mchakachuaji192
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 366
- 68
Minael Msuya
CHAMA cha Wananchi CUF, kimemshauri Rais Jakaya Kikwete kuacha kupoteza muda mwingi kwenda nje ya nchi kutafuta wawekezaji na badala yake atafute uvumbuzi wa tatizo la umeme.
Kwa mujibu wa CUF, Serikali imeshindwa kubuni vyanzo mbalimbali vya kufua umeme na kusababisha nchi kuwa katika hali mbaya kiuchumi kutokana na mgawo wa umeme uliopo na kupunguza ajira nchini.
Akizungumza na wanahabari mjini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Julius Mtatiro alisema Serikali imeshindwa kueleza ukweli kuhusu tatizo la umeme badala yake inatoa sababu zisizo za msingi na kwamba ahadi za miradi ya kuzalisha takribani Megawati 1,300 za umeme ni uongo na haiwezi kutekelezeka.
Mgawo wa umeme ni tatizo la taifa kama wanavyosema viongozi wa Serikali ya CCM, athari zake ni kubwa mno kwa wananchi na hata katika uzalishaji wa uchumi wa nchi, alisema Mtatiro.
Alisema: Hapo hapo Serikali inashindwa kueleza kwamba imezidiwa kutokana na mahitaji makubwa ya huduma ya umeme kuliko uzalishaji badala yake inasema mabwawa hayajajaa, mitambo imeharibika, mafuta yayamekwisha, sababu ambazo hazina msingi wowote kwa nchi inayohesabu miaka 50 tangu kupata uhuru,.
Mtatiro alisema tatizo la umeme nchini haliwezi kumalizika kama Serikali haitaweza kubuni vyanzo mbadala vya kufua umeme kwa kuwa mahitaji ya umeme ni zaidi ya Megawati 3,000 na unaozalishwa ni Megawati 800.
Kwa maana nyingine Rais anapotafuna fedha za umma kwa safari za nje kila kukicha, kiguu na njia kuonana na wawekezaji na kuwashawishi waje kuwekeza Tanzania anawahadaa na kuwadanganya, alisema Mtatiro.
Alisema watendaji walioko ndani ya Serikali wanaogopa kuanzisha vyanzo vipya vya umeme asili kutokana na kukosa miradi ya kukatiwa asilimia 10.
Mtatiro alisema Waziri wa Nishati na Madini, Wiliam Ngeleja anapaswa kujiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia Shirika la Umeme Tanesco na kazi yake kupewa kiongozi mwingine ambaye ataiondoa nchi katika tatizo la mgawo wa umeme usiokwisha.
Alisema vipo vyanzo mbadala vinavyoweza kufua umeme na kwamba maeneo ya maporomoko ya maji yanaweza kufua umeme wa megawati 5,000 ukilinganisha na uwezo wa sasa wa megawati 562 .
Vyanzo vingine ni makaa ya mawe ambayo yamesgunduliwa na yanaweza kufua umeme wa megawati 1,000 kwa zaidi ya miaka 50 ijayo, Gesi ya Mnazi Bay inaweza kufua pia umeme wa megawati 1,000, Madini ya Uranium na umeme wa jua na upepo vitaweza kupunguza tatizo hili, alisema.
CHAMA cha Wananchi CUF, kimemshauri Rais Jakaya Kikwete kuacha kupoteza muda mwingi kwenda nje ya nchi kutafuta wawekezaji na badala yake atafute uvumbuzi wa tatizo la umeme.
Kwa mujibu wa CUF, Serikali imeshindwa kubuni vyanzo mbalimbali vya kufua umeme na kusababisha nchi kuwa katika hali mbaya kiuchumi kutokana na mgawo wa umeme uliopo na kupunguza ajira nchini.
Akizungumza na wanahabari mjini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Julius Mtatiro alisema Serikali imeshindwa kueleza ukweli kuhusu tatizo la umeme badala yake inatoa sababu zisizo za msingi na kwamba ahadi za miradi ya kuzalisha takribani Megawati 1,300 za umeme ni uongo na haiwezi kutekelezeka.
Mgawo wa umeme ni tatizo la taifa kama wanavyosema viongozi wa Serikali ya CCM, athari zake ni kubwa mno kwa wananchi na hata katika uzalishaji wa uchumi wa nchi, alisema Mtatiro.
Alisema: Hapo hapo Serikali inashindwa kueleza kwamba imezidiwa kutokana na mahitaji makubwa ya huduma ya umeme kuliko uzalishaji badala yake inasema mabwawa hayajajaa, mitambo imeharibika, mafuta yayamekwisha, sababu ambazo hazina msingi wowote kwa nchi inayohesabu miaka 50 tangu kupata uhuru,.
Mtatiro alisema tatizo la umeme nchini haliwezi kumalizika kama Serikali haitaweza kubuni vyanzo mbadala vya kufua umeme kwa kuwa mahitaji ya umeme ni zaidi ya Megawati 3,000 na unaozalishwa ni Megawati 800.
Kwa maana nyingine Rais anapotafuna fedha za umma kwa safari za nje kila kukicha, kiguu na njia kuonana na wawekezaji na kuwashawishi waje kuwekeza Tanzania anawahadaa na kuwadanganya, alisema Mtatiro.
Alisema watendaji walioko ndani ya Serikali wanaogopa kuanzisha vyanzo vipya vya umeme asili kutokana na kukosa miradi ya kukatiwa asilimia 10.
Mtatiro alisema Waziri wa Nishati na Madini, Wiliam Ngeleja anapaswa kujiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia Shirika la Umeme Tanesco na kazi yake kupewa kiongozi mwingine ambaye ataiondoa nchi katika tatizo la mgawo wa umeme usiokwisha.
Alisema vipo vyanzo mbadala vinavyoweza kufua umeme na kwamba maeneo ya maporomoko ya maji yanaweza kufua umeme wa megawati 5,000 ukilinganisha na uwezo wa sasa wa megawati 562 .
Vyanzo vingine ni makaa ya mawe ambayo yamesgunduliwa na yanaweza kufua umeme wa megawati 1,000 kwa zaidi ya miaka 50 ijayo, Gesi ya Mnazi Bay inaweza kufua pia umeme wa megawati 1,000, Madini ya Uranium na umeme wa jua na upepo vitaweza kupunguza tatizo hili, alisema.