Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,150
Jumanne Feb 17, 2009
Habari za Kitaifa Habari zaidi!
COTWU yapinga likizo bila malipo ATCL
Basil Msongo
Daily News; tuesday,February 17, 2009 @19:56
Habari nyingine
Waliokutwa na vyeti haramu Mzumbe wavisafisha
Dawa mpya ya malaria yazinduliwa
Anayedaiwa kuuza mtoto aenda kupimwa akili
Gari lenye maiti laua mtu mmoja
Viongozi Dodoma wapewa somo
COTWU yapinga likizo bila malipo ATCL
Tanzania yathamini misaada ya China
Masha kushitaki magazeti ya IPP Media
Mshitakiwa III alia na Zombe
SMZ, China kuwawezesha wafanyabiashara
Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi Tanzania (COTWU) kimepinga mpango wa uongozi wa Kampuni ya Ndege (ATCL) kuwapeleka wafanyakazi likizo bila malipo, ingawa wako tayari kuachishwa kazi.
Taarifa kutoka ndani ya kampuni hiyo zilisema leo kuwa uongozi wa Cotwu ATCL ulitoa msimamo huo kwa Mkurugenzi Mkuu, David Mattaka, katika mkutano uliofanyika leo Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa juu wa Cotwu tawi la ATCL ambaye hakuta jina lake liandikwe gazetini, alisema hawakukubaliana chochote na Mattaka, hivyo walimwomba idhini ya kukutana na wafanyakazi leo, ombi ambalo alilikubali.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika mkutano huo, Mattaka aliwaeleza viongozi hao kwamba kinachofanywa na uongozi wa kampuni ni agizo la Serikali la kutaka kupunguzwa kwa idadi ya wafanyakazi ili iweze kujiendesha kwa ufanisi.
Hata hivyo, wafanyakazi kupitia chama chao, walimweleza Mattaka kuwa wako tayari kuachishwa kazi lakini wanapinga kwenda likizo bila malipo kwa kuwa sheria za kazi hazitambui hilo. Gazeti hili halikuweza kumpata Mattaka kuzungumzia suala hili. Ijumaa iliyopita, wafanyakazi hao walipinga mapendekezo ya kutakiwa kwenda likizo bila malipo baada ya kuelezwa na uongozi kwamba kampuni haiwezi kujiendesha kwa idadi ya sasa ya wafanyakazi na haina fedha za kuwaachisha kazi.
Habari za Kitaifa Habari zaidi!
COTWU yapinga likizo bila malipo ATCL
Basil Msongo
Daily News; tuesday,February 17, 2009 @19:56
Habari nyingine
Waliokutwa na vyeti haramu Mzumbe wavisafisha
Dawa mpya ya malaria yazinduliwa
Anayedaiwa kuuza mtoto aenda kupimwa akili
Gari lenye maiti laua mtu mmoja
Viongozi Dodoma wapewa somo
COTWU yapinga likizo bila malipo ATCL
Tanzania yathamini misaada ya China
Masha kushitaki magazeti ya IPP Media
Mshitakiwa III alia na Zombe
SMZ, China kuwawezesha wafanyabiashara
Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi Tanzania (COTWU) kimepinga mpango wa uongozi wa Kampuni ya Ndege (ATCL) kuwapeleka wafanyakazi likizo bila malipo, ingawa wako tayari kuachishwa kazi.
Taarifa kutoka ndani ya kampuni hiyo zilisema leo kuwa uongozi wa Cotwu ATCL ulitoa msimamo huo kwa Mkurugenzi Mkuu, David Mattaka, katika mkutano uliofanyika leo Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa juu wa Cotwu tawi la ATCL ambaye hakuta jina lake liandikwe gazetini, alisema hawakukubaliana chochote na Mattaka, hivyo walimwomba idhini ya kukutana na wafanyakazi leo, ombi ambalo alilikubali.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika mkutano huo, Mattaka aliwaeleza viongozi hao kwamba kinachofanywa na uongozi wa kampuni ni agizo la Serikali la kutaka kupunguzwa kwa idadi ya wafanyakazi ili iweze kujiendesha kwa ufanisi.
Hata hivyo, wafanyakazi kupitia chama chao, walimweleza Mattaka kuwa wako tayari kuachishwa kazi lakini wanapinga kwenda likizo bila malipo kwa kuwa sheria za kazi hazitambui hilo. Gazeti hili halikuweza kumpata Mattaka kuzungumzia suala hili. Ijumaa iliyopita, wafanyakazi hao walipinga mapendekezo ya kutakiwa kwenda likizo bila malipo baada ya kuelezwa na uongozi kwamba kampuni haiwezi kujiendesha kwa idadi ya sasa ya wafanyakazi na haina fedha za kuwaachisha kazi.