CHADEMA si kimbilio la wasomi!

Hao unao waona wavijiweni pia wanapiga kura lakini mkisha pata madaraka mnawa sahau leo hii unawaona hawafai?

Narudia tena mlipo sema ajira mlimaanisha nini? Kama hao wangewezeshwa kwa mikopo na mambo mengine kimaendeleo leo hii wasinge kaa vijiweni bila kufanya chochote.

Cdm watu kama hao ni muhimu tenaa sana kwani cdm ni chama cha watanzania wote bila kujali hali zo kiuchumi.

Hakika maneno unayo yatoa dhidi ya watu hawa hakuna mwana ccmweli wa kuwadharau watu hao kiasi hiki, na chukulia hili kama ni lako binafsi na upeo wako.
Hao unao waona wa vijiweni ndio wanafanya cdm ichukiwe kisa wana wasapoti cdm kama wange kua hawana umuhimu wasinge tumia nguvu nyingi kuwaonga ili wasitoe suport.

Siamini kama hujui mchango wa hawa watu lasivyo hizo data umeziandika bila kufanya utafiti vizuri.

Unashangaza sana.
Mwenzangu unanifumbua macho, hivi ni nini faida ya watu wa vijiweni? Ikiwa toka kuche mpaka jua lizame wenzetu wanapiga hadithi vijiweni, kweli wanaweza kula hadithi. Na watoza kodi watachukua nini kwao?

Sasa naelewa kwa nini CDM katika kampeni zao hutangaza kila kitu NI BURE WAKISHINDA.
 
Haya twambie juhudi gani imefanya serikali yako iliyo jaa wasomi ili kutatua hili tatizo.

Halaf nia yako watu waamini kuwa wanao waunga mkono cdm hawafanyi kazi na kama ingekuwa kweli baasi hili lingekuwa taifa la ajabu,

serikali yako iliwafata hao hao wa vijiweni na kuwaomba kura na kuwaahidi kuwasaidia katika shughuli za maendeleo mkaahamua kuwatupa.

Wameamua kuwaunga mkono cdm wakati wewe una wadharau wenzio walio ndani ya ccm wanaweweseka kwani wanajua umuhimu wao.

Wameamua kuunga mkono cdm maana chama kimewapa matumaini badala ya kutupwa na ccm.

Tangu tumepata uhuru ccm inaongoza kwa hiyo inabidi uwaonyooshee viongozi wako kidole wao ndio sababu ya vijana kukosa kazi, pesa wameficha uswis zote.

Jiulize viwanda vingefufuliwa hao vijana wangebaki vijiweni?
Huu ni ubinafsi na uzembe wa serikali ya ccm ndio umeleta hayo matatizo.

Eti ccmweli ina wasomi twambie faida yao kama viwanda vinaendelea kufa na vingine vimetupwa!
Uchumi unadolola kila kukicha na tuna wasomi, sasa wana tusaidia nini?


Ni kweli mabadiliko huletwa na tabaka la chini, lakini nafikiri hukumuelewa Max kuwa kazi ndio msingi wa maendeleo. Kama Max angekuja TZ na kupewa nchi vijana wa vijiweni wote angewaswaga na kuwapeleka mashambani mfano Gezaulole.

Kifupi Tabaka la chini la wavivu haliwezi kuleta mabadiliko hata siku moja. Kuandamana peke yake hakutoshi, ndio maana ninataka kusikia viongozi wa chadema kuwaambia ukweli wanachama wao kuwa baada ya kuandamana na kuwabwaga CCM, ni nini kitafuata kwa hawa wa kijiweni. Mkishindwa kuwaambia ukweli, na viongozi wenu ni matapeli.

Mwanasiasa ni kiongozi anayewaambia wananchi kile wanachopaswa kusikia, sio kile wanachopenda kusikia. Je mnaweza hayo?
 
