Chama cha Mapinduzi chabomoka Njombe,kada wake ajiuzulu na kurudisha kadi

lutondwe

Senior Member
Dec 20, 2010
150
74
kada maarufu wa chama cha mapinduzi Njombe ambaye alikuwa katibu mwenezi wa kata ya Njombe mjini,Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya jumuiya ya wazazi wilaya ya Njombe pia mjumbe wa mkutano mkuu wa jumuiya ya wazazi Taifa Bwana Lupenza leo amejiondoa rasmi kwenye chama hicho.

Tukio hili ni kubwa kwa hapa Njombe kwani huyu ni moja kati ya makada maarufu wa chama cha mapinduzi waliokuwa mstari wa mbele kupambana na vyama vingine vilivyopo Njombe.

Kujiondoa kwa kada huyo ni ishara tosha kuwa mapigo ambayo yalifanywa na chadema kwenye uchaguzi wa udiwani hapa Njombe mjini yalikuwa ni makubwa kupita kiasi.

Mara baada ya uchaguzi kumalizika na ccm KUPOTEZA kwa kura nyingi kuliko sehemu yoyote Tanzania kumekuwa na vita kubwa ndani ya chama cha mapinduzi hoja kubwa ikiwa ni matumizi mabaya ya fedha za kampeni zilizotolewa na makada wa chama hicho kizee.

Inadaiwa kuwa wapo makada wa chama waliochukua fedha nyingi kwa ajili ya kampeni lakini hawakufikisha kwa wananchi jambo ambalo baadhi ya makada wa ccm hawakubaliani nalo na hivyo kutangaza nia ya kuhama chama.

Baada ya Lupenza kutangaza kujitoa katika chama hicho kuna taarifa za uhakika kuwa wapo pia viongozi wawili waandamizi wa chama hicho ambao wanatarajia kujitoa kuanzia tarehe 12.3.2014.

Kwa namna yoyote ili upepo wa chama cha mapinduzi hapa Njombe ni mbaya sana hasa kutokana na kuongozwa na viongozi wachovu kama chama chenyewe kilivyochoka na kukosa mvuto kwa wananchi.

Bwana Lupenza ametangaza uamuzi wake wa kujitoa ccm katika kituo cha Radio Uplands ya Njombe mjini.Pia ameahidi kujiunga na chama makini kabisa kilichopo hapa Tanzania bila kutaja ni chama gani.
 
kumekucha anataka kujiunga na sagasaga na nyagawa kwenye operation ondoa aliyuyo nini?
 
safi saaana ni vyeema na ni haki kujitambua! Hakuna kulala mpaka jimbo liwe la mfano kama vile lilivyofanya kwenye udiwani
 
Akimbilie nafasi act maana chadema hakuna masihala kwatakiwa wapambanaji na wazalendo wa kweli,,akitaka kujiunga chadema lazima aungame au aombe msamaha wana njombe kwakuwapoteza miaka mingi pia kuleta familia yake yote cdm
 
Kweli sasa naanza kumuamini Askofu Kakobe, yani hawa jamaa wameshaanza kujichangana na huu mnara wa babeli kabla ya 2015.
 
Safi sana.wazalendo tuungane kuleta mapinduzi ya kweli. Makinda tunakupa utawala bora we kaa pembeni
 
Wenye akili timamu hawatabaki CCM. Wanaobaki ni wala nchi tu, na mwisho wao unakaribia kufika.
 
Lutondwe nenda kahamasishe Lupembe kondoo wa kule wamekosa mchungaji.Lupembe wanapenda mabadiliko lakini hakuna mhamasishaji
 
kada maarufu wa chama cha mapinduzi Njombe ambaye alikuwa katibu mwenezi wa kata ya Njombe mjini,Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya jumuiya ya wazazi wilaya ya Njombe pia mjumbe wa mkutano mkuu wa jumuiya ya wazazi Taifa Bwana Lupenza leo amejiondoa rasmi kwenye chama hicho.

Tukio hili ni kubwa kwa hapa Njombe kwani huyu ni moja kati ya makada maarufu wa chama cha mapinduzi waliokuwa mstari wa mbele kupambana na vyama vingine vilivyopo Njombe.

Kujiondoa kwa kada huyo ni ishara tosha kuwa mapigo ambayo yalifanywa na chadema kwenye uchaguzi wa udiwani hapa Njombe mjini yalikuwa ni makubwa kupita kiasi.

Mara baada ya uchaguzi kumalizika na ccm KUPOTEZA kwa kura nyingi kuliko sehemu yoyote Tanzania kumekuwa na vita kubwa ndani ya chama cha mapinduzi hoja kubwa ikiwa ni matumizi mabaya ya fedha za kampeni zilizotolewa na makada wa chama hicho kizee.

Inadaiwa kuwa wapo makada wa chama waliochukua fedha nyingi kwa ajili ya kampeni lakini hawakufikisha kwa wananchi jambo ambalo baadhi ya makada wa ccm hawakubaliani nalo na hivyo kutangaza nia ya kuhama chama.

Baada ya Lupenza kutangaza kujitoa katika chama hicho kuna taarifa za uhakika kuwa wapo pia viongozi wawili waandamizi wa chama hicho ambao wanatarajia kujitoa kuanzia tarehe 12.3.2014.

Kwa namna yoyote ili upepo wa chama cha mapinduzi hapa Njombe ni mbaya sana hasa kutokana na kuongozwa na viongozi wachovu kama chama chenyewe kilivyochoka na kukosa mvuto kwa wananchi.

Bwana Lupenza ametangaza uamuzi wake wa kujitoa ccm katika kituo cha Radio Uplands ya Njombe mjini.Pia ameahidi kujiunga na chama makini kabisa kilichopo hapa Tanzania bila kutaja ni chama gani.

USAHIHI WA HILI JAMBO UPO NA NIMEONA KWA MACHO YANGU, LAKINI NAOMBA TUSISHABIKIE SANA NA KUFURAHIA YANAYOTOKEA KWA WENZETU. nAOMBEMENI HII IKITOKEA KWA WENZETU SISI TUKAZE BUT ILI OPPORTUNITY HII TUITUMIE VEMA KUIMARISHA CHADEMA NJOMBE. CHADEMA HAINA KASI YA KUTOSHA KWASABABU YA VIONGOZI WETU HAWANA KNOWLEDGE YA KUTOSHA NA NEW LEARNINGS TOKA KWA WALIOFANIKIWA ZAIDI YETU HAPA NJOMBE. NA INAWEZEKANA PENGINE INATOKANA NA KUWA NA VIONGOZI WANAOKAIMISHWA TU MARA KWA MARA KUPELEKEA KUTO KUWA NA VIONGOZI WA KUDUMU WALIOSIMIKWA NA WANANCHI/WANACHAMA. TUNAPENDA SANA KUWA NA VYEO VYA KUKAIMISHWA. INAWEZEKANA NIMEKOSEA SANA ILA HUU NI MTAZAMO WANGU TU, PIA SIJAONA HARAKATI ZIKIFANYWA KUWA NA VIONGOZI WA JIMBO. BILA SHAKA NYAGAWA UNAWEZA KUFANYA KAZI HII KWAKUWA NI KIONGOZI NINAEKUAMINI, ILA UKUMBUKE WALE VIONGOZI WALIO NG'OLEWA HAWANAFIFA YA KUENDELEA KUWA VIONGOZI.
 
mbona misukule ya buk 7 haionekani kwenye hii sred????
nimemis uharo wao! sometimes huwa yanatuburudisha kwa pumba yanazomwaga hapa jukwaani!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom