Naam! Umenikumbusha 2000/1 hapo ndani ya Chuchu sound kuna Chuchu Yusuph(rip), Mao Santiago, Hababuu mwana Zanzibar, Omari Mkali, Joniko flower-maua (sasa Machozi band), Gabi Katanga(rip) na wengineo. Walikuwa wapo juu sana miaka hiyo. bendi yao ilivunjika ikiwa bado iko juu-mambo ya mapato. Naamini wanamziki wote waliopitia chuchu bado wanaikumbuka sana bendi yao.
Nikirudi kwenye mada, mi nakushauri ukanunue albamu yao kariakoo au hata pale buguruni unaweza ukaipata. Ndio, kitu kizuri, tuwe tayari kukigharamia, sikushauri uka-burn.
Labda uwe specific kariakoo duka gani, hata huko buguruni ni duka lipi, kununua au kulipia sio tatizo nathamini kazi za watu ni busara kuzinunua.
salam aleykum
ningependa kuomba mtu anisaidie kujua wapi nitapata nyimbo za chuchu sound ile ya akina mao santiago
jamani mwenye nyimbo ya kusema sema na marafiki naomba anitumie zote za chuchu sound band