Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Chadema ilifanikiwa kushika usukani wa kuliongoza jiji la Mwanza, Meya wa jiji akiwa ni wa Chadema. Mara baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita, Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbroad Slaa alitamka hadharani kwenye vyombo vya habari kwamba wanakusudia Jiji la Mwanza linaloongozwa na Chadema kuwa ndio dira ya mfano wa uongozi uliotukuka ambao wakishika nchi watafanya kweli. Wengi tuliamini na kuwa na matumaini hayo tukifikiria Jiji la Mwanza kuwa dira ya mafanikio Chadema katika kuongoza nchi.
Je, matumaini hayo yamefifia? Hapana, nadhani wana nafasi ya kujipanga upya, wameteleza kidogo.
Kosa ambalo viongozi wa juu Chadema wamelifanya ni kutokuwa karibu na uongozi wa halmashari ya jiji la Mwanza ambalo walikalia kiti cha Umeya. Walitakiwa kuwa karibu na kujitahidi kuwapa mbinu na kusaidia kutatua matatizo yaliyokuwa yakijitokeza ili kuleta picha kwa wapiga kura kwamba viongozi wa juu ni wafuatiliaji katika utendaji wa watumishi wa umma.
Matokeo yamekuwa kinyume cha hayo kwani imefikia Madiwani wa Chadema ndio walifanikisha azima ya kumtosa nje ya kiti cha umeya meya wao. Uongozi wa Juu Chadema ukakurupuka kuwafukuza madiwani wake ambao walitumia haki zao kikatiba bila woga wa sera ya uwajibikaji wa pamoja kichama.
Jambo la kujiuliza, uongozi wa Chadema kitaifa walikuwa wapi siku zote hadi waje dakika za majeruhi kufukuza madiwani wake? Kama uongozi wa juu Chadema wangekuwa karibu na wadiwani wake matatizo yaliyojitokeza yangetatuliwa mapema na kusingetokea haya ya kufukuzana na kuachia ngazi jiji la Mwanza kurudi mikononi mwa wahasimu wao CCM.
Makosa yaliyojitokeza Chadema Mwanza:
- Chadema Taifa kutokuwa karibu kufuatilia maendeleo ya uongozi wao jiji la Mwanza.
- Chadema kuelekeza nguvu zote kukijenga chama (M4C) na kusahau kulinda ardhi iliyokumbolewa na hivyo adui kuirudisha kwenye himaya yake.
- Madiwani kukosa uzalendo wa uwajibikaji wa pamoja kwani walikuwa na nafasi ya kumshauri meya wao, kama ilishindikana basi wangeomba uongozi wa juu kuokoa jahazi lisizame.
- Madiwani wa Chadema walisaliti kuungana na CCM badala ya kuomba Chadama taifa wasaidie kuziba nyufa zilizojitokeza.
- Kosa la kushindwa kutamalaki jiji la Mwanza ni hoja ya CCM kuonyesha uchaguzi ujao udhaifu wa Chadema kushika dola.
Binafsi ningependa kuelekeza kosa kwa viongozi wa Chadema taifa badala ya kuwalaumu madiwani wa Mwanza pekee, na pengine uongozi wa CCM mkoa Mwanza unahaki ya kubebeshwa gunia hili la misumari. Mwanza kuna wabunge kadhaa ambao kwa uzoefu wao wa kuwa bungeni wangeweza kuona tatizo hilo mapema na kutafuta njia mwafaka wa kulitatua kuliko kuacha ufa uzidi kupanuka na kufikisha hatua ya sasa.
Chadema wanatakiwa kuangalia kasoro hii na kuanza kujipanga upya, maana kosa ni kosa, na kurudia kosa ni ni mwanguko. Hata hivyo picha isiyo ya kawaida imetokea kutokana na kauli Dr. Slaa kuwa jiji la Mwanza kuwa kielelezo cha mfano wa mafanikio ya Chadema na sasa kugeuka kuwa kitendawili.