Chadema CUF TLP NCCR - LIVE from Urafiki Social Hall

i) Siasa ni mapenzi ya mtu ndugu yangu. Vyama vya upinzani sio walinzi wa kuhakikisha watu hawarudi CCM. Ni jukumu la mtu mwenyewe kuamua anataka chama gani na yupo huru kuhama na kuhamia chama kimoja kwenda kingine wakati wowote. Kwa hiyo Njelu Kasaka alikuwa na hiari ya kutoka CCM na kurudi huko kama alivyofanya kwa jinsi akili yake ilivyomtuma. Kwa vyovyote vile upinzani haukupaswa kuwajibika na wala sasa hauwajibiki kumlinda Kasaka asirudi CCM. Hiyo ni juu yake.
Ooo pu!, Nashukuru, nilisahau kaka yangu kwamba na wewe ulikuwa CCM, kwa ridhaa yako ukaondoka, alafu kwa ridhaa yako pia waweza urudi huko CCM... kweli bwana Katiba ina[wa|ku]linda

ii) In the second issue, you are really missing the point. Binafsi sipo hapa kutafuta kura. This is not a vote fetching forum. We are exchanging views about the fate of our beloved country. Kama wewe upo hapa kukitafutia chama fulani kura, endelea lakini usifikiri na wengine tunafanya kazi hiyo.
Kwa vyovyote vile mimi siye kabisaaa niondoe huko, angalia sijawahi thubutu hata kuwa mwanachama wa chama kimojawapo kama wewe ambaye tayari umeshakuwa mwanachama wa at-least vyama viwili..
Lakini Nashukuru kwa kujua kwama kumbe hapa ni ThinkTank yenu,,,

iii) Niseme pia hili maana linajirudiarudia sana. Katika upinzani na hasa CHADEMA tunaamini katika tofauti ya mawazo, maadili na unyoofu. Hatuamini katika ghiliba. Kwa hiyo hatupo tayari kupata kura kwa ghiliba, na kama ghiliba ndio njia pekee ya kushinda uchaguzi Tanzania basi tupo tayari tubaki kuwa wapinzani milele! Tutauza mawazo yetu na wananchi watatupima kwa yale tunayoyafikiri, kusema na kuyatenda. Tunatekeleza wajibu wetu kama chama, uamuzi bado ni wananchi wenyewe.

Saafi sana, nimeipenda sana, umeiweka vizuri, kwa kweli umuandishi mzuri, na mpangiliaji point mzuri,,, naomba tu ili niipate kwa msisitizo unielekeze kwenye kifungu cha katiba yenu ili niweze kuhakiki kwamba hii ni kauli ya CHADEMA na wala sio kwamba ni imani yako,,, wakati wengine probably sio hivyo... Otherwise Nakuaminia ndugu yangu.
URL inatosha sana mkuu sipendi kukuchosha.
 
Saafi sana, nimeipenda sana, umeiweka vizuri, kwa kweli umuandishi mzuri, na mpangiliaji point mzuri,,, naomba tu ili niipate kwa msisitizo unielekeze kwenye kifungu cha katiba yenu ili niweze kuhakiki kwamba hii ni kauli ya CHADEMA na wala sio kwamba ni imani yako,,, wakati wengine probably sio hivyo... Otherwise Nakuaminia ndugu yangu.
URL inatosha sana mkuu sipendi kukuchosha.

Kaka

Maelezo ya Kitila ni msimamo rasmi wa chama uliopo kwenye katiba na Kanuni ya CHADEMA- Itikadi ya CHADEMA inazungumza wazi kuhusu uhuru(ikiwemo uhuru wa mawazo) na maadili(rejea http://www.chadema.net/nyaraka/itikadi.php). Pia suala la kusimamia ukweli na uadilifu ni sehemu ya msimamo wa chama katika kanuni na dhana hii inasilishwa na rangi nyeupe katika bendera yetu(rejea http://www.chadema.net/chama/bendera.php).

Kwa maelezo zaidi tembelea katiba ya CHADEMA inapatikana hapa tembelea www.chadema.net itapata nakala Katiba ya CHADEMA.

Nashukuru sana kwa maoni yako kuhusu upinzani kuboresha udhaifu wa ndani ili kuweza kukishinda chama cha zamani, Chama Cha Mafisadi

Mabadiliko yanawezekana, kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona

JJ
 
Mnyika,,, Mnikiamini na Kutekeleza Haya ninyi Mtakuwa Chama Kizuri sana....


Kauli moja tu ambayo inaenda kinyume na maadili yenu na ambayo umeitoa wewe ni hii hapa

Nashukuru sana kwa maoni yako kuhusu upinzani kuboresha udhaifu wa ndani ili kuweza kukishinda chama cha zamani, Chama Cha Mafisadi

Hii kauli haitendei haki wananchama wa CCM na Watanzania wengine, Kumbuka CCM ni ya viongozi na Wanachama, sasa kunaweza kuwa na viongozi wachache Mafisadi, kama ambavyo wapo pia kunye upinzani, lakini hii haifanyi chama chote kiwe hivyo,,, otherwise hata wanachama mnaowapata kutoka CCM ni mafisadi, na hivyo wanaweza kufanya chama chenu pia kiwe cha Mafisadi.

Kwa kuwa CCM ni ya wanachama, unataka kusema unauambia Umma kwamba Mzee Rashid Kawawa ni Fisadi, Unataka Kusema DR. SAS ni fisadi, Mtu wa Pwani naye fisadi, FD naye fisadi, tunajenga taifa gani hapa?

Kama Kiongozi na Mwanachama wa Chama Makini, naomba-u-withdraw usemi wako...




Itikadi ya Chama

CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI (center party).

CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.


CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.


CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.


CHADEMA inaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri.


CHADEMA inaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo za haki.


CHADEMA inaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa.


CHADEMA inaweka umuhimu wa pekee katika familia kama moja ya taasisi muhimu ya kijamii.


CHADEMA inaamini katika umuhimu wa uhuru wa kuamini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola.


CHADEMA inaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu.


CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.


CHADEMA inaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake.
 
Mhh Itikadi Yao Imtulia Je?ya Ccm Ni Ipi Kwa Sasa?

Mpaka Kieleweke

Asante, ila hii itikadi isomwe baada kwanza ya kusoma falsafa ya CHADEMA hapa http://www.chadema.net/nyaraka/falsafa.php

Falsafa ni FIKRA(ipo akilini); Itikadi ni IMANI(ipo moyoni); ukichanganya yote mawili ndio unapata CHADEMA- chama mbadala kinachoamini katika falsafa ya nguvu ya umma na itikadi ya mrengo wa kati.

Kilitime

Nitaondoa ile kauli kama utaondoa kauli yako kwamba CHADEMA "itakuwa chama makini na kizuri hapo baadae"; naomba usema chadema ni chama makini na kizuri.

Ni kweli kuna viongozi wachache wazuri ndani ya CCM, na wachama wengi tu wazuri ambao wanakubali kuburutwa na viongozi mafisadi. Ndio maana utasikia kauli "CCM inawenyewe na watu kibao!" Sasa hao watu kibao naweza nikawaondoa kwenye kundi la Chama Cha Mafisadi lakini sio hao MAFISADI.

Enyi wema mlioko CCM, endeeleni kukaa kimya badala ya kusimama na kuhesabiwa- au mmekumbwa na Luficer Effect? (rejea makala ya Kitila)

Wakati ndio sasa, mkane sasa ama mtakuwa wanachama wa Chama Cha Mafisadi!

JJ
 
Mabadiliko ya Kweli hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale eti kwa ari, nguvu na kasi mpya, kwa falsafa ya chukua chako mapema ya Chama Cha Mafisadi, Tanzania yenye neema haiwezekani. Enyi wanaCCM asili- ni wakati wa kuwaondoa mafisadi kwenye chama chenu mwezi huu wa Novemba. Mkiwanyamazia, msiendelee kulaumu tukisema mna chama cha zamani, Chama Cha Mafisadi
 
Mnyika,

Kwenye uongozi wenu mna nafasi ya katibu mwenezi? Kama mnayo nakuomba kwa heshima na taadhima uichangamkie inakufaa sana.... Unakumbuka yule waziri wa habari wa Saadam Hussien,,, kwa hili uko juu mkuu!!! Lakini kwa uongozi mwingine nakushauri endelea kujifunza zaidi...baadaye utakuwa kiongozi mzuri sana, make the base now!!! do not rush...

Mhh Itikadi Yao Imtulia Je?ya Ccm Ni Ipi Kwa Sasa?

Kuhusu upande wa CCM naomba niweke hapa kunogesha mjadala

Binadamu wote ni Sawa
Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru


AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI


(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
(3) Nitajitolera nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashjirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
 
Back
Top Bottom