Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Nikiwa kama mkazi wa kudumu wa Mwanza na ninayeitakia mema CDM katika harakati zake nimefurahishwa sana na CDM kupoteza kiti cha umeya wa jiji. Hii itawapa furs nzuri sana CDM kuepukana na lawama za hali ya juu huko tuendako. Jiji la Mwanza chini ya mkurugenzi aliyepo sasa Bw Wilson Kabwe kupata maendeleo ni ndoto za mchana, hata kama Meya atakuwa Tundu Lissu au my favorite Mnyika. Ili Meya wa jiji afanye kazi yake vizuri anatakiwa kuwa na timu nzuri na yenye mtazamo wa maendeleo toka upande wa halmashauri, kwa Mwanza hilo halipo. Ukienda jiji la Mza utashangaa sana kuona wafanyakazi waliojaa mtazamo wa rushwa na uvivu wa hali ya juu. Kiburi kiko kwa muhudumu wa ofisi hadi mkuu wa idara, mkurugenzi ndio muasisi wa kiburi. Huyu jamaa ana nguvu kuliko waziri mkuu Pinda, anachoamua yeye hakuna wa kuuliza au kupinga. Madiwani wote wa CDM wallop ajitokeze mmoja humu jukwaani na kusema alipingana hadharani na Kabwe!!
Jiji lina ofisi za hovyo, wafanyakazi wamebanana ofisini, wanazurura kutwa nzima kwenye makorido, hakuna customer service kabisa, vyoo ni vichafu hadi aibu... Meya gani ataleta ,maendeleo katika mazingira hayo, heir kuwaachia CCM waendelee kushindwa. Wakuu wa idara jiji pale hawakai ofisini wanakimbizana na posho tu kila siku! Nani atakaa na madiwani wa CDM kupanga na kutekelezeka mipango ya maendeleo wakati watendaji ni wavivu na wabinafsi namna hiyo. Furahieni kupata fursa nzuri ya kujitenga na utendaji mbovu wa Kabwe hadi wakati muafaka utakapofika. Meya na mkurugenzi wanatakiwa kufanyakazi kama timu, umeona wapi timu inayochanganya Mwizi na Mkimbiza Mwizi au mpambanaji wa ufisadi.
Sidhani kama CDM wanalo la kujivunia katika mwaka mmoja na nusu wa umeya, Kama lipo naomba nikosolewe. Barabara ni za mavumbi na nyingi hadi Leo greda halijapita toka mvua zilipoisha. Wakati Pinda kaja Mza nilikutana na greda linatengeza barabara ya Buswelu Kiseke saa 4 usiku na madiwani wa CDM huenda walishiriki kuhalalisha huu usanii Kama walivyoshiriki kuhalalisha ujenzi wa barabara ya lami kwenda kwenye hotel moja tu ya Malaika yenye urefu wa Kilometa 10 kwa ajili ya hotel ya vyumba 24 wakati maelfu ya wakazi wa Buswelu hawana barabara hata ya kiwango cha vumbi. Mkandarasi jasco yup hadi leo site anajenga barabara kwa fedha za msaadanwa benki ya dunia kwenda kwenye hotel ya tajiri mmoja
Ni kwa mazingira hayo Mimi Ulukolokwitanga Ng'wizukulunzungu nimefurahishwa na nafasi kifisadi kurudisha kwa mafisadi hadi katiba mpya itakapoweka wazi nafasi ya meya na mkurugenzi
Jiji lina ofisi za hovyo, wafanyakazi wamebanana ofisini, wanazurura kutwa nzima kwenye makorido, hakuna customer service kabisa, vyoo ni vichafu hadi aibu... Meya gani ataleta ,maendeleo katika mazingira hayo, heir kuwaachia CCM waendelee kushindwa. Wakuu wa idara jiji pale hawakai ofisini wanakimbizana na posho tu kila siku! Nani atakaa na madiwani wa CDM kupanga na kutekelezeka mipango ya maendeleo wakati watendaji ni wavivu na wabinafsi namna hiyo. Furahieni kupata fursa nzuri ya kujitenga na utendaji mbovu wa Kabwe hadi wakati muafaka utakapofika. Meya na mkurugenzi wanatakiwa kufanyakazi kama timu, umeona wapi timu inayochanganya Mwizi na Mkimbiza Mwizi au mpambanaji wa ufisadi.
Sidhani kama CDM wanalo la kujivunia katika mwaka mmoja na nusu wa umeya, Kama lipo naomba nikosolewe. Barabara ni za mavumbi na nyingi hadi Leo greda halijapita toka mvua zilipoisha. Wakati Pinda kaja Mza nilikutana na greda linatengeza barabara ya Buswelu Kiseke saa 4 usiku na madiwani wa CDM huenda walishiriki kuhalalisha huu usanii Kama walivyoshiriki kuhalalisha ujenzi wa barabara ya lami kwenda kwenye hotel moja tu ya Malaika yenye urefu wa Kilometa 10 kwa ajili ya hotel ya vyumba 24 wakati maelfu ya wakazi wa Buswelu hawana barabara hata ya kiwango cha vumbi. Mkandarasi jasco yup hadi leo site anajenga barabara kwa fedha za msaadanwa benki ya dunia kwenda kwenye hotel ya tajiri mmoja
Ni kwa mazingira hayo Mimi Ulukolokwitanga Ng'wizukulunzungu nimefurahishwa na nafasi kifisadi kurudisha kwa mafisadi hadi katiba mpya itakapoweka wazi nafasi ya meya na mkurugenzi