Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 925
- 4,319
Mijadala mikuu nchini kwa sasa ni umuhimu wa katiba mpya itakayolinda rasilimali za Tanganyika na Muungano kwa ujumla.
Mjadala mwingine ni kuhusu rushwa katika uchaguzi na namna ambavyo CCM inatuhumiwa kutumia fedha hata kwenye chaguzi za vyama vya upinzani
Mjadala wa tatu ni kuhusu ACT Wazalendo na Wabunge kumi na tisa wa upinzani kuungana na CCM dhidi ya Chadema
Mijadala hii yote imezua mgawanyiko mkubwa kwenye chama cha Mapinduzi hasa ikizingatiwa wanachama wengi wasio na madaraka wanatamani kuwepo na katiba mpya waache kunyamazishwa kisa hawana connection na wakubwa.
CCM imepoteza vijana wengi kwa sababu wanaogopa wakisema ukweli wataitwa wasaliti na kuzuiliwa kupata teuzi na mambo kama hayo. Wakati huo vijana wa upinzani wanazidi kuwa wasemaji wakubwa ili wapate ajira na heshima ndani ya chadema na endapo wakihitajika kununuliwa kwenda CCM basi dau liwe kubwa. Kwa muktadha huu vijana wengi wamechagua kuwa upinzani hadi pale watakapopewa chakula.
Kuhusu upinzani ni dhahiri kwamba zito Kabwe pamoja na kuachia madaraka yapo mambo anayofanya kwa hasira ya kuondolewa chadema. Miaka yote yeye anawaona kama chadema ni wapinzani wake wakubwa
Kibaya kinachomsumbua zito ni kuona amapoteza mvuto na anakwenda kufa kisiasa kama walivyokuwa wakina Cheyo, Lipumba na Mrema. Maono na ushawishi wake umemezwa na vipande vya fedha jambo ambalo hakutegemea.
Wakati CCM ikijitafakari , akina Dr Slaa wanazidi kupata uungwaji mkono nje chama cha siasa na hivyo kuifanya ngome ya chadema wakati wa kampeni kupata wapiga kampeni wengi huku CCM ikiwa haina uhakika kama itapata watu zaidi ya akina JK ambao tayari jamii unawaona kama wasaliti na walioshiriki kuuza rasilimali zetu.
Hoja ya DP world na Muungano inakwenda kuwasumbua CCM kwenye chaguzi hasa pale kauli mbiu inapokuwa kwanini bandari za znz hazijauzwa? Kuwaondoa Wamasai Loliondo nako kimahesabiwa kama njia nyingine ya kuufanya uchaguzi uwe mgumu kwani inasadikiwa kuwa wameondolewa kupisha waarabu wamiliki eneo hili kama alivyoanzisha uuzaji mzee Ruksa.
Mijadala hii ni migumu hasa unapokuwa na jamii ya watu wanafiki wanaokuchea huku wakiwa na chuki na wewe. cCm wanafahamu vyema kwamba kura ina siri kubwa na wanaowachekea siyo wote wana wakubali.......Je, CCM itatoka vipi kwenye hizi agenda? Chadema itakuja na agenda gani zaidi ya hizi?
Mjadala mwingine ni kuhusu rushwa katika uchaguzi na namna ambavyo CCM inatuhumiwa kutumia fedha hata kwenye chaguzi za vyama vya upinzani
Mjadala wa tatu ni kuhusu ACT Wazalendo na Wabunge kumi na tisa wa upinzani kuungana na CCM dhidi ya Chadema
Mijadala hii yote imezua mgawanyiko mkubwa kwenye chama cha Mapinduzi hasa ikizingatiwa wanachama wengi wasio na madaraka wanatamani kuwepo na katiba mpya waache kunyamazishwa kisa hawana connection na wakubwa.
CCM imepoteza vijana wengi kwa sababu wanaogopa wakisema ukweli wataitwa wasaliti na kuzuiliwa kupata teuzi na mambo kama hayo. Wakati huo vijana wa upinzani wanazidi kuwa wasemaji wakubwa ili wapate ajira na heshima ndani ya chadema na endapo wakihitajika kununuliwa kwenda CCM basi dau liwe kubwa. Kwa muktadha huu vijana wengi wamechagua kuwa upinzani hadi pale watakapopewa chakula.
Kuhusu upinzani ni dhahiri kwamba zito Kabwe pamoja na kuachia madaraka yapo mambo anayofanya kwa hasira ya kuondolewa chadema. Miaka yote yeye anawaona kama chadema ni wapinzani wake wakubwa
Kibaya kinachomsumbua zito ni kuona amapoteza mvuto na anakwenda kufa kisiasa kama walivyokuwa wakina Cheyo, Lipumba na Mrema. Maono na ushawishi wake umemezwa na vipande vya fedha jambo ambalo hakutegemea.
Wakati CCM ikijitafakari , akina Dr Slaa wanazidi kupata uungwaji mkono nje chama cha siasa na hivyo kuifanya ngome ya chadema wakati wa kampeni kupata wapiga kampeni wengi huku CCM ikiwa haina uhakika kama itapata watu zaidi ya akina JK ambao tayari jamii unawaona kama wasaliti na walioshiriki kuuza rasilimali zetu.
Hoja ya DP world na Muungano inakwenda kuwasumbua CCM kwenye chaguzi hasa pale kauli mbiu inapokuwa kwanini bandari za znz hazijauzwa? Kuwaondoa Wamasai Loliondo nako kimahesabiwa kama njia nyingine ya kuufanya uchaguzi uwe mgumu kwani inasadikiwa kuwa wameondolewa kupisha waarabu wamiliki eneo hili kama alivyoanzisha uuzaji mzee Ruksa.
Mijadala hii ni migumu hasa unapokuwa na jamii ya watu wanafiki wanaokuchea huku wakiwa na chuki na wewe. cCm wanafahamu vyema kwamba kura ina siri kubwa na wanaowachekea siyo wote wana wakubali.......Je, CCM itatoka vipi kwenye hizi agenda? Chadema itakuja na agenda gani zaidi ya hizi?