CUF Mtaliwa wote, tafuteni suluhu! Shauri yenu!

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,429
CUF acheni kutunishiana misuli, wenye hekima tushaona mnavyoenda mnaenda kubaya wote na sasa tunaona ipo haja ya kuwashauri kwa hekma ili muweze kunusurika.

Kimsingi kwa mtu yeyote ambaye ni mdau wa demokrasia, hawezi kufurahia kuona migogoro ndani ya vyama vya siasa ambayo inatishia kuviua vyama hivyo. Kwa mantiki hiyo, umefika muda sasa wa wadau wa demokrasia kuwasaidia CUF kupata suluhu ya mgogoro unaowakabili. Aidha, kwa kuwa CUF ni chama cha upinzani, vyama vingine vya upinzani vina jukumu la kuwasaidia CUF kufikia Suluhu kuliko mtu mwingine yeyote.

HATARI ILIYOPO KAMA MGOGORO HUU UTAENDELEA KAMA ULIVYO;
Ikiwa, mgogoro huu utaendelea kama ulivyo bila kusuluhishwa kwa njia za kidiplomasia, madhara ya fuatayo yanatarajiwa kujitokeza.
1. Kuzidi kwa chuki miongoni mwa wana CUF wenyewe kwa wenyewe hasa chuki kati ya wana CUF wa zanzbar/ pemba dhidi ya wale wa Bara.

2. Kuzidi kwa chuki ambayo haiwezi kuwa na faidia kwa yoyote kati ya Prof. Lipumba na Maalim.
3. Kwa upande mmoja CUF ya maalim Seif itakufa kwa kukosa uungwaji mkono wa kitaasisi na kisheria (kutokana na position ya mgogoro kwa sasa) na kwa upande mwingine CUF ya Lipumba itakufa vile vile kwa kukosa uungwaji mkono wa kutosha Zanzibar lakini pia kwa kukosa "Cause and Purpose" bara. CUF itapoteza wabunge wengi toka pande zote. Kwa hiyo wakiendelea hivi matokea yanatarajiwa kuwa "Zero sum game" kwa pande zote.

NINI CHA KUFANYA;
Kwa kuanzia,
1.Tunaziomba pande zote (Maalim na Prof. Lipumba) kwanza waache kutoleana kauli kali na za kuudhi ambazo zitaendelea kuleta uhasama.

2. Maalim aitishe vyombo vya habari akiwa pemba na kueleza wafuasi wake kuwa yuko tayari kufikia maridhiano na prof. Lipumba na Lipumba aitishe Press Dar akieleza utayari wake wa kufikia maridhiano na Maalim.

3. ACT (kwa sababu wanaweza kuaminika na pande zote), wawasaidie CUF kuwatafutia msuluhishi ambaye anaaminika na pande zote ambaye kwa haraka sana ataita wajumbe wa pande zote na kuanza hatua za maridhiano, kwa kuangalia uwezekano wa Lipumba kuendelea kuwa Mwenyekiti na Maalim kuwa Katibu kama ilivyokuwa awali.

MSULUHISHI
Napendekeza Msuluhishi awe ni Shekhe, Maalim Ally Basalleh wa dar es salaam. Hii ni kwa sababu kwa sasa kitu pekee kinachowaunganisha Lipumba na Seif ni dini, wote wanamfahamu vizuri Basalleh na wamekuwa wakiswali nyuma yake mara kwa mara. Aidha Shekhe basalleh ni msomi, mtu mzima, muelewa na mwenye busara kubwa sana.Naamini suluhu itafikiwa.

Nawatakieni suluhu njema.
 
Ushauri mzuri.

Kwa upande wangu nashauri Maalim Seif ahamie chadema pamoja na wabunge wake , na chadema wamuachie Maalim seif chadema upande wa visiwani ambapo ataweka wagombea wake anaowataka yaani aliotoka nao cuf.Hii itazididha uimara wa chadema na upinzani kwa ujumla.

Hasara yake Cuf itakufa.Lakini hata Maalim asipohama bado cuf itakufa tu maana sioni Lipumba akilegeza kamba wakati huo Maalim kabanwa
 
Ushauri mzuri.

Kwa upande wangu nashauri Maalim Seif ahamie chadema pamoja na wabunge wake , na chadema wamuachie Maalim seif chadema upande wa visiwani ambapo ataweka wagombea wake anaowataka yaani aliotoka nao cuf.Hii itazididha uimara wa chadema na upinzani kwa ujumla.

