Mkuu, uswazi hii kawaida sana.
mbona hata chumba chenyewe kimoja na kuna watoto watatu??
Na chumba hiccho hicho ni jiko na sebule na dinning na sehemu ya kulala
Duh uswazi raha sana
Mkuu, uswazi hii kawaida sana.
mbona hata chumba chenyewe kimoja na kuna watoto watatu??
Unajua mkuu tatizo linakuja juu ukisimama tu unaonekana juu kuanzia mabegani
Hahaha!! BiggyHahahaa...........hapo lazima uwe unawahi sana kibaruani.............yani saa kumi ushaondoka.
unaingia chooni/bafuni saa tisa usiku!!!
Yeah hiyo ngazi mpwa ila ya miti ishu inakuja umepatwa na tumbo la kuhalisha unakimbia ukiteleza lazima ujinyee
Hahaha unatoka nduki uchi
Hahahahaha ndo hapo sasa hapo chalii maji yamemwagika si unajua kule chooni unaenda na maji kwenye kopo?
Au ni pale gunia au kanga uliyotegemea mlangoni inapodondoka wakati mtu mzima umejipaka sabuni huoni kinachoendelea
halafu wamama wa kiswahili wamekaa nje wanapiga soga zao
Na kule hakuna cha toilet paper wala nini ni balaa hapo na huwezi kumwita mtu akuletee maji mle
Alafu unajua foleni yake wanafanyaje unaweka ndoo mlangoni kama kuna mtu yupo ndani anaoga
Choo cha passport size hakuna kuremba. Kila mmoja anaoga kwa muda wake. Kwanza hakina uwezo wa kuhimili uzito wa watu wawili na ndoo. Njoo huku kwetu kwa mtogole ujifunze matumizi ya vyoo vya passport size.
Sasa pale kama tumbo limefuluga alafu unarusha mabomu akina mama wamekaa nje utasikia vicheko na sauti za kimbeya "haloooo babu weye umekula visivyo lika babu weyeee!!" mzee unashusha pratatatata mbuuuuuuuu phewwwwwww yaani balaa tupo huko nje noma
raha ni pale wababa na vitambi vyao wanatoka na taulo ambalo hata rangi yake haijulikani limefungwa tumboni na lina vitobotobo kibao wanaenda kuoga ni full kicheko
Hahahaha akitoka kuoga mswaki anauchomeka kwa ubavuni kwenye taulo tumbo hilo