Wakuu
kweli ccm imeshikwa pabaya na bila shaka inajua mwaka 2015 ndio mwisho wake na hili la kamati kuu ya ccm kukubali kwamba matokeo ya urais yawe na pingamizi yamedhihirisha hilo
natoa hoja...
DOMA
Kila mtu makini,mzalendo na mwanamapinduzi wa nchi hii anajua kabisa kuwa CCM wanaona MAJI YAMEZIDI UNGA ndiyo maana kwa sasa wameshaanza kuboresha sheria na taratibu ambazo huko nyuma zilikuwa zinakilinda CHAMA TWAWALA!
CCM wamesoma alama za nyakati na wanajua kabisa Watanzania wamechoka na chama hiki cha wababaishaji ambacho kwa zaidi ya NUSU KARNE tangu nchi imepata uhuru mwaka 1961 HAKUNA MAENDELEO YOYOTE KWA WATANZANIA. Kila kunapokucha hali za Watanzania walio wengi zinazidi kuwa mbaya huku wakidanganywa kuwa HAYO NDIYO MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.
Mimi nawashauri CCM wasiishie tu kwenye kuweka pingamizi kwenye matokeo ya Urais baali pia na hili la Rais kushtakiwa Mahakamani kama alikiuka katiba na sheria wakti akiwa madarakani wakubaliane nalo.Hiyo ndiyo DEMOKRASIA!
Halmashauri kuu ya Chama chochote kile haina haki wala mandate ya kuwaamulia watanzania watoe maoni ya aina gani tunapoelekea katika mchakato wa katiba. CCM haiwezi kukimbia kivuli chake yenyewe ni nani asiyejua kuwa CCM ndiyo imekuwa kikwazo cha mgombea binafsi kwa kuingilia uhuru wa mahakama?.
Suala la katiba mpya halipaswi kuwa politicised, we will all fail tusipoangalia.
Wamechanganyikiwa hawa, wamekuwa wakisema kuwa Katiba mpya ni wazo Lao, sheria wametunga wao, tena kwa kutoa matusi mengi kwa wapinzani, vitu vya kujadili na kutojadili wameweka wao, tume wameteua wao, tena kwa mbwembwe kibao, wajumbe wengi ni wao, kabla tume haijaanza kazi wao tayari wameshaanza kutoa maoni. Kama Ndio maoni Yao na serikali ni Yao kulikuwa na sababu gani ya kuunda sheria si wangeagiza tu serikali Yao ifanye wanavyotaka, kuliko Kupoteza hela bure.
Wahenga walisema mfa maji haachi kutapatapa.
WAzee wa upinzanI na politiki, Dalili za kufa CCM hizo!!!!!!!!!!