Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kama ni kuwa limbukeni basi nionavyo Chadema wanaelekea huko kwani mengi wayafanyayo inakuwa kama ni mambo ya Mshamba ,inasemwa mshamba kaingia mjini.
Ukiangalia mambo ya Chadema utaona hayalingani ni mambo yanazuka kisha husikii kitu kimya ,Chadema walikuja na mizinga sijui wenyewe wanaita mabomu bungeni yakiozwa na kiongozi walimwita mpambanaji ,mabomu sijui maguruneti yao yalitikisa nchi na kuona sasa hivi nchi itapata Chama tawala kipya,lakini wapi yamepita na yaliobakia ni mapovu tu ,hakuna faida hata moja iliyopatikana hadi hii leo ,kama ipo tuambieni ni faida gani ,tokea mzushe hoja bungeni hadi hii leo ,kipi kimejiri huko bungeni ?
Sasa inaonekana kama Chama kinachochochea fujo katika Taifa hili la Tanzania kwani hawasimamii hoja zao ,wanakuwa kama kinyonga wanabadilika badilika ,leo wanasema hivi baada ya sikumbilitatu inakuwa kama sio wao ,wanazusha jipya ,yaani ni watu wa ajabu ajabu kabisa.
Baada ya Uchaguzi mkuu ,Chadema walishindwa vibaya sana ,kinyume na matarajio yao kuona hivyo ,wakazuka ghafla kuwa hatumtambui ushindi wa Kikwete na hata kwenye kikao Cha bunge wakasusia ,hii ilikuwa kuonyesha msimamo wao kuwa hata serikali hawaitambui ,hatukuona usimamiaji wa hoja yao hiyo kuwa CCM haikushinda uchaguzi na Kikwete sio Raisi halali wa nchi ,na leo hii humsikii yeyote yule kujaribu angalau kugusia tu kuwa Kikwete sio Raisi halali ,hakuna hata mmoja mwenye ubavu wa kutamka hayo hadharani ,sasa hivi wamefulia maana wameshindwa kuendeleza msimamo wa kutomtambua Raisi hata kwa mwezi mmoja.
Juzi juzi wanazua hoja ya kuporwa umeya wakati walizidiwa akili ,wakaitisha maandamano yasiokubalika na vyombo vya ulinzi ,matokeo yake tumeyaona ,yanasikitisha na yanatia huruma, hoja yao ya kusema uchaguzi ulikuwa una mizengwe haikuendelea ,mahakamani hatukuwaona kufikisha madai,inamaana walipelekesha watu kupambana na vyombo vya dola wakati hawana mipango endelevu ,misimamo yao inafia njiani na kuwaacha wananchi solemba.
Labda tuangalie misimamo ya CUF ,utaona hawakumtambua Raisi kwa miezi mnayoijua nyinyi ,hawakuingia kwenye vikao vya uwakilishi kwa miezi mnayoijua nyinyi ,walipinga mambo ya muafaka wa Butiama kwa marefu na mapana na walisema hawatorudi mezani na kweli hawakurudi walisimamia msimamo wao ,sasa hapa mwananchi mwananchama wa kawaida unapata moyo na kutoa sapoti ya hali na mali ikibidi maisha ili kudumisha msimamo wa Chama Chako na unaitikia mwito ukijua Chama kipo nyuma yako ,na hii imetokana na kuwa viongozi wanamsimamo uliothabiti na wanaousimamia na kuuendeleza hadi madai yatekelezwe au serikali ikubali kukaa mezani na kupatikana muafaka japo baadae utavunjika ,lakini serikali imewajibika.
Chadema (Viongozi) sivyo walivyo hawasimamii maelekezo na misimamo yao naweza kusema wanayumba na baada ya kutokea patashika hawaonekani kutetea hoja yao iliyosababisha purukushani.Hivyo ulimbukeni waliokuwa nao ni ule wa kufanya mambo ambayo kwao yanakuwa kama ndoto ,unaamka asubuhi kumekucha nayo imeshapita.
