Chadema Kortini tena Arusha

Crashwise

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
22,227
8,735
MAMIA ya wakazi wa Jiji la Arusha leo wanatarajia kujitokeza kwenda Mahakamani kusikiliza kesi inayowakabili vigogo wa Chadema, wakiongozwa na Mweyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe na Katibu mkuu, Dk Wilbrod Slaa.
Viongozi hao wa chadema , wakiwepo pia wabunge watatu, Philemon Ndesamburo (Moshi mjini), Joseph Selasini (Rombo) na Godbless Lema (Arusha mjini) na wafuasi wengine 24 wanakabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali Januari 5 mwaka huu.

Kesi hiyo, inayosikilizwa na hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa Arusha, Charles Magesa imekuwa ikihudhuriwa na mamia ya watu hatua ambayo husababisha ulinzi kuimarishwa mahakamani.

Katika kesi hiyo, washitakiwa hao, wanatetewa na Mawakili, Method Kimomogoro na Abert Msando wakati upande wa mashitaka unaongozwa na mwanasheria wa serikali Zakaria Elisaria na wenzake.

Kwa mara ya kwanza leo, Mchumba wa Dk Slaa, Josephine Mushumbusi anatarajiwa kuungana na washitakiwa wengine mahakamani baada ya kukosekara mara mbili kutokana na ugonjwa.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba pia anatarajiwa leo kuunganishwa na watuhumiwa wengine katika kesi hiyo baada ya kukamatwa hivi karibuni na polisi na kushitakiwa kwa kosa hilo moja la kufanya mkusanyiko usio halali.

Washitakiwa wote wapo nje kwa dhamana, kesi hiyo ilitokana na maandamano waliofanya wafuasi wa Chadema, kupinga uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo (CCM) ambapo Chadema wamekuwa wakidai alichaguliwa kinyume cha taratibu.

Katika maandamano hayo, watu watatu waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa kwa risasi baridi na moto.


Source: Mwananchi
 
Mkuu, ngoja ni'lobby kwa mkoloni nichomokee huko...Hii ni never miss bana!
 
MAMIA ya wakazi wa Jiji la Arusha leo wanatarajia kujitokeza kwenda Mahakamani kusikiliza kesi inayowakabili vigogo wa Chadema, wakiongozwa na Mweyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe na Katibu mkuu, Dk Wilbrod Slaa.
Viongozi hao wa chadema , wakiwepo pia wabunge watatu, Philemon Ndesamburo (Moshi mjini), Joseph Selasini (Rombo) na Godbless Lema (Arusha mjini) na wafuasi wengine 24 wanakabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali Januari 5 mwaka huu.

Kesi hiyo, inayosikilizwa na hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa Arusha, Charles Magesa imekuwa ikihudhuriwa na mamia ya watu hatua ambayo husababisha ulinzi kuimarishwa mahakamani.

Katika kesi hiyo, washitakiwa hao, wanatetewa na Mawakili, Method Kimomogoro na Abert Msando wakati upande wa mashitaka unaongozwa na mwanasheria wa serikali Zakaria Elisaria na wenzake.

Kwa mara ya kwanza leo, Mchumba wa Dk Slaa, Josephine Mushumbusi anatarajiwa kuungana na washitakiwa wengine mahakamani baada ya kukosekara mara mbili kutokana na ugonjwa.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba pia anatarajiwa leo kuunganishwa na watuhumiwa wengine katika kesi hiyo baada ya kukamatwa hivi karibuni na polisi na kushitakiwa kwa kosa hilo moja la kufanya mkusanyiko usio halali.

Washitakiwa wote wapo nje kwa dhamana, kesi hiyo ilitokana na maandamano waliofanya wafuasi wa Chadema, kupinga uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha, Gaudence Lyimo (CCM) ambapo Chadema wamekuwa wakidai alichaguliwa kinyume cha taratibu.

Katika maandamano hayo, watu watatu waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa kwa risasi baridi na moto.


Source: Mwananchi
Hapo kwenye red nimepafurahia sana...mwenye macho na aone!...na mapambano na yaendelee!
Kila la heri Albert Msando, na kuna maelfu kwa maelfu ya watu wanaokusaidia kimoyomoyo!, amini usiamini.
 
Police arusha wamejiandaa kuwakabili wafuasi wa chadema wanaotaka kwenda kusikiliza kesi inayowakabili viongozi wao leo

Nawasihi wafuasi wa CDM wasienda maana virungu vya police vitawaumiza
 
Polisi wanajiandaa kwenda kuwalaki CDM, mbona hamkujiandaa kuwalinda wananchi Gongo la Mboto?
 
kwenda kusikiliza kesi ni haki ya kila raia na ni darasa zuri tu. Mimi nilianza kuhudhuria mahakamani kusikiliza kesi tangu miaka ya 1980 kila nilipokuwa likizo. na ilipa uwezo mkubwa na ufahamu mzuri wa kujieleza na kujitetea. hao polisi waache upuuzi.
 
Kwani CDM wameonyesha nia ya kufanya maandamano? kwenda tu mahakamani na kusikiliza kesi kwangu mimi si shida, unless kama chadema wameonyesha nia mbaya yoyote.
Kazi ya polisi ni kuangalia usalama wa maeneo hayo. sio kupiga au kuzuia watu kwenda kusikiliza kesi, wana haki ya kujua kinachoendelea mahakamani juu ya viongozi wao.

Ombi: Wanachadema Arusha endeleeni kuonyesha mshikamano, ila tunawasihi msionyeshe nia yoyote au ishara yoyote ya vurugu au kubishana na hao jamaa. ninachohisi, hawa polisi wanafuata amri walizopewa, na sasa chadema inachukiwa na kuwekewa mikakati. so onyesheni uzalendo na Mungu atawatangulia.
 
Police arusha wamejiandaa kuwakabili wafuasi wa chadema wanaotaka kwenda kusikiliza kesi inayowakabili viongozi wao leo

Nawasihi wafuasi wa CDM wasienda maana virungu vya police vitawaumiza
Acha virungu Gadaffi alitumia mpaka ndege za kivita na helicopter na mwisho kakimbia, nguvu ya umma haizuiwi na kirungu hata siku moja.
 
Hata mimi ni mmoja wao nitakwenda kusikiliza kesi hii inayowahusu wakombozi wa taifa hili!
 
Back
Top Bottom