Weston Songoro
JF-Expert Member
- Feb 17, 2014
- 2,793
- 1,083
Chama cha Wananchi, CUF kimeendelea kusambaratishwa Tanzania Bara. Maelfu kwa maelfu ya wafuasi wake wameendelea kukikimbia chama hicho na kujiunga na chama kubwa, CCM. Safari hii ni zamu ya vijana zaidi ya 300 walioachana na CUF na kujiunga na CCM ambapo kwa sasa wameamua kuchapa kazi kupitia kikundi chao za ujasiriamali kinachojishughulisha na kilimo cha mbogamboga.
Wanachama hao wamepokelewa na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Anastazia Wambura alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo.
Vijana hao wamesema kuwa wakati wanajiunga na CUF walishawishiwa kipindi ambacho kulikuwa na vuguvugu la gesi. Kwa sasa ukweli wameuona na wameamua kuachana na vyama vya kitapeli na kilaghai.
Chanzo: TBC1 Habari
Wanachama hao wamepokelewa na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Anastazia Wambura alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo.
Vijana hao wamesema kuwa wakati wanajiunga na CUF walishawishiwa kipindi ambacho kulikuwa na vuguvugu la gesi. Kwa sasa ukweli wameuona na wameamua kuachana na vyama vya kitapeli na kilaghai.
Chanzo: TBC1 Habari