Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemrejeshea cheo cha Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, na kupanga mikakati ya kukabili CCM katika mikoa yote nchini.
Uamuzi huo ulifikiwa jana na Kamati Kuu ya Chadema, kwenye mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo walipanga bajeti ya kufanikisha mipango yao ya kujiimarisha mikoani.
Zitto alinyang'anywa cheo hicho Novemba mwaka jana kwa kile kilichoelezwa ni kwenda kinyume na uamuzi wa chama.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilieleza kwamba uamuzi huo ulifikiwa baada ya mjadala mzito.
Baadhi ya wajumbe walimlaumu Zitto kwamba msimamo wake wa kutangaza hadharani kupitia vyombo vya habari kuwa hakubaliani na uamuzi wa chama kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, ulisababisha kukigawa chama.
My take:
Hongera NEC-Chadema kwa kutoa maamuzi ya busara na kufikia mwafaka juu ya jambo hili naamini vikao vyenu vilitawaliwa na kuongozwa na vichwa vyenye hekima na busara kubwa mmeonyesha ukomavu wa kisiasa.
Kinachotakiwa sasa muweke pembeni tofauti zenu na muanze kufanyakazi mliyotumwa na wananchi kumbukeni muda siku zote huwa hautoshi.
Uamuzi huo ulifikiwa jana na Kamati Kuu ya Chadema, kwenye mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo walipanga bajeti ya kufanikisha mipango yao ya kujiimarisha mikoani.
Zitto alinyang'anywa cheo hicho Novemba mwaka jana kwa kile kilichoelezwa ni kwenda kinyume na uamuzi wa chama.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilieleza kwamba uamuzi huo ulifikiwa baada ya mjadala mzito.
Baadhi ya wajumbe walimlaumu Zitto kwamba msimamo wake wa kutangaza hadharani kupitia vyombo vya habari kuwa hakubaliani na uamuzi wa chama kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, ulisababisha kukigawa chama.
My take:
Hongera NEC-Chadema kwa kutoa maamuzi ya busara na kufikia mwafaka juu ya jambo hili naamini vikao vyenu vilitawaliwa na kuongozwa na vichwa vyenye hekima na busara kubwa mmeonyesha ukomavu wa kisiasa.
Kinachotakiwa sasa muweke pembeni tofauti zenu na muanze kufanyakazi mliyotumwa na wananchi kumbukeni muda siku zote huwa hautoshi.