The Invincible
JF-Expert Member
- May 6, 2006
- 6,003
- 3,269
Ndugu Wapenzi wa CCM, hili swala ni zito kuliko chaguzi hizi kama mnavyoweza kumpeleka JK nchi za nje na El kuwa ofisini mwake akipata lunch na viongozi wengine wakiweka sahihi mikataba haraka haraka kabla ya zengwe halijapatiwa kikomo. Huyo diwani ataongoza kitu gani ikiwa nchi ni muflis... si ndio yale ya kusema Diwani fulani hafai hata kwa kulumangia!.. Huo udiwani chukueni lakini mchekecho utapokuja tokea pumba zote ikiwa ni pamoja na chaguzi kama hizi zitajitenga. Tunaanza na juu huko chini kutanyooka bila hata joto kali.
Vipi mnakuwa wepesi kutazama viongozi wa Upinzani ktk chaguzi za madiwani 16 lakini sio viongozi wa CCM ambao sii ajabu tayari fedha za benki zimeisha miminwa ktk wilaya zao kuhakikisha Ushindi pasipo kusimamisha Ufisadi.
SiSi M ni wahuni tu. Vibaraka wao wanakuja humu kujaribu kupotosha hoja ya msingi. Hamtafanikiwa. Lazima uozo ufukuliwe, tuone tunavyoliwa mchana kweupeee.
Halafu JK kiguu na njia kwenda kuomba misaada nje na kuitangaza kama mafanikio ya serikali yake. Mimi binafsi natafsiri kuomba misaada kama kuuza uhuru wetu kwa bei chee. Ukoloni huooo unarudi. JK hana uwezo wa kuongoza nchi huru/inayojitegemea?
Are our leaders(governing) a bunch of thieves?