Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Napenda kutoa ushauri kwa wana CCM kuwa huu ni wakati ambao tutajilaumu na kuwalaumu wengi baada ya kupoteza jimbo la Arumeru Mashariki. Huku tukituma timu nzito.
Tunaweza kulaumiana kwa yafuatayo AU KUWALAUMU WAFUATAO.
1. LUSINDE KWA MATUSI YALIYOPOROMOSHWA MKUTANONI BILA SONI.
2. MKAPA KUSEMA UONGO ULIOTUGHARIMU kwa kukanushwa na familia NA KUTUFANYA TUSIAMINIKE ( YEYE ZAIDI) KWA MANENO YALIYOFUATA.
3. WASIRA KUENDELEZA UONGO WA MKAPA NA KUMPONDA SLAA BILA KUJUA ANAOONGEA NAO na hatimaye kanisa kukanusha.
4. KUTUMAINI WAGANGA WA KIENYEJI NA KUWATUMIA KATIKA KAMPENI KINYUME NA IMANI YA WENGI.
5.KUMCHUKUA SIOI KWA NGUVU YA PESA BADALA YA SARAKIKYA ALIYEKUWA CHAGUO LA WENGI.
6. KUMTUMIA LOWASA mwenye tuhuma nyingi za kujibu.
7.VIONGOZI WA CHAMA KUTOKUKEMEA LUGHA YA MATUSI ILIYOTUMIKA KIASI CHA WATU KUJUA NI UJUMBE WA CCM.
8.KUWADHARAU WANANCHI KWA KUSEMA AU KUONYESHA HAWAHITAJI SERA BALI VIJEMBE.
9. WATU WAZIMA WENYE HESHIMA KUNENA UONGO kwa kurudia bila kujali.
10. SLAA ameaminiwa sana kwa kuwa kila alichokisema dhidi yetu hatimaye ilikuja kugundulika ni ukweli.
Ni rahisi kulaumiana kwa sababu hizo hapo juu. Lakini ukweli tutulie tuchukue hatua juu ya magamba tuliyoahidi tutayatoa ili turudishe imani iliyopotea. Ni vigumu kuaminisha watu kuwa unaweza kuwasaidia wakati familia yako imekushinda na haina msaada. Kama tumeshindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa walioko kwenye chama ni nani atakayeamini kuwa tutaweza kuendelea kuongoza serikali? Hatua yetu hii inaendelea kutoa umaarufu kwa upinzani. Wao wanachangiwa na wananchi sisi tunawahonga wananchi ili watuchague. TUSIPOCHUKUA HATUA BASI TUWE TAYARI KUPOTEZA KILA JIMBO LITAKALOKUWA WAZI NA KILA NAFASI YA UDIWANI. Hatua dhidi ya rushwa, wizi na ubadhirifu ni ya muhimu, Vinginevyo hata sisi wachache tuliobaki tunaondoka.
Hatuwezi kuona chama kikifa mikononi mwetu huku hakuna hatua inayochukuliwa. Kuogopana hakuwezi kuendelea kuwa asili yetu.
TUTAFAKARI TUCHUKUE HATUA ZA HAKI NA ZA KWELI AU TUBAKI TUKIENDELEA KUSEMA TUNAVUA GAMBA HUKU MIAKA IKIPITA. We have lost our moral authority. It will be very hard to keep on convincing people to trust us.
Tunaweza kulaumiana kwa yafuatayo AU KUWALAUMU WAFUATAO.
1. LUSINDE KWA MATUSI YALIYOPOROMOSHWA MKUTANONI BILA SONI.
2. MKAPA KUSEMA UONGO ULIOTUGHARIMU kwa kukanushwa na familia NA KUTUFANYA TUSIAMINIKE ( YEYE ZAIDI) KWA MANENO YALIYOFUATA.
3. WASIRA KUENDELEZA UONGO WA MKAPA NA KUMPONDA SLAA BILA KUJUA ANAOONGEA NAO na hatimaye kanisa kukanusha.
4. KUTUMAINI WAGANGA WA KIENYEJI NA KUWATUMIA KATIKA KAMPENI KINYUME NA IMANI YA WENGI.
5.KUMCHUKUA SIOI KWA NGUVU YA PESA BADALA YA SARAKIKYA ALIYEKUWA CHAGUO LA WENGI.
6. KUMTUMIA LOWASA mwenye tuhuma nyingi za kujibu.
7.VIONGOZI WA CHAMA KUTOKUKEMEA LUGHA YA MATUSI ILIYOTUMIKA KIASI CHA WATU KUJUA NI UJUMBE WA CCM.
8.KUWADHARAU WANANCHI KWA KUSEMA AU KUONYESHA HAWAHITAJI SERA BALI VIJEMBE.
9. WATU WAZIMA WENYE HESHIMA KUNENA UONGO kwa kurudia bila kujali.
10. SLAA ameaminiwa sana kwa kuwa kila alichokisema dhidi yetu hatimaye ilikuja kugundulika ni ukweli.
Ni rahisi kulaumiana kwa sababu hizo hapo juu. Lakini ukweli tutulie tuchukue hatua juu ya magamba tuliyoahidi tutayatoa ili turudishe imani iliyopotea. Ni vigumu kuaminisha watu kuwa unaweza kuwasaidia wakati familia yako imekushinda na haina msaada. Kama tumeshindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa walioko kwenye chama ni nani atakayeamini kuwa tutaweza kuendelea kuongoza serikali? Hatua yetu hii inaendelea kutoa umaarufu kwa upinzani. Wao wanachangiwa na wananchi sisi tunawahonga wananchi ili watuchague. TUSIPOCHUKUA HATUA BASI TUWE TAYARI KUPOTEZA KILA JIMBO LITAKALOKUWA WAZI NA KILA NAFASI YA UDIWANI. Hatua dhidi ya rushwa, wizi na ubadhirifu ni ya muhimu, Vinginevyo hata sisi wachache tuliobaki tunaondoka.
Hatuwezi kuona chama kikifa mikononi mwetu huku hakuna hatua inayochukuliwa. Kuogopana hakuwezi kuendelea kuwa asili yetu.
TUTAFAKARI TUCHUKUE HATUA ZA HAKI NA ZA KWELI AU TUBAKI TUKIENDELEA KUSEMA TUNAVUA GAMBA HUKU MIAKA IKIPITA. We have lost our moral authority. It will be very hard to keep on convincing people to trust us.