Hasara yake Cuf itakufa.Lakini hata Maalim asipohama bado cuf itakufa tu maana sioni Lipumba akilegeza kamba wakati huo Maalim kabanwa
Nadhani hii ndio tiba haswaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri mzuri.

Kwa upande wangu nashauri Maalim Seif ahamie chadema pamoja na wabunge wake , na chadema wamuachie Maalim seif chadema upande wa visiwani ambapo ataweka wagombea wake anaowataka yaani aliotoka nao cuf.Hii itazididha uimara wa chadema na upinzani kwa ujumla.

Hasara yake Cuf itakufa.Lakini hata Maalim asipohama bado cuf itakufa tu maana sioni Lipumba akilegeza kamba wakati huo Maalim kabanwa
Niamini CDM na CUF zina wenyewe, na Maalim Seif anapenda kujimilikisha chama, madaraka, na nguvu ya kufanya maamuzi ambayo atakalo yeye ndio lifanyike. Na CDM kuna mafahari kadhaa tayari, Lowassa, Lissu na Mbowe. Kumuongeza fahari mwingine (i.e Seif) ni kwenda kukitibua chama kingine cha upinzani. Kati ya wote hao Mbowe mjanja sana.
 
KAMA TUNAVYOJUA CUF YENYE NGUVU NI YA MAALIM.

HATA LIPUMBA AFANYE NINI HAWEZI KUPUNGUZA NGUVU YA CUF ZANZIBAR.

LIPUMBA ANAATHIRI NGUVU YA UPINZANI BARA

KAMA KWELI WAPINZANI WANA NIA YA KUIONDOA CCM MADARAKANI 2020 MUHIMU NI

1. WAACHANE NA CUF NA LIPUMBA WAKE.

2. WAPINZANI WAANZISHE MCHAKATO WA KUUNGANI VYAMA VYAO NA KUPATA CHAMA KIPYA KIKUBWA CHA UPINZANI NCHINI. NA KIWE TAYARI KWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019.

3. HATA HIVYO KWA MASLAHI YA UMMA NA WANANCHI MAALIM NA VYAMA VINGINE VYA UPINZANI BARA NA ILI TUWAAMINI KUWA NA WAO HAWAKO KWA AJILI YA MATUMBO YAO KAMA LIPUMBA NI WAZIMA WAFANYE MAAMUZI MAGUMU, HADI MWAKANI MWEZI KAMA HUU WANAPASWA WAWE WESHAJIPANGA KUJIUZULU NA KUHAMIA CHAMA KIMOJA KIPYA CHA UPINZANI NA WAINGIE KWENYE KINYANG'ANYIRO UCHAGUZI MDOGO.

4. MWISHO LAZIMA VYAMA VYA UPINZANI WAELEWE KUWA HAWAKUPATA KURA NYINGI KWA SABABU YA LOWASA NO, MBONA NLD NA NCCR WAHAKUWA NA KURA NYINGI..... VIONGOZI WANAPASWA KUFAHAMU KUWA WANANCHI WALIICHOKA NA BADO WAMEICHOKA CCM. LAKINI MARA HII WANANCHI WATAPATA NGUVU IKIWA WAPINZANI WATAONGESA KUWA WANAAMUA KUSUCRIFY NA WAO KWA KUACHA PESA NA KUANZA UPYA HARAKATI ZA KUMUONDOA MKOLONI CCM.. NA NJIA KEPEE NI WAO KUANZISHA CHAMA KIMOJA NA SIASA ILI HATIMAE WAVIACHE VYAMA VYAO NA KIJIUNGA NA CHAMA KIMOJA KIPYA.. KAMA NI UKAWA AU RAINBOW, JUBILEE SAWA TU
 
KAMA TUNAVYOJUA CUF YENYE NGUVU NI YA MAALIM.

HATA LIPUMBA AFANYE NINI HAWEZI KUPUNGUZA NGUVU YA CUF ZANZIBAR.

LIPUMBA ANAATHIRI NGUVU YA UPINZANI BARA
mkuu, kama CUF wasipotafuta suluhu, inakufa safari hii, si bara si visiwani tutabakia kuisoma kwenye vitabu vya historia. Kwa sasa ishu ni kuinusuru CUF isife na wala sio kushinda uchaguzi 2020. Upinzani kwa ssa wako very disorganized hawawezi kushinda 2020. Unasema waungane wawe kitu kimoja, shida kila chama kina power mongers tena ambao ni myopic! kama kungekuwa na visionary leaders humo tungewaona wakipambana kusuluhisha mgogoro wa CUF. kama ni vyama vya upinzani kuungana, wangeshaungana toka kitambo, kwa kuwa sababu za kuungana zilikuwepo toka kitambo
 
Ushauri mzuri.

Kwa upande wangu nashauri Maalim Seif ahamie chadema pamoja na wabunge wake , na chadema wamuachie Maalim seif chadema upande wa visiwani ambapo ataweka wagombea wake anaowataka yaani aliotoka nao cuf.Hii itazididha uimara wa chadema na upinzani kwa ujumla.

Hasara yake Cuf itakufa.Lakini hata Maalim asipohama bado cuf itakufa tu maana sioni Lipumba akilegeza kamba wakati huo Maalim kabanwa
unashauri msaliti aachiwe brand name "CUF" ??
 
Tena nimekumbuka Maalim keshakichimbia kaburi CUF kwa kauli yake ya kuwapa matumaini wazanzibar kuwa KWA KUWA ALISHINDA 2015 basi muda si mrefu ataapishwa. Kama hatoapishwa hadi 2020, na ilivyo hatoapiswa....... manake wazanzibar watakuwa weshakatishwa tamaa na kupiga kura wengi watasusa kuendelea kupiga kura na matokeo yake chama twawala kitaendele kutawala

mkuu, kama CUF wasipotafuta suluhu, inakufa safari hii, si bara si visiwani tutabakia kuisoma kwenye vitabu vya historia. Kwa sasa ishu ni kuinusuru CUF isife na wala sio kushinda uchaguzi 2020. Upinzani kwa ssa wako very disorganized hawawezi kushinda 2020. Unasema waungane wawe kitu kimoja, shida kila chama kina power mongers tena ambao ni myopic! kama kungekuwa na visionary leaders humo tungewaona wakipambana kusuluhisha mgogoro wa CUF. kama ni vyama vya upinzani kuungana, wangeshaungana toka kitambo, kwa kuwa sababu za kuungana zilikuwepo toka kitambo
 
Kiukweli hali ya CUF ni mbaya sana..

Mpaka Prof Lipumba ameamua kufukuza wabunge 8 wa Maalim maana yake hiki CUF hivi sasa kipo shimoni...

Sasa Ndugai akiingia tu kwenye mtego wa kuwafukuza ( likely to be),CUF ndio basi tena.
 
Kiukweli hali ya CUF ni mbaya sana..

Mpaka Prof Lipumba ameamua kufukuza wabunge 8 wa Maalim maana yake hiki CUF hivi sasa kipo shimoni...

Sasa Ndugai akiingia tu kwenye mtego wa kuwafukuza ( likely to be),CUF ndio basi tena.
Ila yaani kuna miujiza kwenye hii nchi! yaani wapinzania wanategemea tena hekima za Spika ndugai huyu huyu ambaye wamekuwa wakimlaumu muda wote ndio awanusuru? sijui kwa nini hawasaidiani wao kwa wao angalau ndio wakashindwa? yaani wako kimya kana kwamba hakuna kinachotokea halafu siku spika akisema ameamua kuyafanyika kazi maombi na nafasi ziko wazi wataanza kumlaumu anaua upinzani. yaani ni maajabu kweli.
 
KAMA TUNAVYOJUA CUF YENYE NGUVU NI YA MAALIM.

HATA LIPUMBA AFANYE NINI HAWEZI KUPUNGUZA NGUVU YA CUF ZANZIBAR.

LIPUMBA ANAATHIRI NGUVU YA UPINZANI BARA

KAMA KWELI WAPINZANI WANA NIA YA KUIONDOA CCM MADARAKANI 2020 MUHIMU NI

1. WAACHANE NA CUF NA LIPUMBA WAKE.

2. WAPINZANI WAANZISHE MCHAKATO WA KUUNGANI VYAMA VYAO NA KUPATA CHAMA KIPYA KIKUBWA CHA UPINZANI NCHINI. NA KIWE TAYARI KWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019.

3. HATA HIVYO KWA MASLAHI YA UMMA NA WANANCHI MAALIM NA VYAMA VINGINE VYA UPINZANI BARA NA ILI TUWAAMINI KUWA NA WAO HAWAKO KWA AJILI YA MATUMBO YAO KAMA LIPUMBA NI WAZIMA WAFANYE MAAMUZI MAGUMU, HADI MWAKANI MWEZI KAMA HUU WANAPASWA WAWE WESHAJIPANGA KUJIUZULU NA KUHAMIA CHAMA KIMOJA KIPYA CHA UPINZANI NA WAINGIE KWENYE KINYANG'ANYIRO UCHAGUZI MDOGO.