1. Hapo kwenye RED tatizo unakaa bila kuwa na kumbukumbu kama CCM ina wanachama wengi kwa nini uchaguzi mkuu 2010 walifunga vyuo vyote na kuwakosesha wanafunzi hao haki yao ya kupiga kura?

2. Hapo kwenye blue bado nakukumbusha tena mafisadi tunaowazungumzia hivi sasa ni wazalendo? na waadilifu? na ni wanachama wa chama gani?

3. Na nakukumbusha tena baraza la mawaziri lililofanyiwa marekebisho hivi karibuni tatizo na sababu hasa za kufanya marekebisho hayo ni nini? na hao mawaziri ni wa chama gani?

4. Kundi kubwa la wauza madawa ya kurevya, majambazi sugu wanalindwa na chama gani? na ni wanachama wa chama gani?

Ukijibu hayo maswali utapata majibu sio kuandika mambo ya kimahaba mahaba na hicho chama unachojifanya kukipenda.

Hapo kwenye red sidhani kama ulikua ni mpango wa serikali kuwanyima wanachuo haki yao ya msingi ya kupiga kura, tusiwe wavivu wa kufikiri jamani. Serikali hii ambayo imekuwa ikitumia nguvu nyingi na rasilimali kuamasisha kwa kuelimisha jamii kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu.

Leo unadiriki kudanganya umma wa watanzania kwamba inatumia mbinu za kufunga chuo ili wanachuo wasishiriki?

Hapo kwenye ufisadi ntatumia maneno yafuatayo "watu wanabadilika", watu hatuwezi kuwa static mkuu, we tend to change kwa kufuata muda na mazingira. Mkuu wa kaya anapowapa heshima mawaziri akurupuki, anateua watu wenye sifa stahili, sema hayo yanayotokea ni huruka ya wachache kati ya wengi tulio kwenye chama. Haikupi nguvu ya kuitimisha kuwa wote CCM sio wasafi kwa kuangalia uovu wa vichwa viwili vitatu. Huko upinzani nadhani mnajua mtu wenu Zitto + Halima Mdee walivyobadilika.

Mambo mengine uliyoandika naona ni tuhuma ambazo vijana wa vijiweni wanapenda sana kuziongelea, sasa sijui na wewe ni mmoja wao? CCM chama kilichounda serikali makini na sikivu, ambacho kina miiko na maadili jambo ambalo ni la kuigwa na vyama vya upinzani kwa kukosa kwao maadili, UNAKIUSISHA NA KUWALINDA MAJAMBAZI?

HII NCHI HATUTAKUJA KUWA NA SHUKRANI KWA HALI HII, ujambazi na uhalifu wa kutumia silaha za moto umekaushwa na kutokomezwa kabisa tangu jembe liingie 2005 na ungefatilia hotuba aliyoitoa bungeni mwaka huo 2005 katika inauguration day, alisema atautokomeza ujambazi na kutowaruhusu majambazi kutamba. MHESHIMIWA AMEFANYA KAMA ALIVYOAHIDI, wewe unakuja kuandika upuuzi gani? muwe mnafatilia matukio ya nchini jamani, mkiona hali ni shwari hivi usidhani imejitengeneza yenyewe. THERE ARE PEOPLE RESPONSIBLE. CCM IDUMU CCM ITAWALE DAIMA.
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.

Utafiti wangu ni kwamba wasomi wengi wanapendelea Chadema, iwe wanachama na wasio wanachama. Wasomi wanaopenda CCM ni wale wanaotafuta nafasi za upendeleo wa kupata UDC.
 
Mbona hutaki kuonesha msaada wa shule kubwa kama za kina Mwigulu nchemba kwa taifa?

Mchumi first class ametusaidia nini kuzui inflation au hao wasomi unao waongelea ndio hao wanao sema vijijini hakuna inflation?

