CHADEMA, Tusiuogope ukweli, tukubali kukosolewa

Nimekuwa nikifuatilia kwa makini mwenendo wa viongozi wa CHADEMA na wafuasi wake na kugundua ni wagumu mno kukubali kukosolewa pale Chama kinapo kuwa kimekwenda visivyo.
Viongozi wa CHADEMA karibuni wamebebeshwa mzigo wa kuzuka kwa vurugu kwenye mikutano mingi na kusababisha mauaji.Hizi ni shutuma nzito,lakini pro-CHADEMA wengi wamekuwa wakikabili yeyote atakaye-challenge uhusika wa CHADEMA katika haya kwa dhihaka,matusi na kejeli.
Hata mambo kadhaa yaliyo ikumba na kuitikisa CHADEMA hujibiwa kwa dhihaka,kejeli na hata matusi toka kwa pro-CHADEMA wengi na hata viongozi mara nyingine.
Mimi kama miongoni mwa mashabiki wa CHADEMA nakuwa na wasiwasi kwa mwenendo huu,CHADEMA itakapo shika dola si itageuka kipofu na kuwa mbaya kuliko CCM?
Nashauri pro-CHADEMA tugeuze mtazamo na kuitazama CHADEMA kwa mtazamo chanya na kujibu hoja kwa hoja na wala si matusi,dhihaka na kebehi.Hii haijengi bali inabomoa chama.
Viongozi wa CHADEMA nao wawe responsible kwa kutupeleka watanzania kuelekea Tanzania tuitakayo!
TANZANIA,nakupenda sana.

Umeona eeh? tazama wanavyotokwa na povu!
 
Hata ARUSHA hamkuona? Kamwela anazungumzia suala la kuwa objective mbona mnaleta ushabiki? Inamaana darasa hili haliwahusu?

Waambie Mkui. Wamesajau hata reaction ya Slaa. dhidi ya ushauri wa Six. Aliishia kutoa matusi badala ya kuchukua hatua za kujisahihisha
 
Watanzania, penye ukweli, watu hukubali kukosolewa, ila hapa JF, kuna watu wako kwenye 'ajira' ya CCM. Wanalipwa kwa kuleta uongo kila siku ili kuchafua wengine. Inasikitisha maana mpaka viongozi CCM wanasema uongo ili kuchafua wengine.

Ndugu yangu uko sahihi na unachokizungumza, we all talks about fact, we should consider where does that fact come from........hasa kwetu sisi vijana tujifunze kufikiri kwa mawazo yetu, na si wa mawazo ya watu wengine.......
 
Si slaa tu , waitwao makamanda wote hawaonekani si Iringa hata Morogoro hawaonekeni. Wanaopata madhara ni watu dhalili hasa hawa wanaoandika humu ndani na CDM haiwajui. Kelele nyingiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

wewe unatoa ushauri gani? Au unaunga mkono? Sijui kama cdm ingekuwa haitakikukosolewa sijui kama inge ungwa mkono na wananchi kiasi hiki!

Haya mafanikio ni matunda ya ushauri na kukubali makosa pale yanapotokea kweli si kukubali kila kitu unacho ambiwa!
Maana umeng'ania slaa haonekani
 
Umemaliza kila kitu! Kama ni ushauri ambao unatolewa humu wa kukikejeli chama na wanachama sijui ana tegemea nini!

Mimi siamini kama wana CHADEMA hawapendi kukosolewa, la hasha. Watu wanachotaka ni kukosoana kwenye ukweli ndani yake. Mtu anapoamka na kusema CHADEMA ni chama cha kikanda unataka ajibiwe nini?? Remember people are entitled to their opinions but not facts. Facts have to be true. Unakosoa ikiwa una facts then watu watasikiliza, lakini maneno ya uzushi na fitna lazima watu watakushambulia. Mbona kuna thread nyingi tu za kushauri CHADEMA humu na zinaheshimika??
 

Kwanini Unaogopa kuwakosoa WAISLAMU; Wanaandamana WENGI TU HAKUNA POLISI, HAKUNA FFU na MABOMU hakuna

Sasa WAO NDIO Wanaweza kuingoza NCHI VIZURI SANA sababu MKUU WA POLISI NI MWISLAMU; JAJI MKUU MWISLAMU;

MKUU WA MAJESHI MWISLAMU na JAJI KIONGOZI MWISLAMU... Sasa wewe UKILINGANISHA na CHADEMA, CHADEMA

hakina Chochote unakiita kidhaifu... Kimbilia kwa WAISLAMU Wao naona wataweza kuongoza DOLA vizuri...

Mkuu hapa umepotoka, kuandamana waislamu kunahusiana nin na uwepo wa mabomu, je ni halali kwa kila muandamanaji apigwe mabomu.........

Hoja kama hizi ndo zile zinazochochea udini,mkuu wa majeshi, jaji kiongozi, mkuu wa polisi, jaji mkuu kuwa muislamu kunahusiana nini na maandamano ya waislamu, kunahusiana nini na maandamo ya wadai haki (iwe ni chama, taasisi au mtu binafsi?) Jipange mkuu.........ushauri wa bure "FIKIRI KWA MAWAZO YAKO USIFIKIRI KWA MAWAZO YA MTU MWINGINE"
 
Try to think twice my dear!
Amejaribu kukupa mfano halisi wewe umekimbilia ambako haukupaswa badala ya kjibu hoja?
Maswali ya msingi?
1.je sensa imekwisha?

2. Je wao hawavunji sheria

3.je ingekuwa ni cdm sema kutoka moyoni hali ingekuwa kama ya leo hapo?

4. Kwa hili una kubali kuwa kuvunja sheria hukumu yake si kupigwa mabomu na risasi?

5. Kwa hili la leo umekubali jeshi la polisi lina mapungufu mengi?

Mkuu hapa umepotoka, kuandamana waislamu kunahusiana nin na uwepo wa mabomu, je ni halali kwa kila muandamanaji apigwe mabomu.........

Hoja kama hizi ndo zile zinazochochea udini,mkuu wa majeshi, jaji kiongozi, mkuu wa polisi, jaji mkuu kuwa muislamu kunahusiana nini na maandamano ya waislamu, kunahusiana nini na maandamo ya wadai haki (iwe ni chama, taasisi au mtu binafsi?) Jipange mkuu.........ushauri wa bure "FIKIRI KWA MAWAZO YAKO USIFIKIRI KWA MAWAZO YA MTU MWINGINE"
 
Try to think twice my dear!
Amejaribu kukupa mfano halisi wewe umekimbilia ambako haukupaswa badala ya kjibu hoja?
Maswali ya msingi?
1.je sensa imekwisha?

2. Je wao hawavunji sheria

3.je ingekuwa ni cdm sema kutoka moyoni hali ingekuwa kama ya leo hapo?

4. Kwa hili una kubali kuwa kuvunja sheria hukumu yake si kupigwa mabomu na risasi?

5. Kwa hili la leo umekubali jeshi la polisi lina mapungufu mengi?


I tried to think more than twice kupata hasa hoja, lakini cjaona hoja hapo mkuu, hebu fikiria kauli kama KUWEPO KWA JAJI MKUU, MKUU WA MAJESHI, MKUU WA POLISI.....AMBAO NI WAISLAMU KUNAHUSIANA NINI HASA NA UDHAIFU WA SERIKALI YA (JK), nimejaribu kuhoji mantiki ya yeye kuhusisha uislamu, na kupigwa mabomu........mantiki ya yeye kuhusisha kuwepo kwa viongozi waislam ndani ya serikali ya jua kali(JK) udhaifu wa utendaji kazi wa JK,
(jaribu kutafakari tena fanya tafakuri zito uone kilichonyuma ya hoja kama hizi)

Mapungufu ya jeshi la polisi hayaonekani mpaka mtu apigwe mabomu tu, mapungufu ya polisi hayaonekani pale waislamu wakiandamana bila kupigwa mabomu, mapungufu ya polisi hayaonekani, pale kunapkuwa na viongozi waislam au waikristo..... bali mapungufu ya jeshi la polisi yanaonekana pale wanaposhindwa kutimiza jukmu lao la kulinda haki na usalama wa raia......

Im not a pro-cdm or pro-ccm, who i am.......ni kuwa huwa nafikri na kuchambua kila lisemwalo na mtu kabla ya kulifanyia maamuzi regardless huyo aliyelisema ni nani (i think its a gud tip kwako pia)

thanks
 
Ni rahisi kuikosoa CCM kwa sababu ya misingi iliyowazi na kwa kanuni zilizoijenga CCM wakati wa kuanzishwa kwake ambayo ikikiukwa inakuwa rahisi kukosolewa…kwaiyo misingi iliyowazi, sera pamoja na itikadi sahihi inayoeleweka kwa wanachama huifanya chama kujipatia wanachama, wapenzi pamoja na washabiki. Hii ndivyo ilivyokuwa kwa ccm wakati wa kuzaliwa kwake. Hivyo basi chama chochote cha siasa hukosolewa kwa kanuni zake, itikadi zake pamoja na sera zake pale tu viongozi wanapokiuka, na hivi ndivyo ilivyo kwa ccm. Tunawakosoa leo kupitia "itikadi yake" ya kwamba ccm ni chama cha wakulima na wafanyakazi wanaamini ktk ujamaa na kujitegemea, sera mbovu na megineyo ambayo yanakiuka miiko ya chama.
Nina mswali haya yanayonisumbua kuhusu cdm;

  1. nini itikadi ya cdm? Iko wazi na inaeleweka kwa wanachama?
  2. Ni nini miiko ya cdm?
  3. Vp kuhusu kununi ya cdm"
wanaJF kwa mtazamo wangu haya mambo yakiwa wazi kabisa yatasaidia ikiwa viongozi wa chama watapotoka itakuwa rahisi kukosolewa…
 
Viongozi wa CHADEMA wanakosolewa wao si Miungu wa kusema kwamba hawawezi kufanya makosa katika maamuzi mbali mbali au katika kauli zao hivyo wanakosolewa tu na hata hapa jamvini wameshakosolewa mara nyingi tu.
 
Polisi ssm ndiyo wanaleta vurugu mbona jana msiba nguvu ya umma ndiyo ililiyolinda ! Arusha hakuna haja ya polisi sisi wananchi tunatosha
 
Back
Top Bottom