4. MWISHO LAZIMA VYAMA VYA UPINZANI WAELEWE KUWA HAWAKUPATA KURA NYINGI KWA SABABU YA LOWASA NO, MBONA NLD NA NCCR WAHAKUWA NA KURA NYINGI..... VIONGOZI WANAPASWA KUFAHAMU KUWA WANANCHI WALIICHOKA NA BADO WAMEICHOKA CCM. LAKINI MARA HII WANANCHI WATAPATA NGUVU IKIWA WAPINZANI WATAONGESA KUWA WANAAMUA KUSUCRIFY NA WAO KWA KUACHA PESA NA KUANZA UPYA HARAKATI ZA KUMUONDOA MKOLONI CCM.. NA NJIA KEPEE NI WAO KUANZISHA CHAMA KIMOJA NA SIASA ILI HATIMAE WAVIACHE VYAMA VYAO NA KIJIUNGA NA CHAMA KIMOJA KIPYA.. KAMA NI UKAWA AU RAINBOW, JUBILEE SAWA TU


kwa UTAWALA HUU MSAJILI KAMWE HATAKISAJILI HICHO CHAMA KIPYA, YAANI WAPINZANI WATAKUWA WAMEJITOA KWENYE KINYANG'ANYILO WENYEWE
 
Ila yaani kuna miujiza kwenye hii nchi! yaani wapinzania wanategemea tena hekima za Spika ndugai huyu huyu ambaye wamekuwa wakimlaumu muda wote ndio awanusuru? sijui kwa nini hawasaidiani wao kwa wao angalau ndio wakashindwa? yaani wako kimya kana kwamba hakuna kinachotokea halafu siku spika akisema ameamua kuyafanyika kazi maombi na nafasi ziko wazi wataanza kumlaumu anaua upinzani. yaani ni maajabu kweli.


Mkuu unaongea kama upo Kenya vile ,eti wapinzani hawaongei, spika akitajwa moto ,ukitaja Rais moto zaidi na kupewa kesi ya uchochezi.

Kwa mfano naomba uvae viatu vyao ungefanyaje? Chadema wameshaingilia mara nyingi wakazodolewa ,tena walitaka wakamtoe kabisa Lipumba Biguruni ,we mwenyewe shahidi kilichotekea .Kwa kifupi wabunge waongeaji wote chadema tayari wanakesi si chini ya 4 kila mtu.Labda Zitto na Mbatia wasio na kesi wabebe jukumu hilo
 
Mkuu unaongea kama upo Kenya vile ,eti wapinzani hawaongei, spika akitajwa moto ,ukitaja Rais moto zaidi na kupewa kesi ya uchochezi.

Kwa mfano naomba uvae viatu vyao ungefanyaje? Chadema wameshaingilia mara nyingi wakazodolewa ,tena walitaka wakamtoe kabisa Lipumba Biguruni ,we mwenyewe shahidi kilichotekea .Kwa kifupi wabunge waongeaji wote chadema tayari wanakesi si chini ya 4 kila mtu.Labda Zitto na Mbatia wasio na kesi wabebe jukumu hilo
Wewe, kwa hiyo spika na rais ndio wanawafanya msichikue hatua yoyote? Ningefanya je kwani hapa nimefanya je?

usitembee juu ya ardhi kwa majivuno
 
KAMA TUNAVYOJUA CUF YENYE NGUVU NI YA MAALIM.

HATA LIPUMBA AFANYE NINI HAWEZI KUPUNGUZA NGUVU YA CUF ZANZIBAR.

LIPUMBA ANAATHIRI NGUVU YA UPINZANI BARA

KAMA KWELI WAPINZANI WANA NIA YA KUIONDOA CCM MADARAKANI 2020 MUHIMU NI

1. WAACHANE NA CUF NA LIPUMBA WAKE.

2. WAPINZANI WAANZISHE MCHAKATO WA KUUNGANI VYAMA VYAO NA KUPATA CHAMA KIPYA KIKUBWA CHA UPINZANI NCHINI. NA KIWE TAYARI KWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019.

