CHADEMA Ukonga: John Heche Kuunguruma Ukonga Mazizini Jumapili hii...

Nyahende Thomas

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
211
104
Ndugu wanaJF.

Kwa niaba ya uongozi wa Chadema kata ya Ukonga ninapenda kutumia fursa hii kuwakaribisha katika mkutano wa hadahara utakaofanyika jumapili hii tarehe 04/08/2013 kuanzia majira ya saa 8:00 mchana katika mtaa wa mazizini Kata ya Ukonga Jimbo la Ukonga. Mkutano utafanyika katika uwanja uliopo karibu kabisa na ofisi ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa mazizini.

Mgeni wa heshima ambaye pia atakuwa msemaji mkuu wa mkutano huo atakuwa mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la vijana Chadema kamanda John Heche Suguta, akiambatana na vijana machachari wa CHASO mkoa wa Dar es salaam.

Nawakaribisheni wote mtakaokuwa na nafasi siku hiyo hasa wakazi wa Ukonga, Segerea, Kitunda, Pugu, Gongolamboto, Majohe, Kivule, Banana na maeneo mengine ya jirani mnakaribishwa sana ili tupate kujumuika kwa pamoja kujadiliana juu ya masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa kata yetu ya Ukonga, Jimbo la Uchaguzi la Ukonga, mkoa wetu wa Dar es salaam pamoja na masuala mengine yanayoihusu nchi yetu kwa ujumla.

CHADEMA NGUVU YA UMMA.
 
kujadiliana juu ya masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa kata yetu ya Ukonga, Jimbo la Uchaguzi la Ukonga ...kwanini Ukonga imebaki kuwa nyuma kimaendeleo"hasa miundombini yake? -hiyo barabara ya kutoka hapo FFU (Ukonga Mombasa) kupitia Moshi Bar kila mwaka wa fedha iko kwenye Bajeti lakini haijengwi! Tatizo nini, mpaka Makongoro akawaacha kwenye mataa?
 
kuweni makini na vitu vizito vyenye ncha kali , havichelewi kuteleza mikononi mwa maaskari .
 
Futa kwanza kauli yako ya kudai eti sisi wagogo ombaomba. Usipofuta usije maana tumeandaa mawe utapigika mbaya!
 
Ndio tumemaliza kikao cha mwisho kabisa cha maandalizi. Kila kitu kimekamilika kinachosubiriwa ni siku tu ifike na mkutano ufanyike.
Wakati mbunge wa jimbo la Ukonga na diwani wa kata ya Ukonga wakiwa wameyakimbia maeneo yao ya kazi na hivyo kushindwa kufanya japo mkutano mmoja wa kuwashukuru wananchi ama kusikiliza kero zao, sisi kwa upande wetu Chadema tumekuwa tukiwasiliana na wananchi mara kwa mara na kuyawasilisha matatizo yao katika ngazi mbalimbali za kiserikali kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.

CHADEMA YATOSHA! ccm ya nini?
 
kujadiliana juu ya masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa kata yetu ya Ukonga, Jimbo la Uchaguzi la Ukonga
...kwanini Ukonga imebaki kuwa nyuma kimaendeleo "hasa miundombini yake?
-hiyo barabara ya kutoka hapo FFU (Ukonga Mombasa) kupitia Moshi Bar
kali mwaka wa fedha iko kwenye Bajeti lakini haijengwi! Tatizo nini, mpaka Makongoro akawaacha kwenye mataa?

Mkuu kosa kubwa lililofanywa na wakazi wa Ukonga ni kumchagua mbunge wa ccm na kumchagua diwani wa ccm. Tangu walipotangazwa kuwa washindi hawajawahi kurudi kusikiliza kero za wananchi. Pamoja na kuwa wote wawili walitoa ahadi za kushughulikia kero ya barabara hiyo ya mombasa-moshi bar lakini ghafla wameisahau na hawaikumbuki tena!
 
Ndio tumemaliza kikao cha mwisho kabisa cha maandalizi. Kila kitu kimekamilika kinachosubiriwa ni siku tu ifike na mkutano ufanyike. Wakati mbunge wa jimbo la Ukonga na diwani wa kata ya Ukonga wakiwa wameyakimbia maeneo yao ya kazi na hivyo kushindwa kufanya japo mkutano mmoja wa kuwashukuru wananchi ama kusikiliza kero zao, sisi kwa upande wetu Chadema tumekuwa tukiwasiliana na wananchi mara kwa mara na kuyawasilisha matatizo yao katika ngazi mbalimbali za kiserikali kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi. CHADEMA YATOSHA! ccm ya nini?