Kila kukicha taifa linapata matatizo ya uchumi lakini unatwambia tuna wasomi, wanalisaidia vipi taifa?
Bidhaa zina panda bei kila kukicha, thamani ya shilingi ina shuka, wasomi wetu wako wapi kutuokoa? Au ccmweli hakuna wachumi, hayo matatuzi yote yana letwa na uchumi kuyumba tena kwa uzembe tu wakati taifa lina wasomi wengi kutoka ccm, wanafanya kazi gani?
Tulitegemea madini ndio yawe chanzo kikuu cha mapato kwa taifa lakini kutokana na ubinafsi wa wasomi kutoka ccm madini yetu hayatufaidishi leo hii tunategemea pombe , walevi wakigoma kunywa beer taifa lina yumba.



"Vijijini hakuna inflation- msomi malecela"
Ndugu zanguni shule zenu ndogo, soma uelewe. Hapo kwenye shule... nilinukuuu huyo CHADEMA niliyomjibu, angalia alama za nukuu ("....")
 
80% ya wafanyakazi ni wapenzi wa CDM? Alow hapo umechemka. Haya jidanganyeni.

unakumbuka matokeo ya urais na ubunge 2010

vilevile wana ccm wanaipenda cdm ndio maana kila siku wanahangaika kuwazuia na kuwaletea vurugu ktk mikutano yao ili waonekane ni cham cha vurugu. unatuambiaje tukio la kifo cha mwandishi nyololo iringa? je mbona ccm walizindua kampeni hadharani polisi hawakuwapiga mbona hakuna ripoti ya kifo? mbona waislamu walipoandamana bila ulizini wala fujo za polisi hakuna kifo? uache ushabiki
 
Naona umechagua njia ya matusi kunogesha hoja yako.
Matusi ni ishara ya kuzidiwa na uzito wa hoja!

Hapo kwenye red sidhani kama ulikua ni mpango wa serikali kuwanyima wanachuo haki yao ya msingi ya kupiga kura, tusiwe wavivu wa kufikiri jamani. Serikali hii ambayo imekuwa ikitumia nguvu nyingi na rasilimali kuamasisha kwa kuelimisha jamii kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu.

Leo unadiriki kudanganya umma wa watanzania kwamba inatumia mbinu za kufunga chuo ili wanachuo wasishiriki?

Hapo kwenye ufisadi ntatumia maneno yafuatayo "watu wanabadilika", watu hatuwezi kuwa static mkuu, we tend to change kwa kufuata muda na mazingira. Mkuu wa kaya anapowapa heshima mawaziri akurupuki, anateua watu wenye sifa stahili, sema hayo yanayotokea ni huruka ya wachache kati ya wengi tulio kwenye chama. Haikupi nguvu ya kuitimisha kuwa wote CCM sio wasafi kwa kuangalia uovu wa vichwa viwili vitatu. Huko upinzani nadhani mnajua mtu wenu Zitto + Halima Mdee walivyobadilika.

Mambo mengine uliyoandika naona ni tuhuma ambazo vijana wa vijiweni wanapenda sana kuziongelea, sasa sijui na wewe ni mmoja wao? CCM chama kilichounda serikali makini na sikivu, ambacho kina miiko na maadili jambo ambalo ni la kuigwa na vyama vya upinzani kwa kukosa kwao maadili, UNAKIUSISHA NA KUWALINDA MAJAMBAZI?

HII NCHI HATUTAKUJA KUWA NA SHUKRANI KWA HALI HII, ujambazi na uhalifu wa kutumia silaha za moto umekaushwa na kutokomezwa kabisa tangu jembe liingie 2005 na ungefatilia hotuba aliyoitoa bungeni mwaka huo 2005 katika inauguration day, alisema atautokomeza ujambazi na kutowaruhusu majambazi kutamba. MHESHIMIWA AMEFANYA KAMA ALIVYOAHIDI, wewe unakuja kuandika upuuzi gani? muwe mnafatilia matukio ya nchini jamani, mkiona hali ni shwari hivi usidhani imejitengeneza yenyewe. THERE ARE PEOPLE RESPONSIBLE. CCM IDUMU CCM ITAWALE DAIMA.
 
