Chato Kunatisha: Fedha za miradi za Halmashauri zaliwa

Bigirita

Platinum Member
Feb 12, 2007
15,986
7,368
Waziri Mwamri amewawakia mkurugenzi na viongozi wengine wa halmashauri ya wilaya ya Chato kwa madai ya kutafuna fedha za miradi ya zahanati na josho zaidi ya 60million.

wapi Maghufuli sasa................yupo busy na ya wenzake wakatio kwake kunaungua!!!


source: TBC taarifa ya habari.
 
Waziri Mwamri amewawakia mkurugenzi na viongozi wengine wa halmashauri ya wilaya ya Chato kwa madai ya kutafuna fedha za miradi ya zahanati na josho zaidi ya 60million.

wapi Maghufuli sasa................yupo busy na ya wenzake wakatio kwake kunaungua!!!


source: TBC taarifa ya habari.


Magufuli ameshindwa kusimamia fedha za umma kutumika vizuri jimboni kwake na kukimbilia kutafuta sifa za kijinga dar es salaam.

Watu wamekula pesa ya majosho na hospitali bila hofu ya magufuli. Inawezekana jimboni kwake hafiki anaishia kuzurura maeneo mengine.
 
Waziri Mwamri amewawakia mkurugenzi na viongozi wengine wa halmashauri ya wilaya ya Chato kwa madai ya kutafuna fedha za miradi ya zahanati na josho zaidi ya 60million.

wapi Maghufuli sasa................yupo busy na ya wenzake wakatio kwake kunaungua!!!


source: TBC taarifa ya habari.

Acheni kumwandama Magufuli,yeye ni mbunge tu wa Chato,ni mwakilishi wa wananchi wa Chato na sio mtendaji.Mtendaji ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na watendaji wa halmashauri ya Chato.

Kundi hasimu na kundi la Magufuli wameanza kampeni ya kumchafua JEMBE Magufuli...viva Magufuli viva
 
Acheni kumwandama Magufuli,yeye ni mbunge tu wa Chato,ni mwakilishi wa wananchi wa Chato na sio mtendaji.Mtendaji ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na watendaji wa halmashauri ya Chato.

Kundi hasimu na kundi la Magufuli wameanza kampeni ya kumchafua JEMBE Magufuli...viva Magufuli viva
Maghufuli yupo busy kugombana na Mnyika kuhusu mia mbili za Ubungo bus terminal wakati jimboni kwake watendaji wanatafuna fedha, wananchi anaowawakilisha hawana pakipeleka ng'ombe zao.........watu wamelamba hela ya majosho. kituo cha afya watu wamekula 60%........yeye yupo busy na mia mbili za wenzake.
 
Naangalia TBC 1 sahizi taarifa ya habari, nimeuona mh Aggrey mwamri naibu waziri TAMISEMI aking'aka na kufoka kwa hasira kwa mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Chato (jimbo la mh Magufuri) mbele ya wananchi wa Chato na kuagiza kufanyika kwa uchunguzi wa matumizi mabaya ya fedha wilayani humo baada ya kubainika zaidi ya bilioni 100 kwa ajili ya miradi ya maendeleo zimefujwa . Mh naibu waziri amethibitisha kuwa katika miradi yote aliyotembelea hakuna hata mradi mmoja uliotekelezwa kwa uhakika ni uozo mtupu, imeoneshwa jengo la kuhifadhia maiti ikiwa na nyufa kibao kabla hata ya kuanza kutumika, na pia limeoneshwa jengo la halmashauri likiwa limejengwa bila kuwekewa linta.Hii ni aibu kubwa na fedhaha kwa jimbo analotokea Magufuri na kumbe amekuwa akipita na kupiga makelele na kujidai ni bingwa wa kutumia sheria kwenye majimbo ya wenzake na kusahau anakotoka, kajamaa kumbe hakafai kabisa ni mbwembwe tu. SOURCE: TBC1 saa mbili, taarifa hii itarudiwa saa 5 usk leo na kesho saa 1 asb
 
kawawakia then what?wanaendelea kula maisha
Kula na kusahau ndio mtindo wa CCM

lakini Maghufuli anahangaika na jiti mbili mbili za wenzake huku, kwake watu wanakula hata hawasazi wala nini!!!
 
Pamoja na Mwanri kuunguruma, huwa hana ufuatiliaji wa maagizo yake! Amefanya ziara kama hii mwaka juzi lakini hadi leo aliyotolea maelekezo hayajanyiwa kazi na wahusika katika maeneo mbalimbali mfano katika mkoa wa Pwani na leo anatoa maelekezo mengine. Viongozi wawe wafuatiliaji wa maelekezo yao vinginevyo wanajidharaulisha mbele ya watendaji!
 
