa EPA hadi kwenda kuwachukulia dhamana mahakamani huku wakiwadanganya wananchi kwamba wao wanapambana na ufisadi.
Viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema, Grace Kiwelu na Anthony Komu ni miongoni mwa waliowachukulia dhamana watuhumiwa wa EPA. Kabwe Zitto aliripotiwa na gazeti moja kuwa alikwenda Mahakama ya Kisutu na kunongona na Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM wa Mkoa wa Kigoma anayeitwa Maranda ambaye ni mshtakiwa pia. Alizungumza naye hadi alipopewa onyo na Hakimu na kulazimika kutoka nje. Wana siri gani hawa? aliuliza Jussa.
Hata hivyo alipozungumza gazeti hili juu ya tuhuma hizo, Mbunge wa viti maalumu Grace Kiwelu alikiri kwenda mahakamani na kumchukua Ester Komu kwa madai kuwa ni ndugu.
Ester Komu ni mtoto wa mjomba wangu, mahakamani nilikwenda kama ndugu. Hayo ni mambo mawili tofauti nawaomba CUF wasikihusishe chama changu na masuala ya undugu, alisema Kiwelu na kuongeza:
Kama wanataka wafanye uchunguzi wao ili wabaini kweli ni ndugu au siyo ndugu yangu. CUF hawana jipya zaidi ya kutapatapa baada ya kukataa kuwaunga mkono uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini, alisema Kiwelu.
Pia Zitto Kabwe alipoulizwa kuhusu kuwepo Kisutu na kuzungumza na mtuhumiwa wa EPA alisema; yeye alienda kufatilia suala la wanafunzi wa vyuo vikuu waliokuwa wameshikwa kufuatia migomo ya wanafunzi. Akiwa pale alikutana na Maranda na kisha kuamua kumsalimia kwa kuwa ni mjomba wake.
Jussa alieleza pia kwamba viongozi wa juu wa Chadema wamekuwa wakijaribu kutumia rushwa kuwarubuni viongozi mashuhuri wa CUF kukihama chama hicho na kujiunga na chama chao.
Alitaja tukio mojawapo kwamba wakiwa safarini nchini Afrika Kusini mwaka jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alimfuata mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF kutoka Mkoa wa Mara, Mustafa Wandwi, na kumuuliza iwapo alishapokea salamu zake kutoka kwa Ofisa mmoja wa CHADEMA za kumtaka ajiunge na chama hicho pamoja na mzigo wa shilingi milioni moja.
Wandwi alimjibu kwamba hakuwahi kupokea salamu wala fedha hizo. Mbowe alionekana kushangazwa. Hiyo maana yake ni kwamba fedha hizo zililiwa. Sasa hapo kuna ufisadi wa aina mbili, kwanza Mbowe kutaka kutumia rushwa kuwahonga viongozi wa CUF kukihama chama chao na pili Ofisa mwengine wa CHADEMA kuiba fedha aliyopewa kwa ajili ya kumpatia Wandwi. Hivi kweli watu wa aina hii wanataka watuaminishe kwamba wanaweza kupambana na ufisadi? aliendelea kuhoji.
Jitihada za gazeti hili kumpata Mbowe ili afafanue kuhusu tuhuma hizi hazikuzaa matunda kufuatia yeye kuwa katika mikutano ya Oparesheni Sangara lakini akaahidi kuzungumza nasi siku nyingine.
Jussa pia aliyataja matukio mengine ya kurubuni wanachama wao, yanayofanywa na CHADEMA kuwa yamekuwa yakifanywa mikoani na wilayani, ambapo viongozi wa CUF kuitwa na wale wa CHADEMA wakiwemo baadhi ya wenyeviti na makatibu wa wilaya na madiwani na kuwapa ahadi za fedha ili wahame CUF na wajiunge na CHADEMA.
Alisema Makamu Mwenyekiti wa CUF alipofanya ziara ya Mikoa ya Mwanza na Tabora mwaka jana, viongozi wa CUF wa wilaya za Mwanza mjini na Urambo wakiwamo madiwani walimweleza kwamba viongozi wa ngazi ya taifa wa CHADEMA waliwaita katika vikao vya ndani na kuwataka wajiunge na chama hicho huku wakiwaahidi fedha.