Naona umechagua njia ya matusi

Ndugu najitahidi sana kujizui kutukana ingawa hiyo roho ipo, kwakuwa CCM imenijenga kukabiliana na hali yeyote ya ghasia, tufani na hata tsunami, ninakuwa natiririka na hoja bila kuyaingiza matusi. Sasa sijui mtani umeyaona wapi hayo matusi katika hoja yangu?
 
Kikwete fisadi, Mkapa fisadi, Lowassa fisadi, Mwinyi fisadi, Mkullo fisadi, Wabunge wao wote mafisadi wako tayari kuchukua rushwa ili wapitishe makadirio ya bajeti za Wizara mbali mbali. Wale waliokutwa na mapesa chungu nzima kule Switzerland majina yao mpaka leo yanafichwa.

Chama gani Tanzania ni kimbilio la wasomi? Mbona naona chama unachoamini ni kimbilio la wasomi kimegeuka kimbilio la wezi, wala rushwa na waganga njaa? Common, wasomi wapo wapo tu bwana!
 
hao ndiyo Watanzania halisi.na zaidi ndiyo waliopigika na kujua kwanini tunaitaji mabadiliko.

nawapenda sana,hao vijana na watu uliowasema mleta bandiko
 
Zawadi mawazo yako yamefanana na ya gadafi rafiki mkubwa wa ccm alipo ona mambo yanazidi kuwa magumu aliwaita wapinzani wake ni mende, wavuta bangi na wahuni .hongera sana kwa kuona mbali.
 
Nimefanya utafifiti wangu hapa Arusha nimeona ni kweli, naomba nielekeze nitarudisha wapi hii kadi yangu
 
Hakuna msomi anaweza kuwa na muda na chama cha vihiyo. Mnyika ni form six alipata division three halafu wakati wa uchaguzi akadanganya eti ana division 1 ya point 3. Jamani, kuna mbunge wa mpanda wa chadema yeye ni darasa la saba. Jiulize hawa chadema nani amewahi kuwa angalau mkuu wa wilaya. Maprofessor woote ni ccm angalia wakina mwandosa, wangwe, mhongo, tibaijuka. Sasa chade ma ni
professor baregu peke yake. Lweitama ni chakubanga hana sifa za kitaaluma. Kitila mkumbo ni pandikizi amesomea education
Usomi wao unalisiadia nini taifa?Usomi wao uko kwenye makaratasi tu ndio maana wameshindwa hata kujenga kiwanda cha "toothpick"Waana elimu ya ufisadi tu na kulindana?

Hawa jamaa nadhani wengi wao wana degree za kukalili na kuhonga tu.
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
Umeshawahi kuona wapi msomi akaongozwa na kilaza? labda awe msomi wa vyuo kama Modem Commercial,english fontain, Njuweni ndio size ya Mbowe kuwaongoza.
 
hao vijana mnaowadharau na kuwaita wa vijiweni ndio watakao waondoa madarakani....kuna waliokosa mikopo kwa sababu ya kudhaminiana wenyewe......

Vijana wa chuo chungu nzima wapo chadema, ccm hakina mvuto kwa vijana, na mbaya zaidi kuiba na kutafuna keki ya taifa huku wananchi wanabaki na hali duni kunachochea watu kuikataa ccm....

Hata akinamama ambao ndo walikuwa mtaji wa ccm nao wameshtuka,

ccm mnashindwa kujua kuwa watu wanahitaji mabadiliko, wamechoka na mfumo wa chukua chako mapema wakati shilingi 200 ya kununua kipande cha sabuni wanakosa.... Bado mnaleta propaganda zenu za mwaka 2010 hata vuguvugu la mabadiliko hamulioni?

Na wanaoliona wanatumia njia ambazo siyo kuzikabili, mauaji ya kutumia polisi, ukandamizaji wa wananchi, sijui ndo dharau zenu za kuona wananchi wajinga sio wasomi ndo zinawaponza mnadhani wananchi hawaoni? Au ulevi wa madaraka?

