Nawaombeni sana kama mnampenda Nasari kwa moyo wa dhati mwambieni ukweli, kwa kufanya hivyo mtakuwa mmemjenga na mmemsaidia.
Siwezi kukubali kumpamba Nasari ilihali najua kuwa ni kweli kachemka!!ni kweli alikurupuka kuzungumza kauli ile. Anachotakiwa kuelewa ni kwamba kila atakachoongea Nassari kina impact kwa jamii, hivyo basi wote waliomkosoa naungana nao weather wawe wana nia njema au mbaya mimi ninawaunga mkono kwani kauli aliyoitoa hakuipima, ni vizuri Nasari akawa makini kwa kauli yoyote atakayoitoa ajue inauzito kwa jamii kama kiongozi na asikurupuke kuufurahisha umma kwani ataaibika na hii itaweza kuharibu sura na taswira nzuri ya chama chetu hivyo kwa wapenda haki wote tuungane kwa hili tumrekebishe Nasari kwa nia Nzuri kabisa.
CHADEMA viongozi wake ni makini sii watu wa kukurupuka na wanachama wake ni watu makini pia. tusiwashambulie wale wanaompinga kwani hawa wanamsaidia huyu kijana wake.
Viongozi wake wakuu pia naamini hawajaifurahia kauli ile hivyo tukemee tumpime kama atarudia tena naamini yeye atajifunza na akiwa muungwana ataomba samahani kwa kauli yake, kwani CHADEMA haina nia wala mpango wa kuigawa nchi, na viongozi wa CHADEMA hawana mawazo ya kitoto.
Siwezi kukubali kumpamba Nasari ilihali najua kuwa ni kweli kachemka!!ni kweli alikurupuka kuzungumza kauli ile. Anachotakiwa kuelewa ni kwamba kila atakachoongea Nassari kina impact kwa jamii, hivyo basi wote waliomkosoa naungana nao weather wawe wana nia njema au mbaya mimi ninawaunga mkono kwani kauli aliyoitoa hakuipima, ni vizuri Nasari akawa makini kwa kauli yoyote atakayoitoa ajue inauzito kwa jamii kama kiongozi na asikurupuke kuufurahisha umma kwani ataaibika na hii itaweza kuharibu sura na taswira nzuri ya chama chetu hivyo kwa wapenda haki wote tuungane kwa hili tumrekebishe Nasari kwa nia Nzuri kabisa.
CHADEMA viongozi wake ni makini sii watu wa kukurupuka na wanachama wake ni watu makini pia. tusiwashambulie wale wanaompinga kwani hawa wanamsaidia huyu kijana wake.
Viongozi wake wakuu pia naamini hawajaifurahia kauli ile hivyo tukemee tumpime kama atarudia tena naamini yeye atajifunza na akiwa muungwana ataomba samahani kwa kauli yake, kwani CHADEMA haina nia wala mpango wa kuigawa nchi, na viongozi wa CHADEMA hawana mawazo ya kitoto.