"Wananchi Ukonga wataka mbunge wao kujiuzulu"
na Hellen Ngoromera

WANANCHI wa Jimbo la Ukonga, wamemtaka mbunge wao, Eugen Mwaiposa (CCM) kujiuzulu kutokana na kushindwa kushughulikia matatizo yao, hasa kero ya barabara inayowakabili.
Walitoa tamko hilo hivi karibuni jijiniDar es Salaam wakati wa mkutano wao wa kujadili hatima ya adha zinazowakabili watoto wao, wanawake, pamoja na wazee wa jimbo hilo.
Kwa mujibu wa wananchi hao, badala ya kukaa eneo hilo akitatua matatizo ya wananchi wake, Mwaiposa amehama na sasa anaishiMbezi.
Wameeleza kwamba barabara itokayo Ukonga - Mombasa kupitia Moshi Bar kuelekea maeneo mengine haipitiki, hali ambayo huwasababishia adha kubwa wanafunzi, hasa waendapo shule, pia husababisha adha kwa wananachi waendapo hospitali kutokana na aidha nauli kupandishwa kinyemela wakati mwingine kutoka shilingi 300 hadi 500 hali ambayo wakazi wengi hawawezi kuimudu.
Walidai kwamba barabara hiyo inayopita Ukonga Mazizini imekuwaikiiingizia serikali zaidi ya sh milioni 400 kwa mwaka kutokana na ushuru wa machinjio yaliyopo Ukonga.
Naye Mwenyekiti wa kamati teule iliyochaguliwa kushughulikia kero hizo, Amossy Itozya, alisema watoto wanaguswa kwa karibu na kero ya barabara kutokana kupandishiwa nauli mara kwa mara.
Itozya aliongeza kuwa, baadhi ya wajawazito wamekuwa wakijifungulia njiani kutokana na kupata shida kutokana na magari kupita kwa shida kwani barabara nyingi zina mashimo makubwa hali ambayo hufanya ipitike kwa tabu.
Mwingine alieleza kwamba hata Rais Jakaya Kikwete alipokwenda eneo la Moshi bar kuomba kura kwa wananchi, aliahidi kuwa barabara hiyo ingetengenezwa kwa muda mfupi, lakini hilo halijafanyika hadi sasa.
Alipotakiwa kuzungumzia madai hayo ya wananachi mbunge wa huyo alikiri kuwepo kwa ubovu wa barabara hizo, lakini alidai kwamba hawezi kujizulu.
Alisema barabara hiyo ipo chini ya Manispaa ya Ilala na matengenezo yake yalikwama kutokana na wakazi wa Mombasa ambao wanadai fidia ya shilingi bilioni sita.
Nimeshawaagiza manispaa wajenge barabara hiyo kwa wembamba wake ule ule lakini naona hawajafanya hivyo, labda kutokana na upungufu wa fedha, mara nyingi tumekuwa tukimwaga kifusi, lakini mvua ikinyesha inakiondoa chote kutokana na barabara hiyo kutokuwa na mitaro pembeni, alisema mbunge huyo.
Kuhusu madai ya kuhama kwenye makazi yake Mwaiposa alikanusha kuhama Ukonga na kueleza kwamba anaishi Banana eneo la Matembele na kutaka wanaoeneza habari za kuhama kwake kuthibitisha eneo halisi analoishi.

Chanzo: Tanzania Daima
 
Mkuu kosa kubwa lililofanywa na wakazi wa Ukonga ni kumchagua mbunge wa ccm na kumchagua diwani wa ccm. Tangu walipotangazwa kuwa washindi hawajawahi kurudi kusikiliza kero za wananchi. Pamoja na kuwa wote wawili walitoa ahadi za kushughulikia kero ya barabara hiyo ya mombasa-moshi bar lakini ghafla wameisahau na hawaikumbuki tena!

