Chukueni tahadhari na dawa hii, TFDA na Wizara ya Afya mpo wapi?

Kuna dawa ya kutibu malaria maarufu inayojulikana kwa jina la MALAFIN
View attachment 457836

Hiyo dawa hapo juu ndani ina vidonge viwili na huwa inauzwa kwa bei ya sh 1500, na sehemu nyingine huwa ni sh 2000.

Baada ya kuitumia kwa zaidi ya mara tatu, kila muda ninapoitumia imeniletea madhara ikiwemo uvimbe kama mvilio wa damu kwenye kichwa cha uume na ngozi ya uume kuchubuka. Pia mdomo nao kwenye lips kumetokea mchubuko na mvilio wa damu.

Baada ya kwenda hospitali kuonana na doctor kumuelezea hali yangu ilivyo baada ya kuitumia ile dawa nliyonunua pharmacy. Doctor aliniambia kuwa hizo dawa ni hatari sana na zinaweza kupofua macho na hata kuharibu system ya nguvu za kiume na akanitaka iwe mwanzo na mwisho kuzitumia kwa usalama wangu

USHUHUDA

Baada ya kuelezea hili tatizo kwa watu wengine kuna baadhi nao wamesema limeshawatokea. Zaidi ya watu watatu waliniambia kuwa nao tatizo hili liliwapata.

My take

TFDA kama mnadhani huu uzi ni wa kuchafuliana biashara, chukueni sample ya hizi dawa zilizozagaa nchi nzima na huko kwenye mapharmacy ndio zinauzwa kama njugu na watu wanazinunua sana kwa sababu ni bei rahisi.

Baada ya kuzichukua zifanyieni uchunguzi ikibidi na nyie mnywe kabisa ili muone matokeo yake. Hizi dawa ni feki matokeo yake ndio magonjwa ya cancer yanayotuuwa kila siku.

Chukueni Tadhadhari
Issue wewe una allergy na dawa zenye sulpher please usinywe dawa hizo ok wengine haiwaletei madhara unawasaidiaje sasa
 
Ndugu zangu tatizo sio dawa ila tatizo ni watumiaji wanakuwa na mzio (allergy) na dawa hizo, kiufupi wanakuwa allergic to sulphur. Ingawa dawa hizo hazipendekezwi na wizara ya afya ya Tanzania kwa matibabu ya malaria. Ila inaweza kutumika kwa wajawazito kama kinga tu.
Asante dr. kwa mawazo mazuri. Hata dukani kwangu ninazo japo nazitoa kwa mama mjamzito tu.
 
Hii dawa ndo dawa yangu ya kutibu malaria, nkinywa hii napona na nakaa hata zaidi ya miaka 5 bila kuumwa tena malaria, hainisumbui kwa kweli!!
 
Pole sana.
Kwanza nikujulishe ya kuwa dawa hiyo imeshaondolewa katika dawa za kutibu malaria na kwa sasa inatumika kama kinga kwa kina mama wajawazito tu (angalia vizuri box lake na utaona for intermittent prevention of malaria in pregnancy).
Kuhusu yaliyokupa ni kuwa umepata reaction ya sulphur na uwe mwangalifu kwa dawa zote zenye sulphur na mueleze daktari wako kabla hajakuandikia dawa.
Dawa ya kutibu malaria isiyo kali ni MSETO au ALU igawa waswahili tunapenda rahisi hata katika manbo magumu na wengi wanaikimbia ALU kwa wingi wa vodonge.
Mimi natumia hiyo hiyo ya waja wazito na napona, mseto kwa kweli siwezi kutumia, vidonge vingi hatari!!
 
Hizi dawa zenye asili ya SP zilishapigwa marufuku ktk matumizi ya kutibu malaria. Zimeondolewa pia ktk mlolongo wa matibabu ya malaria isipokuwa tu zatumika kwa wamama wajawazito kuwakinga watoto wao na madhara ya malaria. Pia dawa hizi zenye kiambata cha salfa zinawadhulu walio wachache. Kunywa kwa tahadhari dawa hizi ambazo zimesha futwa.
 
Moja ya ingredients zilizotumika kutengeneza hyo dawa ni SULPHUR, mara nyingi sana hyo sulphur imekua inasababisha allergy kwahyo ukipata tatizo ujue upo allergic to sulphur na hizo ni kama side effects lakini kuna watu ambao hawana allergy na sulphur kwahiyo wakitumia hiyo dawa hawapati tatizo lolote nikiwemo mimi
 
Mimi natumia hiyo hiyo ya waja wazito na napona, mseto kwa kweli siwezi kutumia, vidonge vingi hatari!!
Dawa inapoondolewa kwa ajili ya kushindwa kutibu haina maana kuwa ni asilimia mia.Kuna kiwango ambacho kikifikiwa inabidi iondolewe kwani inahatarisha maisha ya wengi kwa manufaa ya wachache kama wewe.
Kitakachotokea ni kuwa ukipata malaria iliyosababishwa na strain (?vinasaba?) ambayo ni sugu kwa SP unayoipenda ina maana ya kuwa utakuwa unasubiria kupona wakati wadudu wa malaria wanaongezeka na hii inaweza kukusababishia kufikishwa hospitali kwa malaria kali ambayo itakuwa inahatarisha maisha yako.
Tujifunze kuwasikiliza wataalamu.
 
