sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
KIKOSI cha wabunge kikiongozwa na Naibu Spika, Job Ndugai, kimesafiri kwenda jijini London, Uingereza, kukutana na Bunge la makabwela la nchi hiyo, ili kuongeza ushawishi na hatimaye mabilioni ya fedha yanayopaswa kurejeshwa nchini kutokana na ununuzi wa kitapeli wa rada, yarejeshwe serikalini.
Sakata hiyo ya rada ilimlazimu waziri wa zamani wa miundombinu, Andrew Chenge, kujiuzulu nafasi yake serikalini baada ya makachero wa Uingereza kukuta zaidi ya dola milioni 1 (bilioni 1.6) kwenye moja ya akaunti za nje za mwanasiasa huyo.
Makachero hao walizihusisha pesa hizo na tuhuma za rushwa ya rada huku Chenge mwenyewe akijitapa kuwa pesa hizo ni vijisenti tu kwake.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana mjini hapa, kikosi kinachoundwa na wabunge wengine takriban wanne, kitakutana na viongozi mbalimbali wa Bunge la Uingereza, ambako ndiko mzozo wa mauzo ya rada ya kijeshi ulikoanzia ukiwa na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataita wa Uingereza, Clare Short.
Sakata hiyo ya rada ilimlazimu waziri wa zamani wa miundombinu, Andrew Chenge, kujiuzulu nafasi yake serikalini baada ya makachero wa Uingereza kukuta zaidi ya dola milioni 1 (bilioni 1.6) kwenye moja ya akaunti za nje za mwanasiasa huyo.
Makachero hao walizihusisha pesa hizo na tuhuma za rushwa ya rada huku Chenge mwenyewe akijitapa kuwa pesa hizo ni vijisenti tu kwake.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana mjini hapa, kikosi kinachoundwa na wabunge wengine takriban wanne, kitakutana na viongozi mbalimbali wa Bunge la Uingereza, ambako ndiko mzozo wa mauzo ya rada ya kijeshi ulikoanzia ukiwa na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataita wa Uingereza, Clare Short.