zimmerman
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 1,628
- 3,155
Waberoya bwana, more theoretical than practical, more mswahili than technical....hivi we unadhani CCM walivyo ka nguruwe pori aliyejeruhiwa wanatafuta visingizio vya vyama vya kisiasa hususan Chadema kwa kila tatizo linalojitokeza nchini ili waweze kupata loophole ya kuwashughulikia viongozi wa Chadema kwa kesi za uhaini. Na hapo ndo watakuwa wamewamaliza Chadema. Ni kwa bahati nzuri sana Chadema wana viongozi wenye akili sana. Ni chama kichanga lakini nguvu zao si za bunduki, wala mahakama, wala pesa. Nguvu zao zipo kichwani. Hawafikirii kwa tumbo, wanafikiria kwa kichwa. Wanasoma majira na nyakati na wana data za kutoka jikoni hivyo ndugu Waberoya hawawezi kufata ushauri wako. Hiyo itakuwa suicidal move.
Ni jana tu nilikuwa Muhimbili, pale kwenye epicenter ya mgomo wa Madaktari. Kuna rafiki yangu tulisoma wote Mzumbe secondary so nilienda kumtembelea. Nikamuuliza swali hivi ni kwa nini ninyi madaktari katika madai yenu hamtaki kuongelea posho za wabunge kuiaibisha serikali kwamba hela wanazo isipokuwa ni walafi wendawazimu wabinafsi wasiowekeza kwenye vitu vya msingi? Akanijibu, akasema si kwamba hawafahamu hilo ila hawataki kabisa kuyafanya madai yao ya kisiasa. Wanataka kubaki disciplined kwenye fani yao kwamba madai yao yana msingi wa kitabibu na ni makosa kuingiza siasa kwenye utaalamu.
Ni kwa kigezo hicho pia Chadema hawapaswi kujipeleka kimbele mbele kwenye migomo inayoendelea. CCM ni watu hatari sana na wanataka kubaki madarakani hata ikiwa ni kwa vita. Wakipata evidence kidogo tu kwamba chama pinzani sana kwao kinafacilitate migomo basi kwao hawataangalia mantiki ya mgomo bali wataona ni mkakati wa Chadema nchi isitawalike na hiyo inatosha kufungua kesi ya uhaini, kuwasweka gerezani kina Slaa na kukifuta Chama kabisa. Ndio maana kwa wakati kama huu Chadema wapaswa kuwa wajanja kama nyoka lakini wapole kama njiwa.
Hoja zako nyingine za viongozi wa Chadema kukarimiwa Ikulu kumewapunguzia makali ni propaganda za kijinga zisizostahili kujibiwa. Mtu yeyote akienda Ikulu kwa appointment maalumu atakirimiwa tu -- pale kuna hela imetengwa kwa ajili hiyo so mi nashangaa watu wanaoshadadia upuuzi wa dizaini hii. Waberoya siwezi kuamini na wewe unaweza kuzisilimisha akili zako chini kabisa kiwango hiki.
Ni jana tu nilikuwa Muhimbili, pale kwenye epicenter ya mgomo wa Madaktari. Kuna rafiki yangu tulisoma wote Mzumbe secondary so nilienda kumtembelea. Nikamuuliza swali hivi ni kwa nini ninyi madaktari katika madai yenu hamtaki kuongelea posho za wabunge kuiaibisha serikali kwamba hela wanazo isipokuwa ni walafi wendawazimu wabinafsi wasiowekeza kwenye vitu vya msingi? Akanijibu, akasema si kwamba hawafahamu hilo ila hawataki kabisa kuyafanya madai yao ya kisiasa. Wanataka kubaki disciplined kwenye fani yao kwamba madai yao yana msingi wa kitabibu na ni makosa kuingiza siasa kwenye utaalamu.
Ni kwa kigezo hicho pia Chadema hawapaswi kujipeleka kimbele mbele kwenye migomo inayoendelea. CCM ni watu hatari sana na wanataka kubaki madarakani hata ikiwa ni kwa vita. Wakipata evidence kidogo tu kwamba chama pinzani sana kwao kinafacilitate migomo basi kwao hawataangalia mantiki ya mgomo bali wataona ni mkakati wa Chadema nchi isitawalike na hiyo inatosha kufungua kesi ya uhaini, kuwasweka gerezani kina Slaa na kukifuta Chama kabisa. Ndio maana kwa wakati kama huu Chadema wapaswa kuwa wajanja kama nyoka lakini wapole kama njiwa.
Hoja zako nyingine za viongozi wa Chadema kukarimiwa Ikulu kumewapunguzia makali ni propaganda za kijinga zisizostahili kujibiwa. Mtu yeyote akienda Ikulu kwa appointment maalumu atakirimiwa tu -- pale kuna hela imetengwa kwa ajili hiyo so mi nashangaa watu wanaoshadadia upuuzi wa dizaini hii. Waberoya siwezi kuamini na wewe unaweza kuzisilimisha akili zako chini kabisa kiwango hiki.