Dawa inapoondolewa kwa ajili ya kushindwa kutibu haina maana kuwa ni asilimia mia.Kuna kiwango ambacho kikifikiwa inabidi iondolewe kwani inahatarisha maisha ya wengi kwa manufaa ya wachache kama wewe.
Kitakachotokea ni kuwa ukipata malaria iliyosababishwa na strain (?vinasaba?) ambayo ni sugu kwa SP unayoipenda ina maana ya kuwa utakuwa unasubiria kupona wakati wadudu wa malaria wanaongezeka na hii inaweza kukusababishia kufikishwa hospitali kwa malaria kali ambayo itakuwa inahatarisha maisha yako.
Tujifunze kuwasikiliza wataalamu.
Wataalamu wenyewe nao ni wasanii tu, Mara chloroquine, Mara quinine, Mara fansida, mara SP, mara mseto, muda si mrefu tutaletewa zingine na kuambiwa mseto haifai!
 
Dawa hiyo ina sulpha ambayo ndo wewe una allergy nayo, hivyo si hiyo tu kuanzia sasa usitumie dawa yoyote yenye ingredient ya sulpha ndani yake unaweza kupata tatizo kubwa zaidi Kama vile Steven Jonson syndrome. Tafadhari muone daktari akuandikie cheti chenye maneno ya ALLERGIC TO SULPHA ili kila unapokwenda kutibiwa uwe nacho kumuallert prescriber yeyote asikuandikie dawa yenye sulpha
 
Wataalamu wenyewe nao ni wasanii tu, Mara chloroquine, Mara quinine, Mara fansida, mara SP, mara mseto, muda si mrefu tutaletewa zingine na kuambiwa mseto haifai!
Hakuna usanii ndugu yangu.Kuna mengi ambayo yanafanyika na ni vigumu kwa raia wa kawaida kuelewa.Miaka ya mwanzo ya UKIMWI ilikuwa mwanamke akigundulika na VVU jambo la kwanza ni kuwa asishike mimba lakini leo mama na baba wenye VVU wanapata mto ASIYE NA VVU,tumshukuru Mungu kwa hili kwani watu hawatakufa bila watoto kwa ajili ya kuwa na VVU.Jambo hili halikutokea kwa bahati ni tafiti nyingi na za gharama kubwa zilizofanywa na hao unaowaita WASANII.Mifano ni mingi lakini kumbuka kuwa wakati umelala usiku wa manane kuna watu wako macho wakihangaika kukabiliana na shida za binadamu.
 
Dawa yoyote haiwezi kuondolewa sokoni kwa sababu ya madhara anayoyapata mtumiaji mmoja mmoja bali kwa kuthibitika kuwa dawa husika haina uwezo wa kutibu ugonjwa ambao dawa ilitegemewa ingetibu.

Kwenye kila dawa huwa wanatoa tahadhari kuwa usitumie endapo itakuletea mzio/allerg au hata reaction yoyote sasa wewe baada ya kukuletea mzio ukaendelea kutumia halafu unawataka TFDA wachukue hatua? hapo ni sawa na uvute sigara ikuletee madhara halafu utegemee kulalama kwa mamlaka husika wakati umeona onyo.

Zaidi ya yote MALAFIN ni intermittent preventive therapy of malaria in Pregnant ambayo inatumiwa na wamama wajawazito kuzuia maambukizi ya malaria nimeshangaa kuona wewe mwenzetu bolo lako likaivia damu hayo ndio madhara ya kununua dawa mitaani mkipatwa na madhara mnaanza kulaumu mamlaka
Mkuu kunywa bia mbili hapo nitakuja kulipa.
 
Hata Mimi ilishawahi kunitokea zaidi ya Mara mbili, hivi sasa nimeacha kabisa kunywa hayo madawa feki.
Nikidhani ni Mimi peke yangu kumbe tupo wengi.
Nipo tayari kutoa ushirikiano wa kuthibitisha madhara ya hizo dawa.!
Ina maana mpaka hapo hujaelewa Maelezo ya watalaamu????
 
Wafanyabiashara wa madawa mpo kazini
We naeleza kabisa kuwa zaidi ya watu watatu nnaowafahamu wanasema tatizo wamekutana nalo
Je wengine ambao sijawaho kuwaona?

Ndg kubaliana na unachoelezwa na uchukuwe hatua sasa, kifupi una mzio na dawa zenye sulphur. Mimi nimewahi kuathirika na dawa za aina, niliugua malaria nikatumia dawa zenye sulphur kilichotokea mzee usiombe, Uume uliweka kama lengelenge kichwani na ngozi ya juu kuvulika kabisa, Pili ulimi ngozi ya juu nayo ikatoka, kuzunguka midomo hali ikawa ile ile. Kumbuka kabla nilikuwa natumia dawa hizo na madhara kwa kuwa yalikuwa ni kidogo na sikujua kuwa yanasababishwa na dawa niliendelea kutumia. Na mara nyingi kama tunavoamini wengi kuwa ukiwa na homa vidonda vikitokea mdomoni ndo homa inatoka. Cha msingi achana na dawa zenye Sulphur zote, zikiwemo Ceptrine na asprin.
 
Sijawahi kunywa dawa aina yoyote ya Malaria tofauti na Malafin,hakuna kichwa cha dudu kuvimba wala kuchubuka,sasa wakizifungia unataka Nitumie dawa gani nikiugua Malaria?
 
Uko sahii me mwenyewe natumiaga hii dawa hii ni Mara yatatu nimechubuka lips siku zote nazani labda ndo malaria inatoka kumbe hii dawa asante kwa kunifungua macho
IMG_20170113_021029.jpg
 
Sijamaliza wiki nimemeza hii dawa. Sima matatizo yoyote. Unaweza kuwa na alegi zako unakuja kupayuka huku.
 
Back
Top Bottom