3. HATA HIVYO KWA MASLAHI YA UMMA NA WANANCHI MAALIM NA VYAMA VINGINE VYA UPINZANI BARA NA ILI TUWAAMINI KUWA NA WAO HAWAKO KWA AJILI YA MATUMBO YAO KAMA LIPUMBA NI WAZIMA WAFANYE MAAMUZI MAGUMU, HADI MWAKANI MWEZI KAMA HUU WANAPASWA WAWE WESHAJIPANGA KUJIUZULU NA KUHAMIA CHAMA KIMOJA KIPYA CHA UPINZANI NA WAINGIE KWENYE KINYANG'ANYIRO UCHAGUZI MDOGO.

4. MWISHO LAZIMA VYAMA VYA UPINZANI WAELEWE KUWA HAWAKUPATA KURA NYINGI KWA SABABU YA LOWASA NO, MBONA NLD NA NCCR WAHAKUWA NA KURA NYINGI..... VIONGOZI WANAPASWA KUFAHAMU KUWA WANANCHI WALIICHOKA NA BADO WAMEICHOKA CCM. LAKINI MARA HII WANANCHI WATAPATA NGUVU IKIWA WAPINZANI WATAONGESA KUWA WANAAMUA KUSUCRIFY NA WAO KWA KUACHA PESA NA KUANZA UPYA HARAKATI ZA KUMUONDOA MKOLONI CCM.. NA NJIA KEPEE NI WAO KUANZISHA CHAMA KIMOJA NA SIASA ILI HATIMAE WAVIACHE VYAMA VYAO NA KIJIUNGA NA CHAMA KIMOJA KIPYA.. KAMA NI UKAWA AU RAINBOW, JUBILEE SAWA TU
Mzee hapa kinachosisitizwa ni maridhiano. Kwa siasa zetu za kibongobongo hakuna chama kilicho salama. Kila chama kina mapungufu yake, leo Maalimu anaweza kuchomoka CUF na kwenda CDM akajikuta anapoteza raha zake za kifikra. Je tumeshasahau yale maneno ya mgombea mwenza wa uchaguzi wa 2015 baada ya kutoka CDM? Unayakumbuka maneno yake?
Sote twafahamu nguvu alizotumia Maalimu Seif kuijenga CUF. Ametumia nguvu kubwa sana na sehemu kubwa sana ya uhai wake. Hakuna anayeweza kuzibeza. Tuanafahamu nguvu alizonazo Maalimu pale CUF. Hivi inashindikana nini wakaelewana na kuanza kutumia njia na taratibu za kichama ili kumuondoa msaliti? Inafika mahala hata wao wote unaweza kuwatilia mashaka. Hivi Maalimu anashindwa kutumia nguvu halali za kichama ili kumuondoa Lipumba? Au wanatuzeveza?
Hapo mwisho unawashawishi wanasiasa waanzishe chama kimoja, ni ngumu sana. Kila mwanasiasa ana mitizamo yake.Wanaweza kuungana na ukashangaa watakavyosambaratisha hicho chama, tena bila aibu na matokeo yake kila mtu atasemwa ni pandikizi, au umesahau mtiti wa NCCR- Mageuzi? Umemsahau Mabere Marando na Mrema walivyosambaratisha chama?
Labda tungekuwa na katiba inayoruhusu vyama kuungana wakati wa uchaguzi kama wenzetu na jirani zetu wa Kenya. Njaa mbaya mjomba, njaa haina adabu!
Ndio maana nasema haya ya CUF yanahitaji maridhiano na wala hayahitaji hasira.
 
Wanajamvi salaam!

Kufuatia taarifa ya spika iliyotolewa leo ambayo inaeleza kwamba spika amejiridhisha kwamba wabunge nane waliokuwa wana muunga mkono Maalim Seif wamefukuzwa uanachama hivyo kukosa sifa za kuwa wabunge.

Kwa kuwa kazi imebaki kwa msajili na tume kujaza nafasi zilizo wazi.

Na kwa kuwa utaratibu wa kujaza nafasi husika unajulikana na unafanywa kwa tume kuteua miongoni mwa majina ambayo yalikwisha pendekezwa na chama kabla ya uchaguzi.

Na kwa kuwa Maalim Seif ndiye aliyependekeza hayo majina ambayo yapo tume ya uchaguzi.

Namshauri Maalim Seif awatafute wanachama wote ambao majina yao yalikwisha kupendekezwa tume ambao ndiyo watakuja kujaza nafasi zilizo wazi ili kuhakikisha anaongea nao na anapata uungwaji mkono la sivyo timu lipumba ikishawateka itazidi kuimarika zaidi na zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom