Mundali
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 749
- 164
CCM mnapoteza muda kudhani strength ya CHADEMA ni viongozi na wafadhili, CHADEMA ni ya wanachama na nguzo yake kuu ni dhamira ya dhati ya ukombozi wa mtanzania huru kutoka katika utegemezi wa kifikra, kiutamaduni na kiuchumi. Mtu mmoja mmoja kamwe hawezi kubadili lengo hili kuu. Aliondoka Katibu mkuu aliyekuwa very strong by then Dr. Amani Waridi Kaburu, akaziba nafasi yake Dr. Wilbrod Slaa, nadhani wote ni mashahidi jinsi chama kinavyozidi kuingia mioyoni mwa watu. Zitto Z. Kabwe alitaka kuuingia mtego wa CCM wa umaarufu, akashituka kabla mambo hayajaharibika. Shibuda kauningia mtego huo, kabaki tia maji tia maji. Kifupi CHADEMA ni chama cha wanachama, CCM mwaweza kumnunua hata Dr. Slaa na umaarufu wake, kesho mimi, wewe na yeye tutakuwa viongozi jahazi litasonga mbele kwa kasi kubwa, maana mtaji wetu ni uadilifu wetu.