Hao ndio wabongo wenye akili maana bila kula pesa ya serikali huwezi kupanda cheo
Sio kweli mkuu...........mimi siafiki ulaji fedha za maendeleo, zilizotengwa kwa maendeleo........isipokuwa zile zilizotengwa kwa ajili ya posho na masaburi allowance, wazitafune tu, hata wasipofanya semina, wakazipiga kavu kavu poa tu!!
 
Mimi huwa bado siafiki fedha za miradi kupelekwa kwenye halmashauri kungekuwa na njia mbadala hata hivyo vyovyote vile nchi imeishaoza fedha zenyewe za misaada nazo wanazipiga panga.
 
Acheni kumwandama Magufuli,yeye ni mbunge tu wa Chato,ni mwakilishi wa wananchi wa Chato na sio mtendaji.Mtendaji ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na watendaji wa halmashauri ya Chato.

Kundi hasimu na kundi la Magufuli wameanza kampeni ya kumchafua JEMBE Magufuli...viva Magufuli viva

Jaribu kulichunguza hilo jembe, utagundua ni JEMBE BUTU
 
Pale Chato mbona zinapigwa mara kibao! Shamba la bibi lile! 2010 palikuwa na kashfa pia! Upande wa mishahara watu walipiga alafu wakalala mbele!
 
Acheni kumwandama Magufuli,yeye ni mbunge tu wa Chato,ni mwakilishi wa wananchi wa Chato na sio mtendaji.Mtendaji ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na watendaji wa halmashauri ya Chato.

Kundi hasimu na kundi la Magufuli wameanza kampeni ya kumchafua JEMBE Magufuli...viva Magufuli viva

Ujinga ni mzigo!!!

Anawawakilisha wananchi katika lipi??, au hujui kuwa ni pamoja usimamizi wa rasilimali za wananchi na kuhakikisha hao watendaji wanafuata misingi ya uongozi bora! poor you!
 
sijawahi kuona zuri lolote alilofanya magufuli.
Ni kiongozi asiyeweza kuhoji, ni sawa na mtoto mkaidi mnafiki kwa wazazi wake.
Ujinga wa sheria bila hekima katika maamuzi
 
Ni Mungu kaamua kumuumbua magufuli na jimbo lake yaani aibu tupu, nilitegemea kwake ni kusafi kumbe kuchafu kupindukia na bado skendo nyingi zitaibuka mpaka ataomba poo. mwanza kuna kaeneo inasemekana amejimilikisha na kana mgogoro nikipata ripoti kamili ntawatupia hapa jamvini.
 
Magufuli ameshindwa kusimamia fedha za umma kutumika vizuri jimboni kwake na kukimbilia kutafuta sifa za kijinga dar es salaam.

Watu wamekula pesa ya majosho na hospitali bila hofu ya magufuli. Inawezekana jimboni kwake hafiki anaishia kuzurura maeneo mengine.

Maghufuli kwake ni nyoka wa kibisa maana hang'ati hata kichwa chake kikitumbukizwa kinywani! Ukweli ni kwamba huyu Bwana yuko bize kutafuta "misifa" Dar na Dodoma wakati ya nyumbani kwake yamemshinda. Ndiyo maana CHADEMA wako popular kule na hata mwenyekiti wa kitongoji chake yaani alikozaliwa yeye pale Bomani ni CHADEMA. Ana mapungufu mengi nyumbani kwake ambako CHADEMA wakiwa smart wanaweza mpelekea kilio. Kiko wapi cha kumsuta Mnyika eti "alishindwa kushughulikia maswala ya Ubungo terminal na mabweni ya chuo kikuu?
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Acheni kumwandama Magufuli,yeye ni mbunge tu wa Chato,ni mwakilishi wa wananchi wa Chato na sio mtendaji.Mtendaji ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na watendaji wa halmashauri ya Chato.

Kundi hasimu na kundi la Magufuli wameanza kampeni ya kumchafua JEMBE Magufuli...viva Magufuli viva

Hakuna suala la kumwandama Maghufuli wala hakuna anayepinga kwamba Maghufuli ni mbunge wa Chato, lakini yeye kama mwakilishi wa wananchi ni mdau wa maendeleo ya jimbo lake na anapaswa kuelewa namna fedha zinazopelekwa jimboni kwake zinatumiwa kadri ya mtarajio . Madudu yaliyogundulika jimboni kwa mtu huyu anayependa kujinadi kama kiongozi makini kabisa ni aibu kubwa kabisa kwa uongozi mzima wa jimbo na wilaya yake yeye akiwa mmojawapo kama mbunge na diwani yaani mwana halmashauri
wa wilaya yake ya Chato. Kama Mbunge anapaswa kusimamia utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo ya jimbo na wilaya yake na kuhoji utekelezaji mbaya wa miradi hiyo kama upo, je bado kuna wanaohangaika kumtafutia dirisha la kutoroka toka kwenye lawama za ubadhirifu uliotokea jimboni kwake? Kumbe! Bwana huyu kwao ni nyoka wa kibisa asiyeng'ata hata kichwa chake kikitumbikizwa kinywani.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Back
Top Bottom