Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
CHADEMA ni chama kilichojisukuma mbele kwa kasi nzuri. Mategemeo ya Chama hicho nio makubwa kuliko uwezo wake. Kwa vile uwezo wa CHADEMA unakuwa siku hata siku kijiografia na ukubwa wa changamoto hukuwa vile vile. Kuna wanaodhani changamoto kubwa sana inayokumbana nayo CHADEMA ni uroho wa kugombania uongozi ndani ya chama hicho. Hakika UROHO si tatizo kubwa, tatizo lipo katika Ujengaji wa Demokrasia uendao sambamba na ukuaji wa chama.
Tatizo la Demokrasia ndani ya CHAMA ndio kaburi la chama hicho. Hili si geni na linafahamika ndani na nje ya chama. Kimsingi kila mwanachama aliyetimiza masharti husika, anauwezo wa kugombea nafasi yeyote ya uongozi ndani ya chama toka udiwani mpaka Urais. Si ajabu hata kama waliodhamiria na kuchukua fomu ya kugombea Urais wakawa 30. Cha msingi hapa ni jinsi au njia gani ya kumpata mgombea mmoja atayekiwakilisha chama iwe katika nafasi ya Ubunge, ubunge wa kuteuliwa, Urais na kadhalika. Huu ndio mtihani ambao CHADEMA hautaupita hata siku moja, na ndio mwisho wa mbio za chama hicho cha Maendeleo.
Mh Slaa aka Dr Slaa ni daktari wa theolijia aliokuzwa na kusomeshwa na kanisa na hata kulitumikia kama Padre. Huyu miakayote amefundishwa kutoichallange Biblia, aamini vyote vilivyoandikwa. Si tu kasoma bali amefanya kazi ndani ya kanisa bila kuwa challanged, asemalo wafuasi husema ndio ni kweli tupu. Leo mtu huyu atoke katika kazi hiyo na kutueleza eti awe mwalimu wa Demokrasia. Sina hakika kama ndani ya moyo wake anaweza kubadilika kwa muda mfupi kiasi hiki. Isitoshe ana washauri kama akina Padre Mapunda, huku ni kuua demokrasia kabisa. Na ni mkwa sababu hizi ndio maana Mh Slaa alikimbia CCM.
Katika mazingira kama haya kinachotakiwa ni kuubadilisha uongozi wa juu na kuwaweka watu waliobobea katika maswala ya Demokrasia au watu waliosoma shule za kawaida(serikali) na kuwa na fani kama sheria, uchumi, uongozi na kadhalika. Vinginevyo chama kinakufa kirahisi, tena baada ya uchaguzi mkuu 2015.
Tatizo la Demokrasia ndani ya CHAMA ndio kaburi la chama hicho. Hili si geni na linafahamika ndani na nje ya chama. Kimsingi kila mwanachama aliyetimiza masharti husika, anauwezo wa kugombea nafasi yeyote ya uongozi ndani ya chama toka udiwani mpaka Urais. Si ajabu hata kama waliodhamiria na kuchukua fomu ya kugombea Urais wakawa 30. Cha msingi hapa ni jinsi au njia gani ya kumpata mgombea mmoja atayekiwakilisha chama iwe katika nafasi ya Ubunge, ubunge wa kuteuliwa, Urais na kadhalika. Huu ndio mtihani ambao CHADEMA hautaupita hata siku moja, na ndio mwisho wa mbio za chama hicho cha Maendeleo.
Mh Slaa aka Dr Slaa ni daktari wa theolijia aliokuzwa na kusomeshwa na kanisa na hata kulitumikia kama Padre. Huyu miakayote amefundishwa kutoichallange Biblia, aamini vyote vilivyoandikwa. Si tu kasoma bali amefanya kazi ndani ya kanisa bila kuwa challanged, asemalo wafuasi husema ndio ni kweli tupu. Leo mtu huyu atoke katika kazi hiyo na kutueleza eti awe mwalimu wa Demokrasia. Sina hakika kama ndani ya moyo wake anaweza kubadilika kwa muda mfupi kiasi hiki. Isitoshe ana washauri kama akina Padre Mapunda, huku ni kuua demokrasia kabisa. Na ni mkwa sababu hizi ndio maana Mh Slaa alikimbia CCM.
Katika mazingira kama haya kinachotakiwa ni kuubadilisha uongozi wa juu na kuwaweka watu waliobobea katika maswala ya Demokrasia au watu waliosoma shule za kawaida(serikali) na kuwa na fani kama sheria, uchumi, uongozi na kadhalika. Vinginevyo chama kinakufa kirahisi, tena baada ya uchaguzi mkuu 2015.