=
Wednesday, July 17, 2013
JESHI LA POLISI LAKUTANA NA VIONGOZI WA WANANCHI WA JIMBO LA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM; MHE MWAIPOSA AONGOZA MAJADILIANO

mwaipo.jpg


Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mhe Eugen Mwaiposa.
JESHI LA POLISI NCHINI LIMEWATAKAWAFANYABIASHARA HUSUSANI WA MAENEO YA STAREHE ZIKIWEMO BAA NA GROCERY KATIKA JIMBO LA UKONGA KUFUATA TARATIBU NA SHERIA ZILIZOWEKWA NA MANISPAA ZAO KATIKA KUENDESHA BIASHARA ZAO ILI KUONDOKANA NA MALALAMIKO YA MARA KWA MARA KUTOKA KWA JAMII INAYOWAZUNGUKA.
AKIZUNGUMZA JIJINI DAR ES SALAAM KATIKA MAJADILIANO YA PAMOJA KATI YA JESHI HILO, VIONGOZI WA WANANCHI NA WAFANYABIASHARA WA ENEO HILO, KAMANDA WA POLISI JAMII NCHINI KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ACP LAZARO MAMBOSASA AMESEMA KUWA JESHI HILO AMBALO LIMEKUWA LIKITUMIA PROGRAMU YA POLISI JAMII KUFANYA ULINZI SHIRIKISHI KATIKA KUSAIDIANA KULINDA AMANI, HALITOSITA KUWACHUKULIA HATUA WALE WOTE WATAKAOBAINIKA KUWA WANAVUNJA SHERIA KWA MAKUSUDI JAMBO AMBALO ASINGEPENDA LITOKEE.
KATIKA KIKAO HICHO AMBACHO PIA KIMEHUDHURIWA NA MBUNGE WA JIMBO HILO MHE EUGEN MWAIPOSA, MADIWANI NA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA, MBUNGE HUYO AMEWATAKA VIONGOZI HAO KULIPA KIPAUMBELE SUALA LA ULINZI SHIRIKISHI KATIKA JITIHADA ZA KUPUNGUZA TATIZO LA UHALIFU KATIKA ENEO HILO NA KUSISITIZA KWAMBA JESHI LA POLISI NI LAZIMA LISHIRIKIANE NA WANANCHI ILI KURAHISISHA MAJUKUMU YAO YA KILA SIKU IKIWEMO KUDHIBITI TATIZO LA UHALIFU.
AIDHA KATIKA HATUA NYINGINE, VIONGOZI NA WAFANYABIASHARA HAO WAMEFANYA HARAMBEE NA KUPATA FEDHA TASLIMU ZAIDI YA LAKI 6 NA AHADI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 1 AMBAZO FEDHA HIZO ZITATUMIKA KATIKA KUNUNUA MATAIRI NA KUJAZA MAFUTA GARI LAPOLISI KWA AJILI YA KUWASAIDIA KUENDESHA DORIA KATIKA MAENEO HAYO.

By: IPS
 
Ndugu wanaJF.

Kwa niaba ya uongozi wa Chadema kata ya Ukonga ninapenda kutumia fursa hii kuwakaribisha katika mkutano wa hadahara utakaofanyika jumapili hii tarehe 04/08/2013 kuanzia majira ya saa 8:00 mchana katika mtaa wa mazizini Kata ya Ukonga Jimbo la Ukonga. Mkutano utafanyika katika uwanja uliopo karibu kabisa na ofisi ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa mazizini.

Mgeni wa heshima ambaye pia atakuwa msemaji mkuu wa mkutano huo atakuwa mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la vijana Chadema kamanda John Heche Suguta, akiambatana na vijana machachari wa CHASO mkoa wa Dar es salaam.

Nawakaribisheni wote mtakaokuwa na nafasi siku hiyo hasa wakazi wa Ukonga, Segerea, Kitunda, Pugu, Gongolamboto, Majohe, Kivule, Banana na maeneo mengine ya jirani mnakaribishwa sana ili tupate kujumuika kwa pamoja kujadiliana juu ya masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa kata yetu ya Ukonga, Jimbo la Uchaguzi la Ukonga, mkoa wetu wa Dar es salaam pamoja na masuala mengine yanayoihusu nchi yetu kwa ujumla.

CHADEMA NGUVU YA UMMA.

:peace:
 
=
Wednesday, July 17, 2013
JESHI LA POLISI LAKUTANA NA VIONGOZI WA WANANCHI WA JIMBO LA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM; MHE MWAIPOSA AONGOZA MAJADILIANO

mwaipo.jpg


Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mhe Eugen Mwaiposa.
JESHI LA POLISI NCHINI LIMEWATAKAWAFANYABIASHARA HUSUSANI WA MAENEO YA STAREHE ZIKIWEMO BAA NA GROCERY KATIKA JIMBO LA UKONGA KUFUATA TARATIBU NA SHERIA ZILIZOWEKWA NA MANISPAA ZAO KATIKA KUENDESHA BIASHARA ZAO ILI KUONDOKANA NA MALALAMIKO YA MARA KWA MARA KUTOKA KWA JAMII INAYOWAZUNGUKA.
AKIZUNGUMZA JIJINI DAR ES SALAAM KATIKA MAJADILIANO YA PAMOJA KATI YA JESHI HILO, VIONGOZI WA WANANCHI NA WAFANYABIASHARA WA ENEO HILO, KAMANDA WA POLISI JAMII NCHINI KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI ACP LAZARO MAMBOSASA AMESEMA KUWA JESHI HILO AMBALO LIMEKUWA LIKITUMIA PROGRAMU YA POLISI JAMII KUFANYA ULINZI SHIRIKISHI KATIKA KUSAIDIANA KULINDA AMANI, HALITOSITA KUWACHUKULIA HATUA WALE WOTE WATAKAOBAINIKA KUWA WANAVUNJA SHERIA KWA MAKUSUDI JAMBO AMBALO ASINGEPENDA LITOKEE.
KATIKA KIKAO HICHO AMBACHO PIA KIMEHUDHURIWA NA MBUNGE WA JIMBO HILO MHE EUGEN MWAIPOSA, MADIWANI NA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA, MBUNGE HUYO AMEWATAKA VIONGOZI HAO KULIPA KIPAUMBELE SUALA LA ULINZI SHIRIKISHI KATIKA JITIHADA ZA KUPUNGUZA TATIZO LA UHALIFU KATIKA ENEO HILO NA KUSISITIZA KWAMBA JESHI LA POLISI NI LAZIMA LISHIRIKIANE NA WANANCHI ILI KURAHISISHA MAJUKUMU YAO YA KILA SIKU IKIWEMO KUDHIBITI TATIZO LA UHALIFU.
AIDHA KATIKA HATUA NYINGINE, VIONGOZI NA WAFANYABIASHARA HAO WAMEFANYA HARAMBEE NA KUPATA FEDHA TASLIMU ZAIDI YA LAKI 6 NA AHADI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 1 AMBAZO FEDHA HIZO ZITATUMIKA KATIKA KUNUNUA MATAIRI NA KUJAZA MAFUTA GARI LAPOLISI KWA AJILI YA KUWASAIDIA KUENDESHA DORIA KATIKA MAENEO HAYO.

By: IPS




Huu ni upuuzi yaani kuhamasisha ulinzi shirikishi aka polisi jamii ndio kwenda kuchangishana hela kununua matairi na petroli kwa gari la polisi kuweza kufanya doria? hawa wanasiasa na viongozi chini ya utawala wa ccm ni bure kabisa, yaani wao ni kufwata pale ambapo raia wamehangaika na kujitengenezea kipato ndio utawakuta wanatengeneza njia za kuwakamua kwa njia yoyote ile ila zile sehemu ambazo ziko duni na miundombinu hakuna wala hawaendi kuhamasisha watu jinsi ya kuboresha mazingira na miundombinu ili njia za kujipatia kipato ziwezekane, inachosa sana.
 
Huu ni upuuzi yaani kuhamasisha ulinzi shirikishi aka polisi jamii ndio kwenda kuchangishana hela kununua matairi na petroli kwa gari la polisi kuweza kufanya doria? hawa wanasiasa na viongozi chini ya utawala wa ccm ni bure kabisa, yaani wao ni kufwata pale ambapo raia wamehangaika na kujitengenezea kipato ndio utawakuta wanatengeneza njia za kuwakamua kwa njia yoyote ile ila zile sehemu ambazo ziko duni na miundombinu hakuna wala hawaendi kuhamasisha watu jinsi ya kuboresha mazingira na miundombinu ili njia za kujipatia kipato ziwezekane, inachosa sana.

... RAIS DKT KIKWETE AONGOZA HARAMBEEE YA KUCHANGIA JIMBOLA UKONGA:
April 25, 2013

339.jpg

Rais Dkt. Jakaya Kikwete akitoa hotuba wakati wa harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiliamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo.


179.jpg

Bendi ya muziki, The Babloom Trio ikitoa burudani wakati wa kuchangia mfuko wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo. kushoto Mkurugenzi wa bendi hiyo Bw.Seif Kisauji pamoja na wanamziki wengine.

246.jpg

Rais Dkt. Jakaya Kikwete akimsikilizaMbunge wa jimbo la Ukonga Mhe.Eugen Mwaiposa wakati akitoa hotuba yake( wapili kushoto kwake) Mwenyekiti wa Ukonga SACCOS Bi.Adivela Ruge akitoa hotuba wakati wa harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiliamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga kuwainua kimaendeleo.


