CCM wajiandaa na kampeni Segerea-Uchaguzi Mdogo

Bei Mbaya

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
2,262
843
Wameanza kujiandaa kwa kampeni za uchaguzi mdogo baada ya kupata taarifa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Mpendazoe(Chadema) dhidi ya Mbunge wa jimbo hilo na Naibu Waziri wa Ajira,Kazi na Vijana Dr.Makongoro Mahanga(CCM) kushindwa kesi hukumu itakayosomwa 02/05/2012.

Wajumbe wa Mitaa na Wenyeviti wamekuwa wakizunguka mitaani na kuulizia namba za Vitambulisho vya Mpigakura, na hasa wamekuwa wakiwalenga watu wa rika la kuanzia miaka 40 na kuendelea kwani ni wazi na rahisi kutoa ushirikiano ikilinganishwa na vijana.

Ushahidi wa polisi ndio uliomkaanga Dr.Mahanga kufuatia kukamatwa na maboksi 12 ya kura siku ya uchaguzi na kufikishwa nayo kituo cha polisi Tabata, pia ktk majumuisho ya vifaa yaliyokuwa yakifanyika kata ya Buguruni inadaiwa maboksi kadhaa kutoonekana na mengine kukutwa wazi bila 'seal' za kufungia baada ya zoezi la kuhesabu kura kurudiwa.

Pamoja na nguvu kubwa kutumika kwa Ikulu kumpigia simu na kumtaka Msimamizi wa Uchaguzi Bw.Fuime kumtangaza mgombea wa CCM mshindi usiku wa manane ktk ukumbi wa Arnatoglou-Mnazi Mmoja, Dr.Mahanga tarehe 02/05 anaenda kuenguliwa.

Ikumbukwe mwaka jana Mpendazoe alikamatwa na maafisa usalama eneo la Airport na kufunguliwa jalada la kumiliki gari la wizi na baada ya kutoa uthibitisho wa umiliki, polisi kituo cha Buguruni walitupilia mbali mashtaka yaliyokuwa yafunguliwe mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika, habari za kiintelijensia zinadai kulikuwa na lengo la kumuua kwa kushukiwa kupora gari maeneo ya Gongo la Mboto baada ya awali kabisa kesi kumuelemea Naibu Waziri mmiliki wa bar maarufu ya Nyantare iliyopo jimboni kwake.
 
Tusubiri tarehe 2!!

Kama kweli polisi walitoa huo ushahidi, sijui magamba yatachomokea wapi??

Tatizo mahakama hazitabiriki
 
tusubiri tarehe 02/05 kwanza, kwani kiuhalisia jimbo lile nila uncle mpendazoe CDM..
 
IKULU YETU IPO MIKONONI MWA mhuni,BABA TAIFA ALIWAHI KUSEMA IKULU ni MAHALI PATAKATIFU.SS KM IKULU INASHINIKIZA MSIMAMIZI ATANGAZE MATOKEO YA TOFAUTI HUU SI UHUNI. VLVL HATA KESI YA LEMA IKULU ILIHUSIKA. Uncle Fredy endelea kukazia mpaka kieleweke,Wanakuchelewesha tu.MUNGU atakungulia na utashinda dhuruma haitozidi haki.
 
Siku Makongoro akivuliwa ubunge nitafurahi sana. Ni mtu mshenzi sana, kwa nini uibe haki ya mwenzako?
 
Na huyu Mpendazoe haaminiki,Nahisi nae ni Gamba ndani CDM!Amulikwe kwelikweli kabla yakumpa post ya CDM Segerea ktk uchaguzi mdogo kama utakuwepo!
 
Wameanza kujiandaa kwa kampeni za uchaguzi mdogo baada ya kupata taarifa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Mpendazoe(Chadema) dhidi ya Mbunge wa jimbo hilo na Naibu Waziri wa Ajira,Kazi na Vijana Dr.Makongoro Mahanga(CCM) kushindwa kesi hukumu itakayosomwa 02/05/2012.

Wajumbe wa Mitaa na Wenyeviti wamekuwa wakizunguka mitaani na kuulizia namba za Vitambulisho vya Mpigakura, na hasa wamekuwa wakiwalenga watu wa rika la kuanzia miaka 40 na kuendelea kwani ni wazi na rahisi kutoa ushirikiano ikilinganishwa na vijana.

Ushahidi wa polisi ndio uliomkaanga Dr.Mahanga kufuatia kukamatwa na maboksi 12 ya kura siku ya uchaguzi na kufikishwa nayo kituo cha polisi Tabata, pia ktk majumuisho ya vifaa yaliyokuwa yakifanyika kata ya Buguruni inadaiwa maboksi kadhaa kutoonekana na mengine kukutwa wazi bila 'seal' za kufungia baada ya zoezi la kuhesabu kura kurudiwa.

Pamoja na nguvu kubwa kutumika kwa Ikulu kumpigia simu na kumtaka Msimamizi wa Uchaguzi Bw.Fuime kumtangaza mgombea wa CCM mshindi usiku wa manane ktk ukumbi wa Arnatoglou-Mnazi Mmoja, Dr.Mahanga tarehe 02/05 anaenda kuenguliwa.

Ikumbukwe mwaka jana Mpendazoe alikamatwa na maafisa usalama eneo la Airport na kufunguliwa jalada la kumiliki gari la wizi na baada ya kutoa uthibitisho wa umiliki, polisi kituo cha Buguruni walitupilia mbali mashtaka yaliyokuwa yafunguliwe mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika, habari za kiintelijensia zinadai kulikuwa na lengo la kumuua kwa kushukiwa kupora gari maeneo ya Gongo la Mboto baada ya awali kabisa kesi kumuelemea Naibu Waziri mmiliki wa bar maarufu ya Nyantare iliyopo jimboni kwake.

Karibu tutafika nchi ya maziwa na asali.
 
BeiMbaya - habari hii umeitoa wapi? ni mawazo yako au una ''source'' ya kuaminika??
 
Back
Top Bottom