Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wapinzani wamsihi Mbowe
Kambi ya upinzani isiyo rasmi bungeni imemuandikia barua Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuomba wachaguliwe kuunda Baraza la Mwaziri Kivuli kwenye Bunge ili waweze kushirikiana kwa dhati kama kambi ya upinzani.
Katika barua ya kambi hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Hamad Rashid na katibu wake David Kafulila kwenda kwa Mwenyekiti wa Chadema wamesema wanaomba ushirikiano huo uanze kwenye Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza Februari mwaka huu.
Kambi hiyo ilimsihi Mbowe kuunda kambi ya upinzani imara ikishirikisha vyama vyote vya upinzani ili kuimarisha nguvu ya upinzani bungeni na kuibana serikali ya CCM kwa pamoja.
Vyama vilivyotoa ombi hilo ni CUF chenye wabunge 33, NCCR Mageuzi chenye wabunge wanne, TLP mbunge mmoja na UDP mbunge mmoja wakati Chadema kikiwa na wabunge 47.
Chadema ambacho ndicho chama kikuu cha upinzani kimeunda kambi ya upinzani peke yake huku mwenyekiti wake akichaguliwa kuwa kiongozi wa kambi hiyo na nafasi nyingine za mawaziri kivuli zikijazwa na wabunge wa chama hicho pekee ..
Habari zaidi katika Mwananchi Jumapili.
Kambi ya upinzani isiyo rasmi bungeni imemuandikia barua Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuomba wachaguliwe kuunda Baraza la Mwaziri Kivuli kwenye Bunge ili waweze kushirikiana kwa dhati kama kambi ya upinzani.
Katika barua ya kambi hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Hamad Rashid na katibu wake David Kafulila kwenda kwa Mwenyekiti wa Chadema wamesema wanaomba ushirikiano huo uanze kwenye Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza Februari mwaka huu.
Kambi hiyo ilimsihi Mbowe kuunda kambi ya upinzani imara ikishirikisha vyama vyote vya upinzani ili kuimarisha nguvu ya upinzani bungeni na kuibana serikali ya CCM kwa pamoja.
Vyama vilivyotoa ombi hilo ni CUF chenye wabunge 33, NCCR Mageuzi chenye wabunge wanne, TLP mbunge mmoja na UDP mbunge mmoja wakati Chadema kikiwa na wabunge 47.
Chadema ambacho ndicho chama kikuu cha upinzani kimeunda kambi ya upinzani peke yake huku mwenyekiti wake akichaguliwa kuwa kiongozi wa kambi hiyo na nafasi nyingine za mawaziri kivuli zikijazwa na wabunge wa chama hicho pekee ..
Habari zaidi katika Mwananchi Jumapili.