438.jpg

Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo

535.jpg

Isaya Lyimo kutoka CRDB akipewa mkono wa pongezi na Mhe.RAIS Jakaya Kikwete.

626.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na wakikundi wa Ukonga SACCOS

729.jpg

Diwani kata ya Kipawa Mhe Bonnah Kaluwaa (katikat)kiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wake.

===
RAIS Jakaya Kikwete ameongoza harambee ya kutunisha mfuko wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wananchi wanaoishi Jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam kuwainua kimaendeleo.
Katika harambee hiyo iliyofanyika jana kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuudhuriwa na wafanyabiashara mbalimbali kutokaWilaya ya Ilala, jumla ya sh. mil 462 zilikusanywa ikiwa ahadi na fedha taslimu huku Rais Kikwete akichangia mil 5.
Rais Kikwete akizungumza katika harambee hiyo alitoa pongezi kwa mbunge wa jimbo hilo Eugen Mwaiposa kwa kuandaa mkakati huo ambao kama utasimamiwa vema utasaidia kuinua vipato vya wafanyabiashara wa wadogo na wananchi wenye hali duni ya kuendesha maisha yao.
Moja ya lengo la harambee hiyo ni kuanzisha SACCOS ambayo itatumikana wafanyabishara wadogo sanjari na wananchi kukopa na kutunisha mitaji yao ya biashara ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Nimefurahishwa na malengo ya kufanya harambee ili kupata fedha zitakazosaidia kuanzisha SACCOS ambayo ni moja ya Ilani yetu, lakini pia nimejisikia faraja zaidi kuniambia mkakati wenu mwingine ni kuifanya kuwa benki ya Wananchi,.Alisema Kikwete.
Aliongeza kuwa Serikali haina uwezo wa kuajiri kila mtu katika fani mbalimbali huku akisisitiza kuwa ajira nyingi zinazopatikana Serikalini ni walimu na madaktari lakini kwa sekta nyingine hakuna nafasi za kutosha.
Hivyo alitoa mwito kwa vyuo vya ufundi Stadi kutoa mafunzo yanayohitajika kwenye soko la ajira ambayo pia yatakayotoa fursa kwa vijana kujiajiri wenyewena kuwaajiri wenzao sanjari na kuwataka vijana kuhakikisha wanachukua mafunzo yatakayowatia ajira kwa uraisi.
Mbunge wa Jimbo hilo, Mwaiposa alisema eneo lake wakazi asilimia 92 ni wajasiriamali wadogo ambao baadhi yao wamo katika nyanja ya Ufugaji na biashara nyingine na wameshindwa kufikia mafanikio kutokana na kuwa na mitaji midogo.
Aliongeza kuwa harambee hiyo ina malengo matatu moja likiwa ni kuwaondolea changamoto zinazowakabili kwa kuanzisha Saccos na kuendeleza Vikoba 54 vilivyopo sasa kati ya 104 vilivyopo awali.
Pili alisema kuwa ni kutoa elimu ya biashara na kutafuta masoko hali ambayo itasidia kufikia malengo katika shughuli zao za ujasiliamali sanjari na kuondoa matatizo ya maji ambayo ni kero kubwa kwa wananchi wa huko.
Kabla ya harambee hiyo iliyofanyika juzi, Jimbo hilo lilikuwa na mtaji wa mil. 26 zilizotokana na vikundi 128 vya vikoba na mahitaji yalikuwa ni kupatikana Sh. mil 600.
Licha ya Rais Kikwete kufanya jitihada kubwa ya kuchangisha fedha zilizopatikana wengine waliochangia ni Mkurugenzi Mkuu wa Jambo Concept, Juma Pinto ambaye alitajwa kuchangia Sh. mil 4 japo hakuwepo katika halfa hiyo na kupongezwa na mkuu huyo wa nchi.
Namshukuru Pinto kwa mchango wake wa kuchangia maendeleo ya jimbo la Ukonga na aendelee kuwa na moyo huo ili kukoa vijana katika dimbwi la ukosefu wa ajiraalisema Kikwete.

BY: FS
 
Mh Mwaiposa anatia huruma kwa wapiga kura wake kwani tulitegemea ahamasise watu wa H/ya wilaya ya Ilala watengeneze barabara yeye anatuletea ulinzi shirikishi?Kwani kuna mtu alienda kwake kumlalamikia juu ya amani ktk jimbo lake?Au amechagua kuegamia huko kwasababu anajua mchango wake ndio huo wa 200000/-?Hasitufanye watoto wadogo kwani tunaelewa sana nini kiongozi bora anatakiwa kufanya.
 
Back
Top Bottom