Alipoulizwa iwapo haoni kuwa hilo ni jambo la kawaida kwa viongozi wa chama kimoja cha siasa kuwashawishi viongozi na wanachama wa chama kingine kujiunga nao ili kujiimarisha, alisema hana tatizo na hilo na anaukubali kuwa ni utaratibu wa kawaida katika demokrasia ya vyama vingi. Hata hivyo, alisema tatizo siyo kushawishi bali ni kuwarubuni kwa kutoa rushwa.
Kuvutia wanachama ni jambo la kawaida lakini si kwa njia ya rushwa. Rushwa ni rushwa tu, na ufisadi ni ufisadi tu. Hauwezi kuwa haramu unapofanyika katika njia moja lakini ukawa halali ukifanywa kwa njia nyingine, alisema Jussa.
Kwa upande mwingine, alisema hata kwa hilo la kushawishiana kwa njia za kawaida linaweza kukubalika inapokuwa kila chama kinafanya mambo yake kivyake. Lakini alisisitiza kuwa CUF, CHADEMA, NCCR na TLP waliingia makubaliano ya ushirikiano na hivyo kuwafuata viongozi wa chama kimojawapo kwenda chama kingine itakuwa ni usaliti wa kisiasa kwa wale unaoshirikiana nao.
Akitoa mfano wa hilo, Jussa alisema Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto, alimfuata Mbunge wa Chake Chake wa CUF, Fatma Maghimbi, na kumtaka aachane na CUF na kujiunga na CHADEMA.
Akizungumzia juu ya madai ya Jussa, mara baada ya kumpata Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na kudai asingeweza kutolea ufafanua maswali hayo kulingana na eneo alilokuwa, Rai ilimtafuta Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe ambapo alitoa ufafanuzi wa madai hayo akisema siku zote chama chake kimekuwa kikifanya mikutano yenye lengo la kupata wanachama wapya na si wanachama wa kununua kama ilivyodaiwa na CUF.
CHADEMA haina fedha za kununua watu inapata ruzuku Sh. milioni 60 kwa mwezi wakati CUF wanapata Sh. milioni 170 ukiangalia nani anaweza kuwa na fedha za kununua watu. CUF hawataki siku zote kuona vyama vingine vya siasa vikikua hususani CHADEMA, wamejigeuza wao wana hati miliki ya upinzani, alisema Zitto
Akizungumzia suala la kutowaunga mkono Mbeya vijini Naibu Katibu Mkuu huyo alitanabaisha wazi kwamba tangu awali katika mazungumzo waliyoyafanya CUF hawakuonyesha ushirikiano
Hawa CUF wanapolalamika eti tuwaunge mkono Mbeya vijijini kwa vile wanakubalika siyo kweli tukiwa kwenye Oparesheni Sangara tumefika kila mahali, kama ni chama kinachopaswa kulalamika kuungwa mkono ni TLP kwani kila tulipokuwa tukiingia tunakuta wapo,alisema Zitto na kuongeza:
Kama utakumbuka mwaka 2005 NCCR- Mageuzi waliiwekea CUF pingamizi Zanzibar kwa kitendo hicho CUF ilihamasisha wananchi wapige kura za maruhani. CHADEMA tumekataa kuwaunga mkono lakini hatujawaambia wananchi wapigie kura za maruhani wala kuwaambia wananchi wasipige kura, alisema Zitto.
Akijibu madai ya kuzungumza na Fatma Magimbi, Zitto alisema ni kweli alizungumza na mama huyo Machi 2005 akiwa ametumwa na chama chake kwa lengo la kutafuta mwanamke kutoka Visiwani atakayeweza kusimama kwa nafasi ya mgombea mwenza wa chama chao.
Si kuzungumza Magimbi pekee yake nilizungumza pia na Naila Jidawi na mwanamke mwingine ninayemkumba kwa jina moja la Ruaida. Lengo letu lilikuwa ni kutaka kuwa na makamu wa rais mwanamke kutoka Zanzibar. Tena wakati huo nilikuwa kijana mdogo sikuwa na wadhifa wowote ndani ya chama nilikuwa na miaka 28, alisema Zitto.
Akifafanua zaidi juu ya suala la Mwananchi Gold Mining na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kuwatetea Zitto alisema mpaka sasa hajaona tuhuma zozote juu ya kampuni ya Mwananchi kujihusisha na ufisadi.
Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati za Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, BoT, Kampuni ya Mwananchi gold mining, pamoja na wengine wote hawa wanaripoti kwenye kamati nimechunguza na kufuatulia kwa kina sijaona mahali wana tuhuma za ufisadi.
Mpaka hivi sasa sijaona chochote cha kuishitaki Mwananchi Gold Mining sijaona chochote cha kushitaki juu ya Jaji Warioba hata kimoja. Nilikutana na BoT, NBC wakanielekezea kuhusu Mwananchi nimekaa na Jaji Warioba kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge mimi si mwanasiasa wa aina ya kwamba kwa vile nipo upinzani basi nipinge tuu, hapana ni mwanasiasa ninayetaka baadaye nije kuwa na heshima katika kuitumia nchi yangu kwa hiyo sitakiwi kumuonea wala kumpendelea mtu, alisema Zitto.
Hakuna rushwa kwenye Mwananchi Gold Mining ilikuwa na malengo mazuri kabisa kwa taifa hili. Ndani ya Mwananchi kuna matatizo madogo madogo ya kawaida tu ambayo ukiingia hata maeneo mengine utayakuta,
Akielezea juu ya Mkapa alisema wapo watu wengi wametaka kiongozi huyo mstaafu aondolewe kinga ya kutoshitakiwa.
Uzoefu unaonyesha si kila nchi zote duniani zilizowaondolea kinga marais wao wastaafu zilifanikiwa. Kwa jambo hili nasema tusiingie kichwakichwa kwa kumuondolea Mkapa kinga, lazima tujiulize je, kuna tija kwa upande wa taifa kuondoa kinga ya rais mstaafu? alihoji Zitto na kuongeza:
Lazima ukumbuke rais mstaafu alifanya mambo mengi sana kwa taifa sasa tunau hakika wa kile tunachokiamini. Nimuhimu tukaelewa kwamba Rais Mkapa si sawa na Mramba, Yona wala Babu Seya. Mkapa ni Rais mstaafu aliyetia saini mtu kunyongwa. Katika hili lazima tuwe na uhakika wa kile tunachotaka kukifanya kwa taifa letu kama kina tija yoyote, alisema Zitto.
Hata hivyo Jussa aliendelea kukituhuma chama hicho kwa kusema kwamba kama mtu akitaka kujua CHADEMA hawana agenda ya kisiasa yenye malengo yanayoeleweka katika mapambano dhidi ya ufisadi bali wanawalaghai Watanzania tu, aangalie undumila kuwili katika suala hilo.
Hebu angalia karibu vitendo vingi vya ufisadi vilivyoibuliwa vilifanywa wakati wa utawala wa Rais Benjamin Mkapa. Watanzania wanapodai kwa nguvu kuwa Rais mstaafu Mkapa aondoshewe kinga ya Kikatiba na baadaye aweze kushtakiwa, Zitto ananukuliwa na Nipashe akisema haungi mkono kumshtaki Mkapa kwa sababu hatua hiyo haitokuwa ufumbuzi wa matatizo ya ufisadi, alibainisha.
Jussa anataja mfano mwingine wa undumila kuwili wa viongozi wa CHADEMA kuwa ni pale Zitto huyo huyo alipojitokeza hadharani kumtetea Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, kwamba hahusiki na ufisadi wa Kampuni ya Mwananchi Gold na kwamba iwapo atakamatwa kwa tuhuma hizo, yeye (Zitto) yuko tayari kumtetea kwa njia zozote na hata kumchukulia dhamana.
Huyu Zitto na wenzake wamekuwa siku zote wakitaka watuhumiwa wa rushwa wafikishwe mahakamani na kwamba Mahakama iachiwe kuamua hatima yao. Kwa kweli, kwa wengine wamefikia hata kuwahukumu kwenye majukwaa ya kisiasa kabla hata hawajafikishwa mahakamani. Kwa nini sasa inapokuja kwa Jaji Warioba hawataki kuiachia Mahakama ifanye kazi yake na wanajaribu kuiingilia hata kabla kesi hiyo haijafikishwa huko? Au wanataka kutuambia kuwa Mwananchi Gold ni safi? alishangaa Jussa. Akizungumzia malumbano kati ya CUF na Chadema kuhusiana na uchaguzi mdogo wa kujaza kiti cha ubunge kilicho wazi cha Mbeya Vijijini, Jussa alisema hakutegemea kama Zitto angefikia hatua ya kusema uongo hadharani kwamba Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, hakuwahi kumuandikia barua Mbowe kumuomba chama chake kimuunge mkono mgombea wa CUF.
Jussa alitoa nakala ya barua ambayo Lipumba alimuandikia Mbowe pamoja na ushahidi wa kupokelewa barua hiyo Makao Makuu ya CHADEMA kwa njia ya dispatch book (kitabu cha kutia sahihi kuthibitisha kupokelewa barua).
Wakati huo huo; Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia amesema hoja za kwamba chama chake ni kibaraka inatokana na umasikini wa mawazo ya wanasiasa wababaishaji ambao si wakweli.
Akizungumza kwa simu na RAI wiki hii, Mbatia alisema kwamba tatizo kubwa unaolikabili taifa la Tanzania kwa sasa ni umaskini mkubwa wa fikra na hoja walizonazo wanasiasa hasa wanaotumia uongo kama mtaji wa siasa.
Mbatia alisema; Sifa ya kiongozi mwoga ni uongo. Watu hawasemi ukweli na hilo linatokana na tatizo kubwa linalolikabili taifa ambalo ni umasikini mkubwa wa fikra na mawazo ya wanasoasa wanaotumia uongo kuwadanganya Watanzania.
Mwenyekiti huyo alisema wakati alitoa hoja yake kama maoni yake juu ya suala la kuwapo kwa Tume ya maridhiano kama njia muafaka ya kulinusuru taifa katika sakata la ufisadi, hoja hiyo imegeuzwa kwa kutaka kumfanya aonekane ni kibaraka wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Sasa tunapokuwa na hoja kama hizo zinazozuia watu kutoa maoni yao, nini manna ya haki ya kujieleza ambayo ni ya kikatiba kwa kila mtu kuwa nayo? alihoji Mbatia.
Akizungumzia juu ya ushirikiano na vyama vingine vya kambi ya upinzani, Mbatia alikanusha kwa chama chake kuwa kibaraka dhidi ya vyama vingine hasa katika uchaguzi.
Mwaka 2000 mgombea wa CUF (Chama cha Wananchi) alimwekea pingamizi mgombea wa NCCR na mwaka 2003 wagombea wa NCCR waliwawekea pingamizi wagombea wa CUF kule Pemba. Pamoja na hiyo kuwa haki za wagombea, lakini iligeuzwa na kupotoshwa kuwa mimi ndiye niliyeiwekea pingamizi CUF, alisema Mbatia na kuongeza;
Jambo la msingi ambalo Watanzania wanapaswa kuelewa ni kuwa wagombea wanapochuana katika nafasi za kuomba kura, haki ya kuwekeana pingamizi ni ya msingi kama utagundua udhaifu wa wagombea wenzako ili kupunguza kazi ya ushindi.
:: Yawahusisha Zitto, Kiwelu na watuhumiwa EPA
:: Wao wakiri kuwa na undugu na wanaotuhumiwa
:: Mbatia naye awataja kuwa ni waongo wa hoja
Benedict Sichalwe na Eliya Mbonea
CHAMA Cha Wananchi (CUF) kimewatuhumu viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa ni mafisadi, wanafiki na waongo na hivyo hawawezi kuaminiwa na Watanzania kuongoza mageuzi ya kisiasa nchini.
Chama hicho kimeibua tuhuma hizo nzito kufuatia kauli za viongozi wa Chadema wa kitaifa na taarifa iliyotolewa na viongozi wa Chadema wa Mkoa wa Tanga kukituhumu CUF kwamba kinashirikiana na CCM kudhoofisha upinzani wa kweli.
Akizungumza na Rai katika mahojiano maalumu, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa CUF, Ismail Jussa, alisema Watanzania hawana haja ya kuelezwa ni chama kipi na viongozi wapi wamekuwa mstari wa mbele kupambana kufa kupona kuleta mabadiliko ya kisiasa Tanzania na wapi ni wanafiki.
