Tukundane
JF-Expert Member
- Apr 17, 2012
- 11,455
- 8,249
Wanachama wa chadema waliwashambulia wanachama wa ccm kwa marungu na kuwajeruhi kwa kuwakata kwapanga usiku wa tarehe 28 kuamkia tarehe29.baada ya kuwafuma wakiwa wanazunguka kila nyumba ya mpiga kura majira ya usiku na kumuhonga kila mpiga kura kiasi cha tsh10000/=.chadema waliamuwa kufanya msako baada ya kutonywa kuwa ccm wanatumia njia hiyo ili waweze kushinda nafasi ya udiwani ambayo ilikuwa inashindaniwa katika kata ya mpapa wilayani mbozi. pia walikamatwa walinzi wa chama hicho na kupigwa kipigo cha mbwa mwizi na kuwapora fedha zote zilizo kuwa zinatumika kuwahonga wapiga kura.wakati huohuo wanachama wa ccm walimtowa nundu mtumishi wa takukuru akiwa kwenye shughuli za kikazi baada ya kuingia kwenye kambi ya wanaccm.