JET SALLI
JF-Expert Member
- Dec 1, 2014
- 1,992
- 1,197
Ndugu wanajamvi uchaguz mkuu wa mwaka 2010 ulipaswa kuwa funzo kwa CCM kujirekebisha kiutendaji.Katika hali ya kurudisha uwajibikaji ndani ya serikali ya CCM Katibu mkuu Abdulahman kinana aliwataja hadharani mawaziri mizigo wanao iangusha serikali na chama,cha ajabu na kushangaza Rais alimpuuza na hakuna hatua zozote ambazo rais alichukua,tulichoona ni kiburi tu kilichowajaa CCM na viongozi wake wa zama hizi cha kutosikiliza mamlaka ya wananchi,kinachotokea leo na Ugumu wa kampeni na kukataliwa na wananchi wala hakimshangazi mtu mwenye akili timamu,hivyo basi CCM kufa ni lazima tarehe 25 oktoba 2015 tena kifo cha kujitakia kwa sababu ya kuwapuuza wananchi.