Shelute Mamu
Member
- Mar 17, 2009
- 37
- 1
Jamani imenishangaza sana kuona kwamba Chama chenye nguvu, wasomi, sera nzuri leo wanaingia kwenye mtego wa CCM. Wameanza kwa kumtumia Mfadhili wa CCM kupewa fedha za msaada, Chadema wakachekelea, CCM wanawatia moyo kusema si dhambi mfadhili wao kufadhili na vyama vingine!! jana inatangazwa kwamba CCJ imevunjwa na wanaungana na Chadema, Kiongozi wa Chadema wanasema wanafurahia na kusema aliyeingia zamani na anayeingia leo wote ni sawa!!! Hivi Chadema hawalioni hili kwamba CCJ ni mamluki ambao wanakwenda kuimaliza Chadema jamani.
Kumbuka jinsi NCCR kilivyovuma sana na Mrema akiwa mstari wa mbele, alipofanikiwa kukisambaratisha akahamia kwingine. Hamuoni hili kwamba hawa wanatumiwa kuja kudhoofisha Chama? Tafadhali viongozi msije mkawaumiza wanachama wenu waaminifu ambao wamewaamini MNO. Ukiambiwa kitu changanya na akili zako.
Kumbuka jinsi NCCR kilivyovuma sana na Mrema akiwa mstari wa mbele, alipofanikiwa kukisambaratisha akahamia kwingine. Hamuoni hili kwamba hawa wanatumiwa kuja kudhoofisha Chama? Tafadhali viongozi msije mkawaumiza wanachama wenu waaminifu ambao wamewaamini MNO. Ukiambiwa kitu changanya na akili zako.