Ukiangalia mambo ya Chadema utaona hayalingani ni mambo yanazuka kisha husikii kitu kimya ,Chadema walikuja na mizinga sijui wenyewe wanaita mabomu bungeni yakiozwa na kiongozi walimwita mpambanaji ,mabomu sijui maguruneti yao yalitikisa nchi na kuona sasa hivi nchi itapata Chama tawala kipya,lakini wapi yamepita na yaliobakia ni mapovu tu ,hakuna faida hata moja iliyopatikana hadi hii leo ,kama ipo tuambieni ni faida gani ,tokea mzushe hoja bungeni hadi hii leo ,kipi kimejiri huko bungeni ?
Sasa inaonekana kama Chama kinachochochea fujo katika Taifa hili la Tanzania kwani hawasimamii hoja zao ,wanakuwa kama kinyonga wanabadilika badilika ,leo wanasema hivi baada ya sikumbilitatu inakuwa kama sio wao ,wanazusha jipya ,yaani ni watu wa ajabu ajabu kabisa.
Baada ya Uchaguzi mkuu ,Chadema walishindwa vibaya sana ,kinyume na matarajio yao kuona hivyo ,wakazuka ghafla kuwa hatumtambui ushindi wa Kikwete na hata kwenye kikao Cha bunge wakasusia ,hii ilikuwa kuonyesha msimamo wao kuwa hata serikali hawaitambui ,hatukuona usimamiaji wa hoja yao hiyo kuwa CCM haikushinda uchaguzi na Kikwete sio Raisi halali wa nchi ,na leo hii humsikii yeyote yule kujaribu angalau kugusia tu kuwa Kikwete sio Raisi halali ,hakuna hata mmoja mwenye ubavu wa kutamka hayo hadharani ,sasa hivi wamefulia maana wameshindwa kuendeleza msimamo wa kutomtambua Raisi hata kwa mwezi mmoja.
Juzi juzi wanazua hoja ya kuporwa umeya wakati walizidiwa akili ,wakaitisha maandamano yasiokubalika na vyombo vya ulinzi ,matokeo yake tumeyaona ,yanasikitisha na yanatia huruma, hoja yao ya kusema uchaguzi ulikuwa una mizengwe haikuendelea ,mahakamani hatukuwaona kufikisha madai,inamaana walipelekesha watu kupambana na vyombo vya dola wakati hawana mipango endelevu ,misimamo yao inafia njiani na kuwaacha wananchi solemba.
Labda tuangalie misimamo ya CUF ,utaona hawakumtambua Raisi kwa miezi mnayoijua nyinyi ,hawakuingia kwenye vikao vya uwakilishi kwa miezi mnayoijua nyinyi ,walipinga mambo ya muafaka wa Butiama kwa marefu na mapana na walisema hawatorudi mezani na kweli hawakurudi walisimamia msimamo wao ,sasa hapa mwananchi mwananchama wa kawaida unapata moyo na kutoa sapoti ya hali na mali ikibidi maisha ili kudumisha msimamo wa Chama Chako na unaitikia mwito ukijua Chama kipo nyuma yako ,na hii imetokana na kuwa viongozi wanamsimamo uliothabiti na wanaousimamia na kuuendeleza hadi madai yatekelezwe au serikali ikubali kukaa mezani na kupatikana muafaka japo baadae utavunjika ,lakini serikali imewajibika.
Chadema (Viongozi) sivyo walivyo hawasimamii maelekezo na misimamo yao naweza kusema wanayumba na baada ya kutokea patashika hawaonekani kutetea hoja yao iliyosababisha purukushani.Hivyo ulimbukeni waliokuwa nao ni ule wa kufanya mambo ambayo kwao yanakuwa kama ndoto ,unaamka asubuhi kumekucha nayo imeshapita.