Au mmeficha vichwa kwenye michanga? Au mnajiandaa kuizika ccm? Hebu chukueni data kuona idadi ya wabunge na madiwani wa chadema wanavyoongezeka kika chaguzi halafu rudi na mazereu yako hapa.........

Hivi mwananchi (ikiwemo hao wezi na wavutabangi) wakiwauliza wasomi wa ccm wameifanyia nini nchi mtajibuje? Wakiwauliza hatma za richmind, rada, deepgreen nk zinazitokana na wasomi wa ccm mtawajibu nini?

Ccm mjipange, badala ya kutuma watu kwenye mitandao kutukana chadema na kuwaida wadini, wavurugu nk ambazo hata sisi wananchi wa kawaida tusio na vyama tunaona ni longolongo tu za ccm, muwatume waelimishe wananchi kuhusu ccm, nini imetenda (kama yapo) ya kuifanya tuipe kura? Uwajibikaji ndani ya ccm upoje? Sio kila tukio kuwatoa kafara vidagaa tu........

Ccm mna kazi kubwa ya kushawishi wananchi badala ya kutumia mbinu chafu na dhaifu zinazozidi kuipaisha chadema
 
HAMY-D,
Ni kweli CCM kuna wenye ELIMU wengi sana lakini hawajaelimika! Wasomi wanaopata Nobel prize ni kwa sababu ya outcome ya kutumia kuelimika kwao au busara zao kuleta suluhisho ya matatizo mbalimbali hapa duniani. Je hao wenye Elimu hapa kwetu wameleta suluhisho gani?
 
Hakuna msomi anaweza kuwa na muda na chama cha vihiyo. Mnyika ni form six alipata division three halafu wakati wa uchaguzi akadanganya eti ana division 1 ya point 3. Jamani, kuna mbunge wa mpanda wa chadema yeye ni darasa la saba. Jiulize hawa chadema nani amewahi kuwa angalau mkuu wa wilaya. Maprofessor woote ni ccm angalia wakina mwandosa, wangwe, mhongo, tibaijuka. Sasa chade ma ni
professor baregu peke yake. Lweitama ni chakubanga hana sifa za kitaaluma. Kitila mkumbo ni pandikizi amesomea education

na wasiwasi na handbrake ya ubongo wako, lazima imeachia,
 
Sasa Mkuu wangu Zawadi Ngoda: if you know that's how a great thinker should be and act, then why doing contrary?!! what is the opposite of the "great thinker"? ..will i dishonour you to call that?!

a great thinker should:

1. Be well informed about the "matter"(and for this matter, i mean REALLY well informed about the topic before posting, probably well informed kuliko wachangiaji)

2. Understand the magnitude of his/her words before uttering them(and be able to take them back when need arises with modesty)

3.Provide Criticism...CONSTRUCTIVE Criticism.

4. HESHIMA- despite destructive criticism from the opponents, yet to withstand the insults for his/her dignity...not by cursing back, but kwa kukubali kukusolewa(VIBAYA) kwani mtu anaweza asiwe informed sana(remember point number ONE)

5. Logical reasoning and Critical analysis( with evidence based au kwa kutoa data)..not kwa ushabiki, mifano isiyo hai n.k


With above and mengine mengi, that's why nikasema kulikuwa na shida katika this topic...yaani ulivyoijenga, yaani title, then contents n.k because with all that italeta kutoeleweka/kudharaulika(kebehi na kubeza) hata kama nia yako was to provide very good insightful knowledge kwetu Mkuu.
 
Zawadi hasara, kwahiyo nyie wasomi ndiyo mlioleta njaa na kukosesha vijana elimu, ajira ili nyie muuendelee kukaa madarakani ktk NCHI YENU, sisi ambao hatujasoma tunakaa vijiweni kumbe ni wakimbizi
 
Back
Top Bottom