Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,722
- 45,125
Ni weekend tena. NBC Premier League inaendelea ambapo Wagosi wa Kaya, Coastal Union watashuka dimbani kuwaalika Mabingwa watetezi wa taji, Yanga katika dimba la Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha.
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana katika dimba hilo mwezi wa saba mwaka huu katika mchezo wa fainali ya Azam Sports Federation ambapo Yanga walibuka na ushindi.
Je leo Juma Mgunda ( Guardiola Mnene) ataweza kuwadhibiti tena Yanga? Tukutane hapa saa 10:00 jioni.
Utabiri wangu: 1-1
=======
00' Kipenga kinapulizwa kuashiria mwanzo wa mchezo, Coastal union VS Yanga
01' Aziz Ki anaachia mkwaju wa kwanzo uliolenga goli, mlinda mlango Mahmud anasimama imara. Coastal union 0-0 Yanga
04' ⚽ Benard Morisson anaandika bao la kwanza kuitanguliza Yanga, akiunganisha pasi maridadi kutoka kwa Jesus Moloko. Coastal Union 0-1 Yanga
07' Yanga wanapata nafasi nyingine lakini Moloko anapaisha juuuuuuu. Mpira uliingizwa kwenye box na Benard Morisson.
10' Yannick Bangala yuko chini baada ya kusiginwa na Juma, nahodha wa Coastal Union. Bangala anamsukuma Juma.
11' 🟡Wote wawili wanapewa kadi ya njano
14' Coastal wanaachia mkwaju wa kwanza uliolenga goli kwa shuti la mkwaju wa adhabu ndogo kutoka kwa Betran, Mshery anakamata mpira barabara.
23' Coasta Union wanafika langoni kwa Yanga lakini juhudi zao zinashindwa kuzaa matunda
25' 🔁 Jesus Moloko ambae kaumia anaenda bench na nafasi yake inachukuliwa na Dickson Ambundo
28' Mabadi anajaribu kufika kwenye lango la Yanga, backline ya Yanga inasimama imara na kuzaa kona isiyo na matokeo.
33' 🟡 Morisson anapewa kadi ya njano baada ya 'kujiangusha' ndani ya box
37' Feisal Salum anaachia mkwaju kutoka nje ya 18, unapaa juuuuuu
40' 🚩Coastal wanapata kona ya tatu na Mrundi wa Coastal anaachia mkwaju mkali unaopanguliwa na Mshery, kona pacha inashindwa kuleta athari
42' Ki Aziz anaachia mkwaju wake wa pili golini lakini bado anashindwa kuanza mkeka wa magoli
52' Aucho anapewa kadi ya njano
53' Coastal wanapata kona tatu mfululizo lakini Yanga wanasimama imara. Coastal union 0-0 Yanga
55' 🔁 Fiston Mayele anaingia kuchukua nafasi ya Makambo upande wa Yanga
57' Maabad wa Coastal Union anaipangua beki ya Yanga lakini Mshery anazuia shambulizi
62' 🟡 Kocha msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze anapewa kadi ya njano
64' 🟡 Mubona anapewa kadi ya njano kwa kuvuta jezi ya Morisson
66' 🚩Aziz Ki anaachia mkwaju wa adhabu ndogo, beki anautoa kwenye njia na kuzaa kona
67' ⚽ Fiston Mayeleeee anaiandikia Yanga bao la pili. Kona ya pili ya mchezo kwa Yanga inazaa goli
71' Coastal Union 0-2 Yanga
71' 🔁 Majimengi anaingia kuchukua nafasi ya Hamza
72' 🔁Farid Mussa anaingia kuchukua nafasi ya mfungaji wa bao la kwanza, Benard Morisson
88' Kila timu inajaribu kufikia lango la mwenzake, Coastal union 0-2 Yanga
89' Yanga wanacheza wenyewe hapa dimba la Sheikh Amri Abeid
90+3 Mpira unatamatika jijini Arusha, Yanga inazoa alama zote tatu na kufikisha alama sita. Coastal union inasalia na alama zake tatu.
Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi ametoa pole kwa mashabiki wa Yanga waliopata ajali pia amewaomba waamuzi kulinda wachezaji kwani ni moja ya jukumu lao akitolea mfano rafu mbaya iliyotokea leo. Pia amekanusha Yanga kuwa na mpango wowote na mchezaji Manzuki.
Kwa upande wa Juma Mgunda, kasema timu yake ina wachezaji wapya wengi na bado wanajenga timu yao na yeye kama kocha anakubali makosa yote yaliyofanyika kwa upande wao.
TAMATI
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana katika dimba hilo mwezi wa saba mwaka huu katika mchezo wa fainali ya Azam Sports Federation ambapo Yanga walibuka na ushindi.
Je leo Juma Mgunda ( Guardiola Mnene) ataweza kuwadhibiti tena Yanga? Tukutane hapa saa 10:00 jioni.
Utabiri wangu: 1-1
=======
00' Kipenga kinapulizwa kuashiria mwanzo wa mchezo, Coastal union VS Yanga
01' Aziz Ki anaachia mkwaju wa kwanzo uliolenga goli, mlinda mlango Mahmud anasimama imara. Coastal union 0-0 Yanga
04' ⚽ Benard Morisson anaandika bao la kwanza kuitanguliza Yanga, akiunganisha pasi maridadi kutoka kwa Jesus Moloko. Coastal Union 0-1 Yanga
07' Yanga wanapata nafasi nyingine lakini Moloko anapaisha juuuuuuu. Mpira uliingizwa kwenye box na Benard Morisson.
10' Yannick Bangala yuko chini baada ya kusiginwa na Juma, nahodha wa Coastal Union. Bangala anamsukuma Juma.
11' 🟡Wote wawili wanapewa kadi ya njano
14' Coastal wanaachia mkwaju wa kwanza uliolenga goli kwa shuti la mkwaju wa adhabu ndogo kutoka kwa Betran, Mshery anakamata mpira barabara.
23' Coasta Union wanafika langoni kwa Yanga lakini juhudi zao zinashindwa kuzaa matunda
25' 🔁 Jesus Moloko ambae kaumia anaenda bench na nafasi yake inachukuliwa na Dickson Ambundo
28' Mabadi anajaribu kufika kwenye lango la Yanga, backline ya Yanga inasimama imara na kuzaa kona isiyo na matokeo.
33' 🟡 Morisson anapewa kadi ya njano baada ya 'kujiangusha' ndani ya box
37' Feisal Salum anaachia mkwaju kutoka nje ya 18, unapaa juuuuuu
40' 🚩Coastal wanapata kona ya tatu na Mrundi wa Coastal anaachia mkwaju mkali unaopanguliwa na Mshery, kona pacha inashindwa kuleta athari
42' Ki Aziz anaachia mkwaju wake wa pili golini lakini bado anashindwa kuanza mkeka wa magoli
52' Aucho anapewa kadi ya njano
53' Coastal wanapata kona tatu mfululizo lakini Yanga wanasimama imara. Coastal union 0-0 Yanga
55' 🔁 Fiston Mayele anaingia kuchukua nafasi ya Makambo upande wa Yanga
57' Maabad wa Coastal Union anaipangua beki ya Yanga lakini Mshery anazuia shambulizi
62' 🟡 Kocha msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze anapewa kadi ya njano
64' 🟡 Mubona anapewa kadi ya njano kwa kuvuta jezi ya Morisson
66' 🚩Aziz Ki anaachia mkwaju wa adhabu ndogo, beki anautoa kwenye njia na kuzaa kona
67' ⚽ Fiston Mayeleeee anaiandikia Yanga bao la pili. Kona ya pili ya mchezo kwa Yanga inazaa goli
71' Coastal Union 0-2 Yanga
71' 🔁 Majimengi anaingia kuchukua nafasi ya Hamza
72' 🔁Farid Mussa anaingia kuchukua nafasi ya mfungaji wa bao la kwanza, Benard Morisson
88' Kila timu inajaribu kufikia lango la mwenzake, Coastal union 0-2 Yanga
89' Yanga wanacheza wenyewe hapa dimba la Sheikh Amri Abeid
90+3 Mpira unatamatika jijini Arusha, Yanga inazoa alama zote tatu na kufikisha alama sita. Coastal union inasalia na alama zake tatu.
Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi ametoa pole kwa mashabiki wa Yanga waliopata ajali pia amewaomba waamuzi kulinda wachezaji kwani ni moja ya jukumu lao akitolea mfano rafu mbaya iliyotokea leo. Pia amekanusha Yanga kuwa na mpango wowote na mchezaji Manzuki.
Kwa upande wa Juma Mgunda, kasema timu yake ina wachezaji wapya wengi na bado wanajenga timu yao na yeye kama kocha anakubali makosa yote yaliyofanyika kwa upande wao.
TAMATI