Viongozi takribani wote wa CUF tumeonja sulubu za CCM na serikali zake katika kupigani mabadiliko. Mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti Machano Khamis, Katibu Mkuu Seif Sharif Hamad, Manaibu Katibu Mkuu, Juma Duni na Wilfred Lwakatare, Kiongozi wa Upinzani Bungeni Hamad Rashid na wajumbe wengi wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa wa CUF wamekwenda jela na hata kuchezea vipigo vya vyombo vya dola kuleta mageuzi hapa nchini. Ni kiongozi gani wa Chadema aliyejitoa muhanga kama huu kwa ajili ya Watanzania, aliuliza Jussa.
Aliongeza kwamba ni muhanga wa wanachama wa CUF wa Januari 26 na 27, 2001 uliofungua mlango wa mageuzi ya msingi ya kidemokrasia hapa nchini na kuhoji tena ni kipi cha maana kimefanywa na CHADEMA hata leo wawe na uthubutu wa kuisema CUF ni kibaraka wa CCM.
Jussa alisema ili kuongoza mageuzi ya aina yoyote yale, ni lazima wale walio mstari wa mbele kuyapigania wawakilishe taswira ya mageuzi hayo na waonekane kuwa ni tofauti na wale wanaowapinga.
Mahatma Gandhi, mmoja kati ya viongozi ninaowaheshimu sana ulimwenguni alisema Be the change you want to see (Onyesha mabadiliko unayoyataka katika nafsi yako kwanza). Sasa ni vipi mafisadi wa CHADEMA wanaweza kupambana na mafisadi wa CCM?, alihoji Jussa.
Akitoa ushahidi wa madai yake, aliwataka viongozi wa Chadema kuwaeleza Watanzania wana ushirikiano gani na watuhumiwa wa ufisadi wa EPA hadi kwenda kuwachukulia dhamana mahakamani huku wakiwadanganya wananchi kwamba wao wanapambana na ufisadi.
Viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema, Grace Kiwelu na Anthony Komu ni miongoni mwa waliowachukulia dhamana watuhumiwa wa EPA. Kabwe Zitto aliripotiwa na gazeti moja kuwa alikwenda Mahakama ya Kisutu na kunongona na Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM wa Mkoa wa Kigoma anayeitwa Maranda ambaye ni mshtakiwa pia. Alizungumza naye hadi alipopewa onyo na Hakimu na kulazimika kutoka nje. Wana siri gani hawa? aliuliza Jussa.
Hata hivyo alipozungumza gazeti hili juu ya tuhuma hizo, Mbunge wa viti maalumu Grace Kiwelu alikiri kwenda mahakamani na kumchukua Ester Komu kwa madai kuwa ni ndugu.
Ester Komu ni mtoto wa mjomba wangu, mahakamani nilikwenda kama ndugu. Hayo ni mambo mawili tofauti nawaomba CUF wasikihusishe chama changu na masuala ya undugu, alisema Kiwelu na kuongeza:
Kama wanataka wafanye uchunguzi wao ili wabaini kweli ni ndugu au siyo ndugu yangu. CUF hawana jipya zaidi ya kutapatapa baada ya kukataa kuwaunga mkono uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini, alisema Kiwelu.
Pia Zitto Kabwe alipoulizwa kuhusu kuwepo Kisutu na kuzungumza na mtuhumiwa wa EPA alisema; yeye alienda kufatilia suala la wanafunzi wa vyuo vikuu waliokuwa wameshikwa kufuatia migomo ya wanafunzi. Akiwa pale alikutana na Maranda na kisha kuamua kumsalimia kwa kuwa ni mjomba wake.
Jussa alieleza pia kwamba viongozi wa juu wa Chadema wamekuwa wakijaribu kutumia rushwa kuwarubuni viongozi mashuhuri wa CUF kukihama chama hicho na kujiunga na chama chao.
Alitaja tukio mojawapo kwamba wakiwa safarini nchini Afrika Kusini mwaka jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alimfuata mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF kutoka Mkoa wa Mara, Mustafa Wandwi, na kumuuliza iwapo alishapokea salamu zake kutoka kwa Ofisa mmoja wa CHADEMA za kumtaka ajiunge na chama hicho pamoja na mzigo wa shilingi milioni moja.
Wandwi alimjibu kwamba hakuwahi kupokea salamu wala fedha hizo. Mbowe alionekana kushangazwa. Hiyo maana yake ni kwamba fedha hizo zililiwa. Sasa hapo kuna ufisadi wa aina mbili, kwanza Mbowe kutaka kutumia rushwa kuwahonga viongozi wa CUF kukihama chama chao na pili Ofisa mwengine wa CHADEMA kuiba fedha aliyopewa kwa ajili ya kumpatia Wandwi. Hivi kweli watu wa aina hii wanataka watuaminishe kwamba wanaweza kupambana na ufisadi? aliendelea kuhoji.
Jitihada za gazeti hili kumpata Mbowe ili afafanue kuhusu tuhuma hizi hazikuzaa matunda kufuatia yeye kuwa katika mikutano ya Oparesheni Sangara lakini akaahidi kuzungumza nasi siku nyingine.
Jussa pia aliyataja matukio mengine ya kurubuni wanachama wao, yanayofanywa na CHADEMA kuwa yamekuwa yakifanywa mikoani na wilayani, ambapo viongozi wa CUF kuitwa na wale wa CHADEMA wakiwemo baadhi ya wenyeviti na makatibu wa wilaya na madiwani na kuwapa ahadi za fedha ili wahame CUF na wajiunge na CHADEMA.
Alisema Makamu Mwenyekiti wa CUF alipofanya ziara ya Mikoa ya Mwanza na Tabora mwaka jana, viongozi wa CUF wa wilaya za Mwanza mjini na Urambo wakiwamo madiwani walimweleza kwamba viongozi wa ngazi ya taifa wa CHADEMA waliwaita katika vikao vya ndani na kuwataka wajiunge na chama hicho huku wakiwaahidi fedha.
Alipoulizwa iwapo haoni kuwa hilo ni jambo la kawaida kwa viongozi wa chama kimoja cha siasa kuwashawishi viongozi na wanachama wa chama kingine kujiunga nao ili kujiimarisha, alisema hana tatizo na hilo na anaukubali kuwa ni utaratibu wa kawaida katika demokrasia ya vyama vingi. Hata hivyo, alisema tatizo siyo kushawishi bali ni kuwarubuni kwa kutoa rushwa.
Kuvutia wanachama ni jambo la kawaida lakini si kwa njia ya rushwa. Rushwa ni rushwa tu, na ufisadi ni ufisadi tu. Hauwezi kuwa haramu unapofanyika katika njia moja lakini ukawa halali ukifanywa kwa njia nyingine, alisema Jussa.
Kwa upande mwingine, alisema hata kwa hilo la kushawishiana kwa njia za kawaida linaweza kukubalika inapokuwa kila chama kinafanya mambo yake kivyake. Lakini alisisitiza kuwa CUF, CHADEMA, NCCR na TLP waliingia makubaliano ya ushirikiano na hivyo kuwafuata viongozi wa chama kimojawapo kwenda chama kingine itakuwa ni usaliti wa kisiasa kwa wale unaoshirikiana nao.
Akitoa mfano wa hilo, Jussa alisema Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto, alimfuata Mbunge wa Chake Chake wa CUF, Fatma Maghimbi, na kumtaka aachane na CUF na kujiunga na CHADEMA.
Akizungumzia juu ya madai ya Jussa, mara baada ya kumpata Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na kudai asingeweza kutolea ufafanua maswali hayo kulingana na eneo alilokuwa, Rai ilimtafuta Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe ambapo alitoa ufafanuzi wa madai hayo akisema siku zote chama chake kimekuwa kikifanya mikutano yenye lengo la kupata wanachama wapya na si wanachama wa kununua kama ilivyodaiwa na CUF.
CHADEMA haina fedha za kununua watu inapata ruzuku Sh. milioni 60 kwa mwezi wakati CUF wanapata Sh. milioni 170 ukiangalia nani anaweza kuwa na fedha za kununua watu. CUF hawataki siku zote kuona vyama vingine vya siasa vikikua hususani CHADEMA, wamejigeuza wao wana hati miliki ya upinzani, alisema Zitto
Akizungumzia suala la kutowaunga mkono Mbeya vijini Naibu Katibu Mkuu huyo alitanabaisha wazi kwamba tangu awali katika mazungumzo waliyoyafanya CUF hawakuonyesha ushirikiano
Hawa CUF wanapolalamika eti tuwaunge mkono Mbeya vijijini kwa vile wanakubalika siyo kweli tukiwa kwenye Oparesheni Sangara tumefika kila mahali, kama ni chama kinachopaswa kulalamika kuungwa mkono ni TLP kwani kila tulipokuwa tukiingia tunakuta wapo,alisema Zitto na kuongeza:
Kama utakumbuka mwaka 2005 NCCR- Mageuzi waliiwekea CUF pingamizi Zanzibar kwa kitendo hicho CUF ilihamasisha wananchi wapige kura za maruhani. CHADEMA tumekataa kuwaunga mkono lakini hatujawaambia wananchi wapigie kura za maruhani wala kuwaambia wananchi wasipige kura, alisema Zitto.
Akijibu madai ya kuzungumza na Fatma Magimbi, Zitto alisema ni kweli alizungumza na mama huyo Machi 2005 akiwa ametumwa na chama chake kwa lengo la kutafuta mwanamke kutoka Visiwani atakayeweza kusimama kwa nafasi ya mgombea mwenza wa chama chao.
Si kuzungumza Magimbi pekee yake nilizungumza pia na Naila Jidawi na mwanamke mwingine ninayemkumba kwa jina moja la Ruaida. Lengo letu lilikuwa ni kutaka kuwa na makamu wa rais mwanamke kutoka Zanzibar. Tena wakati huo nilikuwa kijana mdogo sikuwa na wadhifa wowote ndani ya chama nilikuwa na miaka 28, alisema Zitto.
Akifafanua zaidi juu ya suala la Mwananchi Gold Mining na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kuwatetea Zitto alisema mpaka sasa hajaona tuhuma zozote juu ya kampuni ya Mwananchi kujihusisha na ufisadi.
Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati za Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, BoT, Kampuni ya Mwananchi gold mining, pamoja na wengine wote hawa wanaripoti kwenye kamati nimechunguza na kufuatulia kwa kina sijaona mahali wana tuhuma za ufisadi.
Mpaka hivi sasa sijaona chochote cha kuishitaki Mwananchi Gold Mining sijaona chochote cha kushitaki juu ya Jaji Warioba hata kimoja. Nilikutana na BoT, NBC wakanielekezea kuhusu Mwananchi nimekaa na Jaji Warioba kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge mimi si mwanasiasa wa aina ya kwamba kwa vile nipo upinzani basi nipinge tuu, hapana ni mwanasiasa ninayetaka baadaye nije kuwa na heshima katika kuitumia nchi yangu kwa hiyo sitakiwi kumuonea wala kumpendelea mtu, alisema Zitto.
Hakuna rushwa kwenye Mwananchi Gold Mining ilikuwa na malengo mazuri kabisa kwa taifa hili. Ndani ya Mwananchi kuna matatizo madogo madogo ya kawaida tu ambayo ukiingia hata maeneo mengine utayakuta,
Akielezea juu ya Mkapa alisema wapo watu wengi wametaka kiongozi huyo mstaafu aondolewe kinga ya kutoshitakiwa.
Uzoefu unaonyesha si kila nchi zote duniani zilizowaondolea kinga marais wao wastaafu zilifanikiwa. Kwa jambo hili nasema tusiingie kichwakichwa kwa kumuondolea Mkapa kinga, lazima tujiulize je, kuna tija kwa upande wa taifa kuondoa kinga ya rais mstaafu? alihoji Zitto na kuongeza:
Lazima ukumbuke rais mstaafu alifanya mambo mengi sana kwa taifa sasa tunau hakika wa kile tunachokiamini. Nimuhimu tukaelewa kwamba Rais Mkapa si sawa na Mramba, Yona wala Babu Seya. Mkapa ni Rais mstaafu aliyetia saini mtu kunyongwa. Katika hili lazima tuwe na uhakika wa kile tunachotaka kukifanya kwa taifa letu kama kina tija yoyote, alisema Zitto.
Hata hivyo Jussa aliendelea kukituhuma chama hicho kwa kusema kwamba kama mtu akitaka kujua CHADEMA hawana agenda ya kisiasa yenye malengo yanayoeleweka katika mapambano dhidi ya ufisadi bali wanawalaghai Watanzania tu, aangalie undumila kuwili katika suala hilo.
Hebu angalia karibu vitendo vingi vya ufisadi vilivyoibuliwa vilifanywa wakati wa utawala wa Rais Benjamin Mkapa. Watanzania wanapodai kwa nguvu kuwa Rais mstaafu Mkapa aondoshewe kinga ya Kikatiba na baadaye aweze kushtakiwa, Zitto ananukuliwa na Nipashe akisema haungi mkono kumshtaki Mkapa kwa sababu hatua hiyo haitokuwa ufumbuzi wa matatizo ya ufisadi, alibainisha.
Jussa anataja mfano mwingine wa undumila kuwili wa viongozi wa CHADEMA kuwa ni pale Zitto huyo huyo alipojitokeza hadharani kumtetea Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, kwamba hahusiki na ufisadi wa Kampuni ya Mwananchi Gold na kwamba iwapo atakamatwa kwa tuhuma hizo, yeye (Zitto) yuko tayari kumtetea kwa njia zozote na hata kumchukulia dhamana.
Huyu Zitto na wenzake wamekuwa siku zote wakitaka watuhumiwa wa rushwa wafikishwe mahakamani na kwamba Mahakama iachiwe kuamua hatima yao. Kwa kweli, kwa wengine wamefikia hata kuwahukumu kwenye majukwaa ya kisiasa kabla hata hawajafikishwa mahakamani. Kwa nini sasa inapokuja kwa Jaji Warioba hawataki kuiachia Mahakama ifanye kazi yake na wanajaribu kuiingilia hata kabla kesi hiyo haijafikishwa huko? Au wanataka kutuambia kuwa Mwananchi Gold ni safi? alishangaa Jussa. Akizungumzia malumbano kati ya CUF na Chadema kuhusiana na uchaguzi mdogo wa kujaza kiti cha ubunge kilicho wazi cha Mbeya Vijijini, Jussa alisema hakutegemea kama Zitto angefikia hatua ya kusema uongo hadharani kwamba Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, hakuwahi kumuandikia barua Mbowe kumuomba chama chake kimuunge mkono mgombea wa CUF.
Jussa alitoa nakala ya barua ambayo Lipumba alimuandikia Mbowe pamoja na ushahidi wa kupokelewa barua hiyo Makao Makuu ya CHADEMA kwa njia ya dispatch book (kitabu cha kutia sahihi kuthibitisha kupokelewa barua).
Wakati huo huo; Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia amesema hoja za kwamba chama chake ni kibaraka inatokana na umasikini wa mawazo ya wanasiasa wababaishaji ambao si wakweli.
Akizungumza kwa simu na RAI wiki hii, Mbatia alisema kwamba tatizo kubwa unaolikabili taifa la Tanzania kwa sasa ni umaskini mkubwa wa fikra na hoja walizonazo wanasiasa hasa wanaotumia uongo kama mtaji wa siasa.
Mbatia alisema; Sifa ya kiongozi mwoga ni uongo. Watu hawasemi ukweli na hilo linatokana na tatizo kubwa linalolikabili taifa ambalo ni umasikini mkubwa wa fikra na mawazo ya wanasoasa wanaotumia uongo kuwadanganya Watanzania.
Mwenyekiti huyo alisema wakati alitoa hoja yake kama maoni yake juu ya suala la kuwapo kwa Tume ya maridhiano kama njia muafaka ya kulinusuru taifa katika sakata la ufisadi, hoja hiyo imegeuzwa kwa kutaka kumfanya aonekane ni kibaraka wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Sasa tunapokuwa na hoja kama hizo zinazozuia watu kutoa maoni yao, nini manna ya haki ya kujieleza ambayo ni ya kikatiba kwa kila mtu kuwa nayo? alihoji Mbatia.
Akizungumzia juu ya ushirikiano na vyama vingine vya kambi ya upinzani, Mbatia alikanusha kwa chama chake kuwa kibaraka dhidi ya vyama vingine hasa katika uchaguzi.
Mwaka 2000 mgombea wa CUF (Chama cha Wananchi) alimwekea pingamizi mgombea wa NCCR na mwaka 2003 wagombea wa NCCR waliwawekea pingamizi wagombea wa CUF kule Pemba. Pamoja na hiyo kuwa haki za wagombea, lakini iligeuzwa na kupotoshwa kuwa mimi ndiye niliyeiwekea pingamizi CUF, alisema Mbatia na kuongeza;
Jambo la msingi ambalo Watanzania wanapaswa kuelewa ni kuwa wagombea wanapochuana katika nafasi za kuomba kura, haki ya kuwekeana pingamizi ni ya msingi kama utagundua udhaifu wa wagombea wenzako ili kupunguza kazi ya ushindi.