Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,976
- 32,380
Wanabodi.
Chadema mnatakiwa kujitathimi upya na harakati zenu za kisiasa toka mlipotoka mpaka mnapoelekea hivi sasa. Acheni kuichezea serikali.
Katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, Chadema walianza kwa kupinga matokeo ya Rais yaliyompa ushindi Jakaya Kikwete, wakasusa kuhudhuria tukio la kutangaza matokeo pale viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam. Wakasusa sherehe za kuapishwa kwa Rais, wabunge wao wakatoka nje ya Bunge wakati Rais Kikwete akizindua Bunge la Tanzania, kwa madai ya kutomtambua Rais.
Hawakuishia hapo, baada ya ndoto zao za kuingia Ikulu kusambaratishwa na Watanzania, viongozi wa Chadema wakaanza kuandaa maandamano katika mikoa mbalimbali wakafanya hivyo Arusha, Mwanza, Mbeya, Songea, na Katibu Mkuu Dr Slaa aliendelea kuwahamasisha wafusi wake waingie barabarani kwa madai kaibiwa kura na nchi haitatawalika tena. Baadae huyo huyo Dr Slaa akawaongoza wenzake kwenda Ikulu kupeleka malalamiko yao kwa Rais ambaye hawamtambui.
Chadema wakajiingiza kwenye migogoro ya migomo ya madaktari, walimu wakijifanya wanawasaidia, ziku hizi Chadema inawazushia Idara ya Usalama Taifa inazua kila jambo la hovyo. Walianza kulitumia gazeti moja kuishambulia Idara ya Usalama Taifa. Lakini mpya ni tamko lililotolewa mbele ya waandishi wa habari na Mwenyekiti wake Mbowe, ati wamegundua mpango kabambe wa Idara ya Usalama wa Taifa inataka kuwauwa viongozi wa Chadema. Wakadai wana ushahidi lakini hawako tayari kuupeleka polisi.
Madai kama hayo wanapoyatoa kupitia vyombo vya habari wanataka Watanzania tufanye nini! Tuwaonee huruma, tuione serikali kuwa ni dhalimu, au hao wanaowindwa wana nafasi gani kwa familia zetu? Propaganda za kitoto kabisa.
Serikali isitumie ule msemo wa kiingereza wa "Never urgue with a fool, people will never notice the difference" Hawa si "fools". Walishasema nchi haitatawalika.
Bahati nzuri Watanzania wametoa hukumu sahihi kwenye uchaguzi wa madiwani katika kata 29.
Copy to.. chama, Ngongo, Pasco, zomba, Mungi, na wanabodi wote.
Chadema mnatakiwa kujitathimi upya na harakati zenu za kisiasa toka mlipotoka mpaka mnapoelekea hivi sasa. Acheni kuichezea serikali.
Katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, Chadema walianza kwa kupinga matokeo ya Rais yaliyompa ushindi Jakaya Kikwete, wakasusa kuhudhuria tukio la kutangaza matokeo pale viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam. Wakasusa sherehe za kuapishwa kwa Rais, wabunge wao wakatoka nje ya Bunge wakati Rais Kikwete akizindua Bunge la Tanzania, kwa madai ya kutomtambua Rais.
Hawakuishia hapo, baada ya ndoto zao za kuingia Ikulu kusambaratishwa na Watanzania, viongozi wa Chadema wakaanza kuandaa maandamano katika mikoa mbalimbali wakafanya hivyo Arusha, Mwanza, Mbeya, Songea, na Katibu Mkuu Dr Slaa aliendelea kuwahamasisha wafusi wake waingie barabarani kwa madai kaibiwa kura na nchi haitatawalika tena. Baadae huyo huyo Dr Slaa akawaongoza wenzake kwenda Ikulu kupeleka malalamiko yao kwa Rais ambaye hawamtambui.
Chadema wakajiingiza kwenye migogoro ya migomo ya madaktari, walimu wakijifanya wanawasaidia, ziku hizi Chadema inawazushia Idara ya Usalama Taifa inazua kila jambo la hovyo. Walianza kulitumia gazeti moja kuishambulia Idara ya Usalama Taifa. Lakini mpya ni tamko lililotolewa mbele ya waandishi wa habari na Mwenyekiti wake Mbowe, ati wamegundua mpango kabambe wa Idara ya Usalama wa Taifa inataka kuwauwa viongozi wa Chadema. Wakadai wana ushahidi lakini hawako tayari kuupeleka polisi.
Madai kama hayo wanapoyatoa kupitia vyombo vya habari wanataka Watanzania tufanye nini! Tuwaonee huruma, tuione serikali kuwa ni dhalimu, au hao wanaowindwa wana nafasi gani kwa familia zetu? Propaganda za kitoto kabisa.
Serikali isitumie ule msemo wa kiingereza wa "Never urgue with a fool, people will never notice the difference" Hawa si "fools". Walishasema nchi haitatawalika.
Bahati nzuri Watanzania wametoa hukumu sahihi kwenye uchaguzi wa madiwani katika kata 29.
Copy to.. chama, Ngongo, Pasco, zomba, Mungi, na wanabodi wote.
Last edited by a moderator: