Waziri2025
Senior Member
- Sep 2, 2019
- 148
- 379
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa Wa Arusha kimekutana na kujadili changamoto za urejeshwaji wa fomu za wagombea wake Katika nafasi ya Serikali za Mitaa Kitongoji na Vijiji.
Aidha, chama hicho kimebaini kuwa zoezi hilo lilifanyika bila kuwepo kwa demokrasia kwani wagombea wake walikuwa wananyanganywa fomu na kuchanwa kwa kutumia mabavu huku wakitishiwa kwa bastola kupitia kwa makada Wa CCM
Akizungumza na vyombo vya habari Katibu wa CHADEMA Arusha Innocent Kisanyage Amesema kwamba makada wa chama chamapinduzi CCM wamekua wakitumia nguvu kubwa kunyanganya Fomu za wagombea na kuchana kwa kushirikiana na wasimamizi wa vituo huku watendaji wa Kata wakikimbia vituo vyao vya kazi .
Amesema kitendo hicho kinaonyesha kwamba CHADEMA Mkoa Wa Arusha bado ni tishio kubwa kwakua inatumika nguvu nyingi kuhakikisha kwamba wanashindwa kuwaweka wagombea.
Aidha Baadhi ya wagombea walio nyanganywa fomu zao na kupigwa mapanga na wengine kunyooshewa bastola wamesema walifika kituo kikuu cha Polisi jijini Arusha lakini walijibiwa watoe fomu za kugombea ndio wapate P 3 ili waweze kupatiwa matibabu.
Sakata la urudishwaji wa fomu kwa wagombea wa vyama vya siasa limebubujikwa na sintofahamu kwani watendaji wamekua wakiwarudisha wagombea wa upinzani kwa kile wanacho dai kwamba hawana sifa za kugombea nafasi hizo.
Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema amesema kwamba kitendo hicho nicha kihuni kwani CCM wanatumia nguvu kubwa kuaharibu uchaguzi na kama wanataka upinzani wajitoe waseme kwamba uchaguzi ni wa chama kimoja tu.
Lema ameongeza kwamba, awapo tayari kuona uchaguzi mdogo unatumika nguvu kubwa kuwaumiza wagombea kwa kunyooshewa bastola mapanga kwani nchi hii ni ya kila Mtanzania na sio mtu mmoja peke yake.
Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha Elisa Mungure amesema mpaka sasa vijiji vyote katika jimbo la Arumeru Magharibi na mashariki Munduli akuna mgombea aliyefanikiwa kurejesha fomu na kumekuwepo na uhuni mkubwa kwa kutishiwa na wengine kukimbiwa na watendaji wa kata.
Uchaguzi huo Mdogo kabla kuelekea uchaguzi mkuu mwakani tayari umeonyesha kwamba CCM aikubaliki ndio maana wanatumia jeshi la Polisi kuvuruga uchaguzi huo
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Arusha Msena Bina amesema akuna malalamiko yoyote walio pokea kutoka kwa CHADEMA wala wagombea wa nafasi hizo .
Aidha, chama hicho kimebaini kuwa zoezi hilo lilifanyika bila kuwepo kwa demokrasia kwani wagombea wake walikuwa wananyanganywa fomu na kuchanwa kwa kutumia mabavu huku wakitishiwa kwa bastola kupitia kwa makada Wa CCM
Akizungumza na vyombo vya habari Katibu wa CHADEMA Arusha Innocent Kisanyage Amesema kwamba makada wa chama chamapinduzi CCM wamekua wakitumia nguvu kubwa kunyanganya Fomu za wagombea na kuchana kwa kushirikiana na wasimamizi wa vituo huku watendaji wa Kata wakikimbia vituo vyao vya kazi .
Amesema kitendo hicho kinaonyesha kwamba CHADEMA Mkoa Wa Arusha bado ni tishio kubwa kwakua inatumika nguvu nyingi kuhakikisha kwamba wanashindwa kuwaweka wagombea.
Aidha Baadhi ya wagombea walio nyanganywa fomu zao na kupigwa mapanga na wengine kunyooshewa bastola wamesema walifika kituo kikuu cha Polisi jijini Arusha lakini walijibiwa watoe fomu za kugombea ndio wapate P 3 ili waweze kupatiwa matibabu.
Sakata la urudishwaji wa fomu kwa wagombea wa vyama vya siasa limebubujikwa na sintofahamu kwani watendaji wamekua wakiwarudisha wagombea wa upinzani kwa kile wanacho dai kwamba hawana sifa za kugombea nafasi hizo.
Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema amesema kwamba kitendo hicho nicha kihuni kwani CCM wanatumia nguvu kubwa kuaharibu uchaguzi na kama wanataka upinzani wajitoe waseme kwamba uchaguzi ni wa chama kimoja tu.
Lema ameongeza kwamba, awapo tayari kuona uchaguzi mdogo unatumika nguvu kubwa kuwaumiza wagombea kwa kunyooshewa bastola mapanga kwani nchi hii ni ya kila Mtanzania na sio mtu mmoja peke yake.
Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha Elisa Mungure amesema mpaka sasa vijiji vyote katika jimbo la Arumeru Magharibi na mashariki Munduli akuna mgombea aliyefanikiwa kurejesha fomu na kumekuwepo na uhuni mkubwa kwa kutishiwa na wengine kukimbiwa na watendaji wa kata.
Uchaguzi huo Mdogo kabla kuelekea uchaguzi mkuu mwakani tayari umeonyesha kwamba CCM aikubaliki ndio maana wanatumia jeshi la Polisi kuvuruga uchaguzi huo
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Arusha Msena Bina amesema akuna malalamiko yoyote walio pokea kutoka kwa CHADEMA wala wagombea wa nafasi hizo .