Chochonde,tunapofanya madudu yetu,hebu tuwakumbuke watoto alaaaaa!!

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,712
Inafahamika kuwa,inapotokea mtoto akazaliwa "nje ya ndoa",mtoto yule ndo anaadhibiwa kwa kuitwa jina baya sana,eti mtoto haram(silipendi kabisa jina hili).Pia mwanandoa mmoja anapocheat na akagundulika na ndoa kufa bado watoto wanakuja kupata adhabu ya kuishi malezi ya mzazi mmoja na pengine malezi ya hatari kama mzazi mmoja hatakua imara,na pengine mzazi atawatelekeza watoto na watoto kubadilika jina na kuitwa watoto wa mtaani utafikiri mtaa ndo umewazaa,au huitwa "chokoraa" kwa sababu ya starehe ya mtu mmoja.Yapo matatizo mengi yanayosababisha viumbe hawa wateseke usiku kwa baridi kwa sababu hawana pa kulala kisa mama au baba maisha yamemshinda na kuwatelekeza.Hivi dhambi hizi kubwa namna hii ni mwanadam mwenye akili anazifanya kweli?Wengine unakuta ana watoto utafikiri ameahidiwa zawadi kwa kuzaa,watoto wenyewe shule hawaendi kama wanaenda hawana hata viatu na shati la shule halijulikani rangi,hivi umelazimishwa kuzaa?Jamani haya majina sijui mtoto haram,mtoto wa mtaani n.k,nani kayaleta?Kwanini tuwaadhibu watoto kwa makosa yetu?Jamani tunapofanya madudu hebu tukumbuke viumbe visivyo na hatia aidha vitakavyopatikana kutokana na kitendo hicho au kama unacheat na una watoto,hebu fikiri ukijulikana wanao watakua na maisha gani?
 
Halafu ukimuuliza mtu kwa nini hatumii condom
anasema hapendi ladha yake. Kweli???
 
utoaji mimba uhalalishwe ili kuupuka mimba zisizotarajiwa
 
Inafahamika kuwa,inapotokea mtoto akazaliwa "nje ya ndoa",mtoto yule ndo anaadhibiwa kwa kuitwa jina baya sana,eti mtoto haram(silipendi kabisa jina hili).Pia mwanandoa mmoja anapocheat na akagundulika na ndoa kufa bado watoto wanakuja kupata adhabu ya kuishi malezi ya mzazi mmoja na pengine malezi ya hatari kama mzazi mmoja hatakua imara,na pengine mzazi atawatelekeza watoto na watoto kubadilika jina na kuitwa watoto wa mtaani utafikiri mtaa ndo umewazaa,au huitwa "chokoraa" kwa sababu ya starehe ya mtu mmoja.Yapo matatizo mengi yanayosababisha viumbe hawa wateseke usiku kwa baridi kwa sababu hawana pa kulala kisa mama au baba maisha yamemshinda na kuwatelekeza.Hivi dhambi hizi kubwa namna hii ni mwanadam mwenye akili anazifanya kweli?Wengine unakuta ana watoto utafikiri ameahidiwa zawadi kwa kuzaa,watoto wenyewe shule hawaendi kama wanaenda hawana hata viatu na shati la shule halijulikani rangi,hivi umelazimishwa kuzaa?Jamani haya majina sijui mtoto haram,mtoto wa mtaani n.k,nani kayaleta?Kwanini tuwaadhibu watoto kwa makosa yetu?Jamani tunapofanya madudu hebu tukumbuke viumbe visivyo na hatia aidha vitakavyopatikana kutokana na kitendo hicho au kama unacheat na una watoto,hebu fikiri ukijulikana wanao watakua na maisha gani?

Nakubaliana na wewe, uzembe wa sisi kama wazazi huchangia adhabu na mateso kwa watoto wasio na hatia. Tujaribu kuwa na Utu na Uungwana tunapoishi hapa duniani, yasije tukuta makubwa huko tuendako.
 
Nakubaliana na wewe, uzembe wa sisi kama wazazi huchangia adhabu na mateso kwa watoto wasio na hatia. Tujaribu kuwa na Utu na Uungwana tunapoishi hapa duniani, yasije tukuta makubwa huko tuendako.

Nice one!Congratulation!
 
sikubali kabisa mtoto aitwe Haramu, haramu ni hao wawili waliofanya uzinzi na uasherati, wanajua kitendo hakiruhusiwi ila kwa kukwepa guilty wanamsukumia mtoto

nakataa nakataa nachukiaaaaaaaaaaa
 
Picture this;
Kisha hao watoto wakikua either wawe changudoaz au majambazi. Majambazi wataua watu na kuacha watoto wengine yatima ambao yamkini wakaja kuwa tena watoto wa mitaani. Changudoa wataambukiza ukimwi wanandoa watoto watabaki yatima na wataongeza idadi ya watoto wa mitaani....and so on and so on! Hili ni janga la kijamii- linakuja kuwapata hata wasiohusika!
 
Picture this;
Kisha hao watoto wakikua either wawe changudoaz au majambazi. Majambazi wataua watu na kuacha watoto wengine yatima ambao yamkini wakaja kuwa tena watoto wa mitaani. Changudoa wataambukiza ukimwi wanandoa watoto watabaki yatima na wataongeza idadi ya watoto wa mitaani....and so on and so on! Hili ni janga la kijamii- linakuja kuwapata hata wasiohusika!

Asante sana kwa ufafanuzi wako mzuri!
 
Kuna hii tabia ya wazazi kuweka heshima bar na vilabuni, nyumbani wanae wanashindia mlo mmoja! Au anajifanya mstari wa mbele kuchangia faranga chafu kwenye masherehe na makongamano....wakati watoto wanatembea ma..t..ko wazi! Sio sifa wala nini ujinga tu!!
 
Kuna hii tabia ya wazazi kuweka heshima bar na vilabuni, nyumbani wanae wanashindia mlo mmoja! Au anajifanya mstari wa mbele kuchangia faranga chafu kwenye masherehe na makongamano....wakati watoto wanatembea ma..t..ko wazi! Sio sifa wala nini ujinga tu!!

Tena ujinga mkubwa!
 
utoaji mimba uhalalishwe ili kuupuka mimba zisizotarajiwa

Kwanini mimba zilazimishwe kutoka, wakati mna uwezo wa kuzuia mimba isitungwe vipi kama wewe ungetolewa ungengia JF ukiwa akhera? gharama za uzuiaji zinapatikana bure jamani. Inasikitisha sana kusikia / kuona watoto wakinyanyasika mitaani.
 
Kwanini mimba zilazimishwe kutoka, wakati mna uwezo wa kuzuia mimba isitungwe vipi kama wewe ungetolewa ungengia JF ukiwa akhera? gharama za uzuiaji zinapatikana bure jamani. Inasikitisha sana kusikia / kuona watoto wakinyanyasika mitaani.

Eti bana!Kwanini usubiri mpaka mti uote?